Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Lakini wapemba hawana roho nzuri hata kidogoKama wakwere na wapemba!
ukiona kabeba mimba kajipangaMambo vp wadau??
Ninaomba radhi kwa uandishi m-bovu.
Kuna mama mmoja yeye ni mzaramo. Ni mama mkaanga Samaki amepanga chumba na sebule huku mtaani kwetu (Kodi Jumla 30,000/= kwa mwezi). Huyu mama muwewe alifariki kama mwaka na nusu hivi umepita. Sasa kulikuwa na Binti mmoja alibeba ujauzito hapa mtaani, huyo Binti hana baba wala mama (umri kama miaka 16 au 17 hivi).
Huyu Binti ni Mnyakyusa wa Mbeya wazazi wake wote walifariki katika vipindi tofauti tofauti ila wa mwisho kufa alikuwa ni mama yake mzazi.
Sasa cha kushangaza huyu mama muuza Samaki, ambaye anaishi maisha magumu mno (faida ya Samaki labda ni 10,000 tu kwa siku) ameamua kumchukua huyu binti anakaa naye hapo alipopanga ilhali hana hata undugu naye.
Wanapika, wanakula, jioni wanaenda kuuza Samaki zao za kukaanga barabarani, huyu dada akiwa na tumbo la ujauzito.
Hii roho ya huyu mama mkaanga dagaa mpaka ninaogopa kwa maana katika hali ya kawaida watu wengi wenye vipato vidogo wanaogopa mizigo zaidi, lakini huyu mama kamchukua huyu Binti anakaa naye kama vile ndugu yake. Hivi wakuu, roho kama hizi huwa mtu anazaliwa nazo au inakuwaje??
Watu wa Pwani (Wazaramo, Wandengereko,n.k) Mwenyezi Mungu awabariki sana.
NB: Mimi ni kabila la mkoa wa Mara na sio mtu wa Pwani.
MUNGU ana makusudi yake daimaKweli dada yangu..
Kweli tumetofautiana,wengine furaha wanaipata kwenye kusaidia wengine.Mambo vp wadau??
Ninaomba radhi kwa uandishi m-bovu.
Kuna mama mmoja yeye ni mzaramo. Ni mama mkaanga Samaki amepanga chumba na sebule huku mtaani kwetu (Kodi Jumla 30,000/= kwa mwezi). Huyu mama muwewe alifariki kama mwaka na nusu hivi umepita. Sasa kulikuwa na Binti mmoja alibeba ujauzito hapa mtaani, huyo Binti hana baba wala mama (umri kama miaka 16 au 17 hivi).
Huyu Binti ni Mnyakyusa wa Mbeya wazazi wake wote walifariki katika vipindi tofauti tofauti ila wa mwisho kufa alikuwa ni mama yake mzazi.
Sasa cha kushangaza huyu mama muuza Samaki, ambaye anaishi maisha magumu mno (faida ya Samaki labda ni 10,000 tu kwa siku) ameamua kumchukua huyu binti anakaa naye hapo alipopanga ilhali hana hata undugu naye.
Wanapika, wanakula, jioni wanaenda kuuza Samaki zao za kukaanga barabarani, huyu dada akiwa na tumbo la ujauzito.
Hii roho ya huyu mama mkaanga dagaa mpaka ninaogopa kwa maana katika hali ya kawaida watu wengi wenye vipato vidogo wanaogopa mizigo zaidi, lakini huyu mama kamchukua huyu Binti anakaa naye kama vile ndugu yake. Hivi wakuu, roho kama hizi huwa mtu anazaliwa nazo au inakuwaje??
Watu wa Pwani (Wazaramo, Wandengereko,n.k) Mwenyezi Mungu awabariki sana.
NB: Mimi ni kabila la mkoa wa Mara na sio mtu wa Pwani.
Amen..Kweli tumetofautiana,wengine furaha wanaipata kwenye kusaidia wengine.
Mungu ambariki sana
Hakika Diana wangu..MUNGU ana makusudi yake daima
Binti wa miaka 17 amejipanga nini aisee??ukiona kabeba mimba kajipanga
Uislam haujawalazimisha bali umewafundisha.Hayo mambo ni yakawaida hasa kwa huku mikoa ya pwani kwasababu wengi wao uislamu umewalazimisha kwa msisitizo kuwa kumkirimu mwenye shida unapata thawabu
Mtazame Hayati Maalim Seif au Rais Mstaafu Dr. SheIn, Dr. Hussein Mwinyi.Lakini wapemba hawana roho nzuri hata kidogo
Mkwewe au ulimaanisha mkewe?? Hizi smartphones zinalazimisha sana typing errors (typos)..Huyu mama ni kama Ruth na mkwewe kwenye Bibilia
Yes mkuu wakarimu wapo kila pahala, lakini kesi za kupiga mapanga ulishawahi kuzisikia kwa makabila ya watu wa Pwani?? Hakika Mungu hakupi vyote. Mungu anakupa hiki kisha anakunyima kile. Watu wa Pwani Mungu kawapa utajiri wa roho, amewanyima Mali tu..Wakalim wako kila mahali wabaya wapo kila. Wakalim wapo kila kabila wabaya wapo kila kabila. Pongezi Kwa mama wa kizalamo respect mungu amzidishie
Mambo ya vijana utayaweza basi mke wangu. Ujana una mambo mengi sana plus udadisi..Halafu utasikia "wanawake hawapendani". Alomtia huyo binti mimba, katokomea wala hana habari.
Wenyewe wanakutupia jinikesi za kupiga mapanga ulishawahi kuzisikia kwa makabila ya watu wa Pwani
10K per day kama ni uhakika kila siku hiyo sio pesa ndogo kabisa.faida ya 10,000 ni ndogo?? Mbona ni take home za waajiriwa wengi tu😁
Hizo ni imani ambazo hazina ushahidi ambazo hata serikali haizitambui ndiyo maana huwezi kuzisikia zikipelekwa mahakamani..Wenyewe wanakutupia jini