Mama yangu ana miaka 70. Je, anaweza kupata cheti cha kuzaliwa?

Mama yangu ana miaka 70. Je, anaweza kupata cheti cha kuzaliwa?

kuna documents zina miss... uhamiaji bora upeleke document nyingi zaidi washindwe wao kuliko upeleke ndogo harafu waushitukie mchezo.

ungeweka kitambulisho cha kazi...
ungeambatanisha na mkataba wa ajira...

ila usikate tamaa... utapata fuata ushauri wangu wa juu hapo... harafu cheti cha kuzaliwa kina patikana...upo mkoa gani...? nikuunganishe na mtu wa vizazi na vifo...!​
Sogezaaaa mkonoooo uwee mrefu wala usumbuki binafsi spendiirushwanasipendiusumbufusonikionaaashortcutinansaidiaaaa jiongezeee
 
Muwe na utaratibu wa kudai cheti cha kuzaliwa pindi watoto wanapozaliwa
Sheria hazijui ooh sikuwa na habari
Hii itasaidia sana
 
Afsa uhamiaji wa wapi aliekataa?

Kukataa huko kunaweza kuashiria wewe sio raia na mama sio raia.

Affidavit ni document sahihi kabisa.

Mtu aliezaliwa kabla ya mwaka 1978 halazimishwi kua na cheti cha kuzaliwa. Sheria ya cheti cha kuzaliwa inamtaka mtu yoyote aliezaliwa kuanzia 1978 ndio awe na cheti cha kuzaliwa.

Fuatilia vizuri ujue sababu ya yeye kukataa affidavit ni ipi.
Afisa uhamiaji Kigoma. Mimi ni mzaliwa wa manyara mama mzaliwa wa Arusha
 
Mama hajawahi kuwa na cheti Cha kuzaliwa kutokana na utamaduni wa kabila letu kutozingatia masuala ya documents. Sasa naomba kuuliza, je anaweza kukipata sasa? Nilikuwa nafuatilia passport nikapeleka affidavit baala ya cheti chake cha kuzaliwa lakini afisa uhamiaji wakaikataa. Msaada wa mawazo tafadhali.
Wewe juzi hapa umesema ulitaka kumtwanga makofi afisa wa Uhamiaji kisa hiki hiki. Umeshasanda?
 
hapana ujue...wanao sababisha mambo yawe magumu katika upatikanaji wa pass za kusafiria ni ndugu zetu walio wahi kwenda majuu wengi walienda kwa mishe haramu na wengine walienda bila kuwa na kazi maalum.

wanaishia kuwa wazurulaji huko ugenini ina kuwa hasara na aibu kwa serikali kwani most of them huwa wana rudishwa kama mizigo. ndio maana afisa uhamiaji mpaka akupe passport kwa hapa nyumbani.

ni lazima ajiridhishe sana na mwenye jukumu la kumshawishi ni wewe mwenyewe muombaji.

though ni haki ya kila mtanzania kuwa na Hati ya kusafiria....!​
Hapo pa haki ya kila mtanzania kuwa na hati ya kusafiria, ndipo pa kusimamia.

Mtu kwenda nje ya nchi na kufanya vitu haramu hakulichafui taifa bali ni struggle tu za mtu kujikwamua na umaskini. Viongozi wapo hapa nchini na wachafu vibaya mno, wanaanzaje kuwanyooshea raia kuwa ni wachafu na wanalichafua Taifa??

Nchi nyingine umesikia kwa CDF zinawapambania raia wao waje kwetu na kuingia mpaka chumbani kwenye uongozi, kwa faida za kiintelijensia na kiuchumi kwa nchi husika. Sisi tunasema passport zitoke kwa wachache sana.

Kariakoo maduka ya electronics karibu yote ni ya wasomali, wengine wapo kwenye soka, wengine mawaziri nk wasingefika humo kama wangebaniwa passport na nchi zao. Usafi unatakiwa kufanyika ndani ya nchi na sio nje, huko ni struggle tu.
 
Hapo pa haki ya kila mtanzania kuwa na hati ya kusafiria, ndipo pa kusimamia.

Mtu kwenda nje ya nchi na kufanya vitu haramu hakulichafui taifa bali ni struggle tu za mtu kujikwamua na umaskini. Viongozi wapo hapa nchini na wachafu vibaya mno, wanaanzaje kuwanyooshea raia kuwa ni wachafu na wanalichafua Taifa??

Nchi nyingine umesikia kwa CDF zinawapambania raia wao waje kwetu na kuingia mpaka chumbani kwenye uongozi, kwa faida za kiintelijensia na kiuchumi kwa nchi husika. Sisi tunasema passport zitoke kwa wachache sana.

Kariakoo maduka ya electronics karibu yote ni ya wasomali, wengine wapo kwenye soka, wengine mawaziri nk wasingefika humo kama wangebaniwa passport na nchi zao. Usafi unatakiwa kufanyika ndani ya nchi na sio nje, huko ni struggle tu.
kwa kifupi ukisikia Motoni...motoni kwenyewe ndio hapa Tanzania sasa yani hatutakiwi kuwa na MAENDELEO tunatakiwa kuwa mafukara zaidi ili waendelee kututawala😭😭😭

tupo motoni buda​
 
Mama hajawahi kuwa na cheti Cha kuzaliwa kutokana na utamaduni wa kabila letu kutozingatia masuala ya documents. Sasa naomba kuuliza, je anaweza kukipata sasa? Nilikuwa nafuatilia passport nikapeleka affidavit baala ya cheti chake cha kuzaliwa lakini afisa uhamiaji wakaikataa. Msaada wa mawazo tafadhali.
Kwa nini wameikataa?

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Kwa umri huo anatumia form ya kiapo tu ya kuthibitisha kama ni mtanzania

Ova
 
Uje na wazazi wake ili tujue kama kweli ni wa Tz ndo tunatoa cheti chake
Kuna mwenzie aliyedai wazazi kutoka kijijini walikwenda Kurasini, na bado haikusaidia, tangu mwezi wa 5 mwaka jana mpaka sasa hajafanikiwa.

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Wamesema affidavit siyo mbadala wa cheti Cha kuzaliwa. Nineshangaa kwa sababu kwenye tovuti yao affidavit inatambulika kama mbadala wa cheti Cha kuzaliwa
Labda siku hizi wanatengeza vyeti, pasi yangu niliipata 2018, na wazazi wote hawakuwa na vyeti bali hivyo viapo vilivyowekwa na ndugu zao kuthibitisha wanawajua kwa undani tangu enzi hizo.

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom