Makosa ya Musiba, hayalingani na tamaa ya Membe!

Makosa ya Musiba, hayalingani na tamaa ya Membe!

Akili yako inamatatizo, unadhani hiyo fidia unajipangia tu, hapa umeitukana mahakama, mahakama ndio inaangalia ukubwa wa kosa na unastahili ulipwe kiasi gani kulingana na mtuhumiwa alivyojitetea.Wewe kafue mashuka ya NW
 
Sitetei chochote kuhusu yaliyojiri kumhusu mh Membe yakimhusisha mmiliki wa magazeti ya Tanzanite kumdhalilisha mh Membe kwa kumchafua, na sipangani na sheria yoyote ya nchi iliyotumika, ila naiona tamaa kubwa isiyo na mantiki kutoka kwa mh Bernard Membe ya kutaka ujira mkubwa usiolingana na kile wengi wanakiita ni kudhalilishwa

Hata tungelimshirikisha asiye na akili kuhusu madai hayo ya bilioni 9 kwa kosa tu la kuandikwa vibaya Mh Membe kwenye gazeti, nina hakika angelicheka kwa huzuni na mshangao, naamini, kila kitu Msiba atauza na pesa haitatosha, mwisho wa siku ni nini? Kwa nini asifungwe maisha?

Naamini pia hata watoto wake ikiwa wana utu tu wa mbaali kabisa, wanaishangaa hii hukumu na tamaa iliyopitiza kiwango!

Msiba anayo makosa makubwa na hahitaji kutetewa, lakini bilioni 9 kwa kosa hilo, ni tamaa ya mlipwaji na inamdhalilisha mlipwaji

J.mosi njema
wewe ni mke wa ngapi wa Musiba?
 
Wasiompenda JPM wanashangilia sana kwa sababu .Musiba anakomolewa kupitia sheria na Mahakama inaonekana imetemda haki. Lakini mahakama hiyo hiyo ikiamua dhidi ya wapinzani inaonekana imepokea maagizo na haiko huru.

Waziri mmoja wa zamani wakati anakata rufaa kupinga ushindi wa kesi ya mgombea binafsi katika uchaguzi alisema: Mahakama ni mtu kama mimi na wewe"
Lipumba baada ya uchagu,zi mkuu aliwahi kusema kuwa mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi Zanzibar alihongwa pesa na akanunua nyumba; yule mwenyekiti alienda mahakamani Lipumba alihukumiwa amlipe milioni 30; sasa ukilinganisha kiwango alichohukumiwa Musiba kulipa ni wazi japo hukumu inaheshimiwa lakini kuna hisia kukomolewa. Hivi Musiba hakukata rufaa au rufaa pia alishindwa? Sikuwahi kufuatilia hiyo kesi.

Tujiulize maswali mowili: Hivi JPM angekuwepo hiyo hukumu ingetoka jinsi ilivyo? Ingetekelezeka.?
1.Musiba hajawahi kukanyaga mahakamani, Kiburi tu, unataka mahakama ifanyeje?
 
Ungedaiwa wewe iyo 9B ungeona ni sawa? Mbona kila siku unamsema marehemu kwa kumdhalilisha lakin hujawahi daiwa chochote, lakin maneno ya msiba unayashadadia utadhani kafanya jinai ya kuua mtu, blood kabsaa
Umeishafua mashuka ya guest za Musiba??
 
Unajua thamani ya utu wa mtu?
By all means membe hana thamani ya kufikia bil 9. Sasa kama yeye mwenyewe in totality hana thamani hiyo, huko kudhalilishwa utu wake peke yake utafikaje bil 9?
Ukweli tu ni kwamba membe ametumia advantage ya kujuana na watu kwenye system ya mahakama ili kutaka alipwe kitita hicho kwa sababu ya uroho wa pesa au kutaka kumkomoa msiba. Membe ni tapeli tu kama matapeli wengine.
 
Wewe una akili zaidi ya mahakama iliyotoa hukumu Ile?! Kama madai ya Membe hayafanani na damages aliyopata ingemshauri vinginevyo.
Ni kitu gani kwa membe chenye kufikia thamani hata ya bil moja? Ebu nitajie. Unadhani membe mzima mzima angegongwa na gari akafa huyo dereva, hata angekuwa mwenye makosa, angehukumiwa kulipa hata zaidi ya mil 50?
Huyo hakimu au jaji aliyetoa hiyo hukumu inabidi aangaliwa kwa macho mawili, au kwa darubini ikiwezekana.
 
