Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Mohammed, ninarudia pale pale kwa sababu siku zote mada yako, ushahidi wako ni ule ule. Ni hadithi zile zile, picha zile zile. Nasema siku zote kuwa kitabu chako ni historia ya Abdulwahid Sykes na sio historia ya Tanganyika au TANU. Kuna wakati ulitaka kumfunika Kassanga Tumbo na kumuinua babu yako tukakusahihisha.
Unasema kuwa John Rupia yumo katika kitabu chako lakini hapa unapata kigugumizi kukiri kuwa alikuwa mfadhili mkubwa TANU na ndie aliyelipia sehemu kubwa ya gharama ya safari ya Nyerere kwenda UN 1955. Unasema umemtaja lakini unashindwa kusema ndie aliyelipa fine ya shilingi 3000 aliyotozwa Nyerere katika kesi yake ya 1958. Hauwezi kuwatendea haki watu kama Solomon Eliufoo kwa kuwapachika ndani ya mswada wako unaomzungumzia Ally Kleist Sykes wakati yeye alikuwa mshauri mkubwa wa Julius Nyerere. Mimi sijui kama umemzungumzia Joan Wickens aliyekuwa anaenda kwa baiskeli Ikulu kila siku kutoka kwenye makazi yake Salvation Army.
Mimi siku utakapojitoa katika mipaka uliyokiwekea ndio nitakusoma. Siku utaweza kuwachambua wakina Sykes na waislamu kama unavyomchambua Julius Nyerere na wakristu.

Amandla....
Fundi...
Utanisoma kila siku na utaona haya haya kwa kuwa historia haibadiliki ni ile ile na kila siku napata wanafunzi wapya na narejea somo lile lile na picha zile zile.

Mwaka wa 25 toka kitabu cha Abdul Sykes kichapwe na kila siku kiko midomoni mwa watu.

Kitabu cha Ulotu na Kivukoni chapa mara moja vyote vimekufa.

Ushapata hata kusikia mtu anaviuliza?

Kitabu changu bado kinaishi na kila uchao nahojiwa na FM Stations na TV Stations kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika.

Nimesimama Northwestern University, Evanston, Chicago Illinois na nimezungumza vipi kitabu changu kilivyobadili historia iliyokuwapo na kuweka historia mpya.

Leo mnaisoma upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika na mnaisoma upya historia ya Julius Nyerere.

Zilipoanza kejeli baada ya uhuru kuhusu TAA kuitwa ati "chama cha starehe," Ahmed Rashaad Ali akiumia roho yake na akimtaka Abdul ajibu kejeli zile.

Abdul alikataa na hakufungua kinywa chake akabakia kimya hadi anaingia kaburini mwaka wa 1968.

Katika kifo chake magazeti ya TANU Uhuru na Nationalist hawakuchapa hata taazia.

Taazia iliandikwa na kuchapwa na Brendon Grimshow Mhariri wa Tanganyika Standard.

Katika sherehe za miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika Abdul Sykes na mdogo wake Ally wakapewa Medali ya Mwenge wa Uhuru na Rais Kikwete kwa mchango wao katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Huu ndiyo mwaka ambao baba yao Kleist Sykes maisha yake yaliyotokea katika Dictionary of African Biography (DAB).

Kleist Sykes mwanae Abdul Sykes ndugu na rafiki yangu toka udogoni alifunga safari akaja Tanga kunishukuru.

Kleist akiamini kuwa ni kitabu nilichoandika ndicho kilichosababisha baba zake watambulike.

Kleist alilia machozi kama mtoto mdogo.

Kwetu sisi huu ni ushindi mkubwa.

Mwenyezi Mungu amesema yeye kajiharamishia dhulma.

Kitabu cha Abdul Sykes na yake mengi aliyofanya kupigania uhuru wa Tanganyika ndiyo haya maneno yale yale na picha zile zile zinajirudia kila siku na watu hawachoki kunisikiliza na kunisoma.

Tazama mnavyojazana hapa.
Kitu gani kinawaleteni kwangu?

Kila mnapokuja na maswali hata kama ni ya kejeli najibu.
Niko katika shinikizo kubwa kuwa niandike maisha yangu.

Alhamdulilah Rabilalamin.

1672889842515.png

Tanganyika Standard (Sunday News) 20 October 1968

1672889967573.jpeg

Kulia wa kwanza Mohamed Said na wa tatu ni Kleist Sykes picha hii tulipiga miezi michache baada ya kifo cha Abdul Sykes

1672890140064.jpeg

Kushoto ni Kleist Sykes, Miski Sykes, Mohamed Said nimeshika Medali ya Mwenge wa Uhuru ya Abdul Sykes, Aisha ''Daisy'' Sykes na Ilyaas Sykes picha hii tulipiga nuyumbani kwa Kleist 2017

 
Mohammed, ninarudia pale pale kwa sababu siku zote mada yako, ushahidi wako ni ule ule. Ni hadithi zile zile, picha zile zile. Nasema siku zote kuwa kitabu chako ni historia ya Abdulwahid Sykes na sio historia ya Tanganyika au TANU. Kuna wakati ulitaka kumfunika Kassanga Tumbo na kumuinua babu yako tukakusahihisha.
Unasema kuwa John Rupia yumo katika kitabu chako lakini hapa unapata kigugumizi kukiri kuwa alikuwa mfadhili mkubwa TANU na ndie aliyelipia sehemu kubwa ya gharama ya safari ya Nyerere kwenda UN 1955. Unasema umemtaja lakini unashindwa kusema ndie aliyelipa fine ya shilingi 3000 aliyotozwa Nyerere katika kesi yake ya 1958. Hauwezi kuwatendea haki watu kama Solomon Eliufoo kwa kuwapachika ndani ya mswada wako unaomzungumzia Ally Kleist Sykes wakati yeye alikuwa mshauri mkubwa wa Julius Nyerere. Mimi sijui kama umemzungumzia Joan Wickens aliyekuwa anaenda kwa baiskeli Ikulu kila siku kutoka kwenye makazi yake Salvation Army.
Mimi siku utakapojitoa katika mipaka uliyokiwekea ndio nitakusoma. Siku utaweza kuwachambua wakina Sykes na waislamu kama unavyomchambua Julius Nyerere na wakristu.

Amandla....
Fundi...
Utanisoma kila siku na utaona haya haya kwa kuwa historia haibadiliki ni ile ile na kila siku napata wanafunzi wapya na narejea somo lile lile na picha zile zile.

Mwaka wa 25 toka kitabu cha Abdul Sykes kichapwe na kila siku kiko midomoni mwa watu.

Kitabu cha Ulotu na Kivukoni chapa mara moja vyote vimekufa.

Ushapata hata kusikia mtu anaviuliza?

Kitabu changu bado kinaishi na kila uchao nahojiwa na FM Stations na TV Stations kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika.

Nimesimama Northwestern University, Evanston, Chicago Illinois na nimezungumza vipi kitabu changu kilivyobadili historia iliyokuwapo na kuweka historia mpya.

Leo mnaisoma upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika na mnaisoma upya historia ya Julius Nyerere.

Zilipoanza kejeli baada ya uhuru kuhusu TAA kuitwa ati "chama cha starehe," Ahmed Rashaad Ali akiumia roho yake na akimtaka Abdul ajibu kejeli zile.

Abdul alikataa na hakufungua kinywa chake akabakia kimya hadi anaingia kaburini mwaka wa 1968.

Katika kifo chake magazeti ya TANU Uhuru na Nationalist hawakuchapa hata taazia.

Taazia iliandikwa na kuchapwa na Brendon Grimshow Mhariri wa Tanganyika Standard.

Katika sherehe za miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika Abdul Sykes na mdogo wake Ally wakapewa Medali ya Mwenge wa Uhuru na Rais Kikwete kwa mchango wao katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Huu ndiyo mwaka ambao baba yao Kleist Sykes maisha yake yaliyotokea katika Dictionary of African Biography (DAB).

Kleist Sykes mwanae Abdul Sykes ndugu na rafiki yangu toka udogoni alifunga safari akaja Tanga kunishukuru.

Kleist akiamini kuwa ni kitabu nilichoandika ndicho kilichosababisha baba zake watambulike.

Kleist alilia machozi kama mtoto mdogo.

Kwetu sisi huu ni ushindi mkubwa.

Mwenyezi Mungu amesema yeye kajiharamishia dhulma.

Kitabu cha Abdul Sykes na yake mengi aliyofanya kupigania uhuru wa Tanganyika ndiyo haya maneno yale yale na picha zile zile zinajirudia kila siku na watu hawachoki kunisikiliza na kunisoma.

Tazama mnavyojazana hapa.
Kitu gani kinawaleteni kwangu?

Kila mnapokuja na maswali hata kama ni ya kejeli najibu.
Niko katika shinikizo kubwa kuwa niandike maisha yangu.

Alhamdulilah Rabilalamin.
 
Mohammed, ninarudia pale pale kwa sababu siku zote mada yako, ushahidi wako ni ule ule. Ni hadithi zile zile, picha zile zile. Nasema siku zote kuwa kitabu chako ni historia ya Abdulwahid Sykes na sio historia ya Tanganyika au TANU. Kuna wakati ulitaka kumfunika Kassanga Tumbo na kumuinua babu yako tukakusahihisha.
Unasema kuwa John Rupia yumo katika kitabu chako lakini hapa unapata kigugumizi kukiri kuwa alikuwa mfadhili mkubwa TANU na ndie aliyelipia sehemu kubwa ya gharama ya safari ya Nyerere kwenda UN 1955. Unasema umemtaja lakini unashindwa kusema ndie aliyelipa fine ya shilingi 3000 aliyotozwa Nyerere katika kesi yake ya 1958. Hauwezi kuwatendea haki watu kama Solomon Eliufoo kwa kuwapachika ndani ya mswada wako unaomzungumzia Ally Kleist Sykes wakati yeye alikuwa mshauri mkubwa wa Julius Nyerere. Mimi sijui kama umemzungumzia Joan Wickens aliyekuwa anaenda kwa baiskeli Ikulu kila siku kutoka kwenye makazi yake Salvation Army.
Mimi siku utakapojitoa katika mipaka uliyokiwekea ndio nitakusoma. Siku utaweza kuwachambua wakina Sykes na waislamu kama unavyomchambua Julius Nyerere na wakristu.

Amandla....

Fundi...
Rashidi Mfaume Kawawa uliyotaka kumsoma kutoka kwangu.

Utamsoma pia babu yangu Salum Abdallah na Kassanga Tumbo katika harakati za vyama vya wafanyakazi.

RASHIDI MFAUME KAWAWA SIMBA WA VITA

RASHIDI+KAWAWA+BOOK+COVER.jpg

Kwa mara ya kwanza Tanzania ilishuhudia kuandikwa kwa historia ya mmoja wa viongozi wakuu wake kupitia kitabu “Simba wa Vita Katika Historia ya Tanzania Rashidi Mfaume Kawawa” kilichoandikwa na Dk. John M. J. Magotti. Sidhani kama katika historia ya Tanzania kuna kumbukumbu ya kuandikwa kwa kitabu kinachohusu maisha ya kingozi yoyote achilia mbali kufanyika kwa sherehe ya kukizindua kitabu hicho Ikulu ikiongozwa na rais mwenyewe. Kwa hakika sherehe ilifana sana na tukakisubiri kwa hamu kitabu madukani ili tupate kunufaika na kumbukumbu za Mzee Kawawa.

