Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Utaona kuwa umekazia ushiriki wa wakristu katika vita ya Maji Maji wakiwa upande wa wajerumani lakini umekaa kimya kuhusu ushiriki wa waislamu wakina Mbuwane na Plantan wakiwa upande wa wajerumani.
Mimi nina nadharia kuwa Mbuwane na Plantan hawakuwa wameupokea Uislam wakati wakipigana kama mercenaries wa Wajerumani. Ila ni nadharia tu, naamini Mohamed Said atakuwa na uelewa zaidi kuhusu jambo hili.
 
Nimetumia
Fundi...
Unaghadhibika.

Hakuna sababu ya kutumia lugha kali za "mazuzu."
Mimi nimeeleza safari ya Mwalimu ilivyokuwa.

Ikiwa hutaki basi hatuna sababu ya kugombana.

Mipango yote ya safari ilikuwa ikipangwa nyumbani kwa Abdul Sykes ambako Nyerere alikuwa akitoka Pugu kuja mjini anafikia.

Mwalimu hakuchanja "vaccination" kwa hofu ya hujuma za Waingereza.
Kazi hii Abdul alimkabidhi mdogo wake Abbas.

Kweli unaweza kufananisha historia hii na...
Ipo tofauti kubwa.

Kulia Haruna Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Nyerere, Sheikh Mohamed Ramia na Iddi Faiz Mafungo, Dodoma Train Station 1950s
View attachment 2468827
Kushoto: Rashid Sisso, Robert Makange, Zuberi Mtemvu, Iddi Faiz Mafungo, Julius Nyerere, John Rupia, Titi Mohamed wanamsindikiza Nyerere uwanja wa ndege safari ya kwanza UNO 1955
View attachment 2468830
Kulia: Chiku bint Said Kikusa, Titi Mohamed na Kulia ni Tatu bint Mzee na kati ni wanamsindikiza Julius Nyerere safari ya kwanza UNO 1955


Swali lilikuwa ni nani alilipia tiketi ya Mwalimu na sio suala la "vaccination". Ila hata hapo sijui Mwalimu aliwezaje kuingia Marekani bila kuthibitisha kuwa amechanjwa. Labda useme alipewa cheti cha kufoji. Tiketi ililipiwa kwa kiasi kikubwa na John Rupia. Hilo linakuwia ugumu kulikiri.
Nimesema unatuonaje kutokana na namna unavyoleta hicho unachoita ushahidi. Kwanza ulibandika picha ya wakina mama wa kiislamu kuthibitisha kuwa ni wao ndio waliomsindikiza airport. Sasa umeongeza nyingine ikionyesha kuwa wakina Robert na John nao walikuwapo! Na wote tunajua kuwa mara nyingi wanaopiga picha ni wachache katika kundi kubwa linalomsindiliza mtu wao. Utaona uliowataja ni saba tu wakati kwenye hiyo picha wako wengi zaidi ya hao. Kwa sababu hiyo kutumia hizi picha kama ushahidi kuwa ni waislamu peke yao ndio waliochangia ukuaji wa TANU ni kutaka kutupotosha.

Hauwezi kumfuta mtu kama Rupia kwa sababu tu jina lake ni John na ukawakuza wakina Iddi na Chiku juu yake. Hiyo sio sahihi. Hauwezi kutenda haki kama lengo lako ni kuwaenzi waislamu wenzako tu. Utakuwa hauna tofauti na wale unaodai hawakutaka kutambua mchango wa wakina Abdul katika mafanikio ya Julius.

Amandla...
 
Maisha yote ya Mohamed Said yameegemea kwenye usahihi wa stori alizopewa na Sykes. Yaani ameshupaza shingo miaka yote hii kwa stori za kusimuliwa ambazo ni kinyume na taarifa rasmi.

Waislamu nendeni shule acheni longolongo hapo hamtalazimika kuwachukia wakristo mnapoachwa nyuma. Duka linaonesha bidhaa kibao wewe unalazimisha ni mafuta ya taa na coca cola.
 
Maisha yote ya Mohamed Said yameegemea kwenye usahihi wa stori alizopewa na Sykes. Yaani ameshupaza shingo miaka yote hii kwa stori za kusimuliwa ambazo ni kinyume na taarifa rasmi.

Waislamu nendeni shule acheni longolongo hapo hamtalazimika kuwachukia wakristo mnapoachwa nyuma. Duka linaonesha bidhaa kibao wewe unalazimisha ni mafuta ya taa na coca cola.
Champ...
Tuchunge lugha na heshima zetu tufanye mjadala wa kupendeza.

Iko siku miaka mingi sisi hatupo watakaokuja kutusoma waseme, "Hakika walipita watu."

Hii si taarifa ya mimi kupewa.

Mimi nimeishi nyakati hizo lau nilikuwa mtoto, baba na babu yangu wameishi nyakati hizo na nimewadiriki wengi ninaowataja hapa.

Wengine nimejuananao kwa karibu sana.

Kitabu cha Abdul Sykes hakina mfano wake katika vitabu vilivyoandikwa kuhusu TANU na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kamsome Listowel (1963) Kimambo na Temu (1969), Uloto (1971), Kivukoni (1981) na Shivji at al (2020) utaona tofauti.

Ndugu yangu si kama najisifu nataka nikuzindue utoke ujingani.

Unatuambia Waislamu twende shule wewe una elimu ya kutosha kufanya mjadala wa mada hiyo?

Ushamsoma Ishumi? (sikumbuki mwaka).

Fungua uzi nitakuja kutoa darsa.

Nisome kwa utulivu na njoo kwangu kwa mjadala kwa adabu na heshima.

Mjadala huu si mahali pa lugha "longolongo."

Hapa nipo kwa kuamini pana heshima.
 
Mimi nina nadharia kuwa Mbuwane na Plantan hawakuwa wameupokea Uislam wakati wakipigana kama mercenaries wa Wajerumani. Ila ni nadharia tu, naamini Mohamed Said atakuwa na uelewa zaidi kuhusu jambo hili.
Hakika, ukizingatia na majina yao. Plantan, Shneider, Sykes, Kleist...
 
Hakika, ukizingatia na majina yao. Plantan, Shneider, Sykes, Kleist...
Gagnija,
Hayo nimeeleza katika kitabu cha Abdul Sykes.

Hawa Wazulu waliotoka Kwa Likunyi Imhambane, Mozambique walikuwapo Waislamu miongoni mwao.

Sykes Mbuwane alikuja Germany Ostafrika akiwa na ndugu yake anaitwa Ali Katini.

Ally Sykes jina lake linatokana na Ali Katini ndugu wa babu yake.

Schneider jina lake ni Abdillah, Kleist jina lake Abdallah.

Schneider hakuzaliwa Tanganyika kaja mkubwa.

Mashado Plantan kaja pia mkubwa jina lake Ramadhani.

Wote hawa walizaliwa ndani ya kambi ya jeshi la Wajerumani na wao ndiyo wakifanya tasjila ya watoto na wakiwapa majina ya Kijerumani.

Lakini wazazi wao wakiwapa majina ya Kiislam.

Hawa wote wakizungumza Kijerumani.
 
Hakika, ukizingatia na majina yao. Plantan, Shneider, Sykes, Kleist...
Gagnija,
Hayo nimeeleza katika kitabu cha Abdul Sykes.

Hawa Wazulu waliotoka Kwa Likunyi Imhambane, Mozambique walikuwapo Waislamu miongoni mwao.

Sykes Mbuwane alikuja Germany Ostafrika akiwa na ndugu yake anaitwa Ali Katini.

Ally Sykes jina lake linatokana na Ali Katini ndugu wa babu yake.

Schneider jina lake ni Abdillah, Kleist jina lake Abdallah.

Schneider hakuzaliwa Tanganyika kaja mkubwa.

Mashado Plantan kaja pia mkubwa jina lake Ramadhani.

Wote hawa walizaliwa ndani ya kambi ya jeshi la Wajerumani na wao ndiyo wakifanya tasjila ya watoto na wakiwapa majina ya Kijerumani.

Lakini wazazi wao wakiwapa majina ya Kiislam.

Hawa wote wakizungumza Kijerumani.
 
Kama hakuchanja lakini alipata cheti cha kuthibitisha kuwa amechanja basi kazi hiyo ilikuwa ya kupata cheti cha magumashi! Na biashara ya vyeti hivi waliendelea nayo hata baada ya uhuru.

Amandla...
Fundi...
Unajua mimi nataabika mjadala unapokosa adabu.

Nakusihi ndugu yangu.



N
 
Mkuu, hauna link ya huo uzi?
Natumia browser mkuu nashindwa kupandisha link hapa kama unatumia Jamiiforums App ingia kwenye profile yake tafuta ktk post alizozianzisha utaukuta.

Una replys karibia 700 tuliijadili sana hapa.
 
Nimetumia

Swali lilikuwa ni nani alilipia tiketi ya Mwalimu na sio suala la "vaccination". Ila hata hapo sijui Mwalimu aliwezaje kuingia Marekani bila kuthibitisha kuwa amechanjwa. Labda useme alipewa cheti cha kufoji. Tiketi ililipiwa kwa kiasi kikubwa na John Rupia. Hilo linakuwia ugumu kulikiri.
Nimesema unatuonaje kutokana na namna unavyoleta hicho unachoita ushahidi. Kwanza ulibandika picha ya wakina mama wa kiislamu kuthibitisha kuwa ni wao ndio waliomsindikiza airport. Sasa umeongeza nyingine ikionyesha kuwa wakina Robert na John nao walikuwapo! Na wote tunajua kuwa mara nyingi wanaopiga picha ni wachache katika kundi kubwa linalomsindiliza mtu wao. Utaona uliowataja ni saba tu wakati kwenye hiyo picha wako wengi zaidi ya hao. Kwa sababu hiyo kutumia hizi picha kama ushahidi kuwa ni waislamu peke yao ndio waliochangia ukuaji wa TANU ni kutaka kutupotosha.

Hauwezi kumfuta mtu kama Rupia kwa sababu tu jina lake ni John na ukawakuza wakina Iddi na Chiku juu yake. Hiyo sio sahihi. Hauwezi kutenda haki kama lengo lako ni kuwaenzi waislamu wenzako tu. Utakuwa hauna tofauti na wale unaodai hawakutaka kutambua mchango wa wakina Abdul katika mafanikio ya Julius.

Amandla...
Fundi...
Hakuna tatizo sote mimi na wewe tunachangia katika historia hii.

Tuwaachie wasomaji wasome.

Ndani ya kitabu cha Abdul Sykes nimeandika jinsi Iddi Faiz Mafungo Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na TANU alivyokusanya fedha za safari ya UNO.

Kuna fedha pia zilitolewa katika hazina ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na fedha za "mkopo" kutoka Dar-es-Salaam Municipal Council.

Hiki ni kisa cha kipekee cha Ali Rashid Meli aliyekuwa Bwana Fedha wa Dar es Salaam Municipal Council.
 
Kolola,
Kipande muhimu kimerukwa kukosa kutaja kuwa Mwalimu alikaa kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley.

Akiwa hapo Mama Maria akafungua duka la mafuta ya taa Mtaa wa Mchikichi.

Haikuelezwa kuwa walipohamia Magomeni Maduka Sita Mama Maria akapewa nafasi ya kuweka duka lake la mafuta nyumbani kwa Ali Msham.

Hii ni historia ya wazee wangu na ni jukumu langu kuhakikisha kuwa inahifadhiwa sawasawa.
Waandishi wa hizi historia wengi na ni tofauti,mada zako nyingi zinazungumzia kupondisha historia.

Anaepindisha ni nani hasa,je ni makusudi au kutokua historia vizuri?
 
Fundi...
Unajua mimi nataabika mjadala unapokosa adabu.

Nakusihi ndugu yangu.



N
Tatizo ukiona umezidiwa hoja unakimbilia mambo ya adabu. Nimemsoma fundi mchundo sijaona adabu aliyokukosea. Mzee wetu siku moja weka wazi kwamba unapigania dini yako na wazee wako wa Kariakoo badala ya kujificha kwenye historia Nyerere huku ukipotosha mambo mengi.
 
Champ...
Tuchunge lugha na heshima zetu tufanye mjadala wa kupendeza.

Iko siku miaka mingi sisi hatupo watakaokuja kutusoma waseme, "Hakika walipita watu."

Hii si taarifa ya mimi kupewa.

Mimi nimeishi nyakati hizo lau nilikuwa mtoto, baba na babu yangu wameishi nyakati hizo na nimewadiriki wengi ninaowataja hapa.

Wengine nimejuananao kwa karibu sana.

