Makongoro na ngozi za ng'ombe zimekuwa chakula kinachokidhi mahitaji ya Watanzania. Hali ya maisha ni ngumu

Nilijaribu supu ya ubongo wa ng'ombe nilishindwa kuimaliza. Kichefu chefu kilipanda mpaka puani. Mwe. Mnajirahidi mnaoiweza, nyie hamna mtakachoshindwa kula duniani.
We utakuwa wa kishua
Sisi huku Dom kuna chimbo wanauza supu ya ngozi yaani haijalishi ni ngozi ya nini hata iwe imewambwa kwenye ngoma za shule itabanduliwa na kutengenezwa kitaalamu mpaka iwe supu ukionja huwezi kuacha!
Hapo bado hujakutana na supu ya pumbu
 
Afya yako mgogoro mkuu.

Watu kama wewe mnakuaga na magonjwa nyemelezi mara kwa mara, kipindupindu kikiibuka nyie ndo chap mnakumbwa.
Kauli za watu vijijini ..Kichwa kikubwa ila akili hauna.!
 
😄 🤣 😂. Hebu nielekeze huko unapopasema panafaa. Je kongoro linaandaliwa bila kushikwa kwa mikono?? Je vyombo vinaoshwa na maji ya moto kisha kusuuzwa kwenye maji tiririka/bomba???.
Kimsingi wewe elewa tu kuwa huko kote unapokula supu NI WACHAFU SANA NA UMESHAKULA SANA SUPU ZILIZOBAKIZWA NA WATEJA. NITAKIJE BAA UNAYOIAMINI ILI NIKAIFANYIE KAZI NIKULETEE JIBU. HATA CLIP YA TUKIO NAKULETEA
 
Hakuna chakula kibaya SEMA mapishi tu ndo yanakuaga mabaya
 
binafsi napenda miguu ya n'gombe lakini sio ngozi
 
Makongoro sawa,ila ngozi ya ng'ombe kuliwa mbona kitu kipya kwangu!!!!!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shida siyo kushikwa kwa mkono, mikono inayoshikwa mkono maana, mtu alieshika wakati wa kuandaa alinawa kwanza mikono, maana wakati wa kuanda vyakula vingi, ni ngumu kuto shika kwa mkono. Mchele mtu atachagua kwa mkono, mchicha utakatwa kutumia mkono, nyama ya mchuzi vipande hukatwa kushikwa kwa mkono tena toka buchani.

Maji tililika huwezi kwenda migahawa, na bar ya maana ukakosa maji tililika kama kama ni mkazi wa Dar nenda hata pale kwenye mgawa unaotazamana na mlimani city uone tofauti na huko unakokula, nenda hata mgahawa high way manzese muhudumu hashiki kijiko kitakacho tumika na mteja kwa mkono, na kinawekwa kwenye maji ya moto, sehemu za kunawia zipo maji tililika. Sema, kuna watu tumeumbwa kubisha.
 
Kauli za watu vijijini ..Kichwa kikubwa ila akili hauna.!
Ndo ukweli huo, chunguza afya yako kijana.
Mara hiki huli, kile hili kichafu, hiki huli kimeandaliwa vibaya, kile huli kina kitunguu. Huwa mnaishi kwa vidonge tu maana miili inakosa vitu vingi mwisho ni full kuumwa umwa.

Pole sana mkuu.
 
Kuna kongoro inapikwa Mtwara nyuma ya stand kuu pale town...!! Wanapika wapemba wazee sio kifurushi ningewatumia na ninyi mjaribu.
 
Ndo ukweli huo, chunguza afya yako kijana.
Mara hiki huli, kile hili kichafu, hiki huli kimeandaliwa vibaya, kile huli kina kitunguu. Huwa mnaishi kwa vidonge tu maana miili inakosa vitu vingi mwisho ni full kuumwa umwa.

Pole sana mkuu.
Wakuja baki kijijini na ushamba wako😂😂...unakula kila kitu wewe ni binadamu sio nguruwe ndo hachagui kitu.

Mi nakula seafoods kwa sana sio mauchafu yenu hayo ,njaa kali.!!
 
yaani makongoro na ulimi ndyo mnaita madude? kuweni na heshima basi

kuna mahali supu ya ulimi ni 6000 kongoro buku tano
ni supu moja amaizing....usirudie kuyaita madude tena ukome kabisa
Kwa ulimi hata mimi nilishangaa kidogo, kwa US ulimi ni kama 45$ grocery, na ngozi tena ya kitimoto inatumika kutengneza pork skin chips na inapendwa sana
 
Itakuwa we ndo mshamba mimi nina kijiwe changu lazima kila siku nipate supu ya mkia wa ng'ombe na chapati 2
 
Tanzania nzima kila wilaya, kijiji, kata au tarafa lazima kuna kijiwe cha wauza Makonngoro na ngozi za ng'ombe ambazo watu wanakula na kulinda uhai wao
Wanasema wala makongoro ndiyo hunenepeana sana na kutafsiriwa kuwa wana afya bora
 
Wanasema wala makongoro ndiyo hunenepeana sana na kutafsiriwa kuwa wana afya bora
Kongoro hainenepeshi ile ni protein tupu, zile beer na mikate mnazokula na kongoro ndio vitambi vitupu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…