Mama aliyedaiwa kufanya ukatili na video yake kusambaa mitandaoni akimpiga mtoto akamatwa

Mama aliyedaiwa kufanya ukatili na video yake kusambaa mitandaoni akimpiga mtoto akamatwa

Ila watoto wa siku hizi tunawadekeza sana! Hicho hakiwezi kuitwa kipigo au kumshambulia mtoto. Ni cha kawaida sana kwa mtoto mtovu wa nidhamu. Kama huwa anampiga kila siku hiyo ni habari nyingine lakini kama ni pale anapokosea, ni kawaida sana!
Utawaweza baba na mama junior? Ndio hao wanaona huyo mtoto kapigwa sana yaani angeweza kufa.
 
Watu wanashadadia upuuzi sana.

Mtoto kapewa adhabu ya kawaida sana.

Huwezi kumlea mtoto bila adhabu. Utavuna mabua.

Mtoto hufundishwa akiwa mdogo, utii, nidhamu na uwajibikaji hayaji tu hivi hivi. Awe mama yake au sio mama yake mzazi binafsi sijaona ukatili hapo. Tena kampiga vibao vinne tu kama sijakosea.

Kwa malezi ya online, no wonder watoto wanatukana wazazi wao mitandaoni huko, watoto hawali mpaka uwawekee cortoon zao pendwa, watoto wawatuma hadi dada wa kazi 😂😂
 
Wananchi walipaza sauti Heko kwao...viongozi waliochukua hatua...ndio kazi yao...mwezi huu wanakula mshahara kutoka kwaa wananchi walipa kodi kihalali.
Yaani upige mwanangu kiasi hiki nikuache salama?
Labda sio mimi
 
Utawaweza baba na mama junior? Ndio hao wanaona huyo mtoto kapigwa sana yaani angeweza kufa.
Ukiona mtoto amefikia hatua ya kutosikia ujue chanzo kikuu ni mzazi.
Siku hizi watoto hawana malezi bora na kipigo cha namna hiyo hakisaidii
 
Watu wanashadadia upuuzi sana.

Mtoto kapewa adhabu ya kawaida sana.

Huwezi kumlea mtoto bila adhabu. Utavuna mabua.
Ni ujinga tu kupiga watoto. Ninao wanne wa kwanza 18 wa mwisho 11 sijawahi wapiga hata siku moja na wote wana tabia njema. Tena mitoto inayo pigwa pigwa ndio inakua minunda na katili.
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata Sabrina Shabani, mwenye umri wa miaka 28, mkazi wa Mbezi Mwisho, baada ya video kusambaa mitandaoni ikimuonesha akimshambulia mtoto mdogo. Tukio hilo limeibua masikitiko na hasira kwa umma, na uchunguzi wa awali ulifanywa kwa kushirikiana na Idara ya Ustawi wa Jamii.

Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani mara tu uchunguzi utakapokamilika. Jeshi la Polisi limewataka wananchi kujiepusha na vitendo vya ukatili, likionya kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wahalifu.
Taarifa ya Jeshi la Polisi

Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam linapenda kutoa taarifa kuhusiana na tukio la picha mjongeo (video) zilizoonekana kwenye mitandao ya kijamii zikionesha mwanamke mmoja akimshambulia mtoto mdogo kwenye eneo la makazi. Vitendo hivyo havikubaliki na kwa hali hiyo upelelezi wa awali ulifanyika kwa kushirikiana na idara ya ustawi wa jamii na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa Sabrina Shabani miaka 28 mkazi wa Mbezi mwisho Ubungo Dar es Salaam.
Pia, Soma:
+
Waziri Gwajima kukomesha ukatili baada ya video ya Mama akimshambulia mtoto kusambaa
+ House girl aliyemkata shingo mtoto wa mwajiri wake akamatwa na polisi
+ Kemeo la ukatili dhidi ya mtoto Malik Hashim Kitumbi
+ TLS Yalaani Vikali Udhalilishaji na Ukatili wa Kijinsia wa Binti kutoka Yombo Dovya, Dar es Salaam

