1.
Hizi bado ni allegations bwana mkubwa ni makosa makubwa sana kwa mzee mzima kama wewe kukaa mbele ya keyboard yako na kuropoka maneneo kama haya. Read out loud to yourself what you just wrote and hear how you sound. This kind of conclusion suggests that you are so blinded by prejudice that you can't see things straight.
Zingekuwa bado ni allegations basi msaidizi wake ambaye ni mke wa mtoto wake asingerudi nyumbani mkuu kukimbia uchunguzi , ambao umeshakamilika na waliomchunguza SADC na KGM, wasingeshauri Mama aondolewe na hata kum-brief rais wetu kule Adis, Katibu wa bunge la Tanzania, amesema kuwa Mama Mongella anatakiwa kulipwa na bunge la Tanzania, sasa ilikuwaje akaenda kudai alipwe kule Adis kwa kazi hiyo hiyo aliyokwisha lipwa na bunge letu? Na kasema kuwa tayari ameshaletewa repoti ya huo uchunguzi, mama anaombwa kusema hataki kwa nini na yeye siku zote ni bingwa wa kusema Beijing?
Sasa exactly what is your point eti hizi bado ni allegations? Wakati mashirika mawili independent yaliyomchunguza yamesha shauri aondolewe, na msaidizi ameshakimbia tayari, unasema ni allegations? Hivi ni kweli ninasoma sawa sawa or what eti hizi ni allegations? Allegations wakati tayari head of state wetu ameshafahamishwa? Mkuu unajua maana ya diplomatic relations? huwezi mwambia rais wa nchi au head of state kuwa kuna allegations kuhusu mwanachi wake, unamfahamisha kuwa kuna kesi, unamuonyesha uchunguzi na hukumu, kama rais wetu alivyofahamishwa, hakuna majungu wala blindness hapo ni mama kuondoka tu kama mke wa mtoto wake alivyotangulia kwa kusoma alama za nyakati mapema!
2.
Facts gani tena unahitaji wewe? Do you really need facts or you just want an interminable 20 pages debate wakati umeisha hukumu wenzako?
Mama Mongella, amehukumiwa na SADC na KGM ya Kenya mkuu, na mimi kama mbongo ni wajibu wangu kusema maoni yangu kama Mtanzania niliyeabika kwa vitendo viovu alivyovifanya Mama, it is a shame na haiteteeki kabisa mkuu, kwa kifupi ni aibu n I have nothing to do with it just deal with facts kuwa mama ni mwizi na mndugunization, waliosema ni AU, kwa kushauriwa na SADc na KGM, na wamemfahamisha rais wetu, sio mimi mkuu ni just facts hizo! Kama ni ndugu yako I do not care mkuu hapa hatuangalii uso wa kiongozi hapa ni mawe tu!
3. [
B]You even went as far as using your little scare tactics of PhD. [/B]
Malecela, ana PHD, watoto wake wawili wanazo PHDs, Watoto wake wawili wana Masters, na mmoja ana BA, hizi ni facts mkuu sio opinion zangu, sasa exactly what is your problem kwamba hao wazungu waliwapa tu hizo PHDs kwa sababu ni Malecela? is that so? Scare tactits kama watoto na baba wasingekluwa nazo hizo PHDs, lakini wanazo sasa inakuwaje scare tactics? Scare tactics ni pale unaposema una picha za rais akiwa uchi wakati huna mkuu!
4.
Pamoja na vimatusi vyako vya rejareja vya fitina na majungu wakati wewe ndiye unaongoza kwa fitina na majungu.
Sijawahi kuweka matusi ya reja reja huwa ninaweka vitu straight ninachosema na siku zote ninaeleweka hapa, off course ninaongoza kwa fitina na majungu kwa sababu siku zote ninaweka nyeti za mfisadi ambazo wewe huwezi kuzipata, kwa hiyo ni lazima ziwe majungu kwako na fitina, kama hukulalamika Rosemary Nyerere kuwa mbunge na kaka yake Makongoro kuwa mbunge at the same time kuwa inakuletea conflict of interest, lakini ukaona kwenye Malecela tu ndio problem kwako basi hiyo ndio fitina yenyewe na majungu mkuu!
5.
Ni kinyume na maadili kuajiri wanafamilia moja kwenye kituo kimoja cha kazi. You don't have to be an Einstein to know this.
Tanzania hatujawahi kuwa na haya maadili, Mwalimu alikuwa mwenyekiti wa TANU mdogo wake Joseph Nyerere alikuwa Mwenyekiti wa Umoja wa vijana Wa TANU, yaani TANU Youth League, Bomani akawa waziri mdogo wake Mark akawa AG, Malecela akawa waziri Kaka yake Lusinde akawa Waziri pia, Mwapachu akawa waziri mdogo wake Juma Mwapachu akawa Balozi na sasa ni katibu wa EAC, leo Radhia ni Director Foreign, dada yake ni katibu mkuu wa wizara, Mama Migiro alikuwa waziri wa nje, mdogo wake Radhia akawa HOC London, je ni yeye Mama Migiro aliyempa huo u-HOC? Mkuu Tanzania hatuna hiyo sheria ya maadili ya ndugu au wananchi wa familia moja kufanya kazi pamoja, unless sasa ipo kwa sababu tu ya Malecela, taht is a joke tena a big one mkuu!
