Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Mzee Mohamed Said ulikuwa na miaka 10 mwaka 1962. Kila kitu unachoandika ni kwa kusimuliwa. Katika muktadha huo wewe sio source ya kuaminika kwasababu kwanza uko biased kwenye dini yako lakini pili maelezo yako asilimia kubwa umeyatoa kwa waislamu wenzio ambao mwalimu aliwaweka kando kwasababu walikuwa weupe kichwani.

Kila mahali hutaki kutambua kwamba John Rupia alikuwa na mchango mkubwa sana unalazimisha masimulizi ya Sykes ndio yawe standard. Mimi namuona Sykes ni mtu mwenye wivu baada ya kuwekwa pembeni na mwalimu wakati anaijenga nchi.

Nyerere alifanya akili sana kuwakataa hao wazee wa kiislamu maana nia yao ilikuwa kuleta utawala wa dola ya kiislamu. Kinachowauma nyie ni kwamba mlimpa misaada Nyerere lakini yeye akaamua kuweka utaifa mbele badala ya maslahi yenu ya kidini. Pole sana maana ishatoka hiyo na historia inatambua mwalimu ndiye aliongoza kupigania uhuru mwanzo mwisho.

Wekezeni katika elimu acheni hii ajenda yenu ya kuzaliana muwe wengi mkiamini mtaitawala Tanzania. Hilo sahauni. Juzi hapa watoto wenu mliowazaa bila mpangilio wameuwawa kama panya road huko temeke. Narudia tena jikiteni kwenye elimu ili tujenge taifa lenye maendeleo.
Champ...
Tunaweza kujadili hili suala la elimu na kama nilivyokuambia fungua uzi mpya.
Tusichanganye mada.

Tatizo si kuwa Waislam hawapendi elimu.
Waislam walikuwa wanajenga Chuo Kikuu 1968 chini ya EAMWS.

Huku kwa wao kutaka kujenga Chuo Kikuu ndiyo ikawa sababu ya serikali kuivunja jumuia hiyo na kuunda BAKWATA.

Fungua uzi In Shaa Allah nitakuja kusomesha somo hili.

Nakuhakikishia utapata mengi yenye manufaa ambayo wewe hukuwa unayajua.

Naijua historia hii ya elimu kama ninavyoijua historia ya TANU.

Kuhusu haya mengine kuhusu John Rupia.
Hujasoma kitabu cha Abdul Sykes.

Sasa haifai kujadili jambo usilolijua hivi ni kupoteza wakati wako na wangu.
Soma kitabu cha Abdul Sykes uone mchango wa John Rupia:

''Ally Sykes ana barua ya mwaka 1954 iliyoandikwa kwa penseli toka kwa Zuberi Mtemvu kwenda kwake akimtaarifu juu ya mazungumzo aliyokuwanayo (Mtemvu) na Nyerere kuhusu yeye na TANU; stakabadhi ya hundi ya posta toka kwa Ally Sykes kwenda kwa Japhet Kirilo wakati wa Mgogoro wa Ardhi ya Wameru; nakala ya barua isiyokuwa na tarehe kutoka TAA kwenda kwa Malkia Elizabeth iliyotiwa saini na viongozi wote wa TAA: Rais Julius Nyerere, Makamu wa Rais Abdulwahid Sykes, Katibu Mkuu Dome Okochi, Naibu Katibu Dossa Aziz, Mweka Hazina John Rupia, Naibu Mweka Hazina Ally Sykes ikimpongeza Malkia kwa kutawazwa; barua ya mwaka 1952 toka kwa Rashid Mfaume Kawawa kutoka Bukoba kwenda kwa Ally Sykes ikimfahamisha juu ya hali ya siasa katika Kanda ya Ziwa; barua ya mwaka 1963 toka kwa Lady Judith Listowel, Kenneth Kaunda, Julius Nyerere, Kasela Bantu, Chifu Thomas Marealle ...orodha haina mwisho.''

Majina hayo hapo juu yako kwenye hiyo barua hapo chini kutoka Nyaraka za Sykes.

1672855393070.jpeg
 
Fundi...
Kwangu mimi faraja yangu ni kuwa angalau kitabu cha Abdul Sykes kimefungua mjadala leo tunayazungumza haya hadharani.

Makala yangu ya kwanza iliyochapwa na Africa Events kueleza historia ya kweli ya TANU na uhuru wa Tanganyika gazeti lote toleo zima lilikusanywa na kutolewa kwenye mzunguko.

Makala ile iliwataja Abdul na Ally Sykes na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika katika historia ya kupambana na ukoloni.

Mwandishi akatukanwa na kutishwa asithubutu kutia mambo ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika katika TANU.