By all means membe hana thamani ya kufikia bil 9. Sasa kama yeye mwenyewe in totality hana thamani hiyo, huko kudhalilishwa utu wake peke yake utafikaje bil 9?
Ukweli tu ni kwamba membe ametumia advantage ya kujuana na watu kwenye system ya mahakama ili kutaka alipwe kitita hicho kwa sababu ya uroho wa pesa au kutaka kumkomoa msiba. Membe ni tapeli tu kama matapeli wengine.
Yeye ameona hiyo ndiyo thamani yake na Mahakama imeridhia. Wewe pia ukitukanwa ukaomba fidia ya shilingi moja kama Manji alivyoomba kutoka kwa Mengi napo ni sawa, si ndiyo uonavyokuwa hiyo ndiyo thamani yako?

watekaji nao wakikuteka wataomba walipww kulingana na vile watakavyo kuthaminisha wao kwa vipimo vyao na ndugu zako hawatabisha kwamba eti hauna thamani hiyo.

unapokata BIMA ya maisha kila kampuni inathaminisha kwa viwango vyake

Kuhusu kutumia advantage ya system mbona hamkusema hivyo wakati Musiba anatokana bila hofu ya kufanywa chochote kile na yeyote?
 
Manji alidai hiyo shilingi moja kwasababu Mengi akisema ukweli juu yake hivyo hiyo ndio ilikuwa thamani yake! Ndio maana ile kesi iliisha bila Manji kufuatilia tena Kwani angefuatilia angeshindwa na kulipa fedha nyingi!
MAjibu yako hayana pointi kabisa.

Kama Manji alijua kuwa, Mengi aliesema ukweli asimgekwenda, mahakamani. Pili hata kwa mtu asiye na elimu anajua wazi kuwa Manji ni mmoja wa matajiri wakubwa hapa nchini na hawezi kuwa na thamani ya shilingi moja. Manji alitaka tu ithibitike mahakamani kuwa amekashifiwa.

Kuondoa kesi mahakamani kunaweza kusababisbwa na sababu nyingi kama vile usuluhishi nje ya mahakama.

Mangi kutoendelea na kesi ilitokana na intervention toka nje ( mamlaka) kuwa wamalizane maana ilonekana kuwa mzozo kati yao ulianza kuwagawa watanzania kwa misingoi ya rangi na dini. Kama una kumbukumbu kuna waziri aliwapiga mqrufuku kulumbana hadharani.

Manji hakuogopa kuwa akishindwa atamlipa Mengi fidia; katika sheria hakuna kitu kama hicho; kilichopo ni kuwa ukimlazimisha mtu kwenda mahakamani kwa kumshtaki kwa kesi ya madai ukishindwa unamlipa gharama za kesi na kwa uwezo wa Manji asingeshindwa kumlipa gharama. Ukitaka kulipwa na mtu sharti umfungulie kesi ya madai. Nipe mfano mmoja tu wa mtu aliyewahi kushindwa kesi ya madai aliyomfungulia mtu mahakama i hafu automatically mahakama ikaagiza amlipe aliyemfungulia kesi ( ukiacha gharama za kesi).
 
Ni kitu gani kwa membe chenye kufikia thamani hata ya bil moja? Ebu nitajie. Unadhani membe mzima mzima angegongwa na gari akafa huyo dereva, hata angekuwa mwenye makosa, angehukumiwa kulipa hata zaidi ya mil 50?
Huyo hakimu au jaji aliyetoa hiyo hukumu inabidi aangaliwa kwa macho mawili, au kwa darubini ikiwezekana.
Wakati hicho kinachoitwa kashfa kikifanyika Membe alikuwa tayari ni mstaafu .na hakuathirika chochote kiajira wala kibiashara..

Hawa hawa wanaoshabikia sasa huko mbeleni ndio hawa hawa watakaokuja kulialia humu mwanasiasa wao akiwa cornered na mahakama.
 
Kumbuka kuwa mahakama itakupa tu kile ulichoomba na sio vyote. Hivyo, mahakam hakupi kitu kama hukuomba, mahesabu hufanywa kupitia vile ulivyoviomba na kujustfy.
Kwa hiyo chochote kile utakacho omba Mahakama itakupa!? Basi nazani na Mungu angekua Kama Mahakama naamini Dunia nzima wote tungekua tunaishi kwa rahaa sana, maana kila Mtu anataka Mambo mazuri na hakuna anaetaka shida!!
 
Sitetei chochote kuhusu yaliyojiri kumhusu mh Membe yakimhusisha mmiliki wa magazeti ya Tanzanite kumdhalilisha mh Membe kwa kumchafua, na sipangani na sheria yoyote ya nchi iliyotumika, ila naiona tamaa kubwa isiyo na mantiki kutoka kwa mh Bernard Membe ya kutaka ujira mkubwa usiolingana na kile wengi wanakiita ni kudhalilishwa

Hata tungelimshirikisha asiye na akili kuhusu madai hayo ya bilioni 9 kwa kosa tu la kuandikwa vibaya Mh Membe kwenye gazeti, nina hakika angelicheka kwa huzuni na mshangao, naamini, kila kitu Msiba atauza na pesa haitatosha, mwisho wa siku ni nini? Kwa nini asifungwe maisha?

