Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 7,672
- 9,039
🤣 🤣 🤣Hii Saccos ya mbowe wengi wanao muunga mkono mbowe ni chawa lialia mbali zaidi wajinga toleo la mwisho wasiokuwa na akili timamu.
Wengi wamejificha kwenye chaka la uana harakati lakini ukweli ulio wazi Wanafaidika Kwa pesa kupitia Saccos.
Huwezi Amini yeriko Nyerere kajitokeza hadharani kutetea masilahi yake maana anajua fika Lisu alichukua kijiti Kila kitu kitadoda. Hivyo kilicho Baki ni kumuunga mkono mbowe atawalehadi kifo chake.
View attachment 3185922
Humu jf kuna bifu kati ya mashabiki wa Freeman Mbowe na Tundu Lissu na machawa wa pande zote. Wengi ima hawajui mchezo wa siasa au hawana hata chembe juu ya demokrasia. Chadema, tofauti na CCM ni chama cha kila mmoja. Hivyo, wawili hawa wanapopambana kugombea uenyekiti si tatizo. Siyo sawa na maccm ambayo mwenyekiti wao hajawahi kupigiwa kura popote zaidi ya kutegemea mkono wa Mungu. Hivyo, wanaoona kuwa kuna uhasama kati ya Mbowe na lissu waache siasa na demokrasia vichukue mkondo wake.
wajumbe watumie busara na hekima kumpumzisha mbowe kwenye sanduku la kura ili chadema ipate heshima kuwa ina demokrasia ya kweliKuna tofauti kubwa sana kati ya CCM ya kitaifa na Chadema ya Mbowe.
Endapo Lisu atafanikiwa basi Tanzania itakua nchi ya kwanza Afrika kwa kuwa na chama chenye hadhi sawa na Democratic au Republican.
Kwa sasa bado Chadema ni Chama cha mtu binafsi tena dikteta na mfia chama na muuaji wa demokrasia yaani Mbowe Nkrunzinza. Aliyeingia kwenye Uenyekiti kilaini na kwa favour ya kichaga na sio uwezo maana hakushindanishwa wakati anaingia .