6.
Balozi Maharage ana ndugu yake pale Foreign alikuwa anatumia jina la Maharage. Maharage mdogo alipoajiriwa Foreign, yeye albadili jina kuepuka masuala ya maadili.
Tanzania hauna haya maadili mkuu, huyo Maharage kama ni kwei aliamua kubadili jina mwenyewe tu kwa kutokujiamini, maana basi Karumes wangekua wa kwanza kubadili majina mkuu, wakifuatiwa na Mtengetis, halafu Mwapachus, Cheyos, sasa hawa mbona hawajabadili majina ili wa-fit hayo maadili yako mkuuu na kina Maharage?
7.
Kwani huyo Malecela wa India mpaka aje UN? Si angepelekwa kituo kingine?
Mkuu haya maswali yanahitaji kupelekwa foreign, ambako kuna pannel inayoamua nani aajiriwe na nani aende wapi, we do not do that hapa JF, na mimi binafsi I have nothing to do with it, ninachojua ni kuwa msichana ni mwanasheria tena wa kuaminika sana mkuu, maana huwezi pewa kile kituo cha UN bila kichwa haijawahi kutokea, tena ukafanye kazi na Dr. Mahiga, duh!
8.
Wakati wowote familia ya Malecela inapotajwa unakimbilia fitina na majungu. Vilevile, kuwajua kwako ndugu wengi walioajiriwa kitengo kimoja ambayo ni kinyume cha maadali does not justfy the fact that watu wamekiuka maadili na tuendelee kukiuka maadili.
Ninasema kuwa ni majungu kwa sababu mopja muhimu, nayo ni kwamba sijawahi kusikia Malecela akituhumiwa na shutuma mpya, zaidi ya zile zilizoanzishwa na Mwalimu, in 85, na 95, so far sijawahi kusikia anything new, halafu ninasema ni majungu na fitina kwa sababu siku zote huwa hakuna ukweli, mkuu tafuta hotuba ya Kikwete siku Malecela alipostaafu rasmi, jinsi alivyomtukana Mkapa mbele ya uso wake na Mwalimu, na alisema haya haya ninayoyasema kuwa ni "......majungu na fitina, ndiyo yamesababisha tumchukie Malecela tena hasa sisi viongozi wa juu wa CCM, wananchi hawana kosa ila sisi viongozi wa juu kuanzia wa zamani mpaka wa sasa, na hasa waliostaafu....." Mkuu haya maneno yalisemwa na Rais wa Jamhuri yetu, sasa je na yeye ni kama mimi ambaye kazi yangu kukimbilia kusema majungu na fitina, hebu jaribu kujitokeza na something new against Malecela, just for a change, lakini kusema ninatumia scare tactics kwa kusema ukweli kwamba Malecela na watoto wake wanazo PHDs, Masters, na BA, wakati viongozi wengi wanaomchukia hawana na watoto wao hawana, basi ninakubali kuwa unasema ukweli mkuu!
Ndio maana hiyo hatuba hujawahi kuiona hata siku moja kwenye media zetu, maana ni too much kwa watu ambao wamekuwa wakimtukana mzee bila sababu just necause Mwalimu alisema, lakini ninaifanyia kazi itaanza kupatikana siku za karibuni sana mkuu, mambo siku hizi ni hadharani, si unajua ingekuwa zamaani haya ya Mama Mongella yangezimwa tusingeyasikia mkuu, ila ni aibu kwa taifa letu, Malecela amefanya kazi UN akiwa na in his 20s, akahamia OAU yaanai AU ya sasa akiwa in his 20s na 30s, akahamia EAC akliwa in his 30s, akawa foreign minister wetu wa kwanza akiwa in his 40s, mbona hatukuwahi kusikia kuwa ni mwizi, au mndugunization? sasa WHY Mama Mongelal, tena now?
9.
Hii ni sawasawa na umekamatwa kwa wizi halafu unasema aaah, hata John ni mwizi na ninawajua wezi wengi tu. This is very stupid argument Mr. FM.
Mkuu kwenye ukweli uongo hujitenga, nafikiri nimesema ya kutosha kuhusiana ukweli wa ishu, sasa labda niwaachie wananchi waamue! Ila stupid argument huwa sio tabia yangu, na kama ingekuwa nisingekuwa FMES. Na sina apologies kabisa kama Mama Mongella anakuhusu mkuu.
Ahsante Mkuu!