Mwachiluwi
JF-Expert Member
- Mar 10, 2022
- 25,258
- 48,589
Tafsiri ya kitaalamu inaelezea malezi kuwa ni mchakato wa maandalizi ya mtoto utakaomwezesha kukua, kukubalika na kushiriki katika shughuli za kijamii na kiutamaduni kwa kumlinda, kumjamiisha na kumpatia mahitaji na huduma za msingi.
Iwapo malezi ni mchakato wa maandalizi ya mtoto basi shurti iwepo mipango toka kwa wazazi ili kufanikisha hili. Zama za kujipatia watoto na kuwaacha wakue zinajongea ukingoni. Sasa tunaishi katika wakati wa kuzaa na kulea. Kulea ni pamoja na kuwekeza katika mahitaji muhimu kama vile lishe bora, afya, elimu, ulinzi na hata maji safi na salama.
Mwenendo wa maisha ya wazazi hujumuisha maneno, matendo, tabia na desturi za wazazi wanazotumia katika kuendesha maisha yao ya kila siku katika familia zao na jamii inayowazunguka kwa ujumla. Mahusiano kati ya wazazi, mahusiano na majirani, ndugu, jamaa na marafiki na jinsi unavyowakarimu wageni, nk. Vyote hivi huathiri makuzi na tabia za watoto katika nyanja kuu mbili tofauti; athari chanya na athari hasi. Sote tunajua watoto kwa kiasi kikubwa hujifunza kutoka kwa wazazi wao. Wanachokiona anafanya mzazi, wao pia hufanya.
Hakuna ushuhuda mkuu kuliko kumuona mtu mwenye hadhi na sharafu akipigana na majaribu makubwa, wazazi wanapitia mambo mengi mno kuhakikisha watoto wao wanapata malezi wanayostahiki , wengi hujinyima ili watoto wao wapate licha ya hayo kumekuwa na wazazi ambao huyakimbia majukumu yao na kuwaacha watoto wakiteseka, hiyo hali huleta migogoro baina ya wazazi hao na huwaathiri watoto kiakili na kiafya kwa maana hubaki na maswali mengi kichwani mwao.
Karibu tuangalie kwa pamoja jinsi malezi ya watoto yanavyojenga na kubomo akili za watoto hao, njoo tuisome BARUA KWA MAMA ambayo imeandikwa na mtoto BARAKA, kwanini aandike barua? Ina ujumbe gani? Naam njoo tujumuike pamoja .
◇SEHEMU YA 1◇
Watoto ni kama vichipukizi kwenye bustani ambavyo vinahitaji kutunzwa kwa uangalifu kwa kuwa wao ni viongozi wa kesho na elimu ndiyo huleta mabadiliko yenye mafanikio kutoka utoto hadi utu uzima.Elimu ni muhimu katika kuunda na kukuza nguvu za kihisia na kiakili za mtoto, kumtayarisha kushinda vizuizi vyovyote katika njia yao ya mafanikio kwa kuzingatia hilo kila jamii ya leo imehakikisha watoto wanapewa elimu bila kujali maumbile yao na hali zao za maisha, shule zimesogezwa kwenye jamii zetu ili kila mtoto afaidike nayo.
Haki hiyo ya msingi iliwafikie watoto wa mtaa wa JIULIZE ambapo asilimia kubwa ya wazazi wa mtaa huo walionekana ni wale waliochakazwa na maisha , ndio maisha yaliwachakaza kwani tafuta yao ilikuwa ni kubwa kuliko pata yao, wengi wao walilala kwa kushukuru na walichokipata zaidi ya kile walichotarajia ni wachache mno ambao walijiweza kiuchumi, kiufupi JIULIZE ulikuwa ni mtaa wa walala hoi ndani ya jiji kubwa la TULEANE na ndio mtaa ambao ulikuwa na idadi kubwa ya watoto maana waliamini uzao wao ndio utajiri wao, nyumba zilizochakaa , mitaro iliyohatarisha afya zao na maji ya tabu yaliyokosa usalama ndio ilikuwa sehemu ya maisha ya maisha yao naam hiyo ndio JIULIZE mtaaa ambao mtoto Baraka alikuwa akiishi na mzazi wake wa kike aliyeitwa Sadifa
"Nakwambia usipomaliza kujaza maji ndani hamna kukusanya miguu yako kwenda shule...sasa endelea na ujinga wako maana tokea ulipoamka sujui unakiandika nini hapo " bi Sadifa ambae ni mama Baraka alimfokea mtoto wake huyo huku yeye akimaliza kuchoma vitumbua.
"Lakini mama hiii kazi ningefanya saa ngapi na jana tulilala giza, nilipotaka kwenda kwa kina Mamy ulinikataza unadhani ningefanya nini kama sio kuandika muda huu , halafu bado unataka nikachote na maji hivi huoni kama nitachelewa shul...."
"Eeeeh koma wewe kenge! Wa kusoma utakuwa wewe? Muone vile, yalinishinda mimi mamaako na ndio leo hii unaona hapa napika zangu maandazi na vitumbua" aliwaka bi Sadifa na kumfanya Baraka aufumbe mdomo wake, maana alimjua vizuri mamaake na hakupenda kumkwaza kamwe.
Taratibu Baraka alikusanya madaftari yake kuyaweka kwenye mkoba wake wa kitambaa ambao ulitoka kutolewa unga wa ngano siku za nyuma, aliinua ndoo zake mbili na kuanza safari ya kuelekea kisimani, njiani alikuwa ni mwenye mawazo mno huku akionekana kuchoshwa na vitendo vilivyokuwa vikiendelea kumnyima raha, roho ilimuuma kuona baadhi ya watoto wenziwe wakiwa na sare zao wakielekea shule huku yeye akielekea kisimani.
