Mama wa watoto 8 atorokwa na mumewe, aomba msaada

Mama wa watoto 8 atorokwa na mumewe, aomba msaada

Watu wa vijijini wanaamini Uzazi wa Mpango ni kumzuia asizagamue/ asizagamuliwe.

Hivyo wanapinga sana kwa nguvu zote huku wakijificha kwenye kauli ya Mwenyezi Mungu ya Zaeni Mkaijaze Nchi lakini pointi yao kubwa ni Mizagamuo tu.
Hatari sana..!
 
Waziri Dkt. Gwajima D kuna hii familia ya kuitazama inahitaji msaada wa kiuchumi na kijamii. Mama wa watoto nane, Belita Deus, ambaye mumewe katoroka.

Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto wa Wilaya ya Malinyi, Mkaguzi wa Polisi Michael Rasha, ameguswa na hali ya mama wa watoto nane, Belita Deus (37), ambaye alitorokwa na mumewe kutokana na ugumu wa maisha.
Mkaguzi Rasha, akiwa katika jukumu lake la kutoa elimu katika kijiji na kata ya Kilosa Mpepo, Wilaya ya Malinyi mkoani Morogoro, alipokea ujumbe kutoka kwa mama huyo akiomba msaada wa kutafutiwa mumewe ambaye ametoroka na kumtelekeza pamoja na watoto.
Baada ya kupokea wito huo, Rasha alifika nyumbani kwa Belita na kuelezwa changamoto alizonazo baada ya mume wake kumtoroka. Ameeleza kuwa maisha yamekuwa magumu sana na anakabiliwa na tatizo la makazi, kwani anakaa kwenye kibanda alichopewa na msamaria ambaye sasa anakitaka. Pia, amekosa mahitaji muhimu kwa ajili yake na watoto wake na hawezi kuwaendeleza kielimu.
Belita amesema njia pekee inayomfanya aishi ni kufanya vibarua vya kulima na usafi kwenye nyumba za watu ili apate pesa za kusukuma maisha. Mtoto wake mkubwa ana miaka 14 na alitakiwa kuwa darasa la sita, huku mtoto mdogo akiwa na miezi mitano tu.
Mkaguzi Rasha amempatia Belita kilo 20 za unga, mche wa sabuni, na fedha kidogo ya kujikimu ili kumfariji. Hata hivyo, mama huyo anahitaji msaada zaidi kutoka kwa wasamaria wema walioguswa na hali yake.

Picha: Michael Rasha
Uanzishwe mchango humu tumchangie. Sio kuchangia mpira na siasa pekee. Na akipendeza huyo mama, mjinga aliyekimbia majukumu anajirudisha. Na akina mama wasivyo na hiana, anapachikwa mimba ya 9.
 
Hata kama ni mimi nakukimbia,yaan yeye ikiingia tu imo na hajali kabisa uzazi wa mpango,clinic kumejaa mabango ya uzaz wa mpango alikuwa hayaoni

Ndo maana manesi huwa wanakuwa wakali yaan kila mwaka wanakuona una mimba tu,umekuwa ng'ombe
 
We umejuaje hajatekwa na kuuwawa? Kuna ushahidi gani katoroka?
Mke wake angesema kwamba mme wake haonekani nyumbani muda mrefu pengine kapotea au katekwa.

Lakini mke wake kasema kwamba, mme wake katoroka nyumbani kukwepa majukumu na ugumu wa Maisha.

Usicho elewa ni nini?

Au unataka kutetea upumbavu wa huyo baba mpumbavu?
 
Mke wake angesema kwamba mme wake haonekani nyumbani muda mrefu pengine kapotea au katekwa.

Lakini mke wake kasema kwamba, mme wake katoroka nyumbani kukwepa majukumu na ugumu wa Maisha.

Usicho elewa ni nini?

Au unataka kutetea upumbavu wa huyo baba mpumbavu?
Mtu aliyetekwa na kuuwawa na mtu aliyetoroka, yeye ametofautisha vipi?
 
Contact za mama zipo wapi??? Au tunampataje? Iwe watsup ya huyo police ikiwezekana.
Huwa nina hasira sana na wanaume wanao zalisha hovyo kama mapanya halafu kulea hawawezi.

Mijitu ya namna hii ndio inazalisha umaskini na kuongeza idadi ya maskini kuwa wengi duniani.

