Makundi 4 ya Watanzania waliobaki Njiapanda baada ya Hotuba ya Rais Samia ya Aprili 22, 2021

Makundi 4 ya Watanzania waliobaki Njiapanda baada ya Hotuba ya Rais Samia ya Aprili 22, 2021

Nimekuelewa kote kasoro hapo kwenye timu Magufuli, hao watu ni wakina nani haswa? binafsi siamini kama wana exist.

Wanachama wa CCM wengi ni bendera fuata upepo, leo wote watacheza ngoma ya Samia kwasababu wanachotaka wao ni matumbo yao yajae, so yeyote atakayekuwa juu regardless ya tabia zake watamsapoti tu.

Next time akitokea Magufuli mwingine huko mbele ya safari nae atapata mashabiki wake vilevile, mwenyekiti wa chama chao ndie anashikilia hatma ya wengi wao hasa uwepo wa kule bungeni, lazima wajipendekeze kwake tu.
Team Magufuli wapo! Na bado wana nguvu sana kiasi cha mama kutumia dk za kutosha tu kwenye hotuba yake kuwaonesha yuko pamoja nao.

Kiongozi wao ni yule mtu muongo waliyempigia sana makofi ile jana.
 
4- Watanzania waliokimbia nchi ( exiled ).
hivi unaweza kusema lema kakimbia nchi kwa kuogopa nini alikuwa na impact gani kwa taifa mpaka akimbie huyo ni mhuni anataka sifa za kuitwa et mkimbizi wa kisiasa aseme alichokikimbia ni nini anamwogopa nani
 
hivi unaweza kusema lema kakimbia nchi kwa kuogopa nini alikuwa na impact gani kwa taifa mpaka akimbie huyo ni mhuni anataka sifa za kuitwa et mkimbizi wa kisiasa aseme alichokikimbia ni nini anamwogopa nani
Ukiachana na Lema, kuna matukio ya kutisha sana yametokea ndani ya taifa hili.

  • Azory Gwanda
  • Tundu Lissu
  • Ben Saanane
  • Lwajabe
  • Kanguye

Na waliokuwa wanawatishia maisha na kuwafanyia unyama mpaka leo wapo, na wana madaraka vile vile!
 
Fuatilia bunge ndio utajua.

Kuna wanasiasa wanahisi legacy ( hapa wana maana yale mazuri ya Magufuli ) inahujumiwa.

Na hili limekolezwa baada ya report ya CAG kutoka.
🤣 🤣 🤣 🤣 ni shida kubwa kuwabadili mawazo
 
CHADEMA wamejipinga kuunga mkono uzi,uzi wenyewe ni upupu tu! Ahahahahaha.
 
Lakini hotuba yake bungeni ndio huo uekekeo wa serikali yake.

Kwahiyo hakuna hotuba kubwa kuzidi hiyo.
Hivyo ndio inavyopaswa kuwa, lakini kwenye uhalisia ni tofauti kabisa. Hapa kwetu rais hutekeleza mambo yake kutokana na upepo, ukibadili tu mwelekeo, na yeye anabadilika.
 
Yeye alijua lazima atapitishwa tu, huyu hajiamini ndio maana kila wakati anaongelea swala la kuaminiwa

Kimsingi Magufuli hakuwa anategemea kura toka kwa yoyote, ili mradi ana madaraka basi. Kwake yeye madaraka ilikuwa kila kitu, tena kwa katiba mbovu kama hii, alikuwa anaweza kupanga atakacho bila kujali utaratibu ukoje.
 
Hotuba ninzuri tu, imejikita kuwahakikishia wananchi kwamba uchumi wa nchi utaendelea kukua hasa kwa kuhakikisha miradi yote mikubwa kama umeme, reli, usafiri wa anga, nk,nk,
Pia swala la amani nautulivu pia vitalindwa ipasavyo.

Binafsi naona hayoyote yatawezekana.

Wanao sema ccm niileile wakituliza vichwa wakaangalia utendaji wa Hayati Magu watagundua aliacha fundisho kwamba unaweza kuwa ndani ya ccm na bado unaweza ukafanya vizuri kwa kupambana na wahujumu uchumi hatakama ni makada vigogo.

Na Mama amesema maono na mipango aliokuwanayo Magu hajaendanayo imebakihapa na inafanyiwa kazi kasema moto niule ule.
Binafsi nimefurahi alipo toa onyo kwa wahujumu uchumi maana hawa miakayote ndio walikuwa wana turudisha nyuma.

Lat's keep on wait and see.
 
Fuatilia bunge ndio utajua.

Kuna wanasiasa wanahisi legacy ( hapa wana maana yale mazuri ya Magufuli ) inahujumiwa.

