Mama yangu alifariki huku akijua simpendi

Mama yangu alifariki huku akijua simpendi

Pole mwaya stahamili maana yana mwisho na kwako utakuwa mwisho mzuri, InshaAllah!

Isipokuwa wakati mwingine uwe unaongea nae kumueleza ukweli.

Usimuogope mtu awaye yoyote.

Wakuogopwa ni Mwenyezi Mungu pekee ,

Wanadamu tunaheshimiana.

Amekuona muoga sasa anakutawala!

Tafuta muda kaa nae Penye utulivu mpe ukweli muhimu usimtukane maana ni kosa na ni jinai.

Mpe misimamo yako,

Mwambie wewe bado unapambana huna kikubwa sana muhimu akuombee upate kingi.

Mwambie wewe ni wewe na una maisha yako binafsi na unahitaji kujikimu na future.

Nakwambia atakuheshimu na kukuogopa na atakuomba hela kwa adabu na itakuwa hiyari yako kumpa Au kutompa.
Yote hayo nimeyafanya lakini wapi, zaidi alizidi kunidharau na pia kunamdogo wangu nilimchukua alimaliza Form 4 ikawa kwamba nikimchukua mdogo wangu nilazima nimtumie 50000 [emoji23][emoji23][emoji23]. Kiukweli kunasiku ilibidi nimfokee maana alizidi aisee na pia niliumia sana na nikasema kama ni laana anipe tu.
 
Ilitakiwa umsamehe ...kosa kubwa lisilosameheka kwa mzazi labda kama alikutupa baada ya kukuzaa na ukaokolewa na wengine
Nimemuonea huruma sana
We acha tu, mi sina baba wala mama ila nimelekewa na babu, yaani japo amenilea tangu mdogo alikuwa ananichukia na kila nikifanya kitu kumridhisha naonekana mbaya anataka anyenyekewe, yaani mara ajiite ye ni Mungu wangu. Nikipata likizo unaenda kwa babu unamnunulia kila kitu ndani unamuacha hata na 50000 lakini bdo analeta makasiriko yaani kunawazazi hovyo sana mara kunakipindi nimeajiriwa anataka tugawane mshahara [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Huyo Sasa kiboko
 
We acha tu, mi sina baba wala mama ila nimelekewa na babu, yaani japo amenilea tangu mdogo alikuwa ananichukia na kila nikifanya kitu kumridhisha naonekana mbaya anataka anyenyekewe, yaani mara ajiite ye ni Mungu wangu. Nikipata likizo unaenda kwa babu unamnunulia kila kitu ndani unamuacha hata na 50000 lakini bdo analeta makasiriko yaani kunawazazi hovyo sana mara kunakipindi nimeajiriwa anataka tugawane mshahara [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Aisee
 
Yote hayo nimeyafanya lakini wapi, zaidi alizidi kunidharau na pia kunamdogo wangu nilimchukua alimaliza Form 4 ikawa kwamba nikimchukua mdogo wangu nilazima nimtumie 50000 [emoji23][emoji23][emoji23]. Kiukweli kunasiku ilibidi nimfokee maana alizidi aisee na pia niliumia sana na nikasema kama ni laana anipe tu.



Mkazie hivyo hivyo huku ukionesha kumheshimu lakini jitambue weka kanuni na misimamo yako ya maisha.

Kuwa na maamuzi yako na ujisimamie.

Yeye utamsaidia kile unachoona anastahili kwa kadiri utakavyojaliwa.

Ukikosa basi aelewe tu.

Na sio iwe sheria Eti ya kulipa Fadhili sababu kakulea.

Kwani ulimuomba akulee ?

Ndio maana Ulaya na America wakiona mzazi au mlezi anazingua tu much nao wana wazingua ili kuwekana Sawa na kuenda sawa.

Laana isiyo na sababu haimpati mtu Imeandikwa hivyo.

Ishi maisha yako.

Kukulea iwe nongwa?!

Bila kuwa na misimamo yako ataendelea kujutawala.

