Mama Janeth Magufuli awasili Dodoma akiwa amevaa Barakoa...

Kule Twitter Mkuu watu wanamshauri sana kuhusu umuhimu wa kuvaa barakoa lakini naona katia pamba masikioni. Tunaumia kwa dharau zisizo na kichwa wala miguu.
Labda nae Ikulu imeshamchosha na anataka kwenda Kaburini huko Kwao Unguja Kisiwani Zanzibar Ndugu. We muache tu afanye Masihara na Corona wakati mfano ulio dhahiri ameshauona.
 
Kwani kuna watu wamekatazwa kuvaa barakoa katika hii nchi? Suala la kujikinga wewe kwanini ulazimishe na wengine? Hilo ni gubu,
Unaacha kuwaza ya kukupa ugali unawaza kwanini Mama Janeth kavaa barakoa!
 
Ndege unapanda na barakoa. Namuonea huruma sana Mama Janeth. Lets hope hatasahaulika. Maana msiba huu umekuwa mzito sana kwake
 
Kwa msongamano huu tutarajie yasiyotarajiwa baada ya muda kidogo
Kuna mahala nasikia hapa hapa Afrika tulipo Corona + Parkison na Corona + Ageing ama imelaza Watu Hoi ( Mahututi ) au imeshafyeka Mmoja au Wote wawili. Naendelea Kusisitiza barani Afrika sasa Wewe jifanye una Kiherehere chako halafu uhisi unavyojua Wewe.

Imeisha hiyo!!
 
Acha upumbavu nini kimekushangaza yeye kuvaa barakos???!.
 
Ushabiki wa kijinga katika siasa ni ushamba na kujibebesha chuki ambazo zitakusabsbishia usione uzuri wa jambo hata kama jema. Mkuu achana na kuweka ukakasi kila jambo kutia watu ubaya huko mbinguni mtaenda kuulizwa mlitumia vipi akili zenu?
Tafadhali tusipangiane cha Kuandika JF.
 
Kwani kuna watu wamekatazwa kuvaa barakoa katika hii nchi? Suala la kujikinga wewe kwanini ulazimishe na wengine? Hilo ni gubu,
Unaacha kuwaza ya kukupa ugali unawaza kwanini Mama Janeth kavaa barakoa!
Jitahidi sana upunguze Upumbavu unaokusumbua.
 
Tena amechelewa sana kuchukua hizo hatua
Kuna nyepe nyepe ( tetesi ) zinasema karibia 85% ya Staff wa Majumba Meupe ya Magogoni na Chamwino Wameikaribisha Corona kwa Mikono yao yote Miwili na kwamba kila Mmoja itamlaza kwa muda wake au vile itakavyopenda yenyewe.
 
Tutashuhudia MaRais wakiapishwa Hadi tuchoke. Jiwe aliekuwa ngangari anapiga kazi mpaka saa 8 usiku kazimika kama mshumaa,acha walete utani na corona.
Natamani sana Rais Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan aisome hii post yako Ndugu huko ( pale ) Chamwino aliko sasa kabla Walinzi wake hawajamruhusu kwenda Chumbani Kuyajenga zaidi na Mumewe First Gentleman Mr. Ameir.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…