Aliyenitisha mwaka ule wa 1988 ni yule kiongozi wa jopo la Chuo Cha CCM Kivukoni waliokuwa mwaka wa 1981 wanaandika historia ya TANU aliyehakikisha kuwa historia ya Sykes haiandikwi kwenye kitabu cha TANU.

Iko siku In Shaa Allah nitamweleza Prof. Malima.
Lakini nani mwingine historia yake iliandikwa pamoja na ya Nyerere? Sidhani kama waliachwa wakina Sykes peke yao.

Amandla...
 
1. 32% + 30% + 37% = 99%. What about the 1%?

2. Wahindu hawakuhesabiwa? Au nao ni pagans/local belief? Au ndiyo hiyo 1%?
Mimi jina pagan silipendi kwa sababu lilitumika kubeza imani za mababu zetu. Wageni walipotuletea dini zao kitu cha kwanza walichofanya ni kuzipa jina baya imani zetu.

Amandla...
 
Champ...
Tuchunge lugha na heshima zetu tufanye mjadala wa kupendeza.

Iko siku miaka mingi sisi hatupo watakaokuja kutusoma waseme, "Hakika walipita watu."

Hii si taarifa ya mimi kupewa.

Mimi nimeishi nyakati hizo lau nilikuwa mtoto, baba na babu yangu wameishi nyakati hizo na nimewadiriki wengi ninaowataja hapa.

Wengine nimejuananao kwa karibu sana.

Kitabu cha Abdul Sykes hakina mfano wake katika vitabu vilivyoandikwa kuhusu TANU na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kamsome Listowel (1963) Kimambo na Temu (1969), Uloto (1971), Kivukoni (1981) na Shivji at al (2020) utaona tofauti.

Ndugu yangu si kama najisifu nataka nikuzindue utoke ujingani.

Unatuambia Waislamu twende shule wewe una elimu ya kutosha kufanya mjadala wa mada hiyo?

Ushamsoma Ishumi? (sikumbuki mwaka).

Fungua uzi nitakuja kutoa darsa.

Nisome kwa utulivu na njoo kwangu kwa mjadala kwa adabu na heshima.

Mjadala huu si mahali pa lugha "longolongo."

Hapa nipo kwa kuamini pana heshima.
Mohammed unafananisha machungwa na mananasi. Wewe uliandika historia ya wakina Sykes, hukuandika historia ya TANU au Tanganyika. Ndio maana uliweza kwenda ndani sana kuchambua mchango wa wakina Sykes na wenzao katika historia yetu. Hukujali kilichoendelea Songea, Namtumbo, Iringa au Mbeya kama havikuhusu wakina Sykes na waislamu wenzao. Judith Listowel aliandika " The Makings of Tanganyika" na hivyo wigo wake ulikuwa maana. Alianza na uvamizi wa wajerumani, akazungumzia wale waliowapinga katika pwani ya Tanganyika (1888-9), wahehe (1891-8) na Maji Maji (1905-1907). Wewe hapa ukajikita kwenye ushiriki wa baba yake Kleist Sykes, kwengine hukujisumbua sana zaidi ya kudai kuwa waislamu ndio walioongoza mapambano hayo.
Ikafuata utawala wa wajerumani na waingereza kati ya 1906 hadi 1945. Ya tatu akazungumzia watu maarufu walioshiriki lakini akajikita zaidi kwenye ushiriki wa Nyerere. Listobel alikuwa mzungu na aliangalia historia kupitia macho ya kizungu. Hakuwa historian na hivyo kitabu chake kimekosolewa sana na wengine. Lakini cha msingi ni kuwa alitaka kuandika historia ya Tanganyika na sio ya Nyerere au Sykes. Ndio maana ingawa katika historia yake ya TANU aliwataja wakina Sykes hakwenda ndani kama ulivyofanya wewe. Kitu ambacho wakina Ilife walimkosoa ni yeye kutothamini mchango wa watu wa kawaida katika mpambano huo. Wewe umejitahidi kuwaingiza lakini bahati mbaya umepanua wigo kuwatambua waislamu wenzako waliokuwa wakiishi Dar es Salaam na Tabora. Wale waliokuwa wanaishi sehemu nyingine na hawakuwa waislamu haukuwatambua.
Kwa sababu hizi hauwezi kujisema kuwa ni authority wa kutoa darasa la comprehensive history ya TANU na Tanganyika nje ya mipaka uliyojiwekea. Utakachokifanya ni ku regurgitate grievances zako za siku zote kuhusu ndugu zako na kuweka picha za cover za vitabu vyako na za ndugu zako. Hiyo haitakuwa kutoa darasa bali kujaribu ku indoctrinate. Naona heri nimsome Iliffe.

Amandla...
 
Mohammed unafananisha machungwa na mananasi. Wewe uliandika historia ya wakina Sykes, hukuandika historia ya TANU au Tanganyika. Ndio maana uliweza kwenda ndani sana kuchambua mchango wa wakina Sykes na wenzao katika historia yetu. Hukujali kilichoendelea Songea, Namtumbo, Iringa au Mbeya kama havikuhusu wakina Sykes na waislamu wenzao. Judith Listowel aliandika " The Makings of Tanganyika" na hivyo wigo wake ulikuwa maana. Alianza na uvamizi wa wajerumani, akazungumzia wale waliowapinga katika pwani ya Tanganyika (1888-9), wahehe (1891-8) na Maji Maji (1905-1907). Wewe hapa ukajikita kwenye ushiriki wa baba yake Kleist Sykes, kwengine hukujisumbua sana zaidi ya kudai kuwa waislamu ndio walioongoza mapambano hayo.
Ikafuata utawala wa wajerumani na waingereza kati ya 1906 hadi 1945. Ya tatu akazungumzia watu maarufu walioshiriki lakini akajikita zaidi kwenye ushiriki wa Nyerere. Listobel alikuwa mzungu na aliangalia historia kupitia macho ya kizungu. Hakuwa historian na hivyo kitabu chake kimekosolewa sana na wengine. Lakini cha msingi ni kuwa alitaka kuandika historia ya Tanganyika na sio ya Nyerere au Sykes. Ndio maana ingawa katika historia yake ya TANU aliwataja wakina Sykes hakwenda ndani kama ulivyofanya wewe. Kitu ambacho wakina Ilife walimkosoa ni yeye kutothamini mchango wa watu wa kawaida katika mpambano huo. Wewe umejitahidi kuwaingiza lakini bahati mbaya umepanua wigo kuwatambua waislamu wenzako waliokuwa wakiishi Dar es Salaam na Tabora. Wale waliokuwa wanaishi sehemu nyingine na hawakuwa waislamu haukuwatambua.
Kwa sababu hizi hauna ujuzi wowote wa kutoa darasa la comprehensive history ya TANU na Tanganyika. Utakachokifanya ni ku regurgitate grievances zako za siku zote kuhusu ndugu zako na kuweka picha za cover za vitabu vyako na za ndugu zako. Hiyo haitakuwa kutoa darasa bali kujaribu ku indoctrinate.

Amandla...
Fundi...
Nimekuambia kama unacho kitabu fungua nenda sura baada ya sura uangalie.

Hili hukufanya unarudi hapa na hoja zile zile.

The Life and Times of Abdulwahid Sykes
(1924-1968)
The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika
Mohamed Said

Table of Contents​

Dedication
Acknowledgements
Table of Contents
Introduction

Part One​

Abdulwahid Sykes 1924-1968​

Chapter 1. The Sykes: Origins 1894-1929
The Old Town of Dar es Salaam and its Elites
Kleist Sykes, Pioneer and Man of Ideas: 1894-1949
World War One 1914-1918
The Founding of the African Association and Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Muslim Association of Tanganyika), 1929-1933

Chapter 2.The Second World War and Tanganyika’s Political Foundation, 1939-1945

The Burma Infantry, 1942
Chapter 3. Dar es SalaamDockworkers Movement 1947-1950
Dar es Salaam Port, 1947
Erika Fiah
The Dockworkers’ Union, 1948

Chapter 4. The Genesis of Open Politics in Tanganyika 1950 -1954
The Tanganyika African Association, 1950
TAA Political Subcommittee, 1951
Tanganyika as a Mandate Territory
Kenyan Nationalists in the Struggle of Tanganyika,1950
TAA and KAU: Attempts at Linkage and Solidarity, 1950
The Meru Land Evictions, 1950
Chapter 5. Julius Kambarage Nyerere
The Story of Julius Nyerere, 1952
Tanganyika African National Union (TANU)-The Party of Independence, 1954
Chapter 6. The Pan African Congress of Northern Rhodesia, 1953
Ally Kleist Sykes