Shida ipo kwenye Mimba za utotoni na umasikini. . Unakuta mama katelekezwa na mwanaume haudumii ndo maana unakuta vitendo hivyo vinatokea . Afya ya akili ni muhimu unamkuta mama kajaa tu hasira anachukua maamuzi ya kumpiga mtoto kiasi hicho. Sizani kama familia inapata basic needs kama chakula, maradhi na mavazi pia mama ana hudumiwa ipasavyo hali hio ingetokea. Pia afya ya akili ni muhimu ( huenda huyo mama ana tatizo)


Serikali ingewasaidia kwa kuwapa fedha ili wawe stable kimaisha waondoe Umaskini ndo maaa kero hizo za unyanyasaji kwa watoto zinaendelea kutokea, kumkamataa sio kumaliza tatizo. Tatizo n umasikini na hali ya maisha. Mfikishieni waziri anaehusika.......
 
Bila kupepesa macho nilikuja mbio nikitegemea ntaona ukatili wa hali ya juu na nilipoona yale madumu nikawaza hii video ikiendelea huyu mama atampiga na madumu huyu dogo kumbe duuuh hebu tuwe serious hivi vipigo tulivyopewa na wazee wetu si zaidi ya hivyo hapo jamani
 
Mtoto hufundishwa akiwa mdogo, utii, nidhamu na uwajibikaji hayaji tu hivi hivi. Awe mama yake au sio mama yake mzazi binafsi sijaona ukatili hapo. Tena kampiga vibao vinne tu kama sijakosea.

Kwa malezi ya online, no wonder watoto wanatukana wazazi wao mitandaoni huko, watoto hawali mpaka uwawekee cortoon zao pendwa, watoto wawatuma hadi dada wa kazi 😂😂

Huu ndiyo ujinga wa wazazi wa tamthilia. Wajinga sana!
 
  • Thanks
Reactions: I M
Bila kupepesa macho nilikuja mbio nikitegemea ntaona ukatili wa hali ya juu na nilipoona yale madumu nikawaza hii video ikiendelea huyu mama atampiga na madumu huyu dogo kumbe duuuh hebu tuwe serious hivi vipigo tulivyopewa na wazee wetu si zaidi ya hivyo hapo jamani

Maisha haya ninawaza hadi ninajikuta ninajiuliza hivi kama siyo adhabu na kichapo ningekuwa wapi?

Huwa ninawasikitikia watoto waliodekezwa enzi zetu aisee wamekuwa watu wa hovyo.
 
Ni ujinga tu kupiga watoto. Ninao wanne wa kwanza 18 wa mwisho 11 sijawahi wapiga hata siku moja na wote wana tabia njema. Tena mitoto inayo pigwa pigwa ndio inakua minunda na katili.

😄 Umri wa 18 years bado ni mtegemezi na yupo kwako na bado hujamaliza malezi.

Kawaida tabia halisi ya mtoto ni namna anavyohusiana na jamii ya watu baki haswa akianza kujitegemea.

Wazazi wengi mkiambiwa tabia za wanenu mnakataa na kuwatetetea.

Kudekeza mtoto siyo malezi.
 
Ukiona mtoto amefikia hatua ya kutosikia ujue chanzo kikuu ni mzazi.
Siku hizi watoto hawana malezi bora na kipigo cha namna hiyo hakisaidii
Wewe mbona kipigo kilikusaidia? Watoto wasiosikia mara moja moja unamtandika. Mbona wengi wananyooka tu.
 
Ni ujinga tu kupiga watoto. Ninao wanne wa kwanza 18 wa mwisho 11 sijawahi wapiga hata siku moja na wote wana tabia njema. Tena mitoto inayo pigwa pigwa ndio inakua minunda na katili.
Kuna wazazi siku wanaambiwa watoto wao ni majambazi huwa hawaamini. Hongera kwa kukuza raia wema.
 
Back
Top Bottom