Halafu ukute kuna mtu au watu wanampampu nyuma yake!

Na Pia jitahidi usijiweke kwenye maisha ya hali ya juu ambayo sio halisi.

Usiongelee mafanikio yako kwa watu ambao kisha wanaenda kumwambia huyo babu yako mlezi kuwa siku hizi una hela nyingi.

Angalia mazungumzo yako na watu waliopo Karibu na huyo mlezi.

Pengine Ndiyo yanayokuponza.
 
Kuna mtu kama huyo mama yake aliteseka sana kumtunza kwa kufanya vibarua , anavaa kanga upande etc akafanikiwa kumsomesha ….akapata kazi nzuri sana na pesa zikaanza kuingia ….hakuwahi kumsaidia mama yake alimuacha akaendelea kufanya vibarua vya aibu …na nyumba inaanguka ..akahamia kwa jirani kulikuwa hakuna mtu akawa anaishi kama mlinzi wanamlipa ….
Siku anafariki mtoto wake akatuma pesa kuandaa msiba wa kifahari akaondoka na magari na marafiki zake kwenda kuzika …wakiwa njiani BMW yake ilipata ajali mbaya mke na watoto wakapona wakaenda kuzika yeye akaishia hospotali akapooza huu mwaka wa kumi yupo tu ….mke wake kaingiza mwanamume ndani ….na watoto wake wala hawana muda naye ..yeye ndio anaishi na wheel chair kwenye nyumba mbovu ya mama yake ambayo aliifanyia ukarabati wa voda fasta msiba ulipotokea na kaburi mbele yake …..nayeye anaishi kwa sadaka za “wahitaji” kanisani ….wale wale waliokuwa wanamsaidia mama yake chakula ndio wanampelekea mabaki ya chakula nyumbani ….akiwa na ukiwa na majuto …

Haya mambo sio ya mchezo
Aisee jamaa atakuwa anatamani sana muda urudi nyuma arekebishe makosa yake ila ndio hivyo, huyo mke nae alishindwa kumuhimiza mumewe amjali mama yake au hata yeye alishindwa kumjali mama mkwe khaaa
 
Acha kusingizia ukamilifu
Kuna vitu vingine havihitaji hata maelezo vinahitaji umakini mkubwa hasa wazazi .

Kwanini hukuja kuomba msaada mwanzo ukaamua mwenyewe?
Sasa utaambiwa nini tuku comfort na mzazi ameshakwenda?
Kama ndo kaifahamu jamii now asiombe msaada kisa Alisha kufa kwake Hilo limekuwa gumu ndomana kaja kutafuta njia ya kumuezesha kumsaidia
 
Sababu unakurupuka tu watu wanapitishwa kwenye magumu na wazazi Wai Leo hii kunawatu hawako sawa kiakili kisa malezi na maisha walopitishwa na wazazi Wai hasa Mana wewe Kama ulibahatika kupata mama anae kupenda shukuru watu tuna mengi tumeumezwa na mama afu mtu anaandika Ili apate msaada wewe unaleta mihemko apa
 
Habarini za asubuhi wana MMU poleni na majukumu ya kujenga taifa na familia kiujumla.

Kijana wenu nimekuja hapa mbele yenu sijui nahitajI ushauri ama nahitaj nini ila ntafurahi kama ntarejesha amani ya moyo na akili yangu.

Ni hivi mama yangu mzazi alikufa huku akitambua kua mimi mwanae simpendi na kweli sijawahi kumpenda. Kinachoniuma nilishindwa kulificha hili nilimuonesha moja kwa moja so hadi anakata roho alijua fika simpendi.

Kuna muda nikikaa huwa naona nilikosea sana kumuonesha chuki yangu na hili kosa huwa nalijutia sana. Kila siku nawaza namna ya kujisawazisha ila nakosa majibu.

Naombeni ushauri au maelekezo yoyote yanaweza rejesha amani ya moyo wangu.

Natanguliza shukrani.
Lz
 
Back
Top Bottom