Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
- Thread starter
-
- #221
Fundi...Unadhani wengi wanaangalia captions? Kama uliona wana umuhimu ungewaweka kwenye main body ambamo umemtaja mpaka dereva ambae ni muislamu! Ulishindwaje kujiuliza mbona hii habari haijakamilika? Mbona hamna wakristu? Mbona hamna wanawake? Lakini la hasha, kwako ilitosha kuwa waislamu wako front and centre. Huo ndio upotoshaji.
Amandla...
Mohammed mbona nimekusifia kwa kuwaenzi ndugu na jamaa zako. Ninachokupinga ni pale unapo distort michango yao kuegemea zaidi kwenye dini zao. Kuna wakina Abbas Max wengi tu ambao wamesahauliwa. Historia ndivyo ilivyo, sio wote wanaoshiriki wanaweza kukumbukwa au kupewa uzito sawa. Hauwezi kuwa historian unayekubalika kama unaona mazuri tu ya watu walio karibu nawe. Ungewatendea haki zaidi wakina Sykes kama ungeweza kutueleza mafanikio na mapungufu yao maana wao walikuwa binadamu kama alivyokuwa Nyerere.Fundi...
Huna la kusema jema kwangu kwa kule kuiandika upya historia ya TANU iliyowarudisha watu kama Abbas Max na Abdul Sykes kiasi leo wanafahamika?
Fundi...Mohammed mbona nimekusifia kwa kuwaenzi ndugu na jamaa zako. Ninachokupinga ni pale unapo distort michango yao kuegemea zaidi kwenye dini zao. Kuna wakina Abbas Max wengi tu ambao wamesahauliwa. Historia ndivyo ilivyo, sio wote wanaoshiriki wanaweza kukumbukwa au kupewa uzito sawa. Hauwezi kuwa historian unayekubalika kama unaona mazuri tu ya watu walio karibu nawe. Ungewatendea haki zaidi wakina Sykes kama ungeweza kutueleza mafanikio na mapungufu yao maana wao walikuwa binadamu kama alivyokuwa Nyerere.
Amandla...
Mohammed,Fundi...
Siku moja niko Tanga Ally Sykes kanipigia simu.
Alikuwa mwenye furaha.
"Mohamed leo asubuhi wamekuja watu kutoka Ikulu wamenieleza kuwa mimi na Bwana Abdul tumetunukiwa Medali ya Mwenge wa Uhuru."
Hapa akasimama kisha akacheka.
"'Wameniuliza kwani mimi na Bwana Abdul tumeifanyia nini Tanzania?
Ikawa zamu yangu kucheka.
Fundi...Mohammed,
Si kitu cha kushangaza. Wangapi katika hawa vijana wetu wanawajua wakina John Rupia, Erica Fiah, Vedasto Kyaruzi, Mwapachu, John Mwakangale Dennis Pombeah, Steven Mhando Kassanga Tumbo na hata Oscar Kambona. Huo ni udhaifu wa jamii yetu na unaendelea mpaka sasa hivi. Mapambio yote yanaimbwa kuwasifia viongozi wa juu wakisahau kuwa kuna wengi tu wanaochangia mafanikio yao. Angalau wakina Abdul walitunukiwa medali. Oscar Kambona hata kaburi lake ni la kutafuta.
Amandla...
Mohammed, tuko palepale. Wangapi wanawajua zaidi ya watu wachache ambao wamefanya utafiti wao binafsi? Ndio maana hamna cha kushangaza watu kutojua mchango wa Abdul Sykes.Fundi...
Erica Fiah...
Kwa mara yangu ya kwanza nimemsoma Erika Fiah kupitia kalamu ya Daisy Sykes Buruku, ‘The Townsman: Kleist Sykes’, in Iliffe (ed) Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, pp. 95-114.
Nilikuwa Arusha ndani ya Maktaba ya Taifa ambako nilikikuta kitabu hicho hapo juu alichohariri John Iliffe.
Nilivutiwa sana na mtu huyu khasa jinsi walivyokuwa anagombana na Kleist Sykes katika African Association.
Lakini kalamu ya kwanza kumweleza Erika Fiah haikuwa imeshikwa na mkono wa Daisy.
Erika Fiah kaelezwa katika mswada alioacha Kleist Sykes kabla hajafariki 1949 na Daisy akatumia chanzo hiki cha babu yake kumwandika babu yake na pia Erika Fiah.
Lakini mimi katika utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes nilizungumza na Mzee Islam Barakat mtu aliyewajua wote wawili kwa karibu sana.
Mzee Barakat akimjua Kleist na vilevile Erika Fiah.
Kutoka kwa Mzee Barakat nikamwandika Erika Fiah kwa staili yangu.
Mzee Barakat alinieleza historia ya Dockworker's Union of Dar es Salaam chama cha makuli ambacho General Secretary wake alikuwa Abdul Sykes akiwa kijana mdogo wa miaka 24.
