Malalamiko ya Wananchi kuhusu mabadiliko na gharama za vifurushi yaliyofanywa na mtandao wa Tigo mwaka 2021

Malalamiko ya Wananchi kuhusu mabadiliko na gharama za vifurushi yaliyofanywa na mtandao wa Tigo mwaka 2021

Iko hivi, data ni anasa, huwezani nazo achana nazo sio unakuja kulia lia hapa.

Kama 3,000 ya data inakuliza, utaweza kweli kuhoji akili yangu mimi?
Kweli wewe punguwani. Data ni anasa? Dah! unahasara kinyama mkuu. Yaani hata hujui kuna watu wanafanya kazi kwa kutumia internet? Hakuna ofisi yeyote isiyotumia data.

Kuanzia kuwasiliana na wateja, kutafuta tender na mambo chungu nzima. Okay fanya hivi, kwa huo upeo wako nakuomba jiendeleze kielimu, unatia aibu.
 
Halotel 7GB kwa 5K wiki kupitia halopesa tunateleza.

Mnapenda kulalamika mtazani mmeshikiwa bunduki,kama mmeona gharama kubwa hamieni mitandao mengine.
 
Huu sasa ni upuuzi. Eti sasa hivi Tigo bei ya GB 1 kwa wiki ni TZS 3,000. Kabla ya hii bei ilikuwa GB 2 TZS 3,000. Kabla ya hapo ilikuwa kama sikosei GB1 ilikuwa 1,000. Yaani hawa jamaa kila siku wanazidi kushusha idadi ya gb na kupandisha bei. Serikali tunaomba muingilie kati hili swala.

Haya makampuni sasa yamegeuka kuwa ya kinyonyaji badala ya kuwa msaada kwa wananchi.
Nmetoa 1m hapa wamekata 8000....yaan elfu 8 ya fastaaa..huu ni unyonyaj
 
Nimeona niandike hili juu ya wizi wa kampuni ya (TIGO) kwenye vifurushi vyao, haijarishi ni kifurushi cha dakika au ni cha sms au internet,

Wamekuwa wakipandisha vifurushi vyao bila kujali hali halisi ya maisha tuliyonayo

Jana nimejaribu kununua kifurushi cha internet
ambacho nimezoea kununua cha Tsh 3000 gb 2 kwa wk

Nimekuta kimepunguzwa gb1 na kubakia gb 1 kwa tsh 3000 nimeshindwa kununua kifurushi hicho bado najiuliza nihamie kampuni gani yenye unafuu wa vifurushi tofauti na hawa wezi @tigo_tz

Screenshot_2021-01-28-13-41-29.jpg
 
Back
Top Bottom