Msomaji anaweza kukisoma kitabu chote chenye kurasa 127 kwa muda wa saa moja akawa kakimaliza chote na atakapokiweka chini akawa hakubakia na chochote cha maana katika fikra yake. Kwa nini iwe msomaji asibaki na kumbukumbu yoyote ya kiongozi mkubwa kama Mzee Kawawa mtu aliyeshuhudia kwa macho yake mwenyewe harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na si hivyo tu yeye mwenyewe ni mmoja wa wale waliopigania uhuru wa Tanganyika na kushika nyadhifa kubwa za uongozi chini ya Mwalimu Julius Nyerere. Kwa kawaida vitabu vya maisha ya viongozi hasa wapigania uhuru huwa vina mambo mengi sana ambayo kwa muda mrefu huwa siri, hayafahamiki hadi hapo kitabu kitakapoandikwa ama kwa mkono wake kiongozi mwenyewe au kuandikwa na muandishi. Mifano ipo mingi. Kitabu kama “Mahatma Gandhi” klichoandikwa na Robert Payne au “Long Walk to Freedom” alichoandika Nelson Mandela mwenyewe au “Seeds of Freedom” alichoandika Bildad Kaggia hakika unapomaliza kusoma vitabu hivi lazima urudi nyuma kufungua kurasa hapa na pale kuzisoma upya zile sehemu zinasosisimua.

Huwezi kupata haya katika kitabu cha Mzee Kawawa. Huwezi kuyapata haya kwa kuwa mwandishi hakuandika kitu. Hakuandika kitu si kama Mzee Kawawa hana historia ya kusisimua na kuwa hana mengi ambayo wengi hawayajui katika maisha yake, nadhani mwandishi hakuwezakuja na jipya labda kwa sababu hakufanya utafiti wa kutosha kuweza kuandika kitabu kinachomuhusu simba wa vita aneunguruma. Kuna msemo wa Kiswahili usemao “Aungurumapo simba mcheza ni nani?” Kwa hakika simba wa vita hakuunguruma kabisa katika kitabu hiki. Sijui lawama zielekezwe wapi.

Mimi simjui Mzee Rashidi Kawawa kwa kiwango cha kusema naweza kunyanyua kalamu na kufanya pitio la kitabu kilichoandikwa kuhusu yeye. Nathubutu kuandika kuhusu kitabu chake kutokana na kumjua kwangu mimi nikiwa kama mwandishi na mtafiti ambae katika kutafiti kwangu nimekutana na jina la Mzee Kawawa hapa na pale katika nyaraka zilizo katika hifadhi ya ukoo wa akina Sykes. Nitatumia uzoefu wangu huu kueleza yale niliyoyaona katika nyaraka hizi na ninayojua kuhusu Mzee Kawawa na kufanya tathmini kwa yale niliyoyasoma katika kitabu cha Magotti.

Miaka kama ishirini iliyopita nikiwa kijana mdogo nilipata hamu ya kuandika historia ya kudai uhuru wa Tanganyika. Sikuona mtu wa kumuendea isipokuwa Ally Sykes. Nilipomueleza kuwa nia yangu ni kuandika kitabu kuhusu marehemu kaka yake Abdulwahid Sykes (1924- 1968) Ally Sykes alinambia kuwa atanipa nyaraka zake zote nizipitie kisha ndiyo nakaenae chini kwa mahojiano ya ana kwa ana. Katika nyaraka alizonikabidhi ndani yake nilikuta barua ya mkono aliyoandika Rashid Kawawa mwaka 1952 kutoka Bukoba akimletea Ally Sykes aliekuwa Dar es Salaam. Barua hii ya Mzee Kawawa kwa Ally Sykes ilikuwa ikimfahamisha Ally Sykes hali ya siasa Kanda ya Ziwa. Hii barua hadi leo ipo katika nyaraka za akina Sykes. Nilipokaa na Ally Sykes kutaka maelezo ya barua ile aliyoandikiwa na Kawawa, Ally Sykes alinipa kisa hiki:

''Mwaka 1951 nilichaguliwa kuwa katibu mkuu wa Tanganyika African Government Servants Association (TAGSA). Chama hiki kiliundwa mwaka wa 1927 kwa lengo la kuendeleza maelewano mazuri baina ya serikali ya Malkia na sisi watumishi Waafrika. Rashid Kawawa alikuwa mwana kamati. Mimi nilichaguliwa pamoja na Thomas Marealle kama rais wa TAGSA. Katiba ya TAGSA iliamuru uchaguzi wa kila mwaka, na mimin nilirudishwa madarakani kama katibu mara nne hadi Oktoba, 1954 nilipojiuzulu baada ya kuhamishwa kwenda Korogwe kamaadhabu kwa kuwa miongoni mwa wale wanachama 17 waliounda TANU.

Watu kadhaa walishika urais. Stephen Mhando na Dr Wilbard Mwanjisi wote hao waliwahi kuchaguliwa kuwa marais wa TAGSA. Miongoni mwa wanachama watendaji wa TAGSA walikuwa Dr Michael Lugazia na Rashid Kawawa ambao alichaguliwa kuwa katibu baada ya mimi kujiuzulu. Kupitia TAGSA, Kawawa alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Tanganyika Federation of Labour (TFL).

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa ulipokuja kuzuru Tanganyika Agosti, 1951 kwa mara ya tatu, vyama vyote viwili, TAA na TAGSA, viliwakilisha malalamiko kwa ujumbe huo. TAGSA iliwakilisha malalamiko yake kuhusu ubaguzi katika utumishi serikalini kwa mujibu wa kupanga mishahara kufuatana na rangi ya ngozi. Mshahara wa Mwafrika ulikuwa wa chini zaidi kuliko ule aliokuwa akipokea Mzungu au Muasia kwa kazi hiyo hiyo.

Kwa mfano Mwandishi wa hati mkato Mzungu alikuwa akipata mshahara mkubwa kuliko Mwafrika aliyekuwa na shahada au digrii kutoka chuo Kikuu cha Makerere. TAGSA vilevile tulilalamika kuhusu kuajiri makarani wa kutoka India na hali walikuwepo Waafrika kutoka Afrika ya Mashariki na Nyasaland ambao wangeweza kujaza nafasi hizo kwa urahisi.

Vyama vyetu hivi viwili TAA na TAGSA viliwakilisha malalamiko haya tukifahamu fika kwamba Uingereza ilikuwa ikiitawala Tanganyikachini ya vifungu nambari 76 na 77 vya Umoja wa Mataifa ambavyo viliwekwa ili kuendeleza maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ya nchi zilizokuwa chini ya udhamini. Kama mdhamini Uingereza ilitakiwa kuhimiza na kuheshimu haki za binadamu na uhuru wa kwa wote bila kubagua kwa misingi yajinsia, lugha au dini. Lakini Uingereza ilikuwa ikipuuza vifungu hivi bila aibu. TAGSA tuliwakilisha malalamiko haya ili Umoja wa Mataifa ujue matatizo halisi ya ukoloni nchini Tanganyika.

Mimi nikiwa katibu wa TAGSA nilifuatilia serikalini masuala yaliyoainishwa ndani ya malalamiko yetu. Suala lililokuwa likituhangaisha sanawakati ule ilikuwa uajiri wa Wahindi kutoka India, jambo ambalo niliieleza serikali halikuwa na faida, maadam kulikuwako na Waafrika ndani ya nchi ambao wangeweza kujaza nafasi zile. Jambo hili lilikuwa likisababisha manugíuniko makubwa miongoni mwa Waafrika. Hakuna majibu maridhawa yaliyopatikana kutoka kwa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa.

Barua tulizoandika serikalini juu ya masuala hayo zilipuzwa na Chief Secretary, Bruce Hutt. Katika kufuatilia malalamiko haya, Niliandika barua moja kali sana na kwa mara ya kwanza bila kutafuna maneno niliuliza uhalali wa Waingereza kututawala Waafrika wa Tanganyika. Nillimwambia Katibu Mkuu kuwa kwa kuwa serikali imeshindwa kupata ufumbuzi kwa matatizo ya Waafrika, Uingereza lazima ijitoe Tanganyikana Umoja wa Mataifa utawale Tanganyika.

Barua hiyo ilimkasirisha Katibu Mkuu na siku chache baadaye nilipokea barua kutoka serikalini iliyokuwa imejaa vitisho, dharau, stihizai na makemeo. Nikajibiwa kuwa hakuwa na suala la Umoja wa Mataifa kutekeleza utawala wa moja kwa moja Tanganyika.''

Dkt Mwanjisi alikuwa amegusa suala nyeti sanakwa kuzungumzia matatizo ya ubaguzi wa rangi uliokuwa ukitukabili Waafrika wa . Kawawa, kama mjumbe wa kamati, akaniandikia barua akanitahadharisha nisichapishe ile hotuba ya Dkt Mwanjisi katika jarida la TAGSA bila idhini ya kamati ya utendaji. Kufuatia majibishano haya kati ya TAGSA na serikali, Dkt Mwanjisi kama alivyofanyiwa Dk Kyaruzi kabla yake, akahamishwa kutoka hospitali ya Sewa Haji mjini Dar es Salaamhadi Kingolwira Prison Hospitalkaribu na Morogoro. Kawawa na yeye akapewa uhamisho kwenda Bukoba na mimi nikapewa uhamisho kwenda Mtwara.

Dk Mwanjisi na Kawawa walikubali uhamisho wao na wakaondoka Dar es Salaam. Mimi nilikataa uhamisho na nikabakia Dar es Salaam kupinga uhamisho wangu.

Alipokuwa Bukoba ndipo Kawawa akamwandikia Ally Sykes barua ile ya mwaka 1952 akimweleza hali ya siasa kamaalivyoikuta Kanda ya Ziwa. Huyu ndiye Kawawa niliyemjua mimi kupitia nyaraka na mahojiano na Ally Sykes. Kwa kweli inasikitisha kuwa Dk Magotti hakupata fursa ya kuziangalia nyaraka hizi muhimu sana katika siyo historia ya Kawawa bali katika historia ya kuundwa kwa TANU na kudai uhuru wa Tanganyika. Endapo angepata nafasi ya kuziona hizi nyaraka zingempelekea katika kuwajua wazalendo wengine waliotajwa mle ndani kama Dk. Kyaruzi, Dk. Wilbard Mwanjisi ambao Kawawa alikuwanao katika harakati za TAGSA. Katika majina hayo angeweza kudodosa mengi kutoka kwa Mzee Kawawa na hivyo kuandika yale ambayo hayafahamiki kwa wengi. Hii imgekifanya kitabu kiwe cha maana.

Mathalan Kawawa angeeleza mtafaruku kati ya Mwalimu Nyerere na Dk. Mwanjisi nini chanzo chake na nini ikajakuwa matokeo yake. Halikadhalika angempa fursa Mzee Kawawa kumuhadithia mchango wa Dk. Michael Lugazia katika kuasisi kwa TANU hasa kipindi kile cha 1953 wakati TAA ilipokuwa inatayarisha rasimu ya katiba ya TANU. Kwa ufupi ni kuwa Dk Lugazi alikuwa akijaribu kuamsha ari ya TAA Bukoba ari iliyokufa kutokana na kufungwa kwa kiongozi wa TAA Bukoba Ali Migeyo.

Kisa cha Ali Migeyo ni moja ya visa vinavyosikitisha sana katika historia ya Tanganyika kwani aliwekwa kizuizini na Mwalimu Nyerere kama alivyofungwa na Waingereza. Haiwezekani kuwa Kawawa asiwe na habari na kile kilichopelekea mpigania uhuru hodari kama Ali Migeyo aishie jela tena wakati nchi ikiwa huru. Migeyo alifungwa na wakoloni kwa kuwahamasisha Watanganyika kudai uhuru labda Mzee Kawawa angeulizwa angeeleza ni nini kilitokea wakaamua kumfunga Migeyo kama walivyomfunga Waingereza.

