Makosa kadhaa katika kutoa Pepo (Exorcism). Mapepo/Majini hayaombewi yanafukuzwa

Makosa kadhaa katika kutoa Pepo (Exorcism). Mapepo/Majini hayaombewi yanafukuzwa

C
Nashukuru Kwa response yako mkuu mitale na midimu ,
Bhasi ngoja nijaribu na mimi kujibu kwa ki "jielimu" changu kidogo nilichopataga cha theolojia ya maandiko matukufu.

Cha Kwanza Hautakuja kukuta kwenye Maandiko ya kale (Agano la kale) yoyote ushahidi wa kuonyesha hasa kosa la shetani ila utakuta shetani akitajwa kwenye vitabu vya agano jipya kama baba wa uongo na baba wa kila maovu
Sasa turejee Shida zote zilipoanzia (Kwa mujibu wa Biblia)

Nitarejea aya ulizotoa Mwanzo 2 na mwanzo 3 na nitazitumia hizohzo

Kipindi M/Mungu anawakabidhi Bustani ya Edeni aliwaambia nitanukuu Mwanzo 2:16,17

......Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula,walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika........

Mungu alimwambia Adam na Mkewe pindi atakapokula bhasi atakufa Ngoja niache lugha za kiswahili na kiinglishi nilichunguze neno la MUNGU kwa lugha Mama iliyoandkiwa Kihebrew
kauli inasema ..........
......בְּי֛וֹם אֲכָלְךָ֥ מִמֶּ֖נּוּ מ֥וֹת תָּמֽוּת......

Matamshi;
....Ba yo wm (Ba yaumi) mim men nu Mawt (mowt) Tamut....

Sasa tuone
maneno yaliyotumika... ba yawm ....Mawt tamut...
maneno haya yanamaanisha Siku hiyo hyo mtakayokula ndiyo siku mtakayokufa..... Ni onyo kali sana yani kwa mfano umwambie mtu ukinywa sumu tu umekufa asipokufa bhasi sumu haikuwa sumu...

turudi kwa shetani aliwaambia Adam na Eve
soma kwenye Mwanzo 3:4
........לֹֽא־מ֖וֹת תְּמֻתֽוּן.......

matamshi;
.........La mawt tamutun......

maana yake Hamtafikwa na Umauti au kifo siku hiyo.....
Na pia akawaambia kuwa mtakavyokula hamtakufa ila "mtafumbuliwa macho na mtakuwa na ufahamu nanyi mtakuwa kama mungu Kwa kujua mema na mabaya"

Yaliyotokea baada ya kula tunda

1.Ni kweli hawakufa siku hiyo kama alivyowaambia ila waliishi zaidi ya miaka 900 baada ya siku hiyo

2.Mungu alithibitisha kuwa kwa kula Tunda walikuwa Na ufahamu kama mmoja wao...Soma mwanzo 3:22....
....."Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya".....


biblia bado inamtaja shetani kama ni advocate wa Upande wa malalamiko yaani anashitaki watu kwa mwenyezi Mungu soma 1 petro 5:8, ufunuo 12:10
Neno mshitaki kwa asili linatokana na neno la Kiyunani “Kategoros” au “Kategor”ambalo kwa kiingereza ni “An accuiser”

pia shetani anatajwa kama Ni mtu anayeishi mbinguni au mtu anayehudhuria vikao vya mara kwa mara vya mbinguni.
soma Ayubu 1:6-11 pia soma Ayubu 2:1-5 Bilia inasema hivi “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe?..........

Kitendo cha Mungu kumuuliza ulikwa wapi wewe ni kuonyesha ni mtu aliyetokea kuwepo hapo lakini hakuwepo......

Bado nasubiri jibu langu Mkuu
simtetei shetani ila najenga hoja juu ya Kitabu cha Biblia kuwa kimya juu ya Dhambi hasa ya shetan........