Naamini pia hata watoto wake ikiwa wana utu tu wa mbaali kabisa, wanaishangaa hii hukumu na tamaa iliyopitiza kiwango!

Msiba anayo makosa makubwa na hahitaji kutetewa, lakini bilioni 9 kwa kosa hilo, ni tamaa ya mlipwaji na inamdhalilisha mlipwaji

J.mosi njema
Ww sema ni vile hujawahi kufedheheshwa na ndio vile unatetea upuuzi. Hata huyo magufuli wenu aliyekuwa amekaa kimya bila ya kumuonya musiba aache Undigili wake. Yeye magufuli kipindi alipokuwa waziri alifedheheshwa na Yusuf Manji. Na alipoupata U Rais akalipa kisasi Kwa Kumtaabisha Yusuf Manji. Hivyo Musiba anastahili.
 
Sitetei chochote kuhusu yaliyojiri kumhusu mh Membe yakimhusisha mmiliki wa magazeti ya Tanzanite kumdhalilisha mh Membe kwa kumchafua, na sipangani na sheria yoyote ya nchi iliyotumika, ila naiona tamaa kubwa isiyo na mantiki kutoka kwa mh Bernard Membe ya kutaka ujira mkubwa usiolingana na kile wengi wanakiita ni kudhalilishwa

Hata tungelimshirikisha asiye na akili kuhusu madai hayo ya bilioni 9 kwa kosa tu la kuandikwa vibaya Mh Membe kwenye gazeti, nina hakika angelicheka kwa huzuni na mshangao, naamini, kila kitu Msiba atauza na pesa haitatosha, mwisho wa siku ni nini? Kwa nini asifungwe maisha?

Naamini pia hata watoto wake ikiwa wana utu tu wa mbaali kabisa, wanaishangaa hii hukumu na tamaa iliyopitiza kiwango!

Msiba anayo makosa makubwa na hahitaji kutetewa, lakini bilioni 9 kwa kosa hilo, ni tamaa ya mlipwaji na inamdhalilisha mlipwaji

J.mosi njema
Hukumu alitoa Membe au Mahakama!!
 
Ukitupa mawe kwa Nyumba ya yenyee kioo,usifurahie tu kupasuka kwa Kioo.

Ipo siku mwenye Nyumba yake lazima akufanye mbaya.Tena mbaya ambayo wasiojua watasema kuwa kaonewa..kioo tu?

Tukiachana na siasa na mambo ya bongo.Kwa umri wa Musiba hakupaswa kuwa vile kipindi kile.
Huwezi tegemea watu wazima wakawa kama yeye nyakati zile.

Wacha tamaa ya Membe iwake juu yake.
 
Kama thamani yake ni sh bilioni tisa kwa nini asiwe nazo na anazitafuta kwa mtu mwingine?
Kwa taarifa yako binadamu wote wana thamani sawa .
Nasikia Membe alipeleka record za account zake za bank za ndani na Nje Kama ushahidi wa kuonyesha kua anamiliki zaidi ya hizo b9, nasikia ana Matilioni kibao, ndiyo maana Mahakama ikaona kumbe ka b9 ni Kama kapunje ka mchele kwa Membe, lakini Mahakama wakasahau upande wa musiba kua ka b9 siyo kitu kidogo Kama kwa Membe!!
 
Ni kitu gani kwa membe chenye kufikia thamani hata ya bil moja? Ebu nitajie. Unadhani membe mzima mzima angegongwa na gari akafa huyo dereva, hata angekuwa mwenye makosa, angehukumiwa kulipa hata zaidi ya mil 50?
Huyo hakimu au jaji aliyetoa hiyo hukumu inabidi aangaliwa kwa macho mawili, au kwa darubini ikiwezekana.
Wewe ulitaka alipwe kiasi gani na kwanini?!
Mmtukane kwa raha zenu halafu mumpangie kiasi cha kumlipa?! Pelekeni ujinga wenu huko.
 
Kuna wakati Manji alimshtaki marehemu Mengi kwa kumkashifu lakini akamdai Mengi Amlipe fidia ya shilingi moja, Je kwa uelewa wako thamani ya Bilionea Manji ni shilingi moja?
Hapa hawezi jibu zaidi atajificha kwenye kichaka cha mapungufu ya ki sheria!!
 
Back
Top Bottom