Part Two​

Mass Mobilisation and Independence 1954-1961​

Chapter 7. Mass Mobilisation 1954
The Elders’ Council and Nyerere’s Visit to the United Nations, New York, 1954
Idd Faiz Mafongo
The African Press-Ramadhani Mashado Plantan, 1950
Ahmed Rashad Ali-Radio Free Africa (Radio ya Afrika Huru), 1952
Propagandists-The Bantu Group,1955
Incorporation of Swahili Women’s Societies into the Struggle, 1955
Football As a Political Weapon
Chapter 8. The Formation of the Party in the Provinces
Central Province, 1955
Southern Province, 1955
Western Province, 1955
Tanga Province, 1956
TANU in Mombasa, Kenya, 1957
Chapter 9. The Tabora Conference-The Road to Independence, 1958
The Tanga Strategy, 1958
The Debate for Tripartite Voting
Pan-African Movement of East and Central Africa (PAFMECA), 1958
Independence, 1961

Part Three​

Conspiracy Against Islam 1961-1970​

Chapter 10. The Muslim Factor in Post-Independence Tanzania 1961-1970
Islam: The Ideology of Colonial Resistance
The First Muslim Congress, 1962
Resistance to Change
The Second Muslim Congress, 1963
Proposal for an Islamic University, 1964
The Politics of Islam, Church, State and the African Christian
Chapter 11. The East African Muslim Welfare Society (EAMWS) ‘Crisis’
Fomentation of the BAKWATA ‘Crisis’
Nyerere, Tewa, Bibi Titi Encounter, 1968
The Islamic National Conference, 1968
Omissions Analysed
Betrayal of Ideals
Conspiracy Theory
Epilogue
Bibliography

 
HISTORIA YA TANU NYANDA ZA JUU KUSINI

KUMBUKUMBU ZA UHURU: ABBAS MAX WA IRINGA (1918 - 1993)

Abbas Max ana historia ya kusisimua sana kama ilivyo kwa wazalendo wengi waliopigania uhuru wa Tanganyika lakini kwa bahati mbaya historia imewasahau.

John Iliffe mwanahistoria nguli aliyeiokoa historia ya Tanganyika amepata kusema kuwa historia nyingi ya TANU ipo katika mikono ya watu binafsi.

Iliffe alisema maneno haya katika miaka ya 1960 lakini kwa sasa ni wazi kuwa historia nyingi ya TANU si tu iko katika mikono ya watu binafsi bali iko pia katika masanduku na makabati yaliyoachwa na wazalendo wale waliopigania uhuru ambao takriban wote wameshatangulia mbele ya haki.

Historia hii ndani ya makabati na masanduku ya hawa wazalendo ni picha za "black and white" na nyaraka zilizoandikwa kwa mkono na type writer.

Siku chache zilizopita katika kutayarisha vipindi kwa ajili ya Nyerere Day nilitembelewa na waandishi na katika kuhitimisha mazungumzo yetu wakawa wanataka kujua majina ya wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika lakini wamesahaulika.

Ndipo nilipolitaja jina la Abbax Max katika video ambayo tulikuwa tunarekodi.

Hii video fupi ipo hapo FB.

Mtoto wa Abbas Max, Ally Abbas Max baada ya kuiona hii video siku ya pili tu akanitumia picha ya baba yake na ''cuttings'' za gazeti kuhusu historia ya marehemu baba yake katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Ally Abbas Max kwa miaka mingi alikuwa Marekani na sikutegemea kama atakuwa na kumbukumbu za baba yake huko alikokwenda ughaibuni.

Ally amenitia moyo sana aliponiambia kuwa baba yake ameacha nyaraka na zimehifadhiwa hadi leo zaidi ya miaka 30 toka kufariki kwake, ni kiasi cha kuzifungua tu na bila shaka mengi yatajulikana jinsi yeye na wenzake walivyofungua tawi la kwanza la TANU Iringa mwaka wa 1955.

Naeleza hapa yale niliyoweza kupata kutoka kwa Ally Abbas Max nikichanganya kidogo na yangu.

Inawezekana watu wengi wasijue kuwa Chief Adam Sapi Mkwawa ni mtu wa kwanza kuingia TANU Iringa.

Chief Mkwawa aliwaalika Abdul Sykes na Dossa Aziz Kalenga katika sherehe ya kupokea fuvu la babu yake Chief Mkwawa kutoka Ujerumani.

Hili fuvu liliwasili Dar es Salaam tarehe 9 Julai 1954 siku mbili tu baada ya TANU kuasisiwa.

Katika mazungumzo ya faragha baina ya Chief Adam Sapi Mkwawa, Dossa Aziz na Abdul Sykes, Chief Adam Sapi akakata kadi ya TANU kwa siri.

Abbas Max amewaeleza watoto wake kuwa Abdul Sykes alikuja Iringa wakati tayari TANU ishapamba moto Dar es Salaam na alifikia nyumbani kwake.

Abdul Sykes alikuwa njiani anaelekea Njombe kumtembelea mume mwenzie.
Abbas Max akaamua kumpeleka Njombe na gari yake Peugeot Pickup 203.

