Mama mzazi wa Martha Mwaipaja alia kwa uchungu, akithibitisha kuwa mwanae huyo hamsaidii kutokana na mzozo na mdogo wake Beatrice

Mama huyo anasema amefanya kila awezalo lakini amemshindwa Joan. "Mimi kama mimi nimemshindwa, na ndio maana Beatrice ameamua kuongea, umma umsaidie, naomba mtusaidie," ameeleza.
Kila jambo lina majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu
 
Mama huyo anasema amefanya kila awezalo lakini amemshindwa Joan. "Mimi kama mimi nimemshindwa, na ndio maana Beatrice ameamua kuongea, umma umsaidie, naomba mtusaidie," ameeleza.
Kila jambo lina majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu
 
Mama wa Martha Mwaipaja akihojiwa na Wemu Online TV, mama mzazi wa Martha amesema alizaa watoto watatu wakiwemo Martha na Beatrice ambao wamepishana miaka miwili, amesema mtoto wake wa kwanza alifariki miaka ya nyuma hivyo wamebaki Martha na Beatrice

Mama huyo amesema aliyoongea Beatrice ni kweli kuwa Martha hamhudumii mama yao huyo

Mama huyo amesema yeye ana wajukuu wanne tu ambao wawili ni watoto wa Beatrice, mmoja ni mtoto wa mwanae aliyefariki na mjukuu wake mwingine ni mtoto wa kiume ambaye ni mtoto wa Martha

Hivyo amesema Joan sio mjukuu wake na wala Joan sio mtoto wa Martha bali Joan alikuwa mfanyakazi wa ndani wa Martha ingawa aliambiwa na Martha kwamba Joan ni yatima anamlea

Mama huyo amesema Martha hamhudumii hata mwanae halisi wa kiume anapata shida

Mama huyo amesema ni kama Joan ndie mwamuzi wa mwisho kuhusu maisha ya Martha. Huku akisema kuna wakati aliponea chupuchupu kutapeliwa kiwanja chake na Joan kiwanja ambacho alinunuliwa na mwanae

Mama huyo amesema mifarakano ilianza kuibuka Joan alipoanza kuwa karibu na Martha kwa madai kwamba Joan amekuwa aligeuza maneno kuwagombanisha Martha na Beatrice

View: https://youtu.be/-rsmiaXel2s?si=1Xq2ewRxZONUkk8o
Tazama Video hii
 

Attachments

  • Mama Martha Mwaipaja.mp4
    3.5 MB
Mpuuzi huyo,amlilie mume wake
 
damu ni nzito kuliko maji.
sijaona usaliti kwenye hili na kwakweli shida kubwa iko kwa dada mdogo wa math.

hana uwezo wa kuisaidia familia yake, then anajishebedua kumzuia Matha asiwasaidie wazazi wake. inaonekana ana kiburi ndio maana nae hana familia mpaka sasa.

Hata hivyo,
mambo ya kifamilia humalizwa kifamilia na sio mitandao ya kijamii ambayo kazi yao kubwa ni kuchochea uhasama zaidi.

Kwa Neema na Baraka za Mungu hili nalo litapita, vizuri tu πŸ’
 
Kama ni ndugu watapatana tu. Wasubiri uchaguzi wa chama rafiki CHADEMA uishe tumtume komredi Lucas Mwashambwa akawasuluhishe kwa sababu inaonekana hiyo familia ni kabila moja na Mwashambwa.
 
Ndiyo Mkuu ni neema hiyo. πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚Japo ameongea kinyume chake.

Mimi pia naomba hiyo neema ya mama Martha na Beatrice iniguse na Mimi.

Kumeanza kuchangamka sasa
Mambo ni moto
Martha anasingizia kuwa hataki kujibu
Eti anapost Mungu amfundishe kunyamaza..
Waja hatumuelewi kabisa, tunataka aongee
Kama ni kweli amemsusa mama yake basi asisingizie kunyamaza.

Japo msaada siyo lazima ila ni muhimu , hasa Kwa mzazi aliyekuzaa.
Lakini pia hii imfundishe huyu Mama kwamba aaiyebadilika ni Yesu pekeyake
Wanadamu wanaweza kubadilika, Na kumuacha
Mungu hawezi kukuacha wakati wote.

Tunawaombea neema ya Kristo iwasaidie kutoka katika hizi misunderstandings.
 
Kwa picha tuliyoiona tangu juzi
Naungana na huyu mama kwamba kiini Cha ugomvi ni hiyo Joan .
Atakapotoka huyo,hawa ndugu watakuwa sawa.
 
Kama ni mama yake mbona kama ni mpumbavu kupita kiasi πŸ€”πŸ€” hata kama wana matatizo kuna haja gani ya kuaibisha familia yao namna hiyo πŸ€”πŸ€”
 
Huyo Joan ni mke wa Martha Mwaipaja? Inaonyesha kama wana uhusiono wa kindoa wa ndoa za jinsia moja

Sasa hapo mume ni yupi na mke ni yupi? .
Kwa maelezo ya huyo mama yake inaonyesha huyo Joan ndie ana nguvu sana atakuwa ndie mumewe.Mwaipaja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…