Na hili limekolezwa baada ya report ya CAG kutoka.
Wanapima upepo ili watege vizuri
 
Kuhusu 1. Hiyo ni system ambayo ni mwendelezo ili CCM iwepo madarakani, sioni kwa nini aongelee wakati naye najua wazi kuwa baada ya hii miaka mitano, atataka miaka 10 mingine ambayo ni yake, lazima ajizatiti aendeleze system ili CCM and the gang iendelee kutawala.
Atafanyaje hatujui.

Kuhusu 2. Private sector kaongelea kirefu sana pamoja na kilimo, mining, nk, lakini yote uongelewa, mambo yapo palepale, anayeongea ni CCM, Na CCM wanajulikana kwa nadharia, empty talk.
ni mpuuzi wa maisha tu ndie atakaye tegemea la maana kutoka CCM
 
Jambo la muhimu ni kwamba hofu na giza la awamu iliyopita havitakuwepo ila CCM ni ile ile
 
Hotuba ya Rais Samia hapo jana imeacha watu wengi nija panda. Binafsi naona kama ililenga zaidi kuyapooza makundi yaliyokuwa yanapiga kelele kama:
  • Vyama vya upinzani
  • Team Magufuli
  • Wafanyabiashara
Wananchi wengine kiukweli tumebaki njiapanda, maana hatujui ni upi uelekeo wa Rais hasa unapohusisha makundi yafuatayo:

( Ifahamike kuwa watanzania wengi hawana vyama na siyo wafuasi wa vyama vya siasa)

1- Waliodhulumiwa, kuteswa, kutekwa, kupotea na kuumizwa na awamu ya 5

Je, waliopoteza ndugu zao wakubali matokeo, wazike migomba tu mambo yaishe??

2- Vijana wasio na ajira (Jobless)

Hapa sina maana serikali inaweza kuajiri kila mtu, ila unaposhindwa kuajiri kabisa na wakati huo huo unataka kila kitu kifanywe na serikali hilo ni janga kubwa.

3- Wazee wa mafao na kikokotoo.

Hapa mwelekeo ni upi maana sheria ya kikotoo bado ipo?

Fao la kujitoa vipi?

4- Watanzania waliokimbia nchi ( exiled ).

Hawa hawana uhakika na usalama wao, maana waliowaumiza mpaka leo bado wapo wanadunda na hakuna jipya lolote.

Je, waendelee kubaki huko waliko au warudi nyumbani?

Ni nini mtazamo wako?
Binafsi yangu,,niko njia panda,,,ila ngoja tuone.
 
Hotuba ya Jana, Kwangu mimi haikuwa na mambo yanayotuhusu wananchi moja kwa moja bali mambo ya Kitaifa zaid yaani Kuzungumzia miradi mikubwa bila kuzungumzia mqmbo yanayowagusa wananchi moja kwa moja
Kwa akili yako miradi mikubwa kama bwawa la umeme halikugusi!!!?
au nyie ndio lile kundi ambalo mnaamini uongozi ukibadilika mtakuwa mnaokota pesa barabarani!!??
 
Hotuba ya Rais Samia hapo jana imeacha watu wengi nija panda. Binafsi naona kama ililenga zaidi kuyapooza makundi yaliyokuwa yanapiga kelele kama:
  • Vyama vya upinzani
  • Team Magufuli
  • Wafanyabiashara
Wananchi wengine kiukweli tumebaki njiapanda, maana hatujui ni upi uelekeo wa Rais hasa unapohusisha makundi yafuatayo:

( Ifahamike kuwa watanzania wengi hawana vyama na siyo wafuasi wa vyama vya siasa)

1- Waliodhulumiwa, kuteswa, kutekwa, kupotea na kuumizwa na awamu ya 5

Je, waliopoteza ndugu zao wakubali matokeo, wazike migomba tu mambo yaishe??

2- Vijana wasio na ajira (Jobless)

Hapa sina maana serikali inaweza kuajiri kila mtu, ila unaposhindwa kuajiri kabisa na wakati huo huo unataka kila kitu kifanywe na serikali hilo ni janga kubwa.

3- Wazee wa mafao na kikokotoo.

Hapa mwelekeo ni upi maana sheria ya kikotoo bado ipo?

Fao la kujitoa vipi?

4- Watanzania waliokimbia nchi ( exiled ).

Hawa hawana uhakika na usalama wao, maana waliowaumiza mpaka leo bado wapo wanadunda na hakuna jipya lolote.

Je, waendelee kubaki huko waliko au warudi nyumbani?

Ni nini mtazamo wako?
Moto unabaki uleule. Mgawanyiko, hasira na chuki.
 
Back
Top Bottom