Sakasaka Mao
JF-Expert Member
- Sep 29, 2016
- 12,826
- 17,371
Rudia kusoma comment #164, key board iliparaza.....kuna nini mkuu??
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Rudia kusoma comment #164, key board iliparaza.....kuna nini mkuu??
Wabarikiwe sana....hawa ndiyo wa kuoa na kuolewa nao.Nasemaga kila siku humu, wazaramo pamoja na mapungufu yao ila, Kama kuna kitu wamefanikiwa ni kutokuwa na stress, huwa wanaridhika na vitu vidogo sana kwenye maisha
We jichanganye ujute utaishia kuvaa vijora bila kyupiWabarikiwe sana....hawa ndiyo wa kuoa na kuolewa nao.
Hakuna mbaba mzaramo humu ndani?🤦
Sawa mkuu. Nimesoma ila ninaona umefanya editing. Ni jambo jema pia mkuu..Rudia kusoma comment #164, key board iliparaza.
Ukifanya jambo kwa nia njema, Mungu anakuwekea ulinzi automatically..Hata wewe ulipo, jaribu kufanya utafiti wa kukaa na ndugu baki, au yatima ukimtunza, lazima kuna wepesi flani Mungu huuleta katika maisha yako.
Huyo mama ni mzoefu anajua anachokifanya.
Ugali wa mtu mmoja unaweza kuliwa na watu wawili na maisha yakasonga.
Shetani hilo.mkuu hilo ni tukio moja, nikieleza hapa huwez amini jamaa ana roho mbaya mnooo.
ila yeye sasa anapenda saidiwa balaa, mtaa anao kaa hakuna mtu anapatana nae. ofisini ni mtu mkubwa tu ila akijua haumkubali ama una urafiki na mtu asiye mkubali basi anakupiga zengwe ufukuzwe
kifupi jamaa ana roho mbaya sana
Watu wema, wema vipato vidogo, wapo mkuu..Mungu azidi kuwapigania.
Wazaramo wa high class wapo ila ni wachache sana kama Mh. Suleiman Jaffo..We jichanganye ujute utaishia kuvaa vijora bila kyupi
Kweli bibie wala hujisifii sisi ni mashahidi!Mimi huwa natoa niko hivyo
Mwinyi sio mpemba ila maalim ni mpemba na kweli ni muungwana sanaMtazame Hayati Maalim Seif au Rais Mstaafu Dr. SheIn, Dr. Hussein Mwinyi.
Wapemba wengi (almost 90%) ni watu waungwana sana.
NB: Sifanyi uchawa ili kupata favor au pesa, I'm talking the real thing.
Sasa kupenda taarabu na singling ni kosa?? Si ndo asili yao?? Nyue wasukuma na wakurya mbons mnapenda ngoma zenu? Uswahili huku ndo asili yake!Yes, mkuu. Watu wengi wa Pwani wakiwemo wazaramo na Wandengereko, licha ya watu kuwasema kuwa wanatabia za uswahili kupenda taarabu na singeli, ni watu wenye mioyo mema mnoo..
Wengi ni wale wale tu na hali zaoWazaramo wa high class wapo ila ni wachache sana kama Mh. Suleiman Jaffo..
Maalim alikuwa mpinzani safi sana. Muungwana, hatoi matusi jukwaani.Mwinyi sio mpemba ila maalim ni mpemba na kweli ni muungwana sana
Au sio ila pale kuapishana utasikia ee MUNGU nisaidie, serikali inaamini katika MUNGU?Hizo ni imani ambazo hazina ushahidi ambazo hata serikali haizitambui ndiyo maana huwezi kuzisikia zikipelekwa mahakamani..
Wanapenda sana slope,hicho ndicho kinachonikera Kwa hao jamaaYes, mkuu. Watu wengi wa Pwani wakiwemo wazaramo na Wandengereko, licha ya watu kuwasema kuwa wanatabia za uswahili kupenda taarabu na singeli, ni watu wenye mioyo mema mnoo..
Yes. Upo sahihi mkuu. Wengi ni wa kipato cha chini, lakini Mwenyezi Mungu amewapa mioyo iliyojaa upendo.Wengi ni wale wale tu na hali zao
Kwani mtu wa kipato cha chini akiomba msaada kuna ubaya gani??Wanapenda sana slope,hicho ndicho kinachonikera Kwa hao jamaa
Ningeomba utushirikishe na sisi tumsaidie japo kwa michango kidogo kwa kadri tutakavyo jaaliwa.Mambo vp wadau??
Ninaomba radhi kwa uandishi m-bovu.
Kuna mama mmoja yeye ni mzaramo. Ni mama mkaanga Samaki amepanga chumba na sebule huku mtaani kwetu (Kodi Jumla 30,000/= kwa mwezi). Huyu mama muwewe alifariki kama mwaka na nusu hivi umepita. Sasa kulikuwa na Binti mmoja alibeba ujauzito hapa mtaani, huyo Binti hana baba wala mama (umri kama miaka 16 au 17 hivi).
Huyu Binti ni Mnyakyusa wa Mbeya wazazi wake wote walifariki katika vipindi tofauti tofauti ila wa mwisho kufa alikuwa ni mama yake mzazi.
Sasa cha kushangaza huyu mama muuza Samaki, ambaye anaishi maisha magumu mno (faida ya Samaki labda ni 10,000 tu kwa siku) ameamua kumchukua huyu binti anakaa naye hapo alipopanga ilhali hana hata undugu naye.
Wanapika, wanakula, jioni wanaenda kuuza Samaki zao za kukaanga barabarani, huyu dada akiwa na tumbo la ujauzito.
Hii roho ya huyu mama mkaanga dagaa mpaka ninaogopa kwa maana katika hali ya kawaida watu wengi wenye vipato vidogo wanaogopa mizigo zaidi, lakini huyu mama kamchukua huyu Binti anakaa naye kama vile ndugu yake. Hivi wakuu, roho kama hizi huwa mtu anazaliwa nazo au inakuwaje?
Watu wa Pwani (Wazaramo, Wandengereko,n.k) Mwenyezi Mungu awabariki sana.
From my experience, wengi wenu hamkusoma sana na mna vipato vidogo, lakini Mwenyezi Mungu amewapa mioyo iliyojaa upendo mnoo.
NB: Mimi ni kabila la mkoa wa Mara na sio mtu wa Pwani.
Kweli aisee. Wanakula wanachopata na huridhika na kidogo walichonacho. Hii inaboresha afya ya akiliNasemaga kila siku humu, wazaramo pamoja na mapungufu yao ila, Kama kuna kitu wamefanikiwa ni kutokuwa na stress, huwa wanaridhika na vitu vidogo sana kwenye maisha