Mazungumzo baina yao yalikuwa kuhusu TANU, Nyerere na juhudi za kudai uhuru.
Abbas Max akamwambia Abdul Sykes amwambie Nyerere aje Iringa ili wafungue tawi la TANU na wao wawemo ndani ya juhudi hizi za kupigania uhuru.

Haukupita muda Abdul Sykes akamtumia Abbas Max taarifa kuwa Nyerere atafika Iringa akitokea Lindi, Songea na Njombe.

Abbas Max alitoka na wazalendo wenzake kwenda kumpokea Julius Nyerere njiani nje ya mji wa Iringa.

Nyerere alikuwa ameongozana na Ally Mwinyi Tambwe na Rajab Diwani na dereva wa TANU Omari Simba.

Nyerere alimfahamisha Abbas Max kuwa ili kufungua tawi la TANU kwanza lazima awe na wanachama 12 wanye kadi za TANU.

Watu walikuwa wanaogopa kuingia chama na hiki kikawa kikwazo kikubwa kwa Abbas Max.

Nyerere aifanya mkutano wa hadhara Iringa lakini ulihudhuriwa na watu wachache.
Juu ya haya yote Abbas Max aliweza kupata watu waliokuwa tayari kujiunga na TANU na hawa walikuwa: Saleh Masasi ambae Nyerere alilala nyumbani kwake, Hussein Issa, Hussein Kandoro, Yasin Hamid, Ahmed Mahmoud, Abdulrahman Mwangili, Juma Lipinjime na Khalfani Ally, Abbas Max akiwa Mwenyekiti.

Katika mkutano wa Kura Tatu Tabora mwaka wa 1958 Abbas Max akachaguliwa kuwa mjumbe wa Halmashauru Kuu ya TANU hivyo ikabidi ajiuzulu uenyekiti.

Nafasi yake ikachukuliwa na Chogga.

Chogga ameacha historia ya pekee katika wanasiasa ndani ya TANU waliokuwa mwiba wa koo kwa Julius Nyerere.

Itapendeza sana kama wanahistoria wataandika historia hii yake kwani mwaka wa 1968 Chogga na wenzake walifukuzwa TANU.

Ikutoshe tu kuwa Abbas Max anasema kuwa Chogga alisababisha TANU ifungiwe iringa.

Hii ikapelekea Abbas Max na wenzake waendeshe harakati zao chinichini kupitia Jambo Club waliyoianzisha baada ya TANU kupigwa marufuku.

Safari ya pili Nyerere alipokwenda Iringa alifikia nyumbani kwa Abbas Max.
Abbas Max alitembea kote na Nyerere Nyanda za Kati Kusini katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Charles Mzena ambae wakati wa kupigania uhuru alikuwa Special Branch alipata kumwambia Salum Khamis wakati huo uhuru ushapatikana kuwa, ''Chief Adam Sapi Mkwawa alikuwa ndiyo chief wa Wahehe lakini Abbas Max wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika alikuwa na nafasi yake juu ya Chief Adam Sapi.''

Abbas Max alikuwa na kawaida katika misafara ile na Nyerere kuwa wakati wa kula yeye alikuwa akisubiri hadi dakika ya mwisho wakati chakula kimetengwa na wanaanza kula yeye atampora Nyerere sahani yake na kumpa ya kwake.

Nyakati zile zilikuwa ngumu na Nyerere alikuwa akiwindwa.
Abbas Max alikuwa akisema, ''Hakuna huku wa kunidhuru mimi.''

Historia ya Abbas Max katika kupigania uhuru wa Tanganyika ina mengi sana.

Mimi Inshaa Allah nasubiri siku wanae watakapofungua Nyaraka za baba yao Abbas Max na kuziweka hadharani zisomwe na wanahistoria.

Tunamuomba Allah awarehemu wazee wetu hawa waliopigania uhuru wa nchi yetu kwa hali na mali zao.
Amin.

Picha ya kwanza ni Abbas Max.
Picha ya pili kulia ni Abbas Max, Julius Nyerere na Chande Ali.
Picha ya tatu kushoto ni Abbas Max ameegemea gari akiwa na Julius Nyerere na msafara wake.
Picha ya nne Mzee Abbas Max na mjukuu wake.

252729486_1056203561793688_8467899744738260880_n.jpg
252789922_1056220581791986_5100883259423906521_n.jpg
253251058_1056264835120894_2726486215836840789_n.jpg
253239453_1056265191787525_3466459277300259921_n.jpg
 
Lakini nani mwingine historia yake iliandikwa pamoja na ya Nyerere? Sidhani kama waliachwa wakina Sykes peke yao.

