Malezi Duni na Utandawazi ndio Chanzo cha ongezeko la mijadala ya kupinga na kukosoa ndoa na maisha ya ndoa

Malezi Duni na Utandawazi ndio Chanzo cha ongezeko la mijadala ya kupinga na kukosoa ndoa na maisha ya ndoa

Mkuu kama kwako wanawake wana nafasi kubwa sana katika maisha yako haimaanishi kila mwanaume ana wachukulia wanawake hivyo.

Soma sifa mbalimbali za makundi mbalimbali ya watu.
Hapana hawana nafasi kubwa kwangu bali wana nafasi yao kwangu hasa nikizingatia maandiko ya imani yangu ya kidini
 
Mkuu Mimi naona Maisha ya Mtu kukaa single bila Attachment na Mwanamke ni mazuri Sana

Kula vizuri
Lala vizuri
Sali Sana
Kataa ndoa
Tafuta pesa kwa ajili yako na wazazi na wasiojiweza huu mradi wa Ndoa unawafaidisha wanawake tu.
Mmoja wapo wa wazazi wako angefanya kama ulivyosema usingeandika haya
 
Kwanini niende umbali wote huu kisa tuu ndoa wakati naweza tuu nikapata mtoto na nikamlea vizuri bila hata hayo maisha ya ndoa.
Ingekuwa rahisi hivi, pata mtoto lea mwenyewe. Ila jua wapo wanaoteswa na hao watoto hasa wanapotaka kujua mzazi wake mwingine yupo wapi....utaficha wee ila utaumizwa na mtoto huyohuyo na jamii itaumizwa na mtoto huyohuyo tutasema hana maadili kwasababu alilelewa na mzazi mmoja.
 
Nilichogundua, migogoro ya ndoa siku hizi haihitaji ushauri wa wazee, kwani wazee wetu waliishi maisha yao tofauti na vijana wa sasa, wanatofautiana upendo, malezi, na vingine vingi.

Hivyo watu hao kuwapelekea migogoro ya ndoa leo, ni sawa na kutumia njia zilizopitwa na wakati kutibu tatizo jipya, muhimu vijana hawa hawa wa sasa ndio washauriane namna ya kumaliza matatizo yao ya ndoa, kwasababu wao ndio wanayaishi matatizo ya sasa.
Ndoa zinahitaji ushauri wa kisaikolojia zaidi kuliko wakati wote.
 
wanaume tunamuwakilisha Mungu duniani. sasa tuna declare kushindwa jukumu letu, ni aibu sana

Mwanzo 3:16​

Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.

Mwanzo 2:18​

BWANA Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
Asipokuwa na tamaa kwako huwezi kumtawala
 
Usipooa utaolewa.
Changamoto ni kwamba huwa hamna hoja za kutetea kuoa zaidi ya "negativity words" mmekosa hoja za kutetea ndoa imeishia kutukana.

Sasa sijajua kati ya watoa matusi na wapokea matusi nani ana upungufu wa akili.

Anyway, toeni tusi lolotee hata liwe jipya kiasi gani ila HATUOI.

#YNWA
 
Changamoto ni kwamba huwa hamna hoja za kutetea kuoa zaidi ya "negativity words" mmekosa hoja za kutetea ndoa imeishia kutukana.

Sasa sijajua kati ya watoa matusi na wapokea matusi nani ana upungufu wa akili.

Anyway, toeni tusi lolotee hata liwe jipya kiasi gani ila HATUOI.

#YNWA
Wapi nimekutukana rafiki?
 
Good morning Tanganyika!

Nimeshindwa kuvumilia baada ya kuona ongezeko la mada za kupinga kuoa, ndoa na maisha ya ndoa! Jamii Forums ni kama kioo cha Taifa kwasasa. Think tank kubwa ya nchi nathubutu kusema iko humu JF, sasa kitu kinapotrend sana Jamii forums ni lazima upate picha ya kinachoendelea nchini.

Hili ongezeko la mada za kupinga, kukosoa, kukejeli ndoa na maisha ya ndoa si jambo zuri hata kidogo bali ni msiba kwa taifa zima! Kuna sumu mbaya wamelishwa vijana wetu na imewaingia barabara!

~ Kukataa ndoa ni kukataa kujikubali.
~ Ni kukataa kujitambua.
~ Ni kukataa majukumu.
~ Ni kukosa malezi sahihi.
~ Ni kukosa akili.
~ Ni kukosa hekima.
~ Ni kwenda kinyume na maagizo ya Mwenyezi Mungu (kwa waamini).
~ Ni kukosa upendo upeo na maono!

Tunataka kuunda Taifa gani bila ndoa?
~ Ndoa ndio chanzo cha familia.
~ Ndoa ni dalili njema ya ukomavu wa akili.
~ Ndoa ni msingi wa uwajibikaji kujali, amani, furaha na upendo.
~ Ndoa ni future, bila ndoa future haina maana sana.

~ Makuzi yasiyo sahihi.
~ Wazazi wasiojitambua.
~ Wazazi wasio na muda wala ukaribu na familia zao.
~ Utandawazi.
~ Elimu potofu mitandaoni juu ya dhana nzima ya ndoa na maisha yake ni visababishi vikubwa mno vya matokeo hasi wanayopata vijana kuhusu ndoa na wao bila kujitambua huyafanya hayo kama ndio uhalisia na kuja na mada za kila aina.

Kama maandiko ya misahafu ya kiimani yanawaasa wanaume waishi na wanawake kwa akili, tafsiri yake ni kwamba mkataa ndoa hana akili ndio maana hawezi kuishi maisha ya ndoa.

Ukomavu wa kiakili, maono na hekima hukufanya uitamani ndoa ili kujipima. Uwezo wako wa kumudu maisha ya ndoa. Utayari wako wa kuhudumia ndoa. Ujasiri wako wa kuyakabili magumu ya ndoa nk, nk.

Ndoa ni kwa ajili ya wanaume kamili. Ndoa si kwa ajili ya wavulana!

Mjadala utaendelea.
Masingle madha wa kujitakia (sio hawa waliofiwa na waume zao) ni moja ya sababu kubwa na vijana wa hovyo kwenye taifa la tanzania na dunia kwa ujumla wake ambao ndio hawa kutwa kucha wanaimba mashairi na ngonjera za kukataa na kuponda mahusiano matakatifu ya ndoa.

If I were a president kijana yoyote anayeingia kwenye mahusiano pasipo kuonesha muelekeo wa kuoa au kuolewa cha moto angekiona.
 
Haya ni maneno alitakiwa ayaandike mdada aisee mwanaume unatakiwa uoe, uwe kichwa na uongoze familia
vinginevyo una fail ile mbaya

Kufeli unazungumzia kivipi..
Maana hapa Duniani tunaona wengi waliokimbia ndoa na wakafanikiwa...
Wakina diamond, dangote, na ma actor kibao hull duniani Hawana ndoa na Wana mafanikio makubwaa.

Unapozungumzia kufeli UNAMAANISHA NINI?

#YNWA
 
Back
Top Bottom