Na ndio maana huwa nafurahi sana watoto wa namna hii, wanao kulia katika shida hizi, wanapokuja kufanikiwa na kuwatupilia mbali hao baba zao wapumbavu na wazembe wakwepa majukumu.

Li mzazi la namna hii siku likija kukuomba msamaha wewe mtoto wake, Unamfurumusha na mabapa ya panga akafie mbali.
Mh. Doroth gwajima,huyo afande mpambanie.
Kafanya jambo jema sana
Mngeomba muandaliwe utaratibu ili mtafutiwe wengi zaidi. Nchi nzima hali ni kama hiyo.
 
Mtu aliyetekwa na kuuwawa na mtu aliyetoroka, yeye ametofautisha vipi?
Wewe unathibitisha vipi huyo mme ameuwawa?

Mke kashatoa maelezo kwamba mume wake kamkimbia kutokana na ugumu wa maisha wewe unathibitisha vipi kwamba huyo mme ameuwawa?
 
Waziri Dkt. Gwajima D kuna hii familia ya kuitazama inahitaji msaada wa kiuchumi na kijamii. Mama wa watoto nane, Belita Deus, ambaye mumewe katoroka.

Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto wa Wilaya ya Malinyi, Mkaguzi wa Polisi Michael Rasha, ameguswa na hali ya mama wa watoto nane, Belita Deus (37), ambaye alitorokwa na mumewe kutokana na ugumu wa maisha.
Mkaguzi Rasha, akiwa katika jukumu lake la kutoa elimu katika kijiji na kata ya Kilosa Mpepo, Wilaya ya Malinyi mkoani Morogoro, alipokea ujumbe kutoka kwa mama huyo akiomba msaada wa kutafutiwa mumewe ambaye ametoroka na kumtelekeza pamoja na watoto.
Baada ya kupokea wito huo, Rasha alifika nyumbani kwa Belita na kuelezwa changamoto alizonazo baada ya mume wake kumtoroka. Ameeleza kuwa maisha yamekuwa magumu sana na anakabiliwa na tatizo la makazi, kwani anakaa kwenye kibanda alichopewa na msamaria ambaye sasa anakitaka. Pia, amekosa mahitaji muhimu kwa ajili yake na watoto wake na hawezi kuwaendeleza kielimu.
Belita amesema njia pekee inayomfanya aishi ni kufanya vibarua vya kulima na usafi kwenye nyumba za watu ili apate pesa za kusukuma maisha. Mtoto wake mkubwa ana miaka 14 na alitakiwa kuwa darasa la sita, huku mtoto mdogo akiwa na miezi mitano tu.
Mkaguzi Rasha amempatia Belita kilo 20 za unga, mche wa sabuni, na fedha kidogo ya kujikimu ili kumfariji. Hata hivyo, mama huyo anahitaji msaada zaidi kutoka kwa wasamaria wema walioguswa na hali yake.

Picha: Michael Rasha
Mambo mengine yanachekesha frankly.Ndio mwanamme kamkimbia,na ndiyo anahitaji kupata msaada,lakini wote wawili wamefikaje hapo,yeye na mume wake?Ni wazi kabisa kwamba ujinga ndio uliowafikisha hapo,kwa hiyo kama wasipopata msaada(I hope they will),wasimlalamikie mtu,ila wao wenyewe.Na huyo mwanamme popote alipo asakwe awajibishwe kufuatana na sheria zetu za nchi, na alazimishwe kubeba msalaba wake.Huwezi kusababisha tatizo halafu ukimbie.

All in all,jamani Mungu ametupa maarifa, akili,hekima,busara na utashi,ni lazima tuvitumie vitu hivyo ipasavyo kwa sisi wenyewe na jamii yetu .
 
Huwa nina hasira sana na wanaume wanao zalisha hovyo kama mapanya halafu kulea hawawezi.

Mijitu ya namna hii ndio inazalisha umaskini na kuongeza idadi ya maskini kuwa wengi duniani.

Na ndio maana huwa nafurahi sana watoto wa namna hii, wanao kulia katika shida hizi, wanapokuja kufanikiwa na kuwatupilia mbali hao baba zao wapumbavu na wazembe wakwepa majukumu.

Li mzazi la namna hii siku likija kukuomba msamaha wewe mtoto wake, Unamfurumusha na mabapa ya panga akafie mbali.
Matusi hayasaidii, mama anataka msaada/mumewe.
Wewe na mumewe aliyekimbia mko sawa maana wote hamna Masada!
Weka Na.tutoe michango.
 
Back
Top Bottom