Makongoro Nyerere akutana na Jenerali David Musuguri

Makongoro Nyerere akutana na Jenerali David Musuguri

Mkuu hayo ni mawazo yako na huna haki yoyote ya kuzuia mtu mwingine kutoa mawazo yake,wewe kama unaishangilia ccm sawa na wanaoshabikia wapinzani ni haki yao.ccm wote ni majizi tu na hilo litabaki kuwa ni mtazamo wa kila mpenda haki ktk nchi hii,na hawatakiwi kupewa nafasi ya kuliongoza tena taifa letu.

Mkuu na wewe vile vile huna haki ya kutuamininisha hivyo hapo kwa red

Ila ujue hizi exaggerations zenu zinawaharibia hasa kwa watu neutral
 
Zakumi kafanya nini tena kule? Anakuleteani shida gani kule? Haya ngoja niwaachie great thinkers yenu na mimi nirudi huku uswekeni.

Anyway, kikatiba sifa za kuwa rais anazo. Sifa zilizobakia ni za ziada tu. Rais wa Tanzania hatakiwi kuwa technician au mkuu wa kamati ya ufundi.

Akitumia ujeshi wake na kufuata script anaweza kuwa rais mwenye mafanikio mazuri tu.
Zakumi nafurah kwamba nimekuona huku, leo.
jaman chonde chonde usiondoke kule manake sasa ukiondoka wewe tutabak na nani tena?

BTW mpaka sasa kuna kitu ambacho hakiko sawa kwa watanzania nacho ni wengi wetu hatujui sifa za rais wa nchi hii zinatakiwa ziwe zipi. hizi za kikatiba ni zile za ujumla lkn wasifu wa ndani je tunataka mtu yupi?
hilo bado ni changamoto na sijui kama media na wanaharakati wameweza kutoa elimu ya uraia ya kutosha kwa raia kwa muda huu uliobaki.
 
Last edited by a moderator:
Ulikuwa una hoja lakini umeshindwa kuisimami na ndio maana walio wengi wamekudis ...q. sio kuwa ndani ya CCM hakuna watu wema, wazarendo, wenye kuweza kuwatendea haki wenzao...ndio kusema yaliyokea kwa Zitto ndani ya CDM sio kusema CDM yote ina haiba ya Zitto, Samson Mwigamba na Kitla Mkumbo ..au yaliyotokea CUF sio kusema haiba ya Mzee Hamad Rashid ni sawa na Wanacuf wote.Kugeneralize mambo ni ufinyu wa kujituma kujua ukweli wa jambo..

Kuna watu makini ndani ya vyama vyetu vya siasa kuanzia CCM, CDM, CUF, navinginevyo wana uwezo thabiti wa kupambana na matatizo mazito yanayotusibu kama Rushwa, Wizi, Ufisadi, Maendeleo...lakini jinsi ya kuwaweka na kusimamia Taifa.Kwa kuwa tunao walalamika kuwa wanalitafuna Taifa wako ndani ya MFUMO [System] wa Taifa letu.Wengine ni viongozi, watendaji wakuu, watendaji wadogo na hata wananchi wa kawaida.Na popote penye ufisadi au wizi fahamu kuna mahusiano ya kimaslahi pia ...na jambo linapo husu maslahi tambua lina husu hatima ya VITA katika kutengua hatima hiyo.

Tunaposema Taifa liko kwenye Mtanziko wa UFISADI NA RUSHWA ndio kusema sio Viongozi tu hata sie wananchi wa kawaida tuna mchango wetu kwa kuwa mfumo pia uliojengwa HAKUNA RAIA wa kawaida anae weza kusimama na kusema jambo la UFISADI na RUSHWA bila kusukwa sukwa na mfumo wetu.Hivyo kuna tatizo la kitaifa la Ufisadi na Rushwa lakini si kweli kuwa kila RAIA wa Tanzania ni mla Rushwa na Fisadi kama ambavyo wewe unavyotaka kutuaminisha kuwa Wanccm wote ni tatizo.Jenga hoja kwa misingi ya kujenga FACTS.

Hutaelewa kama ni mpiga mbinja wa Mafisadi..!! Jaribu kujibu au waambie wakusaidie kujibu maswai haya??

Watia nia waccm ni lini wamejipambanua kwetu kuwa wapinga UFISADI?

Kama walijua kuna UFISADI kwanini walikaa kimya mpaka wasubiri siku ya kutangaza nia?