Kitabu kimegusia kazi alofanya Kawawa kama mtumishi wa serikali ya kikoloni katika kambi za raia wa Kenyawalioshukukiwa kuwa ni Mau Mau. Katika hawa wafungwa walikuwawepo wananchama wa TANU ingawa hawa walikuwa Wakenya. Maarufu katika hawa alikuwa Dome Okochi Budohi (ambae kadi yake ya TANU ilikuwa na 6) na Patrick Aoko. Budohi alicheza senema pamoja na Kawawa iliyoitwa “Wageni Wema.”

Kawawa na Budohi walikuwa wakifahamiana vizuri sana kwa sababu wote walikuwa wasanii. Budohi alikuwa mmojawapo katika bendi ya vijana wa mjini iliyojulikana kama Skylarks. Bendi hii baadaye ilibadilisha jina na kuitwa Blackbirds. Matangazo ya radio yalipoanza Tanganyika, Blackbirds midundo ya Blackbirds ilikuwa haikosekani kusikika radioni katika Sauti ya Dar es Salaam. Kawawa kama walivyo vijama wote wa Dar es Salaam wa wakati ule alikuwa mmmoja wa wapenzi wa bendi hii na alikuwa hakosekani Ukumbi wa Arnatouglo bendi hii ikitumbuiza katika ile miaka ya 1950. Ilikuwa katika ule upigaji muziki wa Budohi ndipo alipoungana na Kawawa katika kutengenezwa kwa senama hiyo ya “Wageni Wema” ambayo mwandishi kaitaja lakini aliishia hapo tu.

Budohi na Aoko ni kati ya wafungwa wa Mau Mau waliokuwa Handeni ambako Kawawa alikuwa na jukumu la kuwaangalia. Budohi ndiyo alikuwa mtu wa kati baina ya TAA na KAU na kuanzia hali ya hatari ilipotangazwa Kenya mwaka 1952 Budohi na Aoko wakawa katika jicho kali la makachero. Makachero hawa Waafrika wanafahamika na wengine walikuja kufanya kazi hiyohiyo katika Tanganyikahuru.

Hiki ndicho kipindi ambacho Kaimu Rais wa TAA na Katibu wa TAA Abdulwahid Sykes alipokutana na Kenyatta Nairobi. Wakati Wakenya hawa wanafungwa Tanganyika, viongozi wa KAU akina Bildad Kaggia, Jomo Kenyatta, Kun’gu Karumba, Achieng Oneko, Paul Ngei na Fred Kubai walikuwa wamekamatwa Kenya. Kawawa ni mmoja kati ya viongozi hawa na ingependeza sana kama kupitia kwake tungeelezwa jinsi KAU na TAA ilivyokuwa ikishirikiana kwani haiwezekani kuwa Budohi na Kawawa uswahiba wao ukaishia kwenye kucheza senema tu.

Wanaharakati wote walishtushwa na kutiwa mbaroni kwa Budohi na Aoko. Haiwezekani kuwa iwe Mzee Kawawa kasahau matukio haya muhimu. Budohi na Aoko walikuwa wamefungwa minyororo walipokuwa katika selo pale Kituo cha Kati cha Polisi kwa sasa jumba hiloliko kituo cha mabasi kinachojulikana kama“station.” Waliwekwa pale kwa miezi sita muda wote wakiwa na minyororo miguuni.

Waliwekwa pale kwa miezi sita wakihojiwa kabla hawajapelekwa Handeni walipomkuta Kawawa. Hivi ndivyo vitu ambavyo kwa hakika vingeongeza ladha ya kitabu cha Mzee Kawawa endapo mwandishi angechukua muda kutafiti na kuzungumza na watu waliokuwa katika harakati wakati ule ambao bado wa hai kama Ally Sykes na mdogo wake Balozi Abbas Sykes na wengine wengi ambao walikuwepo wakati ule kama Mzee Chipaka.

Katika migomo ya wakati wa kudai uhuru hakuna mgomo uliofanikiwa na kuvuta hisia za wananchi kamamgomo wa reli wa mwaka 1960 uliodumu kwa siku 62. Ukiachia kutajwa tu kama sehemu ya historia undani wake na jinsi mipango yake ilivyokwenda na nafasi ya viongozi wa Tanganyika Railway African Union (TRAU) walivyopata misaada kutoka nchi za Mashariki hivi havijawekwa wazi. Si treni, meli wala mabasi ya railway yaliyotembea kwa mieizi mitatu.

Mipango ya mgomo huu ilifanyika Tabora ambako ndiko palikuwa na karakana kuu ya reli na hapo ndipo palipokuwa makao makuu ya viongozi wa TRAU, Salum Abdallah mwenyekiti na Kassanga Tumbo katibu. Kawawa ana mengi katika kadhia hii kwa kuwa yeye wakati ule ndiye alikuwa Katibu Mkuu wa TFL. Inasemekana mgomo huu miezi michache kabla Tanganyika haijapata uhuru ndiyo ilikuwa kama zinduo kwa Mwalimu Nyerere kutambua kuwa hakuwa peke yake na sauti kwa wananchi. Walikuwapo viongozi wengine pembeni yake ambao nao wakipiga wananchi wanacheza. Ilimdhihirikia kuwa huko mbeleni wanakokwenda ipo siku atapambana na viongozi hawa. Hivyo ndivyo ilivyotokea.

Inasemekana Mwalimu Nyerere akimtumia Kawawa alianza mipango kabambe ya kujitayarisha hilolisitokee. Hii ilikuwa nukta muhimu sanakwani haukupita muda baada ya uhuru kupatikana mwaka wa 1961 viongozi hawa wa vyama vya wafanyakazi wakajikuta wamewekwa kizuizini. Wasomaji wangependa kujua Kawawa alijihisi vipi wakati viongozi wenzake wa vyama vya wafanyakazi aliofanya nao kazi wakati wa kudai uhuru wakishirikiana na TANU kama Victor Mkello, Paul Pamba, Abdallah Mwamba, Hassan Khupe, Salum Abdallah na wengine wengi walipokamatwa mwaka wa 1964 na kuwekwa kizuizini kwa amri ya Mwalimu Nyerere. Maelezo ya Mzee Kawawa katika mambo haya yangetia mwanga katika yale mengi yasiyofahamika katika historia ya Tanzania.

Waislam wangependa sanakujua hisia za Kawawa kama muumini alihisi vipi wakati makachero walipomvamia mzalendo aliyepigania uhuru wa Tanganyika Mufti wa TanganyikaSheikh Hassan bin Amir usiku wa manane na kumrudisha Zanzibar na kuwekewa masharti kuwa hana ruhusa kurejea Tanzania Bara. Nilitegemea kusoma sakata zima la kukamatwa kwa Sheikh Hassan bin Amir na kuvunjwa kwa East African Muslim Welfare Society (EAMWS) jumuia ya Waislam iliyokuwa ikipanga kujenga Chuo Kikuu Dar es Salaam.

Nilitegemea halikadhalika kusoma mchango wa Mzee Kawawa katika kuunda Bakwata. Mengi yamesemwa kuhusu hujuma hii kwa Waislam moja wapo ni kuwa EAMWS ilivunjwa kwa shinikizo la Kanisa Katoliki likimtumia Mwalimu Nyerere. Hili si jambo la siri tena tafiti mbalimbali zimefanywa na vitabu kuandikwa na waandishi kutoka nje ya Tanzania kuhusu tatizo hili la kujitokeza udini mapema baada ya uhuru kupatikana. Kwa kuwa Kawawa alikuwa pamoja na Mwalimu Nyerere na alishiriki katika kuunda Bakwata wananchi hasa Waislam wangenufaika kusoma hisia zake wakati maamuzi hayo yanapitishwa na serikali. Kwa hakika kuna maamuzi mengi sana ambayo Kawawa alishiriki yaliwaumiza sana Waislam katika juhudi zao za kujitafutia elimu. Waislam wangependa sana kujua ni kipi kilikuwa kinamsukuma kufanya vile.

Kwa yeyote atakaepata bahati ya kusoma kitabu cha maisha ya Mzee Kawawa ni wazi hatakuta jipya ambalo hakuwa akilijua kabla. Kwa ajili hii basi mlango bado uko wazi kwa watafiti wengine kuandika kitabu kuhusu Rashidi Mfaume Kawawa kwani maisha ya Mzee Kawawa bado hayajaandikwa. Hata hivyo tumpongeze mwandishi kwa kazi hii kwani ni baada ya yeye kutuandikia kitabu ndipo nasi tumepata nguvu ya kunyanyua kalamu zetu na kusema.
3rd January 2010
 
RASHIDI MFAUME KAWAWA SIMBA WA VITA

RASHIDI+KAWAWA+BOOK+COVER.jpg
Kwa mara ya kwanza Tanzania ilishuhudia kuandikwa kwa historia ya mmoja wa viongozi wakuu wake kupitia kitabu “Simba wa Vita Katika Historia ya Tanzania Rashidi Mfaume Kawawa” kilichoandikwa na Dk. John M. J. Magotti. Sidhani kama katika historia ya Tanzania kuna kumbukumbu ya kuandikwa kwa kitabu kinachohusu maisha ya kingozi yoyote achilia mbali kufanyika kwa sherehe ya kukizindua kitabu hicho Ikulu ikiongozwa na rais mwenyewe. Kwa hakika sherehe ilifana sana na tukakisubiri kwa hamu kitabu madukani ili tupate kunufaika na kumbukumbu za Mzee Kawawa.

Msomaji anaweza kukisoma kitabu chote chenye kurasa 127 kwa muda wa saa moja akawa kakimaliza chote na atakapokiweka chini akawa hakubakia na chochote cha maana katika fikra yake. Kwa nini iwe msomaji asibaki na kumbukumbu yoyote ya kiongozi mkubwa kama Mzee Kawawa mtu aliyeshuhudia kwa macho yake mwenyewe harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na si hivyo tu yeye mwenyewe ni mmoja wa wale waliopigania uhuru wa Tanganyika na kushika nyadhifa kubwa za uongozi chini ya Mwalimu Julius Nyerere. Kwa kawaida vitabu vya maisha ya viongozi hasa wapigania uhuru huwa vina mambo mengi sana ambayo kwa muda mrefu huwa siri, hayafahamiki hadi hapo kitabu kitakapoandikwa ama kwa mkono wake kiongozi mwenyewe au kuandikwa na muandishi. Mifano ipo mingi. Kitabu kama “Mahatma Gandhi” klichoandikwa na Robert Payne au “Long Walk to Freedom” alichoandika Nelson Mandela mwenyewe au “Seeds of Freedom” alichoandika Bildad Kaggia hakika unapomaliza kusoma vitabu hivi lazima urudi nyuma kufungua kurasa hapa na pale kuzisoma upya zile sehemu zinasosisimua.

Huwezi kupata haya katika kitabu cha Mzee Kawawa. Huwezi kuyapata haya kwa kuwa mwandishi hakuandika kitu. Hakuandika kitu si kama Mzee Kawawa hana historia ya kusisimua na kuwa hana mengi ambayo wengi hawayajui katika maisha yake, nadhani mwandishi hakuwezakuja na jipya labda kwa sababu hakufanya utafiti wa kutosha kuweza kuandika kitabu kinachomuhusu simba wa vita aneunguruma. Kuna msemo wa Kiswahili usemao “Aungurumapo simba mcheza ni nani?” Kwa hakika simba wa vita hakuunguruma kabisa katika kitabu hiki. Sijui lawama zielekezwe wapi.