Kama Erika Fiah alivyopambana na Kleist Sykes katika African Association katika miaka ya 1930, Erika Fiah akapambana na mtoto wa Kleist, Abdul miaka ya meishoni 1940s.
Bahati mbaya hujakisoma kitabu cha Abdul Sykes ka hiyo haya huyajui.
Wakati huo Barakat alikuwa Mwafrika wa kwanza kuwa Labour Inspector na alikuwa katika KAR pamoja Abdul Sykes wakati wa Vita Vya Pili Vya Dunia (1939 - 1945).
Vedasto Kyaruzi...
Ninao mswada wa kitabu chake, ''The Muhaya Doctor.''
Dr. Kyaruzi aliingia katika uongozi wa TAA akiwa President na Abdul Sykes Secretary kwa juhudi kubwa ya Schneider Abdillah Plantan.
Bahati mbaya katika mswada wake hakumtaja popote ila Schneider na wenzake waliowatia hawa vijana madarakani amejumiuishwa katika kundi la ''wazee'' hawana majina.
Hivi ndivyo Nyerere na yeye anavyopenda kuwaeleza wale waliomuunga mkono kuchukua uongozi wa TANU kawatambulisha kama ''wazee'' hawana majina.
Mwapachu...
Mkutano wa kuamua kumuingiza Nyerere ndani ya ''circle'' achukue uongozi wa TAA 1953 kisha mwaka wa 1954 waunde TANU ulifanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu Nansio Ukerewe.
Mazungumzo haya walikuwapo Hamza Mwapachu kama mwenyeji, Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe.
Ali Mwinyi alikuwa Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.
Hii ilikuwa miezi ya mwanzo ya mwaka wa 1953.
Steven Mhando...
''Mkomunisti,'' hivi ndivyo Waingereza walivyokuwa wanamuona.
Alikuwa mjumbe wa TAA Political Subcommittee wajumbe wengine wakiwa Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Sheikh Hassan bin Ameir Mufti wa Tanganyika, Sheikh Said Chaurembo na John Rupia.
Kassanga Tumbo...
Nishamweleza.
Oscar Kambona...
Kuna kitabu chake kinaandikwa.
Tusubiri.
Fundi...Mohammed, tuko palepale. Wangapi wanawajua zaidi ya watu wachache ambao wamefanya utafiti wao binafsi? Ndio maana hamna cha kushangaza watu kutojua mchango wa Abdul Sykes.
Amandla...
Tunarudi pale pale, Mohammed. Kwamba vijana hawawajui hawa wazalendo ni ushahidi wa kutosha kuwa kitabu chako hakisomwi kwa kiasi unachodhania. Na kuwataja tu kama support act katika ufalme wa Abdul Sykes hakuwatendei haki. Kitabu chako kinamfaa mtu anaetaka kujua historia ya Sykes, hakisaidii kujua kwa ukamilifu michango ya hawa wengine.Fundi...
Hao wazalendo wote wamo katika kitabu cha Abdul Sykes.
Ngongo, uliyemnukuu ni 'Fundi Mchundo'. Uliyemtaja ni 'fundimchundo'. Two different peopleAhsante Mkuu fundimchundo nimefuatilia mjadala huu muda mrefu Mzee Mohamed Said ameshindwa pasipo shaka kutetea kitabu chake ambacho amekibandika historia ya Tanu kumbe ni historia ya Wazee wake na WaIslam wa Tanganyika.
Fundi...Tunarudi pale pale, Mohammed. Kwamba vijana hawawajui hawa wazalendo ni ushahidi wa kutosha kuwa kitabu chako hakisomwi kwa kiasi unachodhania. Na kuwataja tu kama support act katika ufalme wa Abdul Sykes hakuwatendei haki. Kitabu chako kinamfaa mtu anaetaka kujua historia ya Sykes, hakisaidii kujua kwa ukamilifu michango ya hawa wengine.
Amandla...
Sio kejeli, Mohammed. Kwako wewe kila kitu ni relative kwa Abdul Sykes, yeye ndio centre kwako. Hii ni dhahiri kwa namna ambavyo title ya kitabu chako ni Maisha ya Abdulwahid Sykes lakini unadai inazungumzia historia ya TANU na Tanganyika! Hivi unaweza kuzungumza chochote kuhusu historia ya nchi yetu bila kutuambia namna wakina Sykes ndio ma star wa hiyo historia_Fundi...
Yawezekana sana kuwa si vijana tu wasiojuwa historia ya uhuru wa Tanganyika ni watu wengi sana kupita kiasi hawajui.
Huo ni ukweli wala hapana shaka.
Lakini ninachoweza kusema ni kuwa hivi sasa katika hao watu wengi wasiojua taratibu ukweli unadhihiri kuwa historia waliyokuwa wakiijua ina upungufu mkubwa.
