Mama yangu kaniumiza sikutegemea

Mama yangu kaniumiza sikutegemea

Katlesi zinarudiwa Valentine’s nimeweka order na cake kwaajili ya shem wako, hii week yote najifua kupika 😹😹🤸‍♀️
Ahahaha andaa pilipili pembeni ya karoti na nyanya tu nyanya tumia moja karot 2
 
Lete recipe ya pilipili ya karoti, hii valentine hakuna kutoka nataka nimuonyeshe tuvitu vitu hapa hapa home 😹
Karoti
Pilipili mwendo kasi
Hoho
Nyanya
Kitunguu maji vyote unasaga ukiwa unasaga unatia mafuta kidogo usiweke maji kabisa then ikaange
 
◇ Sehemu ya 15 ◇

"Lakini mama haya yote umeyataka wewe, kwanini hubadiliki? sio mara ya kwanza hii mamaangu, kama ndio kuna sababu inakufanya hivi kwanini huniweki wazi? Yaani mtaa mzima huu mamaangu tunanuka na tabia zako chafu, nimechokaa!! hadi natamani kuf...... "

"Barakaa........ " hiyo ni sauti ya Mamy ambayo iliwafanya kila mmoja wao kuanza kumtumbulia macho, aliigiaje ndani ? kafata nini ? hayo maswali yalizunguka vichwani mwao.

"Shkamoo mama" Mamy alisalimia ila mama Baraka hakujibu kitu zaidi ya kugeuza uso wake pembeni.

"Mamy... " aliita Baraka na kuweka bakuli chini .

"Naam" kwa upole aliitika huku moyo wake ukiwa na masikitiko ya kutoitikiwa salamu, ukijumlisha na maneno makali aliyoyasikia yakitamkwa na Baraka.

"Unanidai nini? Baraka alihoji huku kichwa cha mamaake kwenye mto.

"Nisikilize Barak.. "

"Sina huo muda, nakuomba uondoke" aliongea Baraka na kumnyooshea kidole mlango wa kutokea nje.

"Sifa kuu ya urafiki mwema ni maelewano ya dhati na kushibana kama hilo halipo unadhani huu urafiki utadumu? B weeeh .....njia yenye miiba ndiyo njia ya kufikia mafanikio makuu tuliyojiwekea, maisha yetu yanabeba sehemu ndogo sana, sehemu kubwa ni nyakati tu amini na hili litapita" kwa sauti ya utii Mamy alijaribu kumshawishi.

"Mamy sitaki kuongea na wewe wala sitaki matatizo yazidi kiupande wangu nakuomba uondoke mamaa" Baraka bado aliendelea na msimamo wake.

"Hivi ndio unataka kusema changamoto ndio zinakufanya ukate tamaa kiasi cha kusahau malengo tuliyojiwekea? alidadisi Mamy.

"Ulitaka nimuache mamangu afe? alihoji Baraka.

"Sina maana hiyo ila nilitaka kukwamb...." kabla hajamaliza Mamy alikatishwa kauli yake na Baraka.

"Mamy maisha yangu hayakuhusu, kama urafiki basi ulikuwa zamani na sio sasa, hupaswi kabisa kuyahofia maisha yangu, kuwa karibu na wewe basi ndio nitaanzisha vita ambavyo sitakua na silaha yoyote ya kujitetetea, Mamy weeh....! kama unanipenda nakuomba uwe mbali na maisha yangu" wakati huu Baraka aliongea kwa upole mno hadi Mamy alimuonea huruma.

"Mamaa ongea na Baraka basi, kwanini hataki tufuatane pamoja kwenye safari hii, kwanini hataki niwe pembeni yake wakati wa matatizo? Mamy uzalendo ulimshinda na kusogea hadi alipokua bi. Sadifa akimpigia magoti.

"Kama uamuzi umetoka kwa Baraka mimi nani nimpinge? hata hivyo mimi mwenyewe nitafurahi kama utamuacha na maisha yake, SIKUPENDI" ingawa maneno hayo yalitoka kwa shida kinywani mwa bi Sadifa ila yalikwenda kuzidisha maumivu kwenye moyo wa Mamy.

Hadi kufikia hapo Mamy alijua kuwa msaada wake hauhitajiki, kiwiliwili kilitamani kuondoka ila nafsi na moyo viligoma kabisa, aliwaangalia Baraka na bi Sadifa kwa macho ya nipokeeni ila hakuna aliyejali , Baraka aliamua kutoka nje kabisa jambo ambalo lilimfanya Mamy na yeye kumfuata.