Mimi simjui Mzee Rashidi Kawawa kwa kiwango cha kusema naweza kunyanyua kalamu na kufanya pitio la kitabu kilichoandikwa kuhusu yeye. Nathubutu kuandika kuhusu kitabu chake kutokana na kumjua kwangu mimi nikiwa kama mwandishi na mtafiti ambae katika kutafiti kwangu nimekutana na jina la Mzee Kawawa hapa na pale katika nyaraka zilizo katika hifadhi ya ukoo wa akina Sykes. Nitatumia uzoefu wangu huu kueleza yale niliyoyaona katika nyaraka hizi na ninayojua kuhusu Mzee Kawawa na kufanya tathmini kwa yale niliyoyasoma katika kitabu cha Magotti.
Miaka kama ishirini iliyopita nikiwa kijana mdogo nilipata hamu ya kuandika historia ya kudai uhuru wa Tanganyika. Sikuona mtu wa kumuendea isipokuwa Ally Sykes. Nilipomueleza kuwa nia yangu ni kuandika kitabu kuhusu marehemu kaka yake Abdulwahid Sykes (1924- 1968) Ally Sykes alinambia kuwa atanipa nyaraka zake zote nizipitie kisha ndiyo nakaenae chini kwa mahojiano ya ana kwa ana. Katika nyaraka alizonikabidhi ndani yake nilikuta barua ya mkono aliyoandika Rashid Kawawa mwaka 1952 kutoka Bukoba akimletea Ally Sykes aliekuwa Dar es Salaam. Barua hii ya Mzee Kawawa kwa Ally Sykes ilikuwa ikimfahamisha Ally Sykes hali ya siasa Kanda ya Ziwa. Hii barua hadi leo ipo katika nyaraka za akina Sykes. Nilipokaa na Ally Sykes kutaka maelezo ya barua ile aliyoandikiwa na Kawawa, Ally Sykes alinipa kisa hiki:

''Mwaka 1951 nilichaguliwa kuwa katibu mkuu wa Tanganyika African Government Servants Association (TAGSA). Chama hiki kiliundwa mwaka wa 1927 kwa lengo la kuendeleza maelewano mazuri baina ya serikali ya Malkia na sisi watumishi Waafrika. Rashid Kawawa alikuwa mwana kamati. Mimi nilichaguliwa pamoja na Thomas Marealle kama rais wa TAGSA. Katiba ya TAGSA iliamuru uchaguzi wa kila mwaka, na mimin nilirudishwa madarakani kama katibu mara nne hadi Oktoba, 1954 nilipojiuzulu baada ya kuhamishwa kwenda Korogwe kamaadhabu kwa kuwa miongoni mwa wale wanachama 17 waliounda TANU. Watu kadhaa walishika urais. Stephen Mhando na Dr Wilbard Mwanjisi wote hao waliwahi kuchaguliwa kuwa marais wa TAGSA. Miongoni mwa wanachama watendaji wa TAGSA walikuwa Dr Michael Lugazia na Rashid Kawawa ambao alichaguliwa kuwa katibu baada ya mimi kujiuzulu. Kupitia TAGSA, Kawawa alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Tanganyika Federation of Labour (TFL).

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa ulipokuja kuzuru Tanganyika Agosti, 1951 kwa mara ya tatu, vyama vyote viwili, TAA na TAGSA, viliwakilisha malalamiko kwa ujumbe huo. TAGSA iliwakilisha malalamiko yake kuhusu ubaguzi katika utumishi serikalini kwa mujibu wa kupanga mishahara kufuatana na rangi ya ngozi. Mshahara wa Mwafrika ulikuwa wa chini zaidi kuliko ule aliokuwa akipokea Mzungu au Muasia kwa kazi hiyo hiyo. Kwa mfano Mwandishi wa hati mkato Mzungu alikuwa akipata mshahara mkubwa kuliko Mwafrika aliyekuwa na shahada au digrii kutoka chuo Kikuu cha Makerere. TAGSA vilevile tulilalamika kuhusu kuajiri makarani wa kutoka India na hali walikuwepo Waafrika kutoka Afrika ya Mashariki na Nyasaland ambao wangeweza kujaza nafasi hizo kwa urahisi.

Vyama vyetu hivi viwili TAA na TAGSA viliwakilisha malalamiko haya tukifahamu fika kwamba Uingereza ilikuwa ikiitawala Tanganyikachini ya vifungu nambari 76 na 77 vya Umoja wa Mataifa ambavyo viliwekwa ili kuendeleza maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ya nchi zilizokuwa chini ya udhamini. Kama mdhamini Uingereza ilitakiwa kuhimiza na kuheshimu haki za binadamu na uhuru wa kwa wote bila kubagua kwa misingi yajinsia, lugha au dini. Lakini Uingereza ilikuwa ikipuuza vifungu hivi bila aibu. TAGSA tuliwakilisha malalamiko haya ili Umoja wa Mataifa ujue matatizo halisi ya ukoloni nchini Tanganyika.

Mimi nikiwa katibu wa TAGSA nilifuatilia serikalini masuala yaliyoainishwa ndani ya malalamiko yetu. Suala lililokuwa likituhangaisha sanawakati ule ilikuwa uajiri wa Wahindi kutoka India, jambo ambalo niliieleza serikali halikuwa na faida, maadam kulikuwako na Waafrika ndani ya nchi ambao wangeweza kujaza nafasi zile. Jambo hili lilikuwa likisababisha manugíuniko makubwa miongoni mwa Waafrika. Hakuna majibu maridhawa yaliyopatikana kutoka kwa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa. Barua tulizoandika serikalini juu ya masuala hayo zilipuzwa na Chief Secretary, Bruce Hutt. Katika kufuatilia malalamiko haya, Niliandika barua moja kali sana na kwa mara ya kwanza bila kutafuna maneno niliuliza uhalali wa Waingereza kututawala Waafrika wa Tanganyika. Nillimwambia Katibu Mkuu kuwa kwa kuwa serikali imeshindwa kupata ufumbuzi kwa matatizo ya Waafrika, Uingereza lazima ijitoe Tanganyikana Umoja wa Mataifa utawale Tanganyika. Barua hiyo ilimkasirisha Katibu Mkuu na siku chache baadaye nilipokea barua kutoka serikalini iliyokuwa imejaa vitisho, dharau, stihizai na makemeo. Nikajibiwa kuwa hakuwa na suala la Umoja wa Mataifa kutekeleza utawala wa moja kwa moja Tanganyika.''

Dkt Mwanjisi alikuwa amegusa suala nyeti sanakwa kuzungumzia matatizo ya ubaguzi wa rangi uliokuwa ukitukabili Waafrika wa . Kawawa, kama mjumbe wa kamati, akaniandikia barua akanitahadharisha nisichapishe ile hotuba ya Dkt Mwanjisi katika jarida la TAGSA bila idhini ya kamati ya utendaji. Kufuatia majibishano haya kati ya TAGSA na serikali, Dkt Mwanjisi kama alivyofanyiwa Dk Kyaruzi kabla yake, akahamishwa kutoka hospitali ya Sewa Haji mjini Dar es Salaamhadi Kingolwira Prison Hospitalkaribu na Morogoro. Kawawa na yeye akapewa uhamisho kwenda Bukoba na mimi nikapewa uhamisho kwenda Mtwara.

Dk Mwanjisi na Kawawa walikubali uhamisho wao na wakaondoka Dar es Salaam. Mimi nilikataa uhamisho na nikabakia Dar es Salaam kupinga uhamisho wangu.
Alipokuwa Bukoba ndipo Kawawa akamwandikia Ally Sykes barua ile ya mwaka 1952 akimweleza hali ya siasa kamaalivyoikuta Kanda ya Ziwa. Huyu ndiye Kawawa niliyemjua mimi kupitia nyaraka na mahojiano na Ally Sykes. Kwa kweli inasikitisha kuwa Dk Magotti hakupata fursa ya kuziangalia nyaraka hizi muhimu sana katika siyo historia ya Kawawa bali katika historia ya kuundwa kwa TANU na kudai uhuru wa Tanganyika. Endapo angepata nafasi ya kuziona hizi nyaraka zingempelekea katika kuwajua wazalendo wengine waliotajwa mle ndani kama Dk. Kyaruzi, Dk. Wilbard Mwanjisi ambao Kawawa alikuwanao katika harakati za TAGSA. Katika majina hayo angeweza kudodosa mengi kutoka kwa Mzee Kawawa na hivyo kuandika yale ambayo hayafahamiki kwa wengi. Hii imgekifanya kitabu kiwe cha maana.

Mathalan Kawawa angeeleza mtafaruku kati ya Mwalimu Nyerere na Dk. Mwanjisi nini chanzo chake na nini ikajakuwa matokeo yake. Halikadhalika angempa fursa Mzee Kawawa kumuhadithia mchango wa Dk. Michael Lugazia katika kuasisi kwa TANU hasa kipindi kile cha 1953 wakati TAA ilipokuwa inatayarisha rasimu ya katiba ya TANU. Kwa ufupi ni kuwa Dk Lugazi alikuwa akijaribu kuamsha ari ya TAA Bukoba ari iliyokufa kutokana na kufungwa kwa kiongozi wa TAA Bukoba Ali Migeyo. Kisa cha Ali Migeyo ni moja ya visa vinavyosikitisha sana katika historia ya Tanganyika kwani aliwekwa kizuizini na Mwalimu Nyerere kama alivyofungwa na Waingereza. Haiwezekani kuwa Kawawa asiwe na habari na kile kilichopelekea mpigania uhuru hodari kama Ali Migeyo aishie jela tena wakati nchi ikiwa huru. Migeyo alifungwa na wakoloni kwa kuwahamasisha Watanganyika kudai uhuru labda Mzee Kawawa angeulizwa angeeleza ni nini kilitokea wakaamua kumfunga Migeyo kama walivyomfunga Waingereza.

Kitabu kimegusia kazi alofanya Kawawa kama mtumishi wa serikali ya kikoloni katika kambi za raia wa Kenyawalioshukukiwa kuwa ni Mau Mau. Katika hawa wafungwa walikuwawepo wananchama wa TANU ingawa hawa walikuwa Wakenya. Maarufu katika hawa alikuwa Dome Okochi Budohi (ambae kadi yake ya TANU ilikuwa na 6) na Patrick Aoko. Budohi alicheza senema pamoja na Kawawa iliyoitwa “Wageni Wema.” Kawawa na Budohi walikuwa wakifahamiana vizuri sana kwa sababu wote walikuwa wasanii. Budohi alikuwa mmojawapo katika bendi ya vijana wa mjini iliyojulikana kama Skylarks. Bendi hii baadaye ilibadilisha jina na kuitwa Blackbirds. Matangazo ya radio yalipoanza Tanganyika, Blackbirds midundo ya Blackbirds ilikuwa haikosekani kusikika radioni katika Sauti ya Dar es Salaam. Kawawa kama walivyo vijama wote wa Dar es Salaam wa wakati ule alikuwa mmmoja wa wapenzi wa bendi hii na alikuwa hakosekani Ukumbi wa Arnatouglo bendi hii ikitumbuiza katika ile miaka ya 1950. Ilikuwa katika ule upigaji muziki wa Budohi ndipo alipoungana na Kawawa katika kutengenezwa kwa senama hiyo ya “Wageni Wema” ambayo mwandishi kaitaja lakini aliishia hapo tu.