Kitabu cha Abdul Sykes hakina mfano wake katika vitabu vilivyoandikwa kuhusu TANU na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kamsome Listowel (1963) Kimambo na Temu (1969), Uloto (1971), Kivukoni (1981) na Shivji at al (2020) utaona tofauti.

Ndugu yangu si kama najisifu nataka nikuzindue utoke ujingani.

Unatuambia Waislamu twende shule wewe una elimu ya kutosha kufanya mjadala wa mada hiyo?

Ushamsoma Ishumi? (sikumbuki mwaka).

Fungua uzi nitakuja kutoa darsa.

Nisome kwa utulivu na njoo kwangu kwa mjadala kwa adabu na heshima.

Mjadala huu si mahali pa lugha "longolongo."

Hapa nipo kwa kuamini pana heshima.
Mzee Mohamed Said ulikuwa na miaka 10 mwaka 1962. Kila kitu unachoandika ni kwa kusimuliwa. Katika muktadha huo wewe sio source ya kuaminika kwasababu kwanza uko biased kwenye dini yako lakini pili maelezo yako asilimia kubwa umeyatoa kwa waislamu wenzio ambao mwalimu aliwaweka kando kwasababu walikuwa weupe kichwani.

Kila mahali hutaki kutambua kwamba John Rupia alikuwa na mchango mkubwa sana unalazimisha masimulizi ya Sykes ndio yawe standard. Mimi namuona Sykes ni mtu mwenye wivu baada ya kuwekwa pembeni na mwalimu wakati anaijenga nchi.

Nyerere alifanya akili sana kuwakataa hao wazee wa kiislamu maana nia yao ilikuwa kuleta utawala wa dola ya kiislamu. Kinachowauma nyie ni kwamba mlimpa misaada Nyerere lakini yeye akaamua kuweka utaifa mbele badala ya maslahi yenu ya kidini. Pole sana maana ishatoka hiyo na historia inatambua mwalimu ndiye aliongoza kupigania uhuru mwanzo mwisho.

Wekezeni katika elimu acheni hii ajenda yenu ya kuzaliana muwe wengi mkiamini mtaitawala Tanzania. Hilo sahauni. Juzi hapa watoto wenu mliowazaa bila mpangilio wameuwawa kama panya road huko temeke. Narudia tena jikiteni kwenye elimu ili tujenge taifa lenye maendeleo.
 
Tatizo ukiona umezidiwa hoja unakimbilia mambo ya adabu. Nimemsoma fundi mchundo sijaona adabu aliyokukosea. Mzee wetu siku moja weka wazi kwamba unapigania dini yako na wazee wako wa Kariakoo badala ya kujificha kwenye historia Nyerere huku ukipotosha mambo mengi.
Mama...
Nizidiwe.

Nizidiwe nini na nani na anizidi kwa yeye kuandika nini katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika?

Fanya utafiti tufahamiane.

Haya ya adabu yanategemea malezi.

Baadhi yetu tunazaliwa mama zetu wanatufunza adabu ya kula ya kuamkia nk.

Tunapelekwa kumbi na chuoni tunafunzwa adabu.
Adabu inakuwa sehemu ya maisha yetu.

Ikiwa huwezi kutofautisha samahani kwa neno hili ''ushenzi,'' uungwana siwezi kukulaumu kwani huenda hukuleleka.

Nadhani umepata kusikia wanafunzi wanawapiga walimu wao.

Wengi wanauliza nini kimetokea katika jamii yetu?

Kuwa napigania dini sawa siwezi kubadili uaminicho sana nitakuuliza kwani ni vibaya kupigania dini yako iwapo pana dhulma?

Kuhusu kupotosha hii ni fursa yako na wewe kuandika historia ambayo haikupotoshwa.

Kitabu kimetimiza miaka 25 na kinakimbilia chapa ya 5 hakijapatikana kitabu kupinga kitabu cha Abdul Sykes.

1672851252921.jpeg
1672851292779.jpeg
1672851340759.jpeg
 
Waandishi wa hizi historia wengi na ni tofauti,mada zako nyingi zinazungumzia kupondisha historia.

Anaepindisha ni nani hasa,je ni makusudi au kutokua historia vizuri?
Zeusi,
Mjadala sasa upo zaidi ya miaka 10.
Ingia hapa fanya search: mohamedsaidsalum.blogspot.com
 
Back
Top Bottom