"Baraka hivi kwanini unaniwekea vikwazo? sipaswi kupendwa na wewe? nina kasoro gani Baraka?

"Mmh! Mamy mimi na wewe hatufanani kabisa, maadui ni wengi kila ninapozidi kuwa karibu na wewe, hemu angalia muda wa vipindi upo kwangu Jee! wazazi wako wakijua? achilia wazazi wako na watu wa mtaani umesema nao?

"Lakini tunaongelea kuhusu Elimu hivyo sioni tatizo kwenye hilo" Mamy alijaribu kujitetea.

"Sioni umuhimu wa shule kabisa kwenye maisha yangu, sioni faida ya kupigania ndoto zangu ikiwa hakuna wa kunishika mkono, kila mtu anachukia uwepo wangu hivi ninachokitafuta nani atakifaidi? safari hii Baraka aliongea kwa uchungu mno hadi machozi yakaanza kumtoka.

"Baraka hemu jipe mfano wa mti uliokuwepo njiani, licha ya kwamba kila apitae huukata vitawi ila hauachi kuchipua , kamwe haujakata tamaa ya kuishi licha ya kwamba watu hawaupi thamani ya kuwa ipo siku unaweza kuwa kivuli kwao" Mamy alimshika hadi bega B wake.

Kitendo cha kushikwa bega kilimkera Baraka kiasi cha kujiondoa haraka kuelekea ndani kwao huku mlango akiufunga na kumuacha Mamy pekee, hakutaka kujiongezea matatizo ukiachana na yale anayopitia, Elimu aliikatia tamaa licha ya kwamba alikuwa na ndoto ambazo aliamini zingewanufaisha wengi, ila kila akijaribu kuzifikia basi anaona kiza kizito kinachomkwamisha kufikia mwanga wa mapambazuko.

" Sijui kwanini nilizaliwa? sioni hata faida ya kuishi ikiwa hakuna anaejivunia uwepo wangu! Mamy naumia kuwa mbali na wewe ila walimwengu ndio wanataka iwe hivo, sitaki upotee kama wanavyopotea watoto wengine , pambana Mamy ili wazazi wako wajivunie uwepo wako siku moja" alilalamika kwenye nafsi yake huku akiwa kaegemea mlango wa nyumba yao.

Mamy kule nje hakuwa na namna nyingine zaidi ya kuondoka kurudi kwao, aliumia na kuyashangaa mabadiliko ya Baraka, hakuamini kama ipo siku mmoja wao angekata tamaa ya kupigania kile walichokiamini na kukipanga muda mrefu, mzigo wa nini anapaswa kufanya ulitua kichwani mwake.

************
Mamy hakuwa na wasiwasi hadi analifikia geti la nyumba ya kwao, funguo zeke alikuwa nazo mkobani hivyo alifungua mlango wao taratibu, tayari ilikuwa ni saa sita kuelekea saba mchana , siku hiyo jua bado lilibaki mawinguni huku mvua ikiwa bado haijanyesha.

"Angalau mama hajarudi ... maana sijui ningemjibu kitu gani? hata kama salamu zitamfikia ila ni vyema anikute nyumbani " alijisemea kwenye nafsi yake huku akiangalia saa ndogo iliyokuwa mkononi mwake.

Alishusha pumzi ndefu alipoifikia sebule ya kwao, ukimya uliomkaribisha ulimpa uhakika wa kutokuwepo mtu yeyote ndani kwao, begi lake la shule alilitupa kwenye sofa dogo ikisha na yeye alijitupa kwenye sofa kubwa na kujiwekea mikono usoni huku akipanga namna ya kusema uongo ambao angeutumia kwa siku ile ili asihukumiwe. Ulimshinda! hakujua ajitetee vipi akirudi mamaake, alipotezea na kujiapia kuwa angejibu chochote wakati wa kuulizwa.

"Najua kwa ufahamu wako huwezi kushindwa jambo , isipokuwa ni maneno ya watu ndio yanakurejesha nyuma, hukuwa muoga hapo kabla ila sijui nini kimekukuta leo, B wangu inaonekana upo kwenye maumivu makali mno ila nitafanya nini peke yangu ikiwa hata wazazi wangu wameanza kukuwekea mashaka? pole sana B" alijiwazia Mamy huku machozi yaliyopenya viganjani yakionekana.