"Hivi mamaangu lini atakua muelewa? Tuseme haujui umuhimu wa elimu? Hemu ona maisha maisha yetu yalivyo kwanini asinitengezee mazingira ya kuwa mkombozi wake hapo baadae? Au tuseme yeye alisharidhika na maisha haya? Na leo nisipokuwa makini nitachelewa tena darasani hata hii kazi niliyoifanya nitakosa kuipeleka kwa mwalimu " Baraka alisema na nafsi yake huku akianza kukazanisha miguu.
" Samahani Bi Mwinde naomba zamu ya kwako nichote mimi maana bila ya hivyo nitachelewa shule" aliomba Baraka mara tu baada ya kumaliza kuwasalimia aliowakuta.
"Mmh imekuwa ni ada yenu eeeh! Mwambie mamaako mbinu zake tumezijua, haiwezekani yeye akae huko sisi tusote hapa na foleni ukija wewe upishwe....hapa leo hupishwi kila mtu ana haraka zake" aliyekua hakuombwa alijibu kwa sauti kubwa, huyu hakuwa mwengine bali ni bi.Kidubwa ambae mtaa mzima alijulikana na tabia yake ya kuwa na maneno mengi.
"Ndio hivo sasa, mamaake na yeye kazidi ujanja, sote hapa tuna watoto na wajukuu wanaosoma na tumewachagulia moja la kufanya, hapo leo uchelewe tu lakini hakuna ruhusa ya kupishwa na mtu" jirani mwengine aliyechoshwa na tabia hiyo na yeye alichangia mada.
Mpaka kufikia hapo Baraka aliona ugumu wa siku hiyo, ni kweli ilikuwa ni kawaida kila akifika pale kupishwa ili awahi shule ila kwa siku hiyo walio wengi walionekana kuchoshwa, mamaake hakuwahi kwenda kisimani na badala yake alimtegemea yeye, bi Mwinde ambae alimtegemea kumtetea siku hiyo mdomo wake haukuwa na jibu lolote kutokana na kauli alizozipokea kutoka kwa wenziwe, macho yake ya huruma yalimfikia bi Mwinde ambae alibaki njia panda asijue wapi kwa kuelekea.
"Kesho ndiyo mwisho wa kila kitu, kama kusoma ni matayarisho ya maisha basi wacha nikatayarishe ya kwangu, nitajua cha kufanya nikifika nyumbani bila ya maji " Baraka alijiwazia baada ya kukosa msaada.
Hakuwa na cha kusubiri zaidi ya kuchanganya hatua za miguu na kuitafuta njia ya kwao, aliuthamini sana muda alionao, kwake yeye elimu ndio alihisi itakwenda kubadilisha maisha ya kwao , aliamini kupitia elimu hiyohiyo atakwenda kuwakomboa wale waliokosa matumaini ya kusoma wakihofia kukosa ajira.
Pumzi kubwa aliishusha baada ya kuona mlango wa nyumba yao, aliuchunguza vizuri kabla ya kuingia na kugundua kuwa uliegeshwa na sio kufungwa , masikio yake mawili aliyoyategesha kusikiliza chochote kutoka ndani yalimpa jibu la ukimya ambao uliashiria hapakua na mtu yoyote, alifurahi kuona mamaake tayari alikwenda kwenye biashara zake .
"Heheeh hapa wacha ninunue kesi , najua hukumu yake itaniumiza mno ila wacha iwe hivyo" alijisemea Baraka huku akipenyeza ndoo zake zilizokosa maji na kubeba madaftari yake kisha safari ya shule ikaanza.
Mwendo wa kijeshi ndio alihisi utamfikisha haraka safari yake , njiani alipishana na baadhi ya wanafunzi ambao kiuhalisia walionekana ni wachelewaji maarufu, akisikitika kuona na yeye ni miongoni mwao ila angefanya nini?
Baada ya mwendo wa robo saa hatimae aliufikia uzio wa shule yao, uzio ambao ulijengewa na senyenge, geti kubwa la bati lenye kibao chenye maandishi yaliosomeka SHULE YA MSINGI SOMENI yalifikisha tamati ya safari yake, pumzi kubwa aliishusha akionekana kushukuru kuwa pale bila ya usumbufu wowote.
"Mungu wangu na leo nimechelewa tena , sikushiriki shughuli yeyote ya usafi ila nitawahi kuingia darasani" aliongea huku akiendelea na mwendo wake wa kijeshi .
Mlango wa mbao uliokuwa umechorwa namba 6B juu ndio ulikua ukomo wa kukaza kwake, kupitia madirisha yenye uwazi alifurahi kuona darasani hakukuwa na mwalimu, tabasamu zito lilimtoka mwanamke ambae alikuwa kasimama akionekana kusubiri kitu kwa muda mrefu, mwanamke huyo aifurahi mno baada ya kuona sura ya Baraka ikiwa mlangoni .
" B lete daftari lako la English haraka sana, ni muda sasa nimechelewesha kuyapeleka nikikusubiri wewe tu " aliongea mwanamke yule akiwa na rundo kubwa la madaftari mkononi mwake.
"Mamy , hivi nisingewahi ungefanya nini" alidadidisi Bakari huku akipekua mkoba wake na kumkabidhi.