Kuhusu usomaji wa vitabu watu wengi hawasomi vitabu hili mimi kana mwandishi nalijua vyema sana.
Ila katika kundi ambalo mimi nililikusudia wasome kitabu hiki nimefanikiwa sana.
Hili la ufalme wa Abdul Sykes sijui hii kejeli imekujaje.
Fundi...Sio kejeli, Mohammed. Kwako wewe kila kitu ni relative kwa Abdul Sykes, yeye ndio centre kwako. Hii ni dhahiri kwa namna ambavyo title ya kitabu chako ni Maisha ya Abdulwahid Sykes lakini unadai inazungumzia historia ya TANU na Tanganyika! Hivi unaweza kuzungumza chochote kuhusu historia ya nchi yetu bila kutuambia namna wakina Sykes ndio ma star wa hiyo historia_
Amandla...
Kwanini waliamua kumuingiza Nyerere katika circle na tena kumpa uongozi wa juu kabisa katika chama chao? Waliona nini kwake? Mbona kulikuwa na watu wenye uwezo mkubwa tu kama Kyaruzi, Mwapachu, Abdul Sykes nk. ambao wangeweza kushika jukumu hilo na badala yake wakampandisha Nyerere.Mwapachu...
Mkutano wa kuamua kumuingiza Nyerere ndani ya ''circle'' achukue uongozi wa TAA 1953 kisha mwaka wa 1954 waunde TANU ulifanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu Nansio Ukerewe.
Nani anaandika kitabu cha Kambona? Ni wewe Mkuu au mwandishi mwingine?Oscar Kambona...
Kuna kitabu chake kinaandikwa.
Tusubiri.
Ulilikusudia kundi gani?Ila katika kundi ambalo mimi nililikusudia wasome kitabu hiki nimefanikiwa sana.
James...Kwanini waliamua kumuingiza Nyerere katika circle na tena kumpa uongozi wa juu kabisa katika chama chao? Waliona nini kwake? Mbona kulikuwa na watu wenye uwezo mkubwa tu kama Kyaruzi, Mwapachu, Abdul Sykes nk. ambao wangeweza kushika jukumu hilo na badala yake wakampandisha Nyerere.
Kwa hivyo kumbe huu uchaguzi ulikuwa ni geresha tu!Ndipo wakafanya uchaguzi wa Arnautoglo Hall Abdul Sykes na Julius Nyerere kugombea nafasi ya President.
Kumbe wazee wako walikuwa hawajaenda shule kabisa? Inasikitisha sana. Ndo maana baadae Mwalimu akaona wana mawazo ya kijinga dawa yao ni kuwazima tu. Kusema Nyerere alishinda kwa kura chache ni chuki yako tu dhidi ya Mwalimu.James...
Mwalimu alikuwa kawazidi wenzake wote kwa mbali sana.
Elimu yake ilikuwa ya juu na hiki TAA walikitaka kwa kuwaonyesha UNO kuwa chama kina viongozi walioelimika sawasawa - Masters Degree University of Edinburgh.
Kabla ya kuja Nyerere Abdul Sykes alimtaka Chief David Kidaha Makwaia achukue uongozi lakini Chief Kidaha hakutaka.
Chief Kidaha alikuwa kasoma Oxford.
Nyerere hakuonyesha kusita kubeba jukumu la uongozi wa TAA.
Jingine ambalo walilitazama na hii ndiyo ulikuwa msimamo wa Hamza Mwapachu ni kuwa kiongozi wa kuongoza mapambano ya kudai uhuru awe Nyerere kwa kuwa ni Mkristo ili kuzimua lile joto la Waislam lililokuwa katika TAA pale New Street.
Hofu ilikuwa wasije Waingereza wakatia fitna kuwa harakati za kudai uhuru ni shinikizo la Waislam peke yao.
India waligombanishwa na Waingereza kukawa na Nehru akiongoza chama cha Wahindu na Mohamed Ali Jinnah akiongoza chama cha Waislam.
Waingereza wasingeshindwa kusajili chama kingine kikiongozwa na Mkristo kwa hofu kuwa TANU imejaa Waislam.
Hili lilijadiliwa kati ya Hamza Mwapachu, Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe nyumbani kwa Mwapachu mwezi April 1953 na muafaka ukafikiwa.
Ndipo wakafanya uchaguzi wa Arnautoglo Hall Abdul Sykes na Julius Nyerere kugombea nafasi ya President.
Nyerere akashinda uchaguzi ule kwa kura chache sana.
James...Kwa hivyo kumbe huu uchaguzi ulikuwa ni geresha tu!
Mama...Kumbe wazee wako walikuwa hawajaenda shule kabisa? Inasikitisha sana. Ndo maana baadae Mwalimu akaona wana mawazo ya kijinga dawa yao ni kuwazima tu. Kusema Nyerere alishinda kwa kura chache ni chuki yako tu dhidi ya Mwalimu.