Mama mwenye hali ngumu anakaa na binti mdogo mjamzito ambaye sio ndugu yake

Mama mwenye hali ngumu anakaa na binti mdogo mjamzito ambaye sio ndugu yake

Mambo vp wadau??

Ninaomba radhi kwa uandishi m-bovu.

Kuna mama mmoja yeye ni mzaramo. Ni mama mkaanga Samaki amepanga chumba na sebule huku mtaani kwetu (Kodi Jumla 30,000/= kwa mwezi). Huyu mama muwewe alifariki kama mwaka na nusu hivi umepita. Sasa kulikuwa na Binti mmoja alibeba ujauzito hapa mtaani, huyo Binti hana baba wala mama (umri kama miaka 16 au 17 hivi).

Huyu Binti ni Mnyakyusa wa Mbeya wazazi wake wote walifariki katika vipindi tofauti tofauti ila wa mwisho kufa alikuwa ni mama yake mzazi.

Sasa cha kushangaza huyu mama muuza Samaki, ambaye anaishi maisha magumu mno (faida ya Samaki labda ni 10,000 tu kwa siku) ameamua kumchukua huyu binti anakaa naye hapo alipopanga ilhali hana hata undugu naye.

Wanapika, wanakula, jioni wanaenda kuuza Samaki zao za kukaanga barabarani, huyu dada akiwa na tumbo la ujauzito.

Hii roho ya huyu mama mkaanga dagaa mpaka ninaogopa kwa maana katika hali ya kawaida watu wengi wenye vipato vidogo wanaogopa mizigo zaidi, lakini huyu mama kamchukua huyu Binti anakaa naye kama vile ndugu yake. Hivi wakuu, roho kama hizi huwa mtu anazaliwa nazo au inakuwaje??

Watu wa Pwani (Wazaramo, Wandengereko,n.k) Mwenyezi Mungu awabariki sana.

NB: Mimi ni kabila la mkoa wa Mara na sio mtu wa Pwani.
ukiona kabeba mimba kajipanga
 
Mambo vp wadau??

Ninaomba radhi kwa uandishi m-bovu.

Kuna mama mmoja yeye ni mzaramo. Ni mama mkaanga Samaki amepanga chumba na sebule huku mtaani kwetu (Kodi Jumla 30,000/= kwa mwezi). Huyu mama muwewe alifariki kama mwaka na nusu hivi umepita. Sasa kulikuwa na Binti mmoja alibeba ujauzito hapa mtaani, huyo Binti hana baba wala mama (umri kama miaka 16 au 17 hivi).

Huyu Binti ni Mnyakyusa wa Mbeya wazazi wake wote walifariki katika vipindi tofauti tofauti ila wa mwisho kufa alikuwa ni mama yake mzazi.

Sasa cha kushangaza huyu mama muuza Samaki, ambaye anaishi maisha magumu mno (faida ya Samaki labda ni 10,000 tu kwa siku) ameamua kumchukua huyu binti anakaa naye hapo alipopanga ilhali hana hata undugu naye.

Wanapika, wanakula, jioni wanaenda kuuza Samaki zao za kukaanga barabarani, huyu dada akiwa na tumbo la ujauzito.

Hii roho ya huyu mama mkaanga dagaa mpaka ninaogopa kwa maana katika hali ya kawaida watu wengi wenye vipato vidogo wanaogopa mizigo zaidi, lakini huyu mama kamchukua huyu Binti anakaa naye kama vile ndugu yake. Hivi wakuu, roho kama hizi huwa mtu anazaliwa nazo au inakuwaje??

Watu wa Pwani (Wazaramo, Wandengereko,n.k) Mwenyezi Mungu awabariki sana.

NB: Mimi ni kabila la mkoa wa Mara na sio mtu wa Pwani.
Kweli tumetofautiana,wengine furaha wanaipata kwenye kusaidia wengine.
Mungu ambariki sana
 
Lakini wapemba hawana roho nzuri hata kidogo
Mtazame Hayati Maalim Seif au Rais Mstaafu Dr. SheIn, Dr. Hussein Mwinyi.

Wapemba wengi (almost 90%) ni watu waungwana sana.

NB: Sifanyi uchawa ili kupata favor au pesa, I'm talking the real thing.
 
Wakalim wako kila mahali wabaya wapo kila. Wakalim wapo kila kabila wabaya wapo kila kabila. Pongezi Kwa mama wa kizalamo respect mungu amzidishie
 
Wakati nakuwa nilikuwa nashangaa sana tabia kama hiyo ya mama yangu Mzaramo na kipato chake kidogo Cha ualimu, Yan pale nyumban Magomen ndugu na majiran walikuwa wanajaa hasa, wakat mwingine hadi wakat wa chakula ilitulazimu tuweke Sasa mduara. Haya yote tisa, kumi mzee wangu alifariki tangu mwaka 1999 kama sikosei ila mpaka Sasa ndugu wa baba walikuwa wakitoka Morogoro kwa wapogoro huko wanafikia nyumban Magomen na yeye bila kinyongo anawakaribisha. Na hao hao ndugu mzee alivyofariki walitaka nyumba iuzwe. Sasa huwa namuuliza bi mkubwa kwanini mpaka leo huwa unawapokea, huwa hunijibu kwa kucheka tu. Mungu amuweke sana bi mkubwa Kwan Sasa ana miaka 74.
 
Wakalim wako kila mahali wabaya wapo kila. Wakalim wapo kila kabila wabaya wapo kila kabila. Pongezi Kwa mama wa kizalamo respect mungu amzidishie
Yes mkuu wakarimu wapo kila pahala, lakini kesi za kupiga mapanga ulishawahi kuzisikia kwa makabila ya watu wa Pwani?? Hakika Mungu hakupi vyote. Mungu anakupa hiki kisha anakunyima kile. Watu wa Pwani Mungu kawapa utajiri wa roho, amewanyima Mali tu..
 
Back
Top Bottom