Pembeni ya ukumbi wao ambapo kulikuwa na uchochoro mdogo alikuwepo mtu ambae alijificha kwa muda mrefu akimuangalia bintie, alimsikitikia baada ya kumuona anateseka kwa yasiyomuhusu, ila masikitiko hayo yalibebwa na hasira ambazo aliona muafaka wake ni kuondoka eneo lile ili asije akachukua maamuzi mabaya, alifanikiwa maana hakuonekana.

Mamy akiwa hana hii wala lile alijondoa kochini pale na kuelekea chumbani kwake kwa mwendo wake wa kiuchovu, aliufungua mlango taratibu na kuzama chumbani mwake, alitumia dakika zisizopungua tano bila ya kufanya chochote chumbani mwake, alisimama tu kwenye kioo cha mlango wa kabati lake la nguo akijitazama.

"Yees!!! Hivi kwanini nisiitumie hii sababu ili niwe huru mimi a B wangu ? Wazazi wanaweza kunielewa na hata B anaweza kurudi shule? Safari hii mawazo yake yaliambatana na tabasamu, tayari alijiona mshindi........ Itaendeleaaaaaa.

Mamy ana wazo gani jipya lililomfurahisha? mzazi yupi aliyepo ndani ya nyumba? msimamo wa Baraka utaishia wapi? tukutane sehemu ijayo.


◇ Sehemu ya 16 ◇

Mashirikiano yenu kwangu madogo mno hivyo sina moyo wa kuileta simulizi hii kwa wakati, Mkitaka ije lwa wakati basi jaribuni kunitidhisha walau comment na like zenu tu! hio simulizi HAIUZWI kabisa! ni BURE.

Ilikuwa ni siku ya sita kwenye zile siku saba zinazokamilisha wiki, bado wingu liliendelea kutawala ardhi ya jiji la Tuleane bila ya matone ya mvua na kufanya hali ya joto kuongezeka hasa kwa wakaazi wa Jiulize ambao nyumba zao zilizokosa mpangilio mzuri..

Baada ya shughuli zote za usafi wa nyumba, Baraka alimsogelea mamaake aliyekua kwenye mkeka, alianza kumkanda maeneo mbalimbali ya mwili kwa kutumia dawa za asili alizopewa na bi Mwinde, alimhurumia mamaake kila alipomtazama ila moyo wake ulizama kwenye tabasamu baada ya kuona mabadiliko kidogo ya hali ya mamaake.

"Mama mimi wacha nielekee kisimani , jitahidi hiyo dawa uimalize ili upone angalau na mimi nafsi yangu iwe na amani " sauti ya Baraka iliyochangamka ilimfanya bi Sadifa aitike kwa kichwa maana bado maumivu hayakumuacha.

Baada ya Baraka kutoka nje hatimae Bi Mwinde alijivuta hadi sebuleni kwa bi Sadifa , hakuhangaika kukaribishwa maana mwenyeji wake alikua mgonjwa , alivuta kibao kidogo tu na kuweka makalio yake, alimsalimia na kumjulia hali mgonjwa wake akiwa makini kumkagua kwa macho .

"Sadifa , najua sipaswi kukwambia maneno haya na vile mwenyewe unachukia ila inapoelekea mimi nitashindwa" bi Mwinde alianzisha mada ambayo ilishtua ngoma za sikio za bibie Sadifa, alijiweka tayari kumsikiliza.

"Bi Mwinde usitake nikubadilikie ikisha lawama za binadamu waliokosa utu zikaniangukia " bi Sadifa alijitutumua kujibu huku maneno yake yakiwa yametoka kwenye uvungu wa maumivu.

" Ni heri ya lawama kuliko fedheha Sadifa, kwanini huna mapenzi kwa mtoto wako? kwanini makosa ya mwengine unampandishia yeye? Kama humuwezi mtafute Mshirazi umpe mzigo wake ikisha na wewe ubaki kwenye maisha yako uliyoyachagua"

" Bi Mwinde....bi Mwinde naomba utoke njee! sitaki kabisa kumsikia huyo kiumbe! kiumbe aliyenifanya dunia kuiona chungu, kiumbe kilichonifanya nikaingia kwenye tabia chafu, naonekana sina malezi wala mapenzi kwa mtoto wangu! Mshirazi..... Mshirazi popote ulipo ulaaniwe" machozi yaliamua kusindikiza maneno ya bi Sadifa .