Mimi ni Muumini mzuri tu.....
Common sense inaniambia shetani alipatikana na kosa la kusema uongo maana ukweli aliujua,na alijua kuwa Mungu ni kweli katika kweli. Kwenye kitabu Cha Mwanzo shetani amechorwa kama Nyoka na adhabu yake ni kupondwa kichwa. Pili, unatakiwa ujue kufa ni mchakato,tunakufa kiroho kabla ya kufa kimwili,Mungu akisema utakufa hakika maana yake saa hiyohiyo umeshakufa kiroho na ita-manifest kimwili soon or later na hii inamaana Neno lake haliwezi kumrudia Bure! Yote katika yote,Shetani ni muasi mbele za Mungu na uasi ni kosa.
 
C

Common sense inaniambia shetani alipatikana na kosa la kusema uongo maana ukweli aliujua,na alijua kuwa Mungu ni kweli katika kweli. Kwenye kitabu Cha Mwanzo shetani amechorwa kama Nyoka na adhabu yake ni kupondwa kichwa. Pili, unatakiwa ujue kufa ni mchakato,tunakufa kiroho kabla ya kufa kimwili,Mungu akisema utakufa hakika maana yake saa hiyohiyo umeshakufa kiroho na ita-manifest kimwili soon or later na hii inamaana Neno lake haliwezi kumrudia Bure! Yote katika yote,Shetani ni muasi mbele za Mungu na uasi ni kosa.
Uongo alisema wapi unaweza kunionyesha
 
Alisema Adamu na Eva hawatakufa lakini walikufa....Soma Uzi wangu vizuri!
Nimesoma vizuri sana lakini umesoma nilichoandika ila ulisoma nilichoandika mimi kabla ya kujibu..?
Unajua maana ya

בְּי֛וֹם אֲכָלְךָ֥ מִמֶּ֖נּוּ מ֥וֹת תָּמֽוּת......

Au inatamkwa ..
....Ba yo wm (Ba yaumi) mim men nu Mawt (mowt) Tamut....
Neno Mim Men nu Linaweka msisitizo wa kwamba Hakuna huruma wala Rehema siku utakayofanya ndo siku hiyo hiyo utakayopata kinachofuata katika sentensi
Na katika sentensi hiyo kinchofuata ni Mawt..
hiyo ni Tafsiri halisi ya lugha ya Kihebrania
kwahyo siku ambayo watadiriki kula ndo aiku watakayokufa...

na ndo maana watafsiri wa biblia wakatumia neno hakika linalimaanisha "verily" maana hakuna uongo siku mtakayokula ndo siku itakayokuwa mwisho wao
na sio watakufa kidogokidgo..

Sasa maneno hayo hyakutokea ila Mungu aliprove kitu alichosema Shetani na kwahyo kama aliprove swali langu linabaki pale pale je shetani ana kosa gani?

aliichosema shetani Mwanzo 3:4-5
Screenshot_20231016-150730.png

Alichosema Mungu Mwanzo 3:22
Screenshot_20231016-150750.png


Hauoni kama Mwanzo 3:22 Ni prove ya kuwa mwanzo 3:4 ilikuwa sawa ...

Kuhusu kufa shetani alitumia na yeye.

La ba yo wm (Ba yaumi) mim men nu Mawt (mowt
au
kwa Kihebrania cha sasa
la mawt tamat ba yamin

kwamba hakika kwa siku hiyo hamtakufa...

narudia tena Kurudisha mpira kwako Kwakuwa Maneno ya Mungu Yameprove maneno ya shetani je shetani ana kosa gani?
 
Hauna akili
wewe unayo akili kweli?lete hoja sio kutukana hapa jamvini nimesha sema Pepo hawezi Kutoka Kwa Damu ya Bwana Yesu Hata wakusanyike Wachungaji wote wa dunia wakitoa Damu ya Yesu pepo mchafu hawezi kutoka ninasema mimi Herbalist Doctor MziziMkavu. Lete wewe hoja yako hapa usilete Maneno yako ya Pumba hapa jamvini.
 