Budohi na Aoko ni kati ya wafungwa wa Mau Mau waliokuwa Handeni ambako Kawawa alikuwa na jukumu la kuwaangalia. Budohi ndiyo alikuwa mtu wa kati baina ya TAA na KAU na kuanzia hali ya hatari ilipotangazwa Kenya mwaka 1952 Budohi na Aoko wakawa katika jicho kali la makachero. Makachero hawa Waafrika wanafahamika na wengine walikuja kufanya kazi hiyohiyo katika Tanganyikahuru. Hiki ndicho kipindi ambacho Kaimu Rais wa TAA na Katibu wa TAA Abdulwahid Sykes alipokutana na Kenyatta Nairobi. Wakati Wakenya hawa wanafungwa Tanganyika, viongozi wa KAU akina Bildad Kaggia, Jomo Kenyatta, Kun’gu Karumba, Achieng Oneko, Paul Ngei na Fred Kubai walikuwa wamekamatwa Kenya. Kawawa ni mmoja kati ya viongozi hawa na ingependeza sana kama kupitia kwake tungeelezwa jinsi KAU na TAA ilivyokuwa ikishirikiana kwani haiwezekani kuwa Budohi na Kawawa uswahiba wao ukaishia kwenye kucheza senema tu.

Wanaharakati wote walishtushwa na kutiwa mbaroni kwa Budohi na Aoko. Haiwezekani kuwa iwe Mzee Kawawa kasahau matukio haya muhimu. Budohi na Aoko walikuwa wamefungwa minyororo walipokuwa katika selo pale Kituo cha Kati cha Polisi kwa sasa jumba hiloliko kituo cha mabasi kinachojulikana kama“station.” Waliwekwa pale kwa miezi sita muda wote wakiwa na minyororo miguuni. Waliwekwa pale kwa miezi sita wakihojiwa kabla hawajapelekwa Handeni walipomkuta Kawawa. Hivi ndivyo vitu ambavyo kwa hakika vingeongeza ladha ya kitabu cha Mzee Kawawa endapo mwandishi angechukua muda kutafiti na kuzungumza na watu waliokuwa katika harakati wakati ule ambao bado wa hai kama Ally Sykes na mdogo wake Balozi Abbas Sykes na wengine wengi ambao walikuwepo wakati ule kama Mzee Chipaka.

Katika migomo ya wakati wa kudai uhuru hakuna mgomo uliofanikiwa na kuvuta hisia za wananchi kamamgomo wa reli wa mwaka 1960 uliodumu kwa siku 62. Ukiachia kutajwa tu kama sehemu ya historia undani wake na jinsi mipango yake ilivyokwenda na nafasi ya viongozi wa Tanganyika Railway African Union (TRAU) walivyopata misaada kutoka nchi za Mashariki hivi havijawekwa wazi. Si treni, meli wala mabasi ya railway yaliyotembea kwa mieizi mitatu. Mipango ya mgomo huu ilifanyika Tabora ambako ndiko palikuwa na karakana kuu ya reli na hapo ndipo palipokuwa makao makuu ya viongozi wa TRAU, Salum Abdallah mwenyekiti na Kassanga Tumbo katibu. Kawawa ana mengi katika kadhia hii kwa kuwa yeye wakati ule ndiye alikuwa Katibu Mkuu wa TFL. Inasemekana mgomo huu miezi michache kabla Tanganyika haijapata uhuru ndiyo ilikuwa kama zinduo kwa Mwalimu Nyerere kutambua kuwa hakuwa peke yake na sauti kwa wananchi. Walikuwapo viongozi wengine pembeni yake ambao nao wakipiga wananchi wanacheza. Ilimdhihirikia kuwa huko mbeleni wanakokwenda ipo siku atapambana na viongozi hawa. Hivyo ndivyo ilivyotokea.

Inasemekana Mwalimu Nyerere akimtumia Kawawa alianza mipango kabambe ya kujitayarisha hilolisitokee. Hii ilikuwa nukta muhimu sanakwani haukupita muda baada ya uhuru kupatikana mwaka wa 1961 viongozi hawa wa vyama vya wafanyakazi wakajikuta wamewekwa kizuizini. Wasomaji wangependa kujua Kawawa alijihisi vipi wakati viongozi wenzake wa vyama vya wafanyakazi aliofanya nao kazi wakati wa kudai uhuru wakishirikiana na TANU kama Victor Mkello, Paul Pamba, Abdallah Mwamba, Hassan Khupe, Salum Abdallah na wengine wengi walipokamatwa mwaka wa 1964 na kuwekwa kizuizini kwa amri ya Mwalimu Nyerere. Maelezo ya Mzee Kawawa katika mambo haya yangetia mwanga katika yale mengi yasiyofahamika katika historia ya Tanzania.

Waislam wangependa sanakujua hisia za Kawawa kama muumini alihisi vipi wakati makachero walipomvamia mzalendo aliyepigania uhuru wa Tanganyika Mufti wa TanganyikaSheikh Hassan bin Amir usiku wa manane na kumrudisha Zanzibar na kuwekewa masharti kuwa hana ruhusa kurejea Tanzania Bara. Nilitegemea kusoma sakata zima la kukamatwa kwa Sheikh Hassan bin Amir na kuvunjwa kwa East African Muslim Welfare Society (EAMWS) jumuia ya Waislam iliyokuwa ikipanga kujenga Chuo Kikuu Dar es Salaam.

Nilitegemea halikadhalika kusoma mchango wa Mzee Kawawa katika kuunda Bakwata. Mengi yamesemwa kuhusu hujuma hii kwa Waislam moja wapo ni kuwa EAMWS ilivunjwa kwa shinikizo la Kanisa Katoliki likimtumia Mwalimu Nyerere. Hili si jambo la siri tena tafiti mbalimbali zimefanywa na vitabu kuandikwa na waandishi kutoka nje ya Tanzania kuhusu tatizo hili la kujitokeza udini mapema baada ya uhuru kupatikana. Kwa kuwa Kawawa alikuwa pamoja na Mwalimu Nyerere na alishiriki katika kuunda Bakwata wananchi hasa Waislam wangenufaika kusoma hisia zake wakati maamuzi hayo yanapitishwa na serikali. Kwa hakika kuna maamuzi mengi sana ambayo Kawawa alishiriki yaliwaumiza sana Waislam katika juhudi zao za kujitafutia elimu. Waislam wangependa sana kujua ni kipi kilikuwa kinamsukuma kufanya vile.

Kwa yeyote atakaepata bahati ya kusoma kitabu cha maisha ya Mzee Kawawa ni wazi hatakuta jipya ambalo hakuwa akilijua kabla. Kwa ajili hii basi mlango bado uko wazi kwa watafiti wengine kuandika kitabu kuhusu Rashidi Mfaume Kawawa kwani maisha ya Mzee Kawawa bado hayajaandikwa. Hata hivyo tumpongeze mwandishi kwa kazi hii kwani ni baada ya yeye kutuandikia kitabu ndipo nasi tumepata nguvu ya kunyanyua kalamu zetu na kusema.
3rd January 2010
historia
 
Fundi...
Utanisoma kila siku na utaona haya haya kwa kuwa historia haibadiliki ni ile ile na kila siku napata wanafunzi wapya na narejea somo lile lile na picha zile zile.

Mwaka wa 25 toka kitabu cha Abdul Sykes kichapwe na kila siku kiko midomoni mwa watu.

Kitabu cha Ulotu na Kivukoni chapa mara moja vyote vimekufa.

Ushapata hata kusikia mtu anaviuliza?

Kitabu changu bado kinaishi na kila uchao nahojiwa na FM Stations na TV Stations kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika.

Nimesimama Northwestern University, Evanston, Chicago Illinois na nimezungumza vipi kitabu changu kilivyobadili historia iliyokuwapo na kuweka historia mpya.

Leo mnaisoma upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika na mnaisoma upya historia ya Julius Nyerere.

Zilipoanza kejeli baada ya uhuru kuhusu TAA kuitwa ati "chama cha starehe," Ahmed Rashaad Ali akiumia roho yake na akimtaka Abdul ajibu kejeli zile.

Abdul alikataa na hakufungua kinywa chake akabakia kimya hadi anaingia kaburini mwaka wa 1968.

Katika kifo chake magazeti ya TANU Uhuru na Nationalist hawakuchapa hata taazia.

Taazia iliandikwa na kuchapwa na Brendon Grimshow Mhariri wa Tanganyika Standard.

Katika sherehe za miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika Abdul Sykes na mdogo wake Ally wakapewa Medali ya Mwenge wa Uhuru na Rais Kikwete kwa mchango wao katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Huu ndiyo mwaka ambao baba yao Kleist Sykes maisha yake yaliyotokea katika Dictionary of African Biography (DAB).

Kleist Sykes mwanae Abdul Sykes ndugu na rafiki yangu toka udogoni alifunga safari akaja Tanga kunishukuru.

Kleist akiamini kuwa ni kitabu nilichoandika ndicho kilichosababisha baba zake watambulike.

Kleist alilia machozi kama mtoto mdogo.

Kwetu sisi huu ni ushindi mkubwa.

Mwenyezi Mungu amesema yeye kajiharamishia dhulma.

Kitabu cha Abdul Sykes na yake mengi aliyofanya kupigania uhuru wa Tanganyika ndiyo haya maneno yale yale na picha zile zile zinajirudia kila siku na watu hawachoki kunisikiliza na kunisoma.

Tazama mnavyojazana hapa.
Kitu gani kinawaleteni kwangu?

Kila mnapokuja na maswali hata kama ni ya kejeli najibu.
Niko katika shinikizo kubwa kuwa niandike maisha yangu.

Alhamdulilah Rabilalamin.
"Tazama mnavyojazana hapa.
Kitu gani kinawaleteni kwangu?"....
hahaha mzee umepigwa spana hadi umekasirika. Hapa sio kwako.. hapa ni JamiiForums. Wewe ulichoandika ni historia ya ndugu zako na sio TANU, UHURU wala NYERERE. Chuki zako za kidini baki nazo hukohuko kwako usizieneze mitandaoni. Nampongeza sana Mwalimu Nyerere kwa kuwafutilia mbali hao wazee wako wapumbavu waliotaka kuleta upumbavu wao kwenye taifa letu. Hata wewe pia ni mtu uliyepuuzwa umebaki kubwabwaja kuhusu Sykes kila siku.
 
"Tazama mnavyojazana hapa.
Kitu gani kinawaleteni kwangu?"....
hahaha mzee umepigwa spana hadi umekasirika. Hapa sio kwako.. hapa ni JamiiForums. Wewe ulichoandika ni historia ya ndugu zako na sio TANU, UHURU wala NYERERE. Chuki zako za kidini baki nazo hukohuko kwako usizieneze mitandaoni. Nampongeza sana Mwalimu Nyerere kwa kuwafutilia mbali hao wazee wako wapumbavu waliotaka kuleta upumbavu wao kwenye taifa letu. Hata wewe pia ni mtu uliyepuuzwa umebaki kubwabwaja kuhusu Sykes kila siku.
Mama...
Umeghadhibika sana.
Katika hali kama hii kukujibu si busara.
 
Fundi...
Utanisoma kila siku na utaona haya haya kwa kuwa historia haibadiliki ni ile ile na kila siku napata wanafunzi wapya na narejea somo lile lile na picha zile zile.

Mwaka wa 25 toka kitabu cha Abdul Sykes kichapwe na kila siku kiko midomoni mwa watu.

Kitabu cha Ulotu na Kivukoni chapa mara moja vyote vimekufa.

Ushapata hata kusikia mtu anaviuliza?

Kitabu changu bado kinaishi na kila uchao nahojiwa na FM Stations na TV Stations kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika.

Nimesimama Northwestern University, Evanston, Chicago Illinois na nimezungumza vipi kitabu changu kilivyobadili historia iliyokuwapo na kuweka historia mpya.