Amandla...
Fundi...
Katika hao walioachwa yupo mwenye historia inayokaribia historia ya akina Sykes kiasi akitolewa historia nzima ya Nyerere na ya uhuru wa Tanganyika inaporomoka?
 
Fundi...
Nimekuambia kama unacho kitabu fungua nenda sura baada ya sura uangalie.
Hili hukufanya unarudi hapa na hoja zile zile.

The Life and Times of Abdulwahid Sykes
(1924-1968)
The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika
Mohamed Said

Table of Contents​

Dedication
Acknowledgements
Table of Contents
Introduction

Part One​

Abdulwahid Sykes 1924-1968​

Chapter 1. The Sykes: Origins 1894-1929
The Old Town of Dar es Salaam and its Elites
Kleist Sykes, Pioneer and Man of Ideas: 1894-1949
World War One 1914-1918
The Founding of the African Association and Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Muslim Association of Tanganyika), 1929-1933

Chapter 2.The Second World War and Tanganyika’s Political Foundation, 1939-1945

The Burma Infantry, 1942
Chapter 3. Dar es SalaamDockworkers Movement 1947-1950
Dar es Salaam Port, 1947
Erika Fiah
The Dockworkers’ Union, 1948

Chapter 4. The Genesis of Open Politics in Tanganyika 1950 -1954
The Tanganyika African Association, 1950
TAA Political Subcommittee, 1951
Tanganyika as a Mandate Territory
Kenyan Nationalists in the Struggle of Tanganyika,1950
TAA and KAU: Attempts at Linkage and Solidarity, 1950
The Meru Land Evictions, 1950
Chapter 5. Julius Kambarage Nyerere
The Story of Julius Nyerere, 1952
Tanganyika African National Union (TANU)-The Party of Independence, 1954
Chapter 6. The Pan African Congress of Northern Rhodesia, 1953
Ally Kleist Sykes

Part Two​

Mass Mobilisation and Independence 1954-1961​

Chapter 7. Mass Mobilisation 1954
The Elders’ Council and Nyerere’s Visit to the United Nations, New York, 1954
Idd Faiz Mafongo
The African Press-Ramadhani Mashado Plantan, 1950
Ahmed Rashad Ali-Radio Free Africa (Radio ya Afrika Huru), 1952
Propagandists-The Bantu Group,1955
Incorporation of Swahili Women’s Societies into the Struggle, 1955
Football As a Political Weapon
Chapter 8. The Formation of the Party in the Provinces
Central Province, 1955
Southern Province, 1955
Western Province, 1955
Tanga Province, 1956
TANU in Mombasa, Kenya, 1957
Chapter 9. The Tabora Conference-The Road to Independence, 1958
The Tanga Strategy, 1958
The Debate for Tripartite Voting
Pan-African Movement of East and Central Africa (PAFMECA), 1958
Independence, 1961

Part Three​

Conspiracy Against Islam 1961-1970​

Chapter 10. The Muslim Factor in Post-Independence Tanzania 1961-1970
Islam: The Ideology of Colonial Resistance
The First Muslim Congress, 1962
Resistance to Change
The Second Muslim Congress, 1963
Proposal for an Islamic University, 1964
The Politics of Islam, Church, State and the African Christian
Chapter 11. The East African Muslim Welfare Society (EAMWS) ‘Crisis’
Fomentation of the BAKWATA ‘Crisis’
Nyerere, Tewa, Bibi Titi Encounter, 1968
The Islamic National Conference, 1968
Omissions Analysed
Betrayal of Ideals
Conspiracy Theory
Epilogue
Bibliography

Usinilazimishe ninunue kitabu chako Mohammed. Title ya kitabu inamhusu Abdulwahid Sykes na sio Tanganyika wala TANU. Hii ina maana focus ni yeye na sio watu wengine. Hao wengine ni bit players katika historia yake. Na mtu ukisoma heading za chapter zako zinaonyesha wazi focus yako ni wakina Sykes na waislamu. Haukukiandika kwa nia ya kutafuta ukweli bali kuzungumzia maonevu ambayo uliamini ndugu zako walifanyiwa. Hivyo sivyo inavyoandikwa historia ya nchi.

Amandla...
 
Usinilazimishe ninunue kitau chako Mohammed. Title ya kitabu inamhusu Abdulwahid Sykes na sio Tanganyika wala TANU. Hii ina maana focus ni yeye na sio watu wengine. Hao wengine ni bit players katika historia yake. Na mtu ukisoma heading za chapter zako zinaonyesha wazi focus yako ni wakina Sykes na waislamu. Haukukiandika kwa nia ya kutafuta ukweli bali kuzungumzia maonevu ambayo uliamini ndugu zako walifanyiwa. Hivyo sivyo inavyoandikwa historia ya nchi.