"Ningekereka sana maana nimekuwa nikikuhimiza mno, ila B jiandae na bakora za mwalimu wa usafi maana na leo tena hukuonekana" Mamy aliongea hayo na kutokomea zake nje.......Itaendelea.
Ndio tumeanza hivyo!!!
Tupia like na comments yako hapo chini, muitiko wenu ndio mwendelezo wangu twende kazi!!
◇SEHEMU YA 2◇
"Mamy, hivi nisingewahi ungefanya nini" alidadidisi Bakari huku akipekua mkoba wake na kumkabidhi daftari la kiswahili.
"Ningekereka sana maana nimekuwa nikikuhimiza mno, ila B jiandae na bakora za mwalimu wa usafi maana na leo tena hukuonekana" Mamy aliongea hayo na kutokomea zake nje huku akimuacha Baraka akijigusa makalio yake.
Mamy ni binti ambae alizaliwa kwenye familia iliyojiweza kiuchumi, licha ya kwamba walikuwa wakiishi ndani ya mtaa wa JIULIZE ila changamoto za maisha walizimudu vyema , mamaake na Mamy alikuwa ni daktari huku babaake akiwa ni bosi mkuu wa kampuni kubwa ya uuzaji vifaa tiba katikati ya jiji la TULEANE mbali kidogo na mtaa wa Jiulize.
Licha ya kuwa walijiweza kiuchumi tofauti na wenzao , Mamy hakuwa mwenye majivuno , alimheshimu kila mmoja na kuishi nae kwenye daraja sawa , Mamy alijenga urafiki na Baraka tokea siku ya kwanza alipofika shuleni hapo wakati huo walikuwa darasa la 5 , kilichomvutia zaidi kutoka kwake ni ile nidhamu ya upole na utulivu awapo darasani, ufahamu katika masomo yake ndio ulimfanya azidi kupendeza kwake hata kama hakuwahi kushika nafasi ya kwanza darasani na hiyo ikitokana na kukosa baadhi ya vipindi na muda mzuri wa kujisomea .
"B.....hivi unajua kuwa kila siku huja na zawadi yake " Baraka alishtushwa na kauli ya Mamy mara tu baada ya kuketi kando yake.
"Hhhh ni wewe hivi umefika muda gani" alihoji Baraka akiwa hakufahamu hata akichoulizwa ingawa alisikia .
"Inaonekana ulikuwa mbali mno kimawazo hemu niambie nini shida B wangu " Mamy aliuliza huku sura yake ikijenga hofu .
"Mamy siku zote sitaacha kuwaza kuhusu maisha yangu maana bado najiona nina safari ndefu mno, changamoto ambazo zinanisumbua muda huu ndizo ambazo zinanifanya nisiache kuwaza , kuna mengi napaswa kuyaweka sawa na nina imani ipo siku nitayamaliza" Baraka alijibu kwa upole mno hadi Mamy huruma ilimuingia.
"Mama kuna siku alinambia ya kwamba "Wito wa maisha ni kuamini, kutumaini na kusonga mbele" hivyo kupitia hamasa hiyo nina imani utakamilisha yale unayotamani yakamilike" Baraka alipewa maneno ya kutia moyo huku akiwa kashikiliwa mikono yake.
"Naamini hilo Mamy na ndio maana kila nikiamka asubuhi basi namshukuru mungu kwa maana nipo hai, napumua na nina akili timamu ya kuweza kufikiria nini natakiwa kufanya ili kusonga mbele......" alijibu Baraka macho yake akiwa kayakaza usoni kwa Mamy.
"Ila ukumbuke kuwa maisha ya ndoto hayapatikani kwa kukaa na kuwaza tu, bali kwa kupigania unachoamini na lazima ndoto yako kutimia kama ukiwa na ujasiri wa kuifukuzia" Mamy alizidi kukazia na kuondoa mikono yake kwa Baraka.
"Tuachane na hayo Mamy , ulipofika ulinisemesha ila sikuwa nimekuelewa kamwe" Baraka alibadili mada.
"Nilikuuliza, hivi unajua kuwa kila siku huja na zawadi yake? Mamy alirudia tena kumuuliza huku akiwa makini kumsoma atajibiwa nini.
"Ahaa ndio naelewa hilo, ila hii zawadi ya leo sifikirii kama ina manufaa kwangu, nimewahi vipindi vya asubuhi ila hadi muda huu hakuna mwalimu aliyeingia jambo ambalo sio kawaida, nimeacha jukumu alilonipa mama ambalo bila ya shaka nikirudi sijajua namna ya kujitetea" ingawa Baraka alijibu kwa masikitiko ila hakuacha kumalizia na kicheko kilichoashiria alijihisi mjinga kwa kukaidi amri ya mamaake.
"Hujapoteza bado na hii ni zaidi ya zawadi kwako, hemu jiangalie jana tokea umerudi kutoka shule umesoma nini? Nilikwambia uje nyumbani ila hukutokea kabisa! Hapa shuleni sikuwa napata muda mzuri wa kujisomea na wewe zaidi ya muda wa mapumziko, Baraka ni wakati wetu huu wa kujisomea na kuwekana sawa pale ambapo hatukuwa tumeelewa na wewe ulipokosa vipindi , kutokuwepo kwa mwalimu darasani kusitufanye tukaona tumepoteza muda " Mamy alimuweka sawa Baraka baada ya kuona kama kapoteza muda na siku yake.
"Ni kweli uyasemayo ila namfikiria sana mamaangu na jinsi gani anavyochukia nisipotekeleza agizo lake, sipendi kumkwaza mamaangu ila kuna muda inanibidi"
"Kwani umemfanya nini mama? Mamy alihoji .