Leo mnaisoma upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika na mnaisoma upya historia ya Julius Nyerere.

Zilipoanza kejeli baada ya uhuru kuhusu TAA kuitwa ati "chama cha starehe," Ahmed Rashaad Ali akiumia roho yake na akimtaka Abdul ajibu kejeli zile.

Abdul alikataa na hakufungua kinywa chake akabakia kimya hadi anaingia kaburini mwaka wa 1968.

Katika kifo chake magazeti ya TANU Uhuru na Nationalist hawakuchapa hata taazia.

Taazia iliandikwa na kuchapwa na Brendon Grimshow Mhariri wa Tanganyika Standard.

Katika sherehe za miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika Abdul Sykes na mdogo wake Ally wakapewa Medali ya Mwenge wa Uhuru na Rais Kikwete kwa mchango wao katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Huu ndiyo mwaka ambao baba yao Kleist Sykes maisha yake yaliyotokea katika Dictionary of African Biography (DAB).

Kleist Sykes mwanae Abdul Sykes ndugu na rafiki yangu toka udogoni alifunga safari akaja Tanga kunishukuru.

Kleist akiamini kuwa ni kitabu nilichoandika ndicho kilichosababisha baba zake watambulike.

Kleist alilia machozi kama mtoto mdogo.

Kwetu sisi huu ni ushindi mkubwa.

Mwenyezi Mungu amesema yeye kajiharamishia dhulma.

Kitabu cha Abdul Sykes na yake mengi aliyofanya kupigania uhuru wa Tanganyika ndiyo haya maneno yale yale na picha zile zile zinajirudia kila siku na watu hawachoki kunisikiliza na kunisoma.

Tazama mnavyojazana hapa.
Kitu gani kinawaleteni kwangu?

Kila mnapokuja na maswali hata kama ni ya kejeli najibu.
Niko katika shinikizo kubwa kuwa niandike maisha yangu.

Alhamdulilah Rabilalamin.
Sasa kama unarudia somo lile lile na picha zile zile unashangaa nini nikikupinga kwa maneno yale yale?
Ni haki yako kuwainua ndugu na rafiki zako. Lakini hauna haki kututaka sote tukubali kuwaabudu hao unaowaabudu. Kwetu sisi wakina Sykes ni binadamu kama wengine na wanastahili heshima na kukosolewa kama binadamu wengine.
Unfortunately unabakia relevant kwa wale ambao wanatafuta uthibitisho wa imani yao kuwa wameonewa na wanaendelea kuonewa kama waislamu katika nchi yao. Hao ndio kila kukicha wanaomba uwape darsa.

Kutoa lecture Chuo Kikuu hakuna maana kuwa unakubalika. Chuo Kikuu ni mahali ambapo siku zote mawazo mbadala yanakaribishwa ili yajadiliwe. Ndio maana kila siku kuna controversies katika vyuo vikuu vya wenzetu kuhusu watu wanaoalikwa kulecture maana wengine wana mitazamo ambayo haikubaliki katika jamii. Utawa impress hao ambao wanataka kuamini kuwa wewe ni msomi uliyebobea katika historia ya nchi yetu na ndio maana una uwezo wa kuonyesha ubaya wa wakristu.
Sisi wengine hatukuoni hivyo. Tunakuona kama mwandishi mzuri wa historia ya ndugu na jamaa zako lakini si historia ya nchi yetu.

Watafiti wazuri siku zote wanatafuta validation ya wanachokigundua kwa kutafuta source tofauti kuhusu jambo hilo. Bahati mbaya simulizi za ndugu zako sio proof ya kutosha. Unachokifanya ni kuwaweka baadhi yao mahali ambapo naamini kuwa wasingefurahi kuwekwa. Unaubadilisha uzalendo wa wakina Sykes kutoka kwenye taifa lao kwenda kwenye dini na kabila lao. Hauwatendei haki.

Amandla...
 
Sasa kama unarudia somo lile lile na picha zile zile unashangaa nini nikikupinga kwa maneno yale yale?
Ni haki yako kuwainua ndugu na rafiki zako. Lakini hauna haki kututaka sote tukubali kuwaabudu hao unaowaabudu. Kwetu sisi wakina Sykes ni binadamu kama wengine na wanastahili heshima na kukosolewa kama binadamu wengine.
Unfortunately unabakia relevant kwa wale ambao wanatafuta uthibitisho wa imani yao kuwa wameonewa na wanaendelea kuonewa kama waislamu katika nchi yao. Hao ndio kila kukicha wanaomba uwape darsa.

Kutoa lecture Chuo Kikuu hakuna maana kuwa unakubalika. Chuo Kikuu ni mahali ambapo siku zote mawazo mbadala yanakaribishwa ili yajadiliwe. Ndio maana kila siku kuna controversies katika vyuo vikuu vya wenzetu kuhusu watu wanaoalikwa kulecture maana wengine wana mitazamo ambayo haikubaliki katika jamii. Utawa impress hao ambao wanataka kuamini kuwa wewe ni msomi uliyebobea katika historia ya nchi yetu na ndio maana una uwezo wa kuonyesha ubaya wa wakristu.
Sisi wengine hatukuoni hivyo. Tunakuona kama mwandishi mzuri wa historia ya ndugu na jamaa zako lakini si historia ya nchi yetu.

Watafiti wazuri siku zote wanatafuta validation ya wanachokigundua kwa kutafuta source tofauti kuhusu jambo hilo. Bahati mbaya simulizi za ndugu zako sio proof ya kutosha. Unachokifanya ni kuwaweka baadhi yao mahali ambapo naamini kuwa wasingefurahi kuwekwa. Unaubadilisha uzalendo wa wakina Sykes kutoka kwenye taifa lao kwenda kwenye dini na kabila lao. Hauwatendei haki.

Amandla...
Fundi...
Kitabu kipo miaka 25 sasa na tunakwenda toleo la 5.

Vitabu vya Ulotu na Kivukoni havijulikani viko wapi.

Baada ya kitabu cha Sykes nikaandika vitabu vingine vya historia na vyote viko sokoni vinasomwa.

Mimi niwe na lipi la kusema zaidi?
Kilichobakia kwangu ni kushukuru.

Lakini mtu anapotaka tufanye mjadala tunafanya kama hivi na kitu kimoja ajabu ya Rahman ni kuwa kila inapotokea tukawa na mjadala mkali kama hivi mauzo ya kitabu cha Sykes yanapanda sana.

Hawa ni wasomaji wapya ninaoendelea kuwapata kila siku.

Historia hii inawasisimua kupita kiasi kwani hawajapata kuisikia wala kusomeshwa shuleni na vyuoni.

Hivi karibuni nilikuwa natoka nje ya duka mtu mmoja simfahamu akaniita kwa sauti, "Mohamed nimekuona kwenye TV Kadi No. 1 Julius Kambarage Nyerere, Kadi No. 2 Ally Kleist Sykes, Kadi No. 3 Abdulwahid Kleist Sykes...

Hapa ndipo kitabu kilipowafikisha watu.
 
HISTORIA YA TANU NYANDA ZA JUU KUSINI

KUMBUKUMBU ZA UHURU: ABBAS MAX WA IRINGA (1918 - 1993)

Abbas Max ana historia ya kusisimua sana kama ilivyo kwa wazalendo wengi waliopigania uhuru wa Tanganyika lakini kwa bahati mbaya historia imewasahau.

John Iliffe mwanahistoria nguli aliyeiokoa historia ya Tanganyika amepata kusema kuwa historia nyingi ya TANU ipo katika mikono ya watu binafsi.

Iliffe alisema maneno haya katika miaka ya 1960 lakini kwa sasa ni wazi kuwa historia nyingi ya TANU si tu iko katika mikono ya watu binafsi bali iko pia katika masanduku na makabati yaliyoachwa na wazalendo wale waliopigania uhuru ambao takriban wote wameshatangulia mbele ya haki.

Historia hii ndani ya makabati na masanduku ya hawa wazalendo ni picha za "black and white" na nyaraka zilizoandikwa kwa mkono na type writer.

Siku chache zilizopita katika kutayarisha vipindi kwa ajili ya Nyerere Day nilitembelewa na waandishi na katika kuhitimisha mazungumzo yetu wakawa wanataka kujua majina ya wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika lakini wamesahaulika.

Ndipo nilipolitaja jina la Abbax Max katika video ambayo tulikuwa tunarekodi.

Hii video fupi ipo hapo FB.

Mtoto wa Abbas Max, Ally Abbas Max baada ya kuiona hii video siku ya pili tu akanitumia picha ya baba yake na ''cuttings'' za gazeti kuhusu historia ya marehemu baba yake katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Ally Abbas Max kwa miaka mingi alikuwa Marekani na sikutegemea kama atakuwa na kumbukumbu za baba yake huko alikokwenda ughaibuni.

Ally amenitia moyo sana aliponiambia kuwa baba yake ameacha nyaraka na zimehifadhiwa hadi leo zaidi ya miaka 30 toka kufariki kwake, ni kiasi cha kuzifungua tu na bila shaka mengi yatajulikana jinsi yeye na wenzake walivyofungua tawi la kwanza la TANU Iringa mwaka wa 1955.

Naeleza hapa yale niliyoweza kupata kutoka kwa Ally Abbas Max nikichanganya kidogo na yangu.

Inawezekana watu wengi wasijue kuwa Chief Adam Sapi Mkwawa ni mtu wa kwanza kuingia TANU Iringa.

Chief Mkwawa aliwaalika Abdul Sykes na Dossa Aziz Kalenga katika sherehe ya kupokea fuvu la babu yake Chief Mkwawa kutoka Ujerumani.

Hili fuvu liliwasili Dar es Salaam tarehe 9 Julai 1954 siku mbili tu baada ya TANU kuasisiwa.

Katika mazungumzo ya faragha baina ya Chief Adam Sapi Mkwawa, Dossa Aziz na Abdul Sykes, Chief Adam Sapi akakata kadi ya TANU kwa siri.

Abbas Max amewaeleza watoto wake kuwa Abdul Sykes alikuja Iringa wakati tayari TANU ishapamba moto Dar es Salaam na alifikia nyumbani kwake.

Abdul Sykes alikuwa njiani anaelekea Njombe kumtembelea mume mwenzie.
Abbas Max akaamua kumpeleka Njombe na gari yake Peugeot Pickup 203.

Mazungumzo baina yao yalikuwa kuhusu TANU, Nyerere na juhudi za kudai uhuru.
Abbas Max akamwambia Abdul Sykes amwambie Nyerere aje Iringa ili wafungue tawi la TANU na wao wawemo ndani ya juhudi hizi za kupigania uhuru.

Haukupita muda Abdul Sykes akamtumia Abbas Max taarifa kuwa Nyerere atafika Iringa akitokea Lindi, Songea na Njombe.

Abbas Max alitoka na wazalendo wenzake kwenda kumpokea Julius Nyerere njiani nje ya mji wa Iringa.

Nyerere alikuwa ameongozana na Ally Mwinyi Tambwe na Rajab Diwani na dereva wa TANU Omari Simba.

Nyerere alimfahamisha Abbas Max kuwa ili kufungua tawi la TANU kwanza lazima awe na wanachama 12 wanye kadi za TANU.

Watu walikuwa wanaogopa kuingia chama na hiki kikawa kikwazo kikubwa kwa Abbas Max.

Nyerere aifanya mkutano wa hadhara Iringa lakini ulihudhuriwa na watu wachache.
Juu ya haya yote Abbas Max aliweza kupata watu waliokuwa tayari kujiunga na TANU na hawa walikuwa: Saleh Masasi ambae Nyerere alilala nyumbani kwake, Hussein Issa, Hussein Kandoro, Yasin Hamid, Ahmed Mahmoud, Abdulrahman Mwangili, Juma Lipinjime na Khalfani Ally, Abbas Max akiwa Mwenyekiti.

