Mama aliyedaiwa kufanya ukatili na video yake kusambaa mitandaoni akimpiga mtoto akamatwa

Mama aliyedaiwa kufanya ukatili na video yake kusambaa mitandaoni akimpiga mtoto akamatwa

Sio mwanae ni mtoto wake wa kambo mama yake alitofautiana na babaye kitambo
 
Huyu Mama kwa bahati mbaya camera imemnasa lakini haya ni mambo yanatokea kila siku kila mitaa na mabaya zaidi ya haya. Siungi mkono kumpiga mtoto kama unapiga mtu mkubwa ziko njia za kumuadhibu mtoto. Mimi sipigi mtoto lakini naogopwa nikimpiga jicho tu atakuja mwenyewe kuomba msamaha anajuwa hapa nimekosa. Sasa sio watoto wote sawa.

Huyu Mama utampa adhabu gani? labda yeye ndio mzazi bora kwa huyo mtoto na ukimfunga huyo mtoto ndio wa kwanza atamlilia Mama yake kwa uchungu, sio kila jambo kuchukulia kisiasa tu na kukaa na mzazi kumpa somo ajue njia sahihi za kumpa adhabu mtoto sio kumpeleka polisi ili iweje? afungwe? alipe fine, mazingira ya nyumbani tu unaona watu mradi kumekucha. Hawa kina Mama wana stress nyingi, hapo labda analea mtoto mdogo, huyu anamsumbua baba haeleweki kama yupo au single mama. Maisha haya yanachangamoto sana, sitaki watoto wapigwe kama watu wazima lakini pia kina Mama wengi wanapitia stress nyingi sana zinazoletwa na sisi wanaume. Hasira za mume zinaishia kwa mtoto.
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata Sabrina Shabani, mwenye umri wa miaka 28, mkazi wa Mbezi Mwisho, baada ya video kusambaa mitandaoni ikimuonesha akimshambulia mtoto mdogo. Tukio hilo limeibua masikitiko na hasira kwa umma, na uchunguzi wa awali ulifanywa kwa kushirikiana na Idara ya Ustawi wa Jamii.

Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani mara tu uchunguzi utakapokamilika. Jeshi la Polisi limewataka wananchi kujiepusha na vitendo vya ukatili, likionya kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wahalifu.
Taarifa ya Jeshi la Polisi

Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam linapenda kutoa taarifa kuhusiana na tukio la picha mjongeo (video) zilizoonekana kwenye mitandao ya kijamii zikionesha mwanamke mmoja akimshambulia mtoto mdogo kwenye eneo la makazi. Vitendo hivyo havikubaliki na kwa hali hiyo upelelezi wa awali ulifanyika kwa kushirikiana na idara ya ustawi wa jamii na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa Sabrina Shabani miaka 28 mkazi wa Mbezi mwisho Ubungo Dar es Salaam.
Pia, Soma:
+
Waziri Gwajima kukomesha ukatili baada ya video ya Mama akimshambulia mtoto kusambaa
+ House girl aliyemkata shingo mtoto wa mwajiri wake akamatwa na polisi
+ Kemeo la ukatili dhidi ya mtoto Malik Hashim Kitumbi
+ TLS Yalaani Vikali Udhalilishaji na Ukatili wa Kijinsia wa Binti kutoka Yombo Dovya, Dar es Salaam
hivi huyu mchukua video alikuwa wapi muda huo. If I may ask!
 
Wananchi walipaza sauti Heko kwao...viongozi waliochukua hatua...ndio kazi yao...mwezi huu wanakula mshahara kutoka kwaa wananchi walipa kodi kihalali.
Hongera sana waziri Gwajima na jeshi la polisi
 
Yeye anafundsha practical halafu yeye akikosea wamfundshe kwa theory??
Utawafunga wangapi. Shida ni hatuna elimu ya kifamilia, ukoo, jando jinsi ya kukuza watoto.

Kumbuka kwa miaka zaidi ya 3000 tulikuwa na system ndio maana upo unaandika hapa. Hizo systems zimeenda wapi? Angeweza kuita mjomba, Babu, jirani enzi zile. Sasa hivi yuko peke yake. Inanidi afanye ananyojua.
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata Sabrina Shabani, mwenye umri wa miaka 28, mkazi wa Mbezi Mwisho, baada ya video kusambaa mitandaoni ikimuonesha akimshambulia mtoto mdogo. Tukio hilo limeibua masikitiko na hasira kwa umma, na uchunguzi wa awali ulifanywa kwa kushirikiana na Idara ya Ustawi wa Jamii.

Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani mara tu uchunguzi utakapokamilika. Jeshi la Polisi limewataka wananchi kujiepusha na vitendo vya ukatili, likionya kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wahalifu.
Taarifa ya Jeshi la Polisi

Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam linapenda kutoa taarifa kuhusiana na tukio la picha mjongeo (video) zilizoonekana kwenye mitandao ya kijamii zikionesha mwanamke mmoja akimshambulia mtoto mdogo kwenye eneo la makazi. Vitendo hivyo havikubaliki na kwa hali hiyo upelelezi wa awali ulifanyika kwa kushirikiana na idara ya ustawi wa jamii na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa Sabrina Shabani miaka 28 mkazi wa Mbezi mwisho Ubungo Dar es Salaam.
Pia, Soma:
+
Waziri Gwajima kukomesha ukatili baada ya video ya Mama akimshambulia mtoto kusambaa
+ House girl aliyemkata shingo mtoto wa mwajiri wake akamatwa na polisi
+ Kemeo la ukatili dhidi ya mtoto Malik Hashim Kitumbi
+ TLS Yalaani Vikali Udhalilishaji na Ukatili wa Kijinsia wa Binti kutoka Yombo Dovya, Dar es Salaam
Huyu dada anatakiwa awe chini ya uangalizi wa ustawi wa jamii, anapokamatwa na kuwekwa mahabusu anayeathirika
zaidi ni mtoto, hata baada ya kupigwa mtoto hakuonfoka hapo nyumbani kwani hakuwa na mahali pa kwenda.
 
Niliona original post sikufungua kwasababu sipendi kuangalia ukatili. Ila leo nimesema ngoja nione. Hii video ndio yote au kuna kipigo kimefichwa? Hebu tuache utani. Huyo dogo ni bingwa wa kupiga yowe tu hakuna kipigo hapo. Au sio mama yake? Kama ni mtoto wa mwingine labda ila mwanae hio adhabu ya kawaida sana.
Kwa hiyo unaona ni sawa mtu mzima kumpiga mtoto mateke kwani hakuna njia nyingine ya kumpa punishment.
 
Niliona original post sikufungua kwasababu sipendi kuangalia ukatili. Ila leo nimesema ngoja nione. Hii video ndio yote au kuna kipigo kimefichwa? Hebu tuache utani. Huyo dogo ni bingwa wa kupiga yowe tu hakuna kipigo hapo. Au sio mama yake? Kama ni mtoto wa mwingine labda ila mwanae hio adhabu ya kawaida sana.
Mie niko nashangaa eti...
 
  • Thanks
Reactions: I M
Afande Muliro anaposema kitendo hicho hakikubaliki..... hakikubaliki na nani ????

Tunataka maafande wanasheria!
 
Hcho ndo kipigo chote ama Kuna chengine hakijaoneshwa mana hcho naona Cha kawaida , hajampiga kichwani Wala kumtoa damu
Ila watoto wa siku hizi tunawadekeza sana! Hicho hakiwezi kuitwa kipigo au kumshambulia mtoto. Ni cha kawaida sana kwa mtoto mtovu wa nidhamu. Kama huwa anampiga kila siku hiyo ni habari nyingine lakini kama ni pale anapokosea, ni kawaida sana!
 
Mtoto unampiga ngumi na mateke halafu unaona sawa tu! Tuchukulie ni mwanao yupo kwa mkeo mdogo ama kwa ndg yako yeyote uingie gafla ukute ananyukwa mangumi. Wewe unaangalia ngumi zinapanda na kushuka ushapiga hesabu ya force ya hizo ngumi?? Huna mtoto wewe hata kama unae basi humpendi na kumthamini kivile
Kuna ngumi hapo kweli? Huu sasa ni uchochezi. Mbona naona kama alikuwa anatumia kiganja kumpiga matakoni? Kitu ambacho ni kawaida sana na mama huyo amekuwa mwangalifu hajampiga makofi kichwani! Jamani watu tumepigwa ati! Hicho cha kawaida mno ukilinganisha na enzi zile!
 
  • Thanks
Reactions: I M
Back
Top Bottom