"Sikujaza maji ndani kwa ajili ya kuwahi shule, nilikuta foleni kubwa kisimani na hata nilipoomba hakuna ambae alitaka tabia yangu iliyojenga mazowea, Mamy toa kitabu tuanze kusoma mambo ya nyumbani hayawezi kumaliza kwa hapa"
"Wa kwanza kuomba msamaha ni jasiri na yule wa kwanza kusamehe na kusahau ni mwenye furaha zaidi" maneno hayo kutoka kwa Mamy yalimfanya Baraka atikise kichwa kama ishara ya kuyaelewa.
"Nitafanya hivyo ila hapo kwenye kusamehewa sifikirii , mimi mamaangu ana......." Baraka alisita baada ya kuona atavuka mipaka na hilo jambo hata Mamy aliligundua na kuamua kupotezea.
"B akili yako ihamishie hapa ili twende sawa , mitihani ya mwisho wa mwaka itakuja kuanza hapa kichwani mtakuwa hamna kitu badala ya matope hahahaaaaa" Mamy aliongea hayo huku akitoa kitabu cha Mathematics (hesabati ) na kumtaka Baraka aongoze mjadala kwa vile aliliwezea hilo somo.
"Na wewe kwa hesabu dduh!! huwezekani sijui unataka kuwa mhasibu wa dunia" alitania Baraka huku akijiweka sawa kumsomesha mtoto wa kike.
Kwa vile walimu walikua na kikao ofisini kwao basi kiongozi wa darasa ambae ni Mamy alitoa tangazo, kila mmoja alikuwa na uhuru wa kufanya anachotaka , wanafunzi wengine na wao walikwenda kujiunga kwenye meza ya akina Baraka huku wengine wakibaki na tabia zao za kufurahia kuweka zogo pale mwalimu akiwa hayupo darasani, wapo waliojisomea wenyewe masomo mengine na wengine waliamua kutoka kabisa nje ya darasa kwenda kuzurura.
*****************
Kama maisha ni kujaribu vitu mpaka upate kinachofanya kazi basi bi Sadifa alikuwa ni mmoja wao, hakuwa mtu wa kutegemea kazi moja imuingizie kipato, ingawa alikutana na changamoto nyingi ila hilo halikumfanya aache kufanya kazi kila iitwayo leo, kila asubuhi alijitahidi kuwahi kufika makutano makubwa ya soko kuu ambalo lilipatikana katika mtaa wao wa JIULIZE, biashara eneo hilo zilichangamka na watu walikuwa wengi mno kwa maana bidhaa nyingi zilipatikana.
Tayari beseni lake la vitumbua na maandazi lilikuwa jeupe, biashara ilikuwa nzuri mno kiupande wake kwa siku hiyo, meno yote yalikuwa wazi kuonyesha ni furaha kubwa kiasi gani alikuwa nayo, alianza kukunjakunja na kuwaaga wenziwe ambao bado biashara iliwadodea.
"Sio bure mimi nawaambia mtu kila siku anaondoka mwanzo yeye? Kuna mchezo anatuchezea huyu mwanamke" alianza kusema mmoja ya wale ambao walikuwa nae pamoja, mama huyo alikuwa na biashara inayofanana na bi Sadifa.
"Kuwa na mapenzi na kazi yako na hapo kila kitu kitajipanga vizuri katika mstari, akili yako ina nguvu kuliko unavyodhani hivyo unatakiwa kuijaza akili yako fikra chanya ili uone mafanikio, Sadifa sio mchawi na wala hamrogi mtu ila umakini wake na ubunifu ndio unamfanya amalize kazi mapema" Mama mwenye hekima zake alimtetea bi Sadifa.
"Unasema nini na wewe? Ina maana mpo shirika moja , hivi wewe umeona ubunifu gani pale? Ubunifu wa kucheka ovyo na waume za watu? Aagh tumemchoka!!! Mwengine na yeye alidakia.
"Munatakiwa mujiamini na muwe na imani juu ya uwezo wenu, bila kuamini uwezo wenu wenyewe kamwe hamuwezi kuwa na mafanikio"
"Aaagh tupishe sisi weeh na darasa lako bovu, hapa kesho akija tunampasulia ! haiwezekani yeye kila siku awe wa kwanza kuondoka, tuseme ndio anajua sana kupika? Halafu na sisi!! Aaah weeeh , hapana kwa kweli kesho akija lazima ameze kichambo, mtu mapema unakuja hapa kabla ya sote kufika kama sio kuroga kitu gani? Aliyeanza mada aliongea kwa jazba na kuwafanya wengine wafurahie na kucheka .
**********
"Leo nitampikia mapema yule mtoto , tena nitampikia vitamu maana nina furaha kubwa mno, lazima ale kuku leo mwanangu, tuna mwaka wa nne huu kazi yetu kula tembele tu na dagaa, kwanza sina hata mteja wa mchana ! " Sadifa aliongea hayo kwa mbwembwe zote beseni likiwa kichwani kukaribia nyumba ambayo walipangishwa.
Alifungua mlango wao wa bati na kuingia zake ndani, hatua ya mwanzo aliweka beseni chini na kukimbilia chooni kwa vile haja ndogo ilimbana, mshangao ulimkumba baada ya kumaliza haja na kuona ndoo zikiwa nyeupe bila ya maji , hasira za wazi zilianza kumvaa na kumfanya apoteze tabasamu lake alilolijenga muda mfupi uliopitia.