Katika mkutano wa Kura Tatu Tabora mwaka wa 1958 Abbas Max akachaguliwa kuwa mjumbe wa Halmashauru Kuu ya TANU hivyo ikabidi ajiuzulu uenyekiti.

Nafasi yake ikachukuliwa na Chogga.

Chogga ameacha historia ya pekee katika wanasiasa ndani ya TANU waliokuwa mwiba wa koo kwa Julius Nyerere.

Itapendeza sana kama wanahistoria wataandika historia hii yake kwani mwaka wa 1968 Chogga na wenzake walifukuzwa TANU.

Ikutoshe tu kuwa Abbas Max anasema kuwa Chogga alisababisha TANU ifungiwe iringa.

Hii ikapelekea Abbas Max na wenzake waendeshe harakati zao chinichini kupitia Jambo Club waliyoianzisha baada ya TANU kupigwa marufuku.

Safari ya pili Nyerere alipokwenda Iringa alifikia nyumbani kwa Abbas Max.
Abbas Max alitembea kote na Nyerere Nyanda za Kati Kusini katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Charles Mzena ambae wakati wa kupigania uhuru alikuwa Special Branch alipata kumwambia Salum Khamis wakati huo uhuru ushapatikana kuwa, ''Chief Adam Sapi Mkwawa alikuwa ndiyo chief wa Wahehe lakini Abbas Max wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika alikuwa na nafasi yake juu ya Chief Adam Sapi.''

Abbas Max alikuwa na kawaida katika misafara ile na Nyerere kuwa wakati wa kula yeye alikuwa akisubiri hadi dakika ya mwisho wakati chakula kimetengwa na wanaanza kula yeye atampora Nyerere sahani yake na kumpa ya kwake.

Nyakati zile zilikuwa ngumu na Nyerere alikuwa akiwindwa.
Abbas Max alikuwa akisema, ''Hakuna huku wa kunidhuru mimi.''

Historia ya Abbas Max katika kupigania uhuru wa Tanganyika ina mengi sana.

Mimi Inshaa Allah nasubiri siku wanae watakapofungua Nyaraka za baba yao Abbas Max na kuziweka hadharani zisomwe na wanahistoria.

Tunamuomba Allah awarehemu wazee wetu hawa waliopigania uhuru wa nchi yetu kwa hali na mali zao.
Amin.

Picha ya kwanza ni Abbas Max.
Picha ya pili kulia ni Abbas Max, Julius Nyerere na Chande Ali.
Picha ya tatu kushoto ni Abbas Max ameegemea gari akiwa na Julius Nyerere na msafara wake.
Picha ya nne Mzee Abbas Max na mjukuu wake.

252729486_1056203561793688_8467899744738260880_n.jpg
252789922_1056220581791986_5100883259423906521_n.jpg
253251058_1056264835120894_2726486215836840789_n.jpg
253239453_1056265191787525_3466459277300259921_n.jpg
Wewe mzee umelewa pombe ya uislamu kiasi kwamba hadi watu wa iringa unawataja waislamu peke yao. Mimi ningekuwa raisi ningehakikisha naukomesha huu udini na hii taswira unayojaribu kuijenga katika vitabu vyako.

Unapambana sana kuonesha ni waislamu ndio walipigania uhuru wakati sote tunafahamu kinara na kiongozi alikuwa Nyerere na maelfu ya watanganyika wasiokuwa na dini waliotapakaa nchi nzima.

Bila aibu hapa unaonesha waislamu 12 ndio walianzisha tanu iringa wakati huko iringa enzi zile hata waislamu hawakuwepo na hata mpaka leo wapo waislamu wachache sana iringa.

Harakati za uhuru zilifanywa pia kwa kiasi kikubwa na wakatoliki kupitia umisheni lakini wewe umejaa udini na kupigania uislamu.
 
Mama...
Umeghadhibika sana.
Katika hali kama hii kukujibu si busara.
Sisi wazalendo tunamshukuru sana Mwalimu Nyerere kwa kuwadhibiti watu kama wewe. Wewe mzee ukiachiwa nafasi ya kueneza hizo propaganda zako amani itapotea. Sisi tunakupinga kuanzia hapa JF ili ujue sio watu wote wajinga kama unavyodhani. Haya mambo yako ya kipuuzi unayopigania ndo yamesababisha nchi nyingi hazina amani
 
Fundi...
Kitabu kipo miaka 25 sasa na tunakwenda toleo la 5.

Vitabu vya Ulotu na Kivukoni havijulikani viko wapi.

Baada ya kitabu cha Sykes nikaandika vitabu vingine vya historia na vyote viko sokoni vinasomwa.

Mimi niwe na lipi la kusema zaidi?
Kilichobakia kwangu ni kushukuru.

Lakini mtu anapotaka tufanye mjadala tunafanya kama hivi na kitu kimoja ajabu ya Rahman ni kuwa kila inapotokea tukawa na mjadala mkali kama hivi mauzo ya kitabu cha Sykes yanapanda sana.

Hawa ni wasomaji wapya ninaoendelea kuwapata kila siku.

Historia hii inawasisimua kupita kiasi kwani hawajapata kuisikia wala kusomeshwa shuleni na vyuoni.

Hivi karibuni nilikuwa natoka nje ya duka mtu mmoja simfahamu akaniita kwa sauti, "Mohamed nimekuona kwenye TV Kadi No. 1 Julius Kambarage Nyerere, Kadi No. 2 Ally Kleist Sykes, Kadi No. 3 Abdulwahid Kleist Sykes...

Hapa ndipo kitabu kilipowafikisha watu.
Sishangai kuwa unapata wasomaji wapya maana unayosimulia yanapendwa sana na sehemu ya jamii yetu. Watu ambao katika dunia ya sasa ya kidigitali bado wanategemea kusomeshwa kila kitu ndio rahisi sana kumeza kila unachosema bila hata kufanya utafiti wao wenyewe. Wao kuikubali hakumaanishi kuwa uko sahihi. Ndio maana sisi wengine hatusiti kukujibu pale ambapo unapotosha historia ili mtu asiwe na kisingizio kuwa hakujua. Na hio hatutaacha maana tunaamini kuwa upotoshaji unaofanya una hatari yake.

Amandla...
 
HISTORIA YA TANU NYANDA ZA JUU KUSINI

KUMBUKUMBU ZA UHURU: ABBAS MAX WA IRINGA (1918 - 1993)

Abbas Max ana historia ya kusisimua sana kama ilivyo kwa wazalendo wengi waliopigania uhuru wa Tanganyika lakini kwa bahati mbaya historia imewasahau.

John Iliffe mwanahistoria nguli aliyeiokoa historia ya Tanganyika amepata kusema kuwa historia nyingi ya TANU ipo katika mikono ya watu binafsi.

Iliffe alisema maneno haya katika miaka ya 1960 lakini kwa sasa ni wazi kuwa historia nyingi ya TANU si tu iko katika mikono ya watu binafsi bali iko pia katika masanduku na makabati yaliyoachwa na wazalendo wale waliopigania uhuru ambao takriban wote wameshatangulia mbele ya haki.

Historia hii ndani ya makabati na masanduku ya hawa wazalendo ni picha za "black and white" na nyaraka zilizoandikwa kwa mkono na type writer.

Siku chache zilizopita katika kutayarisha vipindi kwa ajili ya Nyerere Day nilitembelewa na waandishi na katika kuhitimisha mazungumzo yetu wakawa wanataka kujua majina ya wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika lakini wamesahaulika.

Ndipo nilipolitaja jina la Abbax Max katika video ambayo tulikuwa tunarekodi.

Hii video fupi ipo hapo FB.

Mtoto wa Abbas Max, Ally Abbas Max baada ya kuiona hii video siku ya pili tu akanitumia picha ya baba yake na ''cuttings'' za gazeti kuhusu historia ya marehemu baba yake katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Ally Abbas Max kwa miaka mingi alikuwa Marekani na sikutegemea kama atakuwa na kumbukumbu za baba yake huko alikokwenda ughaibuni.

Ally amenitia moyo sana aliponiambia kuwa baba yake ameacha nyaraka na zimehifadhiwa hadi leo zaidi ya miaka 30 toka kufariki kwake, ni kiasi cha kuzifungua tu na bila shaka mengi yatajulikana jinsi yeye na wenzake walivyofungua tawi la kwanza la TANU Iringa mwaka wa 1955.

Naeleza hapa yale niliyoweza kupata kutoka kwa Ally Abbas Max nikichanganya kidogo na yangu.

Inawezekana watu wengi wasijue kuwa Chief Adam Sapi Mkwawa ni mtu wa kwanza kuingia TANU Iringa.

Chief Mkwawa aliwaalika Abdul Sykes na Dossa Aziz Kalenga katika sherehe ya kupokea fuvu la babu yake Chief Mkwawa kutoka Ujerumani.

Hili fuvu liliwasili Dar es Salaam tarehe 9 Julai 1954 siku mbili tu baada ya TANU kuasisiwa.

Katika mazungumzo ya faragha baina ya Chief Adam Sapi Mkwawa, Dossa Aziz na Abdul Sykes, Chief Adam Sapi akakata kadi ya TANU kwa siri.

Abbas Max amewaeleza watoto wake kuwa Abdul Sykes alikuja Iringa wakati tayari TANU ishapamba moto Dar es Salaam na alifikia nyumbani kwake.

Abdul Sykes alikuwa njiani anaelekea Njombe kumtembelea mume mwenzie.
Abbas Max akaamua kumpeleka Njombe na gari yake Peugeot Pickup 203.

Mazungumzo baina yao yalikuwa kuhusu TANU, Nyerere na juhudi za kudai uhuru.
Abbas Max akamwambia Abdul Sykes amwambie Nyerere aje Iringa ili wafungue tawi la TANU na wao wawemo ndani ya juhudi hizi za kupigania uhuru.

Haukupita muda Abdul Sykes akamtumia Abbas Max taarifa kuwa Nyerere atafika Iringa akitokea Lindi, Songea na Njombe.

Abbas Max alitoka na wazalendo wenzake kwenda kumpokea Julius Nyerere njiani nje ya mji wa Iringa.

Nyerere alikuwa ameongozana na Ally Mwinyi Tambwe na Rajab Diwani na dereva wa TANU Omari Simba.

Nyerere alimfahamisha Abbas Max kuwa ili kufungua tawi la TANU kwanza lazima awe na wanachama 12 wanye kadi za TANU.

Watu walikuwa wanaogopa kuingia chama na hiki kikawa kikwazo kikubwa kwa Abbas Max.

Nyerere aifanya mkutano wa hadhara Iringa lakini ulihudhuriwa na watu wachache.
Juu ya haya yote Abbas Max aliweza kupata watu waliokuwa tayari kujiunga na TANU na hawa walikuwa: Saleh Masasi ambae Nyerere alilala nyumbani kwake, Hussein Issa, Hussein Kandoro, Yasin Hamid, Ahmed Mahmoud, Abdulrahman Mwangili, Juma Lipinjime na Khalfani Ally, Abbas Max akiwa Mwenyekiti.

Katika mkutano wa Kura Tatu Tabora mwaka wa 1958 Abbas Max akachaguliwa kuwa mjumbe wa Halmashauru Kuu ya TANU hivyo ikabidi ajiuzulu uenyekiti.

Nafasi yake ikachukuliwa na Chogga.

