MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,018
- 16,802
Kwa mara ya Kwanza kabisa baada tu ya Kutua Mkoani Dodoma ( Makao Makuu ya Nchi ) ameonekana akiwa amevalia Barakoa na pia akiwa hataki kabisa Kupeana ( Kushirikiana ) Mikono na Watu.
Maswali yangu ni kama yafuatayo..
1. Kwanini Mumewe ( Hayati Rais Dkt. Magufuli ) alipokuwa Hai alikuwa havai Barakoa?
2. Je, Kuvaa Kwake Barakoa Leo anajaribu kutuma Ujumbe gani uliofichika Kwetu Watanzania ambao pengine Kimoyomoyo anatuonea mno Huruma pamoja na Kufurika Kwetu Viwanjani na Barabarani pembezoni?
3. Je, kuna Uwezekano mkubwa kuwa labda Mumewe alipokuwa Hai alikuwa akimshauri avae Barakoa na akawa hapewi Ushirikiano nae na hata Yeye ( Mama Janet ) Kuamriwa kutovaa Barakoa?
4. Je, ni kwanini muda wote alipokuwa Dar es Salaam tena katika Msongamano mkubwa wa Watu ( Waombolezaji ) hakuvaa Barakoa ila amefika tu Dodoma Jioni hii amevalia?
5. Je, kwa Kitendo cha Yeye ( Mama Janet Magufuli ) Mke wa Marehemu Hayati Rais Dkt. Magufuli kuonekana kwa mara ya Kwanza Kavalia Barakoa Uwanja wa Ndege Dodoma ikihisiwa kuwa huenda Dodoma Maambukizi ya Corona ni makubwa sana ila tunafichwa tu tutakuwa tunakosea?
6. Je, kwa Muonekano wa Kimasikitiko ( japo tunajua ana Majonzi makubwa ) siyo kwamba Mama wa Watu pengine ana Maumivu makubwa ya Uzembe juu ya Kupuuzwa kwa Janga la Corona nchini Tanzania?
7. Je, kwa mfano ( nasisitiza tena mfano ) ikitokea labda Mumewe ( sasa Marehemu Rais Dkt. Magufuli ) angefufuka kwa bahati mbaya tu au nzuri Mkewe Mama Janet Magufuli hiyo Barakoa angeitupa kwa Uwoga kwakuwa Mumewe alipinga sana Uvaaji wa Barakoa na hakuwahi Kuvaa au angeificha katika Pochi au angempa Mtu amshikie au ajifanye ni yake?
Mwisho nasema tu tujikinge na Corona.
Imeisha hiyo!!!
Maswali yangu ni kama yafuatayo..
1. Kwanini Mumewe ( Hayati Rais Dkt. Magufuli ) alipokuwa Hai alikuwa havai Barakoa?
2. Je, Kuvaa Kwake Barakoa Leo anajaribu kutuma Ujumbe gani uliofichika Kwetu Watanzania ambao pengine Kimoyomoyo anatuonea mno Huruma pamoja na Kufurika Kwetu Viwanjani na Barabarani pembezoni?
3. Je, kuna Uwezekano mkubwa kuwa labda Mumewe alipokuwa Hai alikuwa akimshauri avae Barakoa na akawa hapewi Ushirikiano nae na hata Yeye ( Mama Janet ) Kuamriwa kutovaa Barakoa?
4. Je, ni kwanini muda wote alipokuwa Dar es Salaam tena katika Msongamano mkubwa wa Watu ( Waombolezaji ) hakuvaa Barakoa ila amefika tu Dodoma Jioni hii amevalia?
5. Je, kwa Kitendo cha Yeye ( Mama Janet Magufuli ) Mke wa Marehemu Hayati Rais Dkt. Magufuli kuonekana kwa mara ya Kwanza Kavalia Barakoa Uwanja wa Ndege Dodoma ikihisiwa kuwa huenda Dodoma Maambukizi ya Corona ni makubwa sana ila tunafichwa tu tutakuwa tunakosea?
6. Je, kwa Muonekano wa Kimasikitiko ( japo tunajua ana Majonzi makubwa ) siyo kwamba Mama wa Watu pengine ana Maumivu makubwa ya Uzembe juu ya Kupuuzwa kwa Janga la Corona nchini Tanzania?
7. Je, kwa mfano ( nasisitiza tena mfano ) ikitokea labda Mumewe ( sasa Marehemu Rais Dkt. Magufuli ) angefufuka kwa bahati mbaya tu au nzuri Mkewe Mama Janet Magufuli hiyo Barakoa angeitupa kwa Uwoga kwakuwa Mumewe alipinga sana Uvaaji wa Barakoa na hakuwahi Kuvaa au angeificha katika Pochi au angempa Mtu amshikie au ajifanye ni yake?
Mwisho nasema tu tujikinge na Corona.
Imeisha hiyo!!!