"Huyu mtoto mshenzi eeeh na atanitambua leo akirudi, kwa maana hakujaza maji hata sehemu moja? Sasa mimi nitanawa na nini? Heeeh nadhani kanisahau" alifoka maneno ambayo yalikwenda kupenya kwenye masikio ya Baraka aliyekuwa
Iwapo malezi ni mchakato wa maandalizi ya mtoto basi shurti iwepo mipango toka kwa wazazi ili kufanikisha hili. Zama za kujipatia watoto na kuwaacha wakue zinajongea ukingoni. Sasa tunaishi katika wakati wa kuzaa na kulea. Kulea ni pamoja na kuwekeza katika mahitaji muhimu kama vile lishe bora, afya, elimu, ulinzi na hata maji safi na salama.
Mwenendo wa maisha ya wazazi hujumuisha maneno, matendo, tabia na desturi za wazazi wanazotumia katika kuendesha maisha yao ya kila siku katika familia zao na jamii inayowazunguka kwa ujumla. Mahusiano kati ya wazazi, mahusiano na majirani, ndugu, jamaa na marafiki na jinsi unavyowakarimu wageni, nk. Vyote hivi huathiri makuzi na tabia za watoto katika nyanja kuu mbili tofauti; athari chanya na athari hasi. Sote tunajua watoto kwa kiasi kikubwa hujifunza kutoka kwa wazazi wao. Wanachokiona anafanya mzazi, wao pia hufanya.
Hakuna ushuhuda mkuu kuliko kumuona mtu mwenye hadhi na sharafu akipigana na majaribu makubwa, wazazi wanapitia mambo mengi mno kuhakikisha watoto wao wanapata malezi wanayostahiki , wengi hujinyima ili watoto wao wapate licha ya hayo kumekuwa na wazazi ambao huyakimbia majukumu yao na kuwaacha watoto wakiteseka, hiyo hali huleta migogoro baina ya wazazi hao na huwaathiri watoto kiakili na kiafya kwa maana hubaki na maswali mengi kichwani mwao.
Karibu tuangalie kwa pamoja jinsi malezi ya watoto yanavyojenga na kubomo akili za watoto hao, njoo tuisome BARUA KWA MAMA ambayo imeandikwa na mtoto BARAKA, kwanini aandike barua? Ina ujumbe gani? Naam njoo tujumuike pamoja .
◇SEHEMU YA 1◇
Watoto ni kama vichipukizi kwenye bustani ambavyo vinahitaji kutunzwa kwa uangalifu kwa kuwa wao ni viongozi wa kesho na elimu ndiyo huleta mabadiliko yenye mafanikio kutoka utoto hadi utu uzima.Elimu ni muhimu katika kuunda na kukuza nguvu za kihisia na kiakili za mtoto, kumtayarisha kushinda vizuizi vyovyote katika njia yao ya mafanikio kwa kuzingatia hilo kila jamii ya leo imehakikisha watoto wanapewa elimu bila kujali maumbile yao na hali zao za maisha, shule zimesogezwa kwenye jamii zetu ili kila mtoto afaidike nayo.
Haki hiyo ya msingi iliwafikie watoto wa mtaa wa JIULIZE ambapo asilimia kubwa ya wazazi wa mtaa huo walionekana ni wale waliochakazwa na maisha , ndio maisha yaliwachakaza kwani tafuta yao ilikuwa ni kubwa kuliko pata yao, wengi wao walilala kwa kushukuru na walichokipata zaidi ya kile walichotarajia ni wachache mno ambao walijiweza kiuchumi, kiufupi JIULIZE ulikuwa ni mtaa wa walala hoi ndani ya jiji kubwa la TULEANE na ndio mtaa ambao ulikuwa na idadi kubwa ya watoto maana waliamini uzao wao ndio utajiri wao, nyumba zilizochakaa , mitaro iliyohatarisha afya zao na maji ya tabu yaliyokosa usalama ndio ilikuwa sehemu ya maisha ya maisha yao naam hiyo ndio JIULIZE mtaaa ambao mtoto Baraka alikuwa akiishi na mzazi wake wa kike aliyeitwa Sadifa
"Nakwambia usipomaliza kujaza maji ndani hamna kukusanya miguu yako kwenda shule...sasa endelea na ujinga wako maana tokea ulipoamka sujui unakiandika nini hapo " bi Sadifa ambae ni mama Baraka alimfokea mtoto wake huyo huku yeye akimaliza kuchoma vitumbua.
"Lakini mama hiii kazi ningefanya saa ngapi na jana tulilala giza, nilipotaka kwenda kwa kina Mamy ulinikataza unadhani ningefanya nini kama sio kuandika muda huu , halafu bado unataka nikachote na maji hivi huoni kama nitachelewa shul...."
"Eeeeh koma wewe kenge! Wa kusoma utakuwa wewe? Muone vile, yalinishinda mimi mamaako na ndio leo hii unaona hapa napika zangu maandazi na vitumbua" aliwaka bi Sadifa na kumfanya Baraka aufumbe mdomo wake, maana alimjua vizuri mamaake na hakupenda kumkwaza kamwe.
Taratibu Baraka alikusanya madaftari yake kuyaweka kwenye mkoba wake wa kitambaa ambao ulitoka kutolewa unga wa ngano siku za nyuma, aliinua ndoo zake mbili na kuanza safari ya kuelekea kisimani, njiani alikuwa ni mwenye mawazo mno huku akionekana kuchoshwa na vitendo vilivyokuwa vikiendelea kumnyima raha, roho ilimuuma kuona baadhi ya watoto wenziwe wakiwa na sare zao wakielekea shule huku yeye akielekea kisimani.