Ufisadi umetokea wao wakiwa ndani ya system.. sasa kama wao wenyewe ni sehemu ya tatizo na wanataka kubebesha Kikwete zigo lote la uozo hawa watu kama si WANAFIKI tuwape sifa gani?

Hivi unatumia kigezo gani kwa hawa watu kwa dhati ya moyo wao kuwa na uwezo wa kupambana na UFISADI?
 
Zakumi nafurah kwamba nimekuona huku, leo.
jaman chonde chonde usiondoke kule manake sasa ukiondoka wewe tutabak na nani tena?

BTW mpaka sasa kuna kitu ambacho hakiko sawa kwa watanzania nacho ni wengi wetu hatujui sifa za rais wa nchi hii zinatakiwa ziwe zipi. hizi za kikatiba ni zile za ujumla lkn wasifu wa ndani je tunataka mtu yupi?
hilo bado ni changamoto na sijui kama media na wanaharakati wameweza kutoa elimu ya uraia ya kutosha kwa raia kwa muda huu uliobaki.
Kule ndiko wapi? Niambieni na mimi jamani nikamfuate Zakumi kule kwani huyu ni mtani wangu wa jadi.
 
Baada ya mkutano wa jana na wakazi wa Butiama hapa Mwitongo -eneo hili ni Mwitongo,lakini nyumba nilisema nimeibatiza jina " Sananda".

Baada ya ule mkutano mdogo wa jana,leo Makongoro atakutana na Jenerali Musuguri kabla na kwenda Dodoma kuchukua fomu.

Ni ajabu hawa watu wanavyopigana vijembe kabla fomu hazijachukuliwa. Jenerali Musuguri ni native wa Butiama.

Ingekuwa vizuri kama wagombea uongozi wanaofika hapa wangekuwa wanakwenda kumsalimu.

Jenerali inaelekea siku hizi anaifikiria ile vita tu;jinsi ilivyokuwa kashkash kubwa na jinsi walivyofanikiwa kushinda.






Mkuu toka mtoke ikulu kipindi cha mshua wako ulishawahi kwendapo tena hata misele tu? Sasa muda si mrefu utakuwa unaenda utakavyo kusabahi broo
 
Hapa sasa urais nchi hii ni kwa watoto wa marais tu. Kwan inavyoelekea wameshajipanga. Anaingia makongoro miaka kumi. Akitoka anaingia hussein mwinyi miaka kumi akitoka anaingia ridhiwan. Miaka kumi. Wengine cjui kama kwa mpango wa urais wa kuridhiana cjui itakuwaje.

Hakuna ubaya, ni haki ya kila mtu kikatiba hata na wewe tangaza tu. sijui utasema nini utakaposikia Salma Kikwete akitangaza
 
Moja ya sifa ya kuchaguliwa kushika nchi,kwa nchi nyingi duniani,ni kushiriki vita vyevyote vya nchi yako ukipambana mstari wa mbele. Ingawa hii si sifa pekee balo inalipa. USA na Israel wanajali sana hilo. Lets see!
 
Zakumi nafurah kwamba nimekuona huku, leo.
jaman chonde chonde usiondoke kule manake sasa ukiondoka wewe tutabak na nani tena?

BTW mpaka sasa kuna kitu ambacho hakiko sawa kwa watanzania nacho ni wengi wetu hatujui sifa za rais wa nchi hii zinatakiwa ziwe zipi. hizi za kikatiba ni zile za ujumla lkn wasifu wa ndani je tunataka mtu yupi?
hilo bado ni changamoto na sijui kama media na wanaharakati wameweza kutoa elimu ya uraia ya kutosha kwa raia kwa muda huu uliobaki.

Back in the day, I was a regular here. But the democratization of the forum, forced some of us kung'atuka.

Baada ya Lowassa kuachia uwaziri mkuu niliandika article kusema kuwa watanzania washukuru their lucky star kwa sababu pamoja na kuwa kashfa ya Richmond ililingizia taifa hasara, ilizima matumaini ya Lowassa kuwa rais. Kutokana mizunguko ya kidunia sikuifanyia editing na sikupata nafasi ya kui-posti.

Vipimo vya matukio vinaonyesha kuwa leo hii Lowassa ana nafasi kama wagombea wengine kuwa rais. Na inawezekana anayo nafasi kubwa ya kuwa rais iwapo CCM itampitisha. Je Lowassa amefanya kitu gani cha maana toka aachie ngazi? Zaidi ya kutoa michango ajafanya chochote kile.

