Mama Mzazi wa Erick Kabendera amuomba Rais Magufuli kumsamehe mwanae

Mama Mzazi wa Erick Kabendera amuomba Rais Magufuli kumsamehe mwanae

Nimemuonea huruma sana huyu bibi na sisi watoto tujifunze tunapokuwa sehemu tujifunze tutii mamlaka tunawapa tabu sana wazazi wetu

Uko sahihi...ukifanya jambo ni vema uifirikirie kwanza familia yako, kwani hao ndio huummia kuliko wewe uliyefanya kosa...
 
Kwani zito anaenda kumuona kabendera bado au amepumzika, namshauli zito aanze kumsaidia huyo mama kabla kabendera hajatoka gerezani maana ndo walikuwa washauri wake, pamoja na washabiki waliokuwa wanamwambia eti ni jembe akomae, sasa wamemsahau. Familia yake ndo inateseka. Washabikichangenipesa mumsaidie huyo mama, ni ushauli tu.
 
Kwani zito anaenda kumuona kabendera bado au amepumzika, namshauli zito aanze kumsaidia huyo mama kabla kabendera hajatoka gerezani maana ndo walikuwa washauri wake, pamoja na washabiki waliokuwa wanamwambia eti ni jembe akomae, sasa wamemsahau. Familia yake ndo inateseka. Washabiki changeni pesa mumsaidie huyo mama, ni ushauli tu.
 
Inasikitisha. Kuna mtu kanitumia hiyo video whatsapp na sikutaka kuifungua nikaamua kuidelete, ingenitoa machozi.
Mkuu wewe Ni mwanaume au Ni mwanamke?
Na Kama utakuwa phillipo mwanaume Inasikitisha Sana kwa ujumbe ulioandika. Ama kweli kila kukicha idadi ya wanaume inaendelea kupungua kwa kasi Sana mtaani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani hili la kabendera nikiliona nacheka tu maana wiki moja baada ya kukamatwa kwak, huku kwenye mitandao ya kijamii kulichafuka na hash tag ya FREE KABENDERA.
na kuna watu ndio wakaifanya kabisaa kuwa ajenda yao, lakini wiki mbili mbele akajikuta anabaki pekee yake, tena nakumbuka siku anaenda kusikiliza kesi yake kwa mara ya kwanza aliingia mahakamani katuna na tabasaamu kwa mbaaali huku pembeni kakaa na zito, ila alivyoanza kugundua kabaki pekee yake hata na rangi ya ngozi ake ikaanza kubadilika.
Hapa kuna funzo kubwa sana kwa kwetu sisi.
 
Mbona ccm hawaposti hii clip kumjulisha rais wa wanyonge kuna mwananchi anateseka

Sent using Jamii Forums mobile app
Wameshapost
FB_IMG_1575832500173.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Asamehewe tu, aliingizwa mkenge na kina...Wao wako huru mtaani, ni kama hawa wa sasa wanaojiita eti wanaharakati?!
Wanaharakati my ass, hawajielewi kabisa...siku ya siku wale wanaowapeleka front utaona wanapeta mtaani na wale wakisota mahakamani na segerea...
 
December13, 2019

Mama Mzazi wa Erick Kabendera amemuomba Rais Magufuli amsaidie na pia amsamehe mwanae.



Source: TopTen TV
 
Mkuu wewe Ni mwanaume au Ni mwanamke?
Na Kama utakuwa phillipo mwanaume Inasikitisha Sana kwa ujumbe ulioandika. Ama kweli kila kukicha idadi ya wanaume inaendelea kupungua kwa kasi Sana mtaani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Haijalishi jinsia mkuu. Rudi kwenye mada punguza dharau za kipumbavu. Viongozi wako wakubwa kabisa wanatoa machozi hadharani umeshawahi kuwauliza jinsia zao?.
 
Verdiana Mjwahuzi (81) ambaye ni mama wa mwandishi wa habari, Erick Kabendera amemuomba Rais wa Tanzania, John Magufuli kumsamehe mwanaye.

Akizungumza kwa huzuni leo Ijumaa Desemba 13, 2019 katika mkutano na waandishi wa habari, Verdiana amesema Kabendera ni mwanaye pekee anayemsaidia katika matibabu.

Kabendera anakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la utakatishaji za zaidi ya Sh173 milioni na tayari amemuandikia barua mkurugenzi wa mashtaka (DPP) kukiri makosa na kuomba msamaha. Oktoba Mosi , 2019 kupitia wakili wake Jebra Kambole, alimuomba msamaha Rais Magufuli kama kuna makosa ameyafanya.

Verdiana amesema kati ya watoto wake wanane, Kabendera ni wa saba kuzaliwa na ndio alikuwa na uwezo wa kumtunza na kumuuguza.

Mheshimiwa Rais na yeye ni mtoto kama walivyo watoto wengine hata kama ni mkubwa. Ni mzazi na analea watoto. Namwomba anionee huruma.”

"Angalia maisha yalivyo magumu, dawa sipati. Naomba Rais anisaidie kama anavyosaidia wazazi wake,” amesema.

Amesema mwanaye alijitahidi kuitunza familia yake, yeye na ndugu zake wengine na kusisitiza kuwa ndio mhimili wa familia.

"Siwezi kumsifia mwanangu, wanaume wengi wakitoka kazini wanakwenda kulewa lakini Eric anafanya kazi zake hapa nyumbani hadi saa saba usiku na wakati mwingine hadi saa nane . Mambo yote aliyopata ni kwa sababu ya kufanya kazi," amesema mama huyo huku akibubujikwa machozi.

Ameongeza, “kule Segerea (gerezani) siwezi kwenda kwa sababu kuna msongamano wa watu, mahakamani kuna ngazi. Lakini mara ya mwisho nilijitahidi nikaenda nilipomuona mwanangu sikulia, nilijikaza lakini chozi moja lilinitoka. Sikujua kama ni yeye, amekonda na ana nywele nyingi kama mwehu. Ni mweusi lakini amezidi kuwa mweusi.

"Huyu mtoto ni Mungu amenizawadia, ni tunu kwangu. Akisikia mama anaumwa anakimbia haraka. Sasa hizo dawa sizipati tena, macho yalikuwa yanauma na moja halioni tena na hili linaloona naona vitu vyeusi."


View attachment 1291137
Daima tukumbuke haya tunayo watendea watoto wa wenzetu kwa kutumia vyeo tulivyopewa na wananchi ndivyo watoto wetu watakavyo tendewa huku tukishuhudia ,wakati huo hatutaweza kufanya lolote sababu tutakuwa hatuna mamlaka yoyote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom