Malumbano kuhusu bandari na uwekezaji utakaofanywa na DP yametosha. Tufunge mjadala, tuchape kazi

Malumbano kuhusu bandari na uwekezaji utakaofanywa na DP yametosha. Tufunge mjadala, tuchape kazi

Tuchapeni kazi, serekali yetu sikivu imesikia inafanyia kazi kwa umakini mkubwa maoni yote. Tufunge sasa mjadala huu imetosha, tunachelewa sana kwa mijadala isiyokwisha na ambayo pengine inaweza kuhatarisha Utaifa na umoja wetu watanzania kwani hata maadui wa Taifa wanaweza kupitia mlango huu huu kuivuruga nchi yetu.

View attachment 2690681

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.
CCM ni sawa na bibi kizee ajuza anaeng'ang'ana kufanya biashara ya kujiuza barabarani. Imechoka mno haina mbele wala nyuma. Inashindwa nini kuweka wazi mpaka leo muda wa kuanza na kuisha makubaliano au mkataba wao wa uwekezaji na makubaliano yenyewe. Kama sio UFILAUNI ni nini?? Unadhani nani atamuamini mama samia hapo. Mbona magufuli aliweka wazi?



Kama hakuna uwazi, huu mkataba utabaki kuwa wa kifilauni na utapitishwa kifilauni kama ulivyopita bungeni. Tuache kusifia kila kitu, jambo lipo wazi hili kuwa kuna kitu kinafichwa hapo. Kama kweli CCM na bibi yao wanajiamini basi waweke hayo wazi halafu waone kama wananchi watapiga kelele
 
Soma article 22 ya mkataba.
Tushasoma, haya jibu hizi hoja..,

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
War with a ghost,wastage of time,NEC imeshapitisha, kila kitakachoimbwa is useless ......! (Kuonyeshwa kamkataba kamoja tu tena kiungwana imekuwa shida, ukionyeshwa wa gas nio watu watazimia na kufa)😁😁😁😁View attachment 2691592
Kwahiyo huu mkataba umesharekebishwa sio? Haya wekeni mkataba uliorekebisjwa na kusainiwa na DP world kwamba wamekubali hayo mabadiliko
 
Back
Top Bottom