Makopo ya ARV yamezagaa mtaani kwangu

Ni kweli ukimwi kila kona lakini utashangaa kuna wanaJF members wengine wanaendekeza eti kimasihara. Na wanajisifu wameuza mechi.
 
Shukuru wewe unayaona unakua alerted

But mengine nasikia wanawapaga kuku wanenepe ,ondoa shaka
Siyo kuku tu, pia ng'ombe na nguruwe.
Huwapa ARVs sababu huwa zinapelekea ku trigger hamu ya kula kwa wanyama hao kuwa juu sana na hivyo miili kuongezeka haraka.
Mbaya ni kwamba watumiaji wa wanyama hao huwa kwenye hatari ya kuanza ku develop vimelea vya kansa na hatimaye kupata kansa
 
Naona ugonjwa umeshazoeleka kiasi kwamba waathirika hawajali kujulikana, wanatupa kopo tu. Mwanzoni ilikuwa siri, aibu na fedheha!
 
Hapo mtaani kwenu kutakua na members wapya wa Arv. Wakishakua mapro hutoweza ona tena hayo makopo kwani pro members hutoa vidonge vyote kwenye makopo akiwa pale pale hospital na kuviweka kwenye mfuko Mara tu anapovipokea.
 
Sikio la kufa halisikii dawa.
 
Watanzania bwana,sijui mtaacha lini Stigmatization,no wonder tutaendelea kuuana kwa hayo mambo ya sirisiri....waacheni watu wajitokeze wawe huru ili tuweze kuwafahamu kwenye jamii zetu
Ili muanze kuwatenga, kuna JAMII nyingine wakisikia hivyo wataanza kunyoosheana vidole. Hata ww usingependa kuanza kujulikana iwapo ungepata ugonjwa kama huo
 
Ukota yote yapeleke hospital
 
Halafu ukishawajua??
nikishawajua niwashauri namna ya kuteketeza hayo makopo na karatasi ili zisizagae hovyo mitaani. Makopo mengine huwa yana mabaki ya dawa watoto wanaweza kuokota na kuanza kula hizo dawa bila ushauri wa daktari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…