"Hayo yote hayasaidii Sadifa, muda ndio huu wa kumuweka wazi mtoto! hivyo unavyofanya humkomoi Mshirazi ila unajikomoa wewe mwenyewe na mtoto , Usipomwambia Baraka ukweli wa maisha yake ipo siku walimwengu watajua na watamwambia, Ishi kwa namna ambayo huna siri ambayo adui ataitumia kukudhuru....... Kwaheri" aliaga bi Mwinde na kumuacha bi Sadifa akilia.

"Naogopa Baraka kukueleza uhalisia wako, naogopa mno wewe bado mdogo mwanangu, muda mwengine nakua napata hisia za kukupenda mwanangu ila nikimuona Mshirazi kwenye sura yako tu hutamani kukufukuza, Mshirazi Mshirazi kwanini ulikuja kwenye maisha yangu? kwa sauti ya chini hi Sadifa aliendelea kujilaumu huku machozi ya uchungu yakimsindikiza.

*********

Wingi wa watu kisimani hapo haukumshitua Baraka kwani ilikuwa ni kawaida ya watu kujazana siku za Jumamosi na Jumapili , wengi walifika na watoto wao kwa lengo la kufua na wengine wengine wakibaki kujaza maji kwenye ndoo na madumu yao, baada ya salamu kwa wakubwa zake alisogea hadi kwenye foleni na kuweka ndoo zake kubwa mbili na madumu mawili.

"Heeh weweh mtoto aliyekwambia leo kuna maji ya kupewa wewe nani hapa? fungasha ndoo zako chafu uondoke! Huyo alikua ni Masha akimfokea Baraka maneno ambayo yalikwenda kuibua vicheko kwa wengine.

"Lakini mbona nimezikosha vizuri Mamaang.."

"Weeh koma! sina mtoto kama wewe mimi, tumbo langu halichukuwi watoto wa uzinzi na utokeee" Masha alimazia maneno yake na kuyapiga teke madoo na madumu ya Baraka.

"Mbona binadamu mumekosa utu? hivi kosa langu ni kuzaliwa na Sadifa au kuna jingine? kwanini makosa yake nihukumiwe mimi? ndoo zangu ni safi ila umediriki kuzitupaa! Alilalama Baraka.

" Ni safi kwenye macho yako ila kwetu sisi zimejaa dhambi! mumezidi wewe na mamaako au lengo lenu muipake maradhi Jiulize yote hii, kila kona mamaako wanaume wote kalala nao , ndoa zimevunjika " Masha alikuwa wa moto siku hiyo.

Uso wa Baraka ulibadilika kutoka kwenye asili yake na kuumuka kwa hasira, alikunja ngumi mbili kuashiria muda wowote atakiwasha, macho yake makubwa meupe muda huo yalibadilika rangi na kuwa mekundu, hasira zilimvaa na shetani alikuwa pembeni yake kumshawishi atekeleze alichoafikiana na nafsi yake, nani awezae kuvumilia maneno machafu dhidi ya kipenzi chake tena Mama, aaah weeh hakuna kama Mamaa!

Miguu ilisogea hadi alipokuwepo Masha, Ile ngumi aliyoikunja ilionekana na wengi kisimani hapo, mikono ilibaki vinywani na kwenye vichwa vyao wasiamini kile kinachokwenda kutokea, Masha mdomo wote kwisha aliona wazi ngumi ile ikimpata basi itavuruga sura yake kwa mara nyingine, alipanga kukimbia ila Baraka tayari alimfikia , alibaki kusimama huku hofu nyingi ikimjaa usoni mwake.

"Barakaa mwanangu sijakulea hivyo, hata kama mamaako nina tabia chafu ila wewe nimekua nakusisitiza heshima na adabu kila siku, hayo ni makosa yangu usimhukumu" sauti ya mamaake ilimjia kichwani mwake ila haikumfanya kukunjua ngumi aliyoikunja muda mrefu.

"Wewe ni mwanaume na pia ni mkombozi wa familia yako, kama uji humfaaa aunywae basi na mtoto humfaa amleaye , wanadamu ukiwachekea sana basi wao hukuzawadia maumivu , liwezekanalo leo basi lifanywe leo au hujui kama ibadilikapo ngoma basi na mdundo wake hubadilika ..... PAMBANA " hii sauti iliyomjia kichwani mwake pia ilimzidisha hasira zaidi ya alizokuwa nazo mwanzoni, alizidi kumtazama Masha kwa jicho baya na mwisho wa siku akaamua aachie ngumi aliyoikunja muda mrefu huku macho yake akiyafumba.