Chogga ameacha historia ya pekee katika wanasiasa ndani ya TANU waliokuwa mwiba wa koo kwa Julius Nyerere.

Itapendeza sana kama wanahistoria wataandika historia hii yake kwani mwaka wa 1968 Chogga na wenzake walifukuzwa TANU.

Ikutoshe tu kuwa Abbas Max anasema kuwa Chogga alisababisha TANU ifungiwe iringa.

Hii ikapelekea Abbas Max na wenzake waendeshe harakati zao chinichini kupitia Jambo Club waliyoianzisha baada ya TANU kupigwa marufuku.

Safari ya pili Nyerere alipokwenda Iringa alifikia nyumbani kwa Abbas Max.
Abbas Max alitembea kote na Nyerere Nyanda za Kati Kusini katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Charles Mzena ambae wakati wa kupigania uhuru alikuwa Special Branch alipata kumwambia Salum Khamis wakati huo uhuru ushapatikana kuwa, ''Chief Adam Sapi Mkwawa alikuwa ndiyo chief wa Wahehe lakini Abbas Max wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika alikuwa na nafasi yake juu ya Chief Adam Sapi.''

Abbas Max alikuwa na kawaida katika misafara ile na Nyerere kuwa wakati wa kula yeye alikuwa akisubiri hadi dakika ya mwisho wakati chakula kimetengwa na wanaanza kula yeye atampora Nyerere sahani yake na kumpa ya kwake.

Nyakati zile zilikuwa ngumu na Nyerere alikuwa akiwindwa.
Abbas Max alikuwa akisema, ''Hakuna huku wa kunidhuru mimi.''

Historia ya Abbas Max katika kupigania uhuru wa Tanganyika ina mengi sana.

Mimi Inshaa Allah nasubiri siku wanae watakapofungua Nyaraka za baba yao Abbas Max na kuziweka hadharani zisomwe na wanahistoria.

Tunamuomba Allah awarehemu wazee wetu hawa waliopigania uhuru wa nchi yetu kwa hali na mali zao.
Amin.

Picha ya kwanza ni Abbas Max.
Picha ya pili kulia ni Abbas Max, Julius Nyerere na Chande Ali.
Picha ya tatu kushoto ni Abbas Max ameegemea gari akiwa na Julius Nyerere na msafara wake.
Picha ya nne Mzee Abbas Max na mjukuu wake.

252729486_1056203561793688_8467899744738260880_n.jpg
252789922_1056220581791986_5100883259423906521_n.jpg
253251058_1056264835120894_2726486215836840789_n.jpg
253239453_1056265191787525_3466459277300259921_n.jpg
Huu ni mfano wa kwa nini nasema una potosha mambo. Historia ya TANU Iringa umewatambua waislamu peke yao. Umeenda mbali hata msafara wa Nyerere ulioutambua ni wenye waislamu peke yao. Lakini humu humu umetuwekea picha ikionyesha walioongozana na Mwalimu kwenda Iringa ni pamoja na Bhoke Munanka na Joseph Nyerere lakini katika simulizi yako ni kama vile Mwalimu alikuwa anasindikizwa na waislamu peke yake. Unamtambulisha Abbas Max akiwa amezungukwa na waislamu watupu lakini tuliowafahamu wakina Max tunajua kuwa hawakuwa na chembe ya udini ingawa simulizi yako inamfanya Abbas aonekane mdini. Hapo ndipo unapo wakosea hawa wazee wetu.

Amandla...
 
MAKALA YA MAMA MARIA NYERERE KUTIMIZA MIAKA 93 NA MAKOSA NDANI YA MAKALA

Kuna makala imewekwa mtandaoni kuhusu Mama Maria Nyerere kutimiza miaka 93 hii leo.

Makala hii imesheheni mengi katika maisha ya Mama Maria.

Nimeisoma na imenifurahisha na kunielimisha katika mengi ambayo sikuwa nayajua vyema.

Juu ya hayo yote makala hii imeruka sehemu muhimu sana katika maisha yake na kwa kweli si yake tu bali na ya mumewe Mwalimu Nyerere na historia ya TANU na pia kuandika mengine ambayo si ya kweli.

Makala hii inazungumza duka alilofungua Mama Maria Magomeni.

Mwandishi anaeleza duka hili kuwa duka lililokuwa linauza bidha kadhaa.

Hii si kweli Mama Maria alikuwa na duka dogo la kuuza mafuta ya taa.

Yako makosa mengi lakini hapa sitayazungumza tutizame hili hapo chini:

‘’In the mid 1950s, Mwalimu & his family were living at Magomeni Mapipa where they rented a small house.

This was after they had stayed in John Rupia's house at Mission Quarter, Kariakoo for one year.

This followed Mwalimu Nyerere's abrupt resignation as a teacher at St. Francis Pugu on March 22, 1955.

Mama Maria, to make ends meet, opened a small shop in their small house at Magomeni to sell sugar, soaps, salt, cooking oil etc.

She believed in living within her means and working hard for everything.

She was a rock to Mwalimu Nyerere's family.’’

Nimerekebisha machache katika historia ya Mama Maria Nyerere kwa kueleza historia yake kwa kutumia maelezo ya wale waliompokea Mwalimu alipofika Dar es Salaam mwaka wa 1952 ili historia muhimu ifahamike vizuri kwa faida ya kizazi hiki na kizazi kijacho:

"Napenda kueleza kitu kidogo katika historia ya Mama Maria Nyerere.

Katika akina mama wa mwanzo kufahamiana na Mama Maria Nyerere alikuwa Bi. Mwamvua bint Mrisho maarufu kwa jina la Mama Daisy.

Walifahamiana kwa kuwa Mama Daisy alikuwa mke wa Abdul Sykes na kama tujuavyo Mwalimu Nyerere baada ya kuacha kazi ya ualimu alikwenda kuishi nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Hapa ndipo Mama Maria na Mama Daisy walipounga udugu.

Hii ilikuwa mwaka wa 1955.

Mama Daisy amenihadithia anasema baada ya miaka mingi kupita alikutana na Mama Maria Ukumbi wa Diamond Jubilee Mwalimu alipotoa hotuba kuwaaga Wazee wa Dar es Salaam.

Mama Maria alichukua fursa hii kuonana na kuzungumza na akina mama wa Dar-es-Salaam.

Mama Maria na Mama Daisy walikumbatiana kwa mapenzi Mama Maria akaieleza hadhira ile kuwa Mama Daisy na mumewe ndiyo waliowapokea yeye na mumewe Dar es Salaam.

Duka la mafuta ya taa la Mama Maria alilifungua Mtaa wa Mchikichi na Livingstone wakati wanaishi nyumbani kwa Abdul Sykes.

Akina mama ambao walikuwa jirani na duka hili walikuwa Bi. Chiku bint Said Kisusa ambae alikuwa anaishi mtaa huo wa Mchikichi kona na New Street (sasa Lumumba Avenue).

Duka la mafuta ya taa la Magomeni Mapipa Mama Maria alilifungua nyumbani kwa Ali Msham Mtaa wa Jaribu.

Ali Msham alikuwa amefungua tawi la TANU nyumbani kwake na Mwalimu alipohamia Maduka Sita Magomeni ikabidi Mama Maria awe anakwenda Kariakoo kila siku.

Ali Msham ndipo alipotoa nafasi nyumbani kwake duka lihamishiwe hapo ili kumpumzisha Mama Maria na shida ya kuparamia mabasi na watoto asubuhi kwenda Kariakoo.

Duka la mafuta ya taa la Mama Maria la hapo Maduka Sita lilikuja baadae.

Tunamtakia Mama Maria umri tawil na afya njema."

Picha hiyo hapo chini ni nyumba ya Mwalimu Maduka Sita Magomeni na huyo anaeingia ndani ya nyumba hiyo ni yeye mwenyewe.

Angalia bango juu ya nyumba linalotangaza duka la mafuta ya taa.

323194726_553729993036637_5201274679647759998_n.jpg
Hivi pale ni Mapipa au Mikumi? Ninavyoelewa, Mpaka wa Mapipa unaishia barabara ya Kigogo/Morocco.
 
Huu ni mfano wa kwa nini nasema una potosha mambo. Historia ya TANU Iringa umewatambua waislamu peke yao. Umeenda mbali hata msafara wa Nyerere ulioutambua ni wenye waislamu peke yao. Lakini humu humu umetuwekea picha ikionyesha walioongozana na Mwalimu kwenda Iringa ni pamoja na Bhoke Munanka na Joseph Nyerere lakini katika simulizi yako ni kama vile Mwalimu alikuwa anasindikizwa na waislamu peke yake. Unamtambulisha Abbas Max akiwa amezungukwa na waislamu watupu lakini tuliowafahamu wakina Max tunajua kuwa hawakuwa na chembe ya udini ingawa simulizi yako inamfanya Abbas aonekane mdini. Hapo ndipo unapo wakosea hawa wazee wetu.

Amandla...
Fundi...
Unanilaumu kwanini sijamtaja Bhoke Munanka.

Sawa ni kweli sikumtaja Bhoke Munanka wala Joseph Nyerere katika historia ya Abbss Max.

Lakini si mimi huyo niliyeandika makala na kuweka hizo picha?
Sasa hapo nimepotosha kitu gani?
 
Fundi...
Unanilaumu kwanini sijamtaja Bhoke Munanka.

Sawa ni kweli sikumtaja Bhoke Munanka wala Joseph Nyerere katika historia ya Abbss Max.

Lakini si mimi huyo niliyeandika makala na kuweka hizo picha?
Sasa hapo nimepotosha kitu gani?
Wewe mzee wetu ni mbishi mno hata kwa kitu kilicho wazi. Mungu amweke mahali pema peponi Mwalimu Nyerere kwa kuwakomesha watu kama wewe.
 
Fundi...
Unanilaumu kwanini sijamtaja Bhoke Munanka.

Sawa ni kweli sikumtaja Bhoke Munanka wala Joseph Nyerere katika historia ya Abbss Max.

Lakini si mimi huyo niliyeandika makala na kuweka hizo picha?
Sasa hapo nimepotosha kitu gani?
Unadhani wengi wanaangalia captions? Kama uliona wana umuhimu ungewaweka kwenye main body ambamo umemtaja mpaka dereva ambae ni muislamu! Ulishindwaje kujiuliza mbona hii habari haijakamilika? Mbona hamna wakristu? Mbona hamna wanawake? Lakini la hasha, kwako ilitosha kuwa waislamu wako front and centre. Huo ndio upotoshaji.

Amandla...
 
Huu ni mfano wa kwa nini nasema una potosha mambo. Historia ya TANU Iringa umewatambua waislamu peke yao. Umeenda mbali hata msafara wa Nyerere ulioutambua ni wenye waislamu peke yao. Lakini humu humu umetuwekea picha ikionyesha walioongozana na Mwalimu kwenda Iringa ni pamoja na Bhoke Munanka na Joseph Nyerere lakini katika simulizi yako ni kama vile Mwalimu alikuwa anasindikizwa na waislamu peke yake. Unamtambulisha Abbas Max akiwa amezungukwa na waislamu watupu lakini tuliowafahamu wakina Max tunajua kuwa hawakuwa na chembe ya udini ingawa simulizi yako inamfanya Abbas aonekane mdini. Hapo ndipo unapo wakosea hawa wazee wetu.

Amandla...
Wewe mzee wetu ni mbishi mno hata kwa kitu kilicho wazi. Mungu amweke mahali pema peponi Mwalimu Nyerere kwa kuwakomesha watu kama wewe.
Mama...
Ikiwa unaniona mbishi sawa.

Sikuwa najua kama Nyerere aliwakomesha watu kama mimi.
 
Back
Top Bottom