"Hivi mamaangu lini atakua muelewa? Tuseme haujui umuhimu wa elimu? Hemu ona maisha maisha yetu yalivyo kwanini asinitengezee mazingira ya kuwa mkombozi wake hapo baadae? Au tuseme yeye alisharidhika na maisha haya? Na leo nisipokuwa makini nitachelewa tena darasani hata hii kazi niliyoifanya nitakosa kuipeleka kwa mwalimu " Baraka alisema na nafsi yake huku akianza kukazanisha miguu.
" Samahani Bi Mwinde naomba zamu ya kwako nichote mimi maana bila ya hivyo nitachelewa shule" aliomba Baraka mara tu baada ya kumaliza kuwasalimia aliowakuta.
"Mmh imekuwa ni ada yenu eeeh! Mwambie mamaako mbinu zake tumezijua, haiwezekani yeye akae huko sisi tusote hapa na foleni ukija wewe upishwe....hapa leo hupishwi kila mtu ana haraka zake" aliyekua hakuombwa alijibu kwa sauti kubwa, huyu hakuwa mwengine bali ni bi.Kidubwa ambae mtaa mzima alijulikana na tabia yake ya kuwa na maneno mengi.
"Ndio hivo sasa, mamaake na yeye kazidi ujanja, sote hapa tuna watoto na wajukuu wanaosoma na tumewachagulia moja la kufanya, hapo leo uchelewe tu lakini hakuna ruhusa ya kupishwa na mtu" jirani mwengine aliyechoshwa na tabia hiyo na yeye alichangia mada.
Mpaka kufikia hapo Baraka aliona ugumu wa siku hiyo, ni kweli ilikuwa ni kawaida kila akifika pale kupishwa ili awahi shule ila kwa siku hiyo walio wengi walionekana kuchoshwa, mamaake hakuwahi kwenda kisimani na badala yake alimtegemea yeye, bi Mwinde ambae alimtegemea kumtetea siku hiyo mdomo wake haukuwa na jibu lolote kutokana na kauli alizozipokea kutoka kwa wenziwe, macho yake ya huruma yalimfikia bi Mwinde ambae alibaki njia panda asijue wapi kwa kuelekea.
"Kesho ndiyo mwisho wa kila kitu, kama kusoma ni matayarisho ya maisha basi wacha nikatayarishe ya kwangu, nitajua cha kufanya nikifika nyumbani bila ya maji " Baraka alijiwazia baada ya kukosa msaada.
Hakuwa na cha kusubiri zaidi ya kuchanganya hatua za miguu na kuitafuta njia ya kwao, aliuthamini sana muda alionao, kwake yeye elimu ndio alihisi itakwenda kubadilisha maisha ya kwao , aliamini kupitia elimu hiyohiyo atakwenda kuwakomboa wale waliokosa matumaini ya kusoma wakihofia kukosa ajira.
Pumzi kubwa aliishusha baada ya kuona mlango wa nyumba yao, aliuchunguza vizuri kabla ya kuingia na kugundua kuwa uliegeshwa na sio kufungwa , masikio yake mawili aliyoyategesha kusikiliza chochote kutoka ndani yalimpa jibu la ukimya ambao uliashiria hapakua na mtu yoyote, alifurahi kuona mamaake tayari alikwenda kwenye biashara zake .
"Heheeh hapa wacha ninunue kesi , najua hukumu yake itaniumiza mno ila wacha iwe hivyo" alijisemea Baraka huku akipenyeza ndoo zake zilizokosa maji na kubeba madaftari yake kisha safari ya shule ikaanza.
Mwendo wa kijeshi ndio alihisi utamfikisha haraka safari yake , njiani alipishana na baadhi ya wanafunzi ambao kiuhalisia walionekana ni wachelewaji maarufu, akisikitika kuona na yeye ni miongoni mwao ila angefanya nini?
Baada ya mwendo wa robo saa hatimae aliufikia uzio wa shule yao, uzio ambao ulijengewa na senyenge, geti kubwa la bati lenye kibao chenye maandishi yaliosomeka SHULE YA MSINGI SOMENI yalifikisha tamati ya safari yake, pumzi kubwa aliishusha akionekana kushukuru kuwa pale bila ya usumbufu wowote.
"Mungu wangu na leo nimechelewa tena , sikushiriki shughuli yeyote ya usafi ila nitawahi kuingia darasani" aliongea huku akiendelea na mwendo wake wa kijeshi .
Mlango wa mbao uliokuwa umechorwa namba 6B juu ndio ulikua ukomo wa kukaza kwake, kupitia madirisha yenye uwazi alifurahi kuona darasani hakukuwa na mwalimu, tabasamu zito lilimtoka mwanamke ambae alikuwa kasimama akionekana kusubiri kitu kwa muda mrefu, mwanamke huyo aifurahi mno baada ya kuona sura ya Baraka ikiwa mlangoni .
" B lete daftari lako la English haraka sana, ni muda sasa nimechelewesha kuyapeleka nikikusubiri wewe tu " aliongea mwanamke yule akiwa na rundo kubwa la madaftari mkononi mwake.
"Mamy , hivi nisingewahi ungefanya nini" alidadidisi Bakari huku akipekua mkoba wake na kumkabidhi.
"Ningekereka sana maana nimekuwa nikikuhimiza mno, ila B jiandae na bakora za mwalimu wa usafi maana na leo tena hukuonekana" Mamy aliongea hayo na kutokomea zake nje.......Itaendelea.
Ndio tumeanza hivyo!!!