wewe unayo akili kweli?lete hoja sio kutukana hapa jamvini nimesha sema Pepo hawezi Kutoka Kwa Damu ya Bwana Yesu Hata wakusanyike Wachungaji wote wa dunia wakitoa Damu ya Yesu pepo mchafu hawezi kutoka ninasema mimi Herbalist Doctor MziziMkavu. Lete wewe hoja yako hapa usilete Maneno yako ya Pumba hapa jamvini.
Shindwaaa
 
Wenzetu hayo mapepo na majini wanayapa soda na nyama yanakaa na kutulia
 
samahani kwa usumbufu Herbalist. dawa maalum za kumtoa pepo zipoje/zinafananaje na huwa zinatumikaje?
Je! huo utaalam maalum wa kutoa pepo huwa unaendana na hizo dawa maalum kabla au baada ya kutumia?
Dawa za kumtoa pepo huwa hazifanani kuna aina mbili ya kumtoa Pepo aina ya kwanza ya kumtoa pepo ni yule anaye pandisha katika kichwa cha mgonjwa kuna dawa zake za kuweza kumtoa na kuna dawa ya kumtoa Pepo mahaba aka jini mahaba na huyo pepo wa mahaba ndio pepo mkorofi sana kuliko yule pepo anaye pandisha katika kichwa cha binadamu. Kwani Pepo mahaba aka jini mahaba ndio pepo Mkorofi sana unapotumia dawa yeye hukaa pembeni mpaka dawa zipate kuisha mwilini hurudi tena na kukuletea usumbufu wake. Lakini kuna mbinu zake za kuweza kumtoa asiweze kurudi tena ingawa kumtoa kwake ni gharama kubwa kwani ndio pepo mbaya zaidi kuliko yule pepo anaye panda katika kichwa cha mgonjwa.
 
Dawa za kumtoa pepo huwa hazifanani kuna aina ya mbili ya kumtoa pepo aina ya kwanza ya kumtoa pepo yule anaye pandisha katika kichwa cha mgonjwa kuna dawa zake za kuweza kumtoa na kuna dawa ya kumtoa Pepo mahaba aka jini mahaba na huyo pepo w amahaba ndio pepo mkorofi sana kuliko yule pepo anaye pandisha katika kichwa cha binadamu. Kwani Pepo mahaba aka jini mahaba ndio pepo korofi sana unapotumia dawa yeye hukaa pembeni mpaka dawa zipate kuisha mwilini hurudi tena kukuletea usumbufu wake. Lakini kuna mbinu zake za kuweza kumtoa asiweze kurudi tena ingawa kumtoa kwake ni gharama kubw akwani ndio pepo mbaya zaidi kuliko yule pepo anaye panda katika kichwa cha mgonjwa.
Kumbe
 
Dawa za kumtoa pepo huwa hazifanani kuna aina mbili ya kumtoa Pepo aina ya kwanza ya kumtoa pepo ni yule anaye pandisha katika kichwa cha mgonjwa kuna dawa zake za kuweza kumtoa na kuna dawa ya kumtoa Pepo mahaba aka jini mahaba na huyo pepo wa mahaba ndio pepo mkorofi sana kuliko yule pepo anaye pandisha katika kichwa cha binadamu. Kwani Pepo mahaba aka jini mahaba ndio pepo Mkorofi sana unapotumia dawa yeye hukaa pembeni mpaka dawa zipate kuisha mwilini hurudi tena na kukuletea usumbufu wake. Lakini kuna mbinu zake za kuweza kumtoa asiweze kurudi tena ingawa kumtoa kwake ni gharama kubwa kwani ndio pepo mbaya zaidi kuliko yule pepo anaye panda katika kichwa cha mgonjwa.
asante kwa maarifa. hizo dawa ni za kunywa au kupaka?
 
Kumekuwa na sintofahamu katika namna ya kushughulikia Hawa vibaraka wa ibirisi. Mapepo Kwa aina zake.

Makosa ambayo nayaona.

1: Watu wanaomba na mapepo, Tena wanapiga na Magoti na kufumba macho.
Hakuna hiyo scene kwenye maandiko. Hatuombei mapepo tunayafukuza. Yakikomaa na sisi tunakomaa Hadi yatoke. Hayo sio maombi Wala Dua.