Alishangaa kuona ngumi yake ikiishia hewani, alipofunua macho yake alishangaa kumuona Mamy mbele yake huku Masha akiwa chini, ni Mamy ndie alimuokoa Masha kutoka kwenye ngumi ya kifo kwa kumsukuma pembeni, Baraka na Mamy walitazamana kwa hasira mno , kila mtu midomo ilimcheza akisubiri wa kuanza kusema.

"Tembo auaye panya hajisifu kwa ushujaa B wangu, mwerevu hupigana kwa ujasiri na sio kwa hasira......naomba tuondoke" uvumilivu ulimshinda Mamy hadi kuropoka maneno ambayo yalipenya vyema kwenye masikio ya waliomzunguka.

"Mamy naomba uniache na ukijaribu kunizuia kwa namna yoyote ile basi utanitambua, kwenye hili werevu nauweka pembeni! Mamaangu mimi kila siku midomoni? yeye ndie wa kwanza kufanya umalaya au dunia nzima hii yeye ndie mwanamke pekee anaweza kuhudumu wanaume wote, Jiulize yenyewe hii inanuka uzinifu halafu muda wote mnamsakam Sadifa? sitovumilia kwa hili na wala hekima sio mahala pake hapaa!!! Baraka alifoka hadi kila mmoja alishangaa maana hawakuwahi kumuona akiwa vile.

Mamy mwenyewe aliogopa maana na yeye hali ile kwake ni ngeni, ila kwa vile hakutaka makubwa zaidi yatokee basi alimsogelea kwa tahadhari kubwa na kumkumbatia kama ishara ya kutuliza hasira zake, alifanikiwa hilo maana Baraka alibaki akitoa machozi tu .

" Mmmh makubwa kumbe kisimani kuna mambo mazuri namna hii na hamsemi ? sijapenda!!" aliropoka mmoja na kufanya wenziwe wamgeukie.

" Na hadi wakiwa shule nasikia hizi ndio tabia zao, haka kabaraka kameanza kurithishwa ukahaba" alinong'ona mmoja kwa sauti ambayo aliidhibiti isije ikamfikia Baraka.

"Weeeh! hivi wazazi wake wanajua kweli? subiri apewe zawadi ya ugonjwa ndio akili itamkaa sawa, hii ndio Jiulize na asubiri majibu" mwengine na yeye alichangia mada.

Wakiwa kwenye majadiliano hayo ghafla kuna mtu alitokea akiwa na........... Itaendeleaaaaaa.

Nani huyo? Masha anusurika na kipigo , Mamy na Baraka bado wpo kwenye kumbatio! unahisi nini kinakwenda kutokea kwenye sehemu ijayo.

Tupia like na comment yako hapo chini, muitiko wenu ndio mwendelezo wa simulizi hii.
 
*******
◇ Sehemu ya 17 ◇
Wakiwa kwenye majadiliano hayo ghafla kuna mtu alitokea akiwa na simu yake janja mkononi, ni macho ndio yalionekana kutokana na sehemu kubwa ya uso wake kufichwa na barakoa aliyoivaa, hakutaka zogo na mtu alichokifanya ni kuwasalimia ikisha akapiga zake picha na kuondoka kwenye kundi lile la watu huku akiacha mijadala .

"Yaani Jiulize hii ina mambo si haba! sasa kutunyima faida ya kumuona sura yake kakusudia nini? Ili umbea wetu usikamilike? Mmmmh...." alilalama mmoja wao.

"Watajua wenyewe, sisi muhimu tunaona kile tunachokitaka tu basi " mwengine alidakia huku akiwaangalia Baraka na Mamy.

"Wenyewe hata hawana habari... tena wewe wasiwasi wako nini? Ukapunguza umbea shoga au subiri yaje yakukute kama Masha"

"Angekuwepo mwenyewe ungemtaja?

"Na nimuogope kwa kipi? Angekua mbabe kweli asingekimbia kipigo cha mtoto kama yule, ila kusukumwa kidogo tu huyoo kakimbia na ndoo zake kaziacha" aliongeza mmoja wao na kuwafanya wenziwe wacheke kwa nguvu hadi Baraka na Mamy wakashtuka.