Tupia like na comments yako hapo chini, muitiko wenu ndio mwendelezo wangu twende kazi!!
◇SEHEMU YA 2◇
"Mamy, hivi nisingewahi ungefanya nini" alidadidisi Bakari huku akipekua mkoba wake na kumkabidhi daftari la kiswahili.
"Ningekereka sana maana nimekuwa nikikuhimiza mno, ila B jiandae na bakora za mwalimu wa usafi maana na leo tena hukuonekana" Mamy aliongea hayo na kutokomea zake nje huku akimuacha Baraka akijigusa makalio yake.
Mamy ni binti ambae alizaliwa kwenye familia iliyojiweza kiuchumi, licha ya kwamba walikuwa wakiishi ndani ya mtaa wa JIULIZE ila changamoto za maisha walizimudu vyema , mamaake na Mamy alikuwa ni daktari huku babaake akiwa ni bosi mkuu wa kampuni kubwa ya uuzaji vifaa tiba katikati ya jiji la TULEANE mbali kidogo na mtaa wa Jiulize.
Licha ya kuwa walijiweza kiuchumi tofauti na wenzao , Mamy hakuwa mwenye majivuno , alimheshimu kila mmoja na kuishi nae kwenye daraja sawa , Mamy alijenga urafiki na Baraka tokea siku ya kwanza alipofika shuleni hapo wakati huo walikuwa darasa la 5 , kilichomvutia zaidi kutoka kwake ni ile nidhamu ya upole na utulivu awapo darasani, ufahamu katika masomo yake ndio ulimfanya azidi kupendeza kwake hata kama hakuwahi kushika nafasi ya kwanza darasani na hiyo ikitokana na kukosa baadhi ya vipindi na muda mzuri wa kujisomea .
"B.....hivi unajua kuwa kila siku huja na zawadi yake " Baraka alishtushwa na kauli ya Mamy mara tu baada ya kuketi kando yake.
"Hhhh ni wewe hivi umefika muda gani" alihoji Baraka akiwa hakufahamu hata akichoulizwa ingawa alisikia .
"Inaonekana ulikuwa mbali mno kimawazo hemu niambie nini shida B wangu " Mamy aliuliza huku sura yake ikijenga hofu .
"Mamy siku zote sitaacha kuwaza kuhusu maisha yangu maana bado najiona nina safari ndefu mno, changamoto ambazo zinanisumbua muda huu ndizo ambazo zinanifanya nisiache kuwaza , kuna mengi napaswa kuyaweka sawa na nina imani ipo siku nitayamaliza" Baraka alijibu kwa upole mno hadi Mamy huruma ilimuingia.
"Mama kuna siku alinambia ya kwamba "Wito wa maisha ni kuamini, kutumaini na kusonga mbele" hivyo kupitia hamasa hiyo nina imani utakamilisha yale unayotamani yakamilike" Baraka alipewa maneno ya kutia moyo huku akiwa kashikiliwa mikono yake.
"Naamini hilo Mamy na ndio maana kila nikiamka asubuhi basi namshukuru mungu kwa maana nipo hai, napumua na nina akili timamu ya kuweza kufikiria nini natakiwa kufanya ili kusonga mbele......" alijibu Baraka macho yake akiwa kayakaza usoni kwa Mamy.
"Ila ukumbuke kuwa maisha ya ndoto hayapatikani kwa kukaa na kuwaza tu, bali kwa kupigania unachoamini na lazima ndoto yako kutimia kama ukiwa na ujasiri wa kuifukuzia" Mamy alizidi kukazia na kuondoa mikono yake kwa Baraka.
"Tuachane na hayo Mamy , ulipofika ulinisemesha ila sikuwa nimekuelewa kamwe" Baraka alibadili mada.
"Nilikuuliza, hivi unajua kuwa kila siku huja na zawadi yake? Mamy alirudia tena kumuuliza huku akiwa makini kumsoma atajibiwa nini.
"Ahaa ndio naelewa hilo, ila hii zawadi ya leo sifikirii kama ina manufaa kwangu, nimewahi vipindi vya asubuhi ila hadi muda huu hakuna mwalimu aliyeingia jambo ambalo sio kawaida, nimeacha jukumu alilonipa mama ambalo bila ya shaka nikirudi sijajua namna ya kujitetea" ingawa Baraka alijibu kwa masikitiko ila hakuacha kumalizia na kicheko kilichoashiria alijihisi mjinga kwa kukaidi amri ya mamaake.
"Hujapoteza bado na hii ni zaidi ya zawadi kwako, hemu jiangalie jana tokea umerudi kutoka shule umesoma nini? Nilikwambia uje nyumbani ila hukutokea kabisa! Hapa shuleni sikuwa napata muda mzuri wa kujisomea na wewe zaidi ya muda wa mapumziko, Baraka ni wakati wetu huu wa kujisomea na kuwekana sawa pale ambapo hatukuwa tumeelewa na wewe ulipokosa vipindi , kutokuwepo kwa mwalimu darasani kusitufanye tukaona tumepoteza muda " Mamy alimuweka sawa Baraka baada ya kuona kama kapoteza muda na siku yake.
"Ni kweli uyasemayo ila namfikiria sana mamaangu na jinsi gani anavyochukia nisipotekeleza agizo lake, sipendi kumkwaza mamaangu ila kuna muda inanibidi"
"Kwani umemfanya nini mama? Mamy alihoji .