Hivyo ukinipata choice, I will go with Makongoro. Whether he's qualified or not, it doesn't matter to me.
 
Andrew Nyerere. Ingawa sijakutana na Mako siku nyingi sana tangu mwaka 1978 alipomaliza form 6 pale TS na kutuachia Kkizigo Jazz yetu, bado ninamuamini sana. Hata kama hapo katikati alifanya mambo ya kipuuzi- kama wengi wetu tulivyofanya kabla ya kutulia na kuwa watu tunaoaminiwa leo katika taaluma zetu- nina imani ana organization na supervison abilities kubwa sana tunazohitaji kwa kiongozi wa Tanzania leo hii.
 
Last edited by a moderator:
Moja ya sifa ya kuchaguliwa kushika nchi,kwa nchi nyingi duniani,ni kushiriki vita vyevyote vya nchi yako ukipambana mstari wa mbele. Ingawa hii si sifa pekee balo inalipa. USA na Israel wanajali sana hilo. Lets see!

Not entirely true, miaka ya vita vya Vietname na kurudi nyuma, kulikuwa na draft ya kujiunga na jeshi nchini Marekani. Na karibu kila kijana alijiunga na jeshi na kupigana. Hivyo kuwa na military credentials ilisaidia katika siasa na zaidi ya nusu ya wanasiasa ilikuwa na uzoefu wa kijeshi na vita.

Wanasiasa wengi wa sasa wa Marekani wana digrii za sheria na hawana uzoefu wa jeshi au kivita.

Kuhusu Israel, kila kijana anatakiwa aende jeshini, na wasioenda wanasababu maalumu. Hivyo karibu kila mwanasiasa kule ni mwanajeshi. Na kutokana na vita vya mara kwa mara na waarabu, kila mtu ana experience ya vita. Hivyo kwenda jeshi na vitani sio ujiko mkubwa kule. Ujiko ni achievement yako kama mwanajeshi au raia.

Hawa wagombeaji wa Tanzania watuambie walipokuwa jeshini walifanya nini? Je walikuwa section or platoon commanders? Au walikuwi wapishi?
 
Kule ndiko wapi? Niambieni na mimi jamani nikamfuate Zakumi kule kwani huyu ni mtani wangu wa jadi.

Nipo Jasusi. Napenda ufalme. Makongoro - Rais. Hussein Mwinyi - Makamu. Joseph Sokoine- Prime Minister. List ya 1983-1984.
 
Baro ongezea hapo :-

6. Ndiye candidate atakayerudisha Katiba ya WARIOBA
7. Ndiye candidate atakayeweza kukemea rushwa na ufisadi bila kumumunya maneno
8. Ndiye candidate atakayeleta heshima kwenye chama, mahakama, polisi, magereza, jeshi, usalama n.k kuna makanjanja wengi wameibuka kwenye hizi nyanja muhimu.
9. Anaweza kurudisha matumaini kwa wanyonge maana wamepoteza matumaini
10....
11....

Queen Esther

Mnajipea sifa tu, Makongoro ana zaidi ya miaka 60 na hajawahi ata kuwa mkuu wa wilaya alafu leo aruke urais?mnaota ndoto za mchana.
 
Baro ongezea hapo :-

6. Ndiye candidate atakayerudisha Katiba ya WARIOBA
7. Ndiye candidate atakayeweza kukemea rushwa na ufisadi bila kumumunya maneno
8. Ndiye candidate atakayeleta heshima kwenye chama, mahakama, polisi, magereza, jeshi, usalama n.k kuna makanjanja wengi wameibuka kwenye hizi nyanja muhimu.
9. Anaweza kurudisha matumaini kwa wanyonge maana wamepoteza matumaini
10....
11....

Queen Esther



Mnajipea sifa tu, Makongoro ana zaidi ya miaka 60 na hajawahi ata kuwa mkuu wa wilaya alafu leo aruke urais?mnaota ndoto za mchana.

Kama unatafuta wale ambao angalu waliwahi kuwa wakuu wa wilaya; basi kiingereza unatafuta kitu kinaitwa "STATUS QUO" yaani hutaki mabadiliko ya aina yoyote bali wale tu waliokulia katika utawala uliotufikisha hapa. Ningekushauri uweke nguvu yako kwa wale ambao hawajawahi kuwa na uongozi serikalini kwa ngazi yoyote- siyo waziri wala mkuu wa wilaya.
 
Back
Top Bottom