"Mamy inatosha kwa sasa wacha niyajaze madumu yangu niwahi nyumbani" kwa sauti yake ya upole Baraka alisisitiza akijitoa kwenye kumbatio.

"Lakini na mimi nina mazungumzo muhimu na wewe Barak...."

"Mamy haya sio wakati wake , napaswa kuwahi nyumbani nikamhudumie mama" Baraka alisisitiza.

"Na vipi kuhusu shule? Mbona umebadilika Baraka? Hutaki hata kunisikiliza ..." alilalamika Mamy.

"Kinyonga hubadili rangi kulingana na mazingira yake, niache Mamy nina mambo muhimu ya kufanya" Baraka aliyasema hayo huku akiyajaza madumu na ndoo zake ambapo kwa wakati ule hakuna aliyeweza kumzuia.

Taratibu alibeba madumu yake na ndoo zake aliziweka pembeni akipanga kuzipitia baadae, alipita kwenye kundi la watu waliobaki na kazi ya kumtazama bila kumwambia chochote, maneno ya Mamy kuhusu kuirejesha elimu yake yalimjia akilini na kumtesa mno ila aliamua kuyapa mgongo, kwa muda ule aliona wazi hana matumaini ya kusoma.

Mamy alimsindikiza kwa macho Baraka hadi alipoishia chochoroni, moyoni mwake alihuzunika kuona wazo lake halikupewa nafasi ya kusikilizwa, hiyo ilimuuma na alijiapia kivyovyote angemwambia tena siku hiyohiyo, ingawa alikuwa mtoto wa kishua ila ndoo za maji aliamua kuzibeba, moja aliiweka kichwani mwake huku nyingine ikiwa mkononi mwake, safari ilianza kwa mwendo wa madaha huku akiwaacha midomo wazi walioshuhudia tukio lile.

"Heeeh! Haya ndio mapenzi jamanii" aliropoka mmoja wao na kuwafanya wengine waangushe kicheko.

Mada za kisimani kwa muda huo zilibadilika kabisa, kama ni bungeni basi tuseme Mamy na Baraka waligeuzwa ajenda, kila mtu aliongea kile alichokijua kuhusu wawili hao, Monah ambae alikua pembeni yao moyo ulimuuma mno, alijiapiza kivyovyote angesambaratisha upendo wao.

**********
Mbio za Masha ziliishia tamati nje ya mlango wa shogaake Ndaze , pumzi zilikuwa zinatoka kwa shida mno kutokana na hali ya mwili wake( kibonge) , kikohozi kilichomjia mfululizo ndicho ambacho kilikwenda kumshtua Ndaze aliyekua chumbani kwake na kutoka nje haraka.

"Heeeh shoga vipi tena asubuhi yote hii" kwa sauti iliyokumbwa na mshangao aliuliza Ndaze, hakupewa jibu lolote zaidi ya kikohozi ambacho kiliendelea kumtesa Masha.

Ndase alipigwa na butwaa pia hakujua afanye nini , hapohapo akili ya kufata maji ndani ilimjia, dakika mbili tu tayari alirudi na na kopo la maji, Masha aliyanywa maji yale kwa pupa hadi mengine kumwagika mwilini.

"Haya.....kulikoni asubuhi yote hii na hali hiyo" aliuliza Ndaze baada ya hali ya Masha kutulia.

"Yaani wewe acha tu, yule mtoto ananitafuta....Nitakuja kuua mtu nakwambia " Masha aliongea kwa uchungu mno.

"Mtoto!!! Hemu nyoosha maelezo mtoto yupi umuue? kwa sababu zipi?

" Awe nani kama sio Baraka mtoto wa kahaba? Yaani alichonifanyia kisimani leo.. sitakaa nikamvumilia hata siku moja , lazima alipie" alisema Masha huku akijipiga kifua.

"Baraka huyu wa Sadifa akufanye nini? Mbona sikuelewi Masha! Siamini ujuwe.."

"Ndaze weeh! ukisikia kuadhirika mtu mzima ndio huku, yule mtoto hafai hata kidogo, usione ukadhani Ndaze! hapa unaponiona nimeponea chupuchupu na ngumi yake nzito" Masha alieleza kwa ufupi hali iliyomfanya Ndaze aachie mdomo wake wazi kwa mshangao.

Baada ya kupewa mkasa mzima Ndaze alichukia mno, walijiapiza kwa pamoja ni lazima wamfuate kwao ili heshima ya Masha irudi