Amandla...
Fundi...
Mimi siuzi vitabu kwa hiyo siwezi kukulazimisha wewe au yeyote awae yule kununua moja ya vitabu vyangu.

Oxford University Press wana idara nzima ya masoko.
 
Fundi...
Katika hao walioachwa yupo mwenye historia inayokaribia historia ya akina Sykes?
Sio lazima wawe na historia ya wakina Sykes kama vile sio lazima historia ya wakina Sykes iwe sawa na ya Nyerere. Naamini kabisa kuwa tungejifunza mengi kama historia za watu kama John Rupia, Kassanga Tumbo, Oscar Kambona, Bibi Titi, Rashid Kawawa, Mwakangale, Eliufoo, Tibandebage na wengine wengi zingeandikwa kama ulivyoandika historia za ndugu zako. Bahati mbaya haikufanywa hivyo ndio maana unaweza kuwatanguliza ndugu zako kuliko wao.

Amandla...
 
Fundi...
Mimi siuzi vitabu kwa hiyo siwezi kukulazimisha wewe au yeyote awae yule kununua moja ya vitabu vyangu.

Oxford University Press wana idara nzima ya masoko.
Nitakisomaje bila kukinunua? Na nikinunua wewe si utafaidika? Ukweli ni kuwa majadiliano yetu na ujengaji wako wa hoja, maandishi yako mengine hayanisukumi ninunue kitabu chako.

Amandla...
 
Nitakisomaje bila kukinunua? Na nikinunua wewe si utafaidika? Ukweli ni kuwa majadiliano yetu na ujengaji wako wa hoja, maandishi yako mengine hayanisukumi ninunue kitabu chako.

Amandla...
Ahsante Mkuu fundimchundo nimefuatilia mjadala huu muda mrefu Mzee Mohamed Said ameshindwa pasipo shaka kutetea kitabu chake ambacho amekibandika historia ya Tanu kumbe ni historia ya Wazee wake na WaIslam wa Tanganyika.
 
Mama...
Nizidiwe.

Nizidiwe nini na nani na anizidi kwa yeye kuandika nini katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika?

Fanya utafiti tufahamiane.

Haya ya adabu yanategemea malezi.
Baadhi yetu tunazaliwa mama zetu wanatufunza adabu ya kula ya kuamkia nk.

Tunapelekwa kumbi na chuoni tunafunzwa adabu.
Adabu inakuwa sehemu ya maisha yetu.

Ikiwa huwezi kutofautisha samahani kwa neno hili ''ushenzi,'' uungwana siwezi kukulaumu kwani huenda hukuleleka.

Nadhani umepata kusikia wanafunzi wanawapiga walimu wao.
Wengi wanauliza nini kimetokea katika jamii yetu?

Kuwa napigania dini sawa siwezi kubadili uaminicho sana nitakuuliza kwani ni vibaya kupigania dini yako iwapo pana dhulma?

Kuhusu kupotosha hii ni fursa yako na wewe kuandika historia ambayo haikupotoshwa.

Kitabu kimetimiza miaka 25 na kinakimbilia chapa ya 5 hakijapatikana kitabu kupinga kitabu cha Abdul Sykes.

Watu hawawezi kupoteza muda kutunga kitabu ili kupinga kitabu chako kama wewe ulivyofanya kwenye huu uzi. Au wewe ulitunga kitabu ili upingwe? Maandishi yako ni historia tu ya baba zako na wazee wengine wa kiislamu. Maandishi yako hayana manufaa yoyote kwa taifa la Tanzania zaidi ya manufaa kwako binafsi na waislamu ambao pia umewabagua na kuwaongelea hao wa Kariakoo tu
 
Watu hawawezi kupoteza muda kutunga kitabu ili kupinga kitabu chako kama wewe ulivyofanya kwenye huu uzi. Au wewe ulitunga kitabu ili upingwe? Maandishi yako ni historia tu ya baba zako na wazee wengine wa kiislamu. Maandishi yako hayana manufaa yoyote kwa taifa la Tanzania zaidi ya manufaa kwako binafsi na waislamu ambao pia umewabagua na kuwaongelea hao wa Kariakoo tu
Mama...
Ahsante nimekusoma.
 