2: Shetani ni muongo na Baba wa Uongo. Usifanyie kazi maneno yake. Ni Ukosefu wa maarifa kumpa maiki Pepo au kumchukua maelezo ili uyafanyie kazi kama facts. Hata Yesu alipohojiana nayo aliyaamuru tu yaende hakufanyia kazi maneno yao. Hata hivyo yalimdanganya, Mwanzoni yaliongea Kwa Umoja baadae yakasema ni mengi region. Na region ilikuwa ni kikosi Cha kijeshi Cha kirumi sio Cha kipepo.

3: Pepo hutolewa Kwa Imani katika Damu ya Yesu tu. Mganga hatoi Pepo anayapoza Kwa kuongezea mengine au kulibembeleza litulie kiaina, asiyemuamini Yesu kuwa ni Mungu aliyeumba Hadi hao Majini/mapepo yakaasi hatoi Pepo Bali anawapoza tu. Nabii potoshi katika UKRISTO pia hatoi Pepo Bali anafanya sanaa ndio maana linapodai limetoka ukikuta a na aliyesimama Kiroho litalipuka Tena.

3: Aliyepewa mamlaka ya kutoa Pepo sio Mchungaji,Mwinjilisti,Kasisi au nabii tu Bali Kila anayemuamini Yesu anapaswa kuogopwa na kufukuza Pepo popote atakapokutana nalo. Nii mamlaka ukiamini unayo unakuwa na superiority complex dhidi ya vimamlaka vyote vya Ibirisi.

4: Mapepo na wachawi wanapenda makanisa,familia au watu wanaoyatajataja na kuyapa airtime. Haya makanisa na familia tunayaita Satan conscious churches/Families. Kanisani au Familia ni Mahali pa kumsifu Mungu, kutaja uwezo wake, ikiwezekana Shetani asimbuliwe kabisa. Hilo kanisa/familia hailiwezi kusumbuliwa mara Kwa mara na nguvu za Giza maana hazijapewa nafasi. Mungu hukaa katikati ya sifa. Mahali ambapo Mungu anasifiwa na kutukuzwa Sana Shetani hakai. Ni suala la Muda tu atachikichia automatically bila kujua siku, saa Wala dakika atatafuta anakopendwa na kutajwatajwa.


5: Hakuna kitu Kinaitwa Territorial spirits. Kwamba Kuna kitengo maalumu Cha Majini au mapepo kinatawala eneo flani tuu. Mapepo ni universal. Sio watu Hadi useme wamefungwa kufanyia kazi sehemu flani tu. Hiyo elimu chanzo chake ni mapepo yenyewe ili kuteka fahamu za watu.

6: Huwezi kumuua Pepo/jini. Hizo elimu chanzo chake ni mapepo yenyewe. Shetani na Malaika wake watauliwa na Yesu siku ya mwisho. Kazi yetu ni kuyafukuza kwenye miili ya watu yasiwatese lakini yatabaki tu yanavizia nafasi hapo au Kwa mwingine.


Leo tuishie hapo.
Mafungu yatakuja Kwa watakaotaka fafanuzi.

Muebrania
Mitale na Midimu.
🙏🙏🙏
 
Pepo aka shetani hawezi kutoka kwa imani ya damu ya Yesu hata siku moja kama ndio hivyo imani yako inavyokwambia Pepo haogopi Damu ya Yesu .Pepo anatolewa kwa dawa maalum za kumfukuza pepo mchafu na ukipewa na kuzitumia atatoka pepo mchafu akitaka asitake. Kuna utaalam maalum wa kuweza kumtoa pepo ndani ya mwili wa mtu au ndani ya nyumba unapoishi sio kutumia imani yako ya damu ya Yesu eti pepo mchafu ataweza kutoka sio rahisi. Mimi ninakataa unavyosema.
Hujui unachoongea; unless kama humjui Yesu. Unaweza kuongea hivi tu kama humjui Yesu.

Siku wakikurushia pepo, nipigie simu tu, wala sitahitaji kuja mahali ulipo.
 
Back
Top Bottom