"Sikujaza maji ndani kwa ajili ya kuwahi shule, nilikuta foleni kubwa kisimani na hata nilipoomba hakuna ambae alitaka tabia yangu iliyojenga mazowea, Mamy toa kitabu tuanze kusoma mambo ya nyumbani hayawezi kumaliza kwa hapa"
"Wa kwanza kuomba msamaha ni jasiri na yule wa kwanza kusamehe na kusahau ni mwenye furaha zaidi" maneno hayo kutoka kwa Mamy yalimfanya Baraka atikise kichwa kama ishara ya kuyaelewa.
"Nitafanya hivyo ila hapo kwenye kusamehewa sifikirii , mimi mamaangu ana......." Baraka alisita baada ya kuona atavuka mipaka na hilo jambo hata Mamy aliligundua na kuamua kupotezea.
"B akili yako ihamishie hapa ili twende sawa , mitihani ya mwisho wa mwaka itakuja kuanza hapa kichwani mtakuwa hamna kitu badala ya matope hahahaaaaa" Mamy aliongea hayo huku akitoa kitabu cha Mathematics (hesabati ) na kumtaka Baraka aongoze mjadala kwa vile aliliwezea hilo somo.
"Na wewe kwa hesabu dduh!! huwezekani sijui unataka kuwa mhasibu wa dunia" alitania Baraka huku akijiweka sawa kumsomesha mtoto wa kike.
Kwa vile walimu walikua na kikao ofisini kwao basi kiongozi wa darasa ambae ni Mamy alitoa tangazo, kila mmoja alikuwa na uhuru wa kufanya anachotaka , wanafunzi wengine na wao walikwenda kujiunga kwenye meza ya akina Baraka huku wengine wakibaki na tabia zao za kufurahia kuweka zogo pale mwalimu akiwa hayupo darasani, wapo waliojisomea wenyewe masomo mengine na wengine waliamua kutoka kabisa nje ya darasa kwenda kuzurura.
*****************
Kama maisha ni kujaribu vitu mpaka upate kinachofanya kazi basi bi Sadifa alikuwa ni mmoja wao, hakuwa mtu wa kutegemea kazi moja imuingizie kipato, ingawa alikutana na changamoto nyingi ila hilo halikumfanya aache kufanya kazi kila iitwayo leo, kila asubuhi alijitahidi kuwahi kufika makutano makubwa ya soko kuu ambalo lilipatikana katika mtaa wao wa JIULIZE, biashara eneo hilo zilichangamka na watu walikuwa wengi mno kwa maana bidhaa nyingi zilipatikana.
Tayari beseni lake la vitumbua na maandazi lilikuwa jeupe, biashara ilikuwa nzuri mno kiupande wake kwa siku hiyo, meno yote yalikuwa wazi kuonyesha ni furaha kubwa kiasi gani alikuwa nayo, alianza kukunjakunja na kuwaaga wenziwe ambao bado biashara iliwadodea.
"Sio bure mimi nawaambia mtu kila siku anaondoka mwanzo yeye? Kuna mchezo anatuchezea huyu mwanamke" alianza kusema mmoja ya wale ambao walikuwa nae pamoja, mama huyo alikuwa na biashara inayofanana na bi Sadifa.
"Kuwa na mapenzi na kazi yako na hapo kila kitu kitajipanga vizuri katika mstari, akili yako ina nguvu kuliko unavyodhani hivyo unatakiwa kuijaza akili yako fikra chanya ili uone mafanikio, Sadifa sio mchawi na wala hamrogi mtu ila umakini wake na ubunifu ndio unamfanya amalize kazi mapema" Mama mwenye hekima zake alimtetea bi Sadifa.
"Unasema nini na wewe? Ina maana mpo shirika moja , hivi wewe umeona ubunifu gani pale? Ubunifu wa kucheka ovyo na waume za watu? Aagh tumemchoka!!! Mwengine na yeye alidakia.
"Munatakiwa mujiamini na muwe na imani juu ya uwezo wenu, bila kuamini uwezo wenu wenyewe kamwe hamuwezi kuwa na mafanikio"
"Aaagh tupishe sisi weeh na darasa lako bovu, hapa kesho akija tunampasulia ! haiwezekani yeye kila siku awe wa kwanza kuondoka, tuseme ndio anajua sana kupika? Halafu na sisi!! Aaah weeeh , hapana kwa kweli kesho akija lazima ameze kichambo, mtu mapema unakuja hapa kabla ya sote kufika kama sio kuroga kitu gani? Aliyeanza mada aliongea kwa jazba na kuwafanya wengine wafurahie na kucheka .
**********
"Leo nitampikia mapema yule mtoto , tena nitampikia vitamu maana nina furaha kubwa mno, lazima ale kuku leo mwanangu, tuna mwaka wa nne huu kazi yetu kula tembele tu na dagaa, kwanza sina hata mteja wa mchana ! " Sadifa aliongea hayo kwa mbwembwe zote beseni likiwa kichwani kukaribia nyumba ambayo walipangishwa.
Alifungua mlango wao wa bati na kuingia zake ndani, hatua ya mwanzo aliweka beseni chini na kukimbilia chooni kwa vile haja ndogo ilimbana, mshangao ulimkumba baada ya kumaliza haja na kuona ndoo zikiwa nyeupe bila ya maji , hasira za wazi zilianza kumvaa na kumfanya apoteze tabasamu lake alilolijenga muda mfupi uliopitia.
"Huyu mtoto mshenzi eeeh na atanitambua leo akirudi, kwa maana hakujaza maji hata sehemu moja? Sasa mimi nitanawa na nini? Heeeh nadhani kanisahau" alifoka maneno ambayo yalikwenda kupenya kwenye masikio ya Baraka aliyekuwa