Sio lazima wawe na historia ya wakina Sykes kama vile sio lazima historia ya wakina Sykes iwe sawa na ya Nyerere. Naamini kabisa kuwa tungejifunza mengi kama historia za watu kama John Rupia, Kassanga Tumbo, Oscar Kambona, Bibi Titi, Rashid Kawawa, Mwakangale, Eliufoo, Tibandebage na wengine wengi zingeandikwa kama ulivyoandika historia za ndugu zako. Bahati mbaya haikufanywa hivyo ndio maana unaweza kuwatanguliza ndugu zako kuliko wao.

Amandla...
Fundi,
Nitarudia kukueleza yale yale mpaka lini?

John Rupia, Titi Mohamed na Rashid Kawawa wako katika kitabu cha Abdul Sykes.

Kassanga Tumbo na babu yangu Salum Abdallah ndiyo walikuwa viongozi wa TRAU kuanzia 1955 hadi walipowekwa kizuizini 1964.

Nitakuwekea hapa historia yao.

Rashid Kawawa utamsoma na babu yangu na Tumbo In Shaa Allah nitakuwekea hapa.

Eliufoo, Mwakangale na Tibandebage...

Kidogo nacheka.

Eliufoo yumo katika mswada huu: "Under the Shadow of British Colonialism The Life of Ally Kleist Sykes. "

Ndiyo nikacheka.
Hujui historia ya uhuru.

Kuna kwengine hapakuwa na chochote.

Nilipokuwa mdogo bibi yangu Mwatum bint Mgeni akinihadithia historia ya babu yangu Sheikh Muhammad Mvamila jinsi alivyokuwa kakaa mbele ya darsa anasomesha.
 
Hizi hadithi za mwl. Nyerere zitaisha lini.

Taifa linahitaji elimu ya uvumbuzi na inayoendana na maendeleo ya teknoloji.

Taifa tupiganie Maendeleo kwenye miundo mbinu.

Ninyi waandishi andikeni vile jamii. Yetu imetawaliwa na udini, ifisadi , rushwa umaskini wa kupindukia. Magonjwa..

Andikeni kutetea tabaka tawaliwa linavyonyonywa na tabaka tawala( mabwanyenye).
 
Fundi,
Nitarudia kukueleza yale yale mpaka lini?

John Rupia, Titi Mohamed na Rashid Kawawa wako katika kitabu cha Abdul Sykes.

Kassanga Tumbo na babu yangu Salum Abdallah ndiyo walikuwa viongozi wa TRAU kuanzia 1955 hadi walipowekwa kizuizini 1964.

Nitakuwekea hapa historia yao.

Rashid Kawawa utamsoma na babu yangu na Tumbo In Shaa Allah nitakuwekea hapa.

Eliufoo, Mwakangale na Tibandebage...

Kidogo nacheka.

Eliufoo yumo katika mswada huu: "Under the Shadow of British Colonialism The Life of Ally Kleist Sykes. "

Ndiyo nikacheka.
Hujui historia ya uhuru.

Kuna kwengine hapakuwa na chochote.

Nilipokuwa mdogo bibi yangu Mwatum bint Mgeni akinihadithia historia ya babu yangu Sheikh Muhammad Mvamila jinsi alivyokuwa kakaa mbele ya darsa anasomesha.
Mohammed, ninarudia pale pale kwa sababu siku zote mada yako, ushahidi wako ni ule ule. Ni hadithi zile zile, picha zile zile. Nasema siku zote kuwa kitabu chako ni historia ya Abdulwahid Sykes na sio historia ya Tanganyika au TANU. Kuna wakati ulitaka kumfunika Kassanga Tumbo na kumuinua babu yako tukakusahihisha.
Unasema kuwa John Rupia yumo katika kitabu chako lakini hapa unapata kigugumizi kukiri kuwa alikuwa mfadhili mkubwa wa TANU na ndie aliyelipia sehemu kubwa ya gharama ya safari ya Nyerere kwenda UN 1955. Unasema umemtaja lakini unashindwa kusema ndie aliyelipa fine ya shilingi 3000 aliyotozwa Nyerere katika kesi yake ya 1958. Hauwezi kuwatendea haki watu kama Solomon Eliufoo kwa kuwapachika ndani ya mswada wako unaomzungumzia Ally Kleist Sykes wakati yeye alikuwa mshauri mkubwa wa Julius Nyerere. Mimi sijui kama umemzungumzia Joan Wickens aliyekuwa anaenda kwa baiskeli Ikulu kila siku kutoka kwenye makazi yake Salvation Army.
Mimi siku utakapojitoa katika mipaka uliyokiwekea ndio nitakusoma. Siku utakapoweza kuwachambua wakina Sykes na waislamu kama unavyomchambua Julius Nyerere na wakristu nitakusoma.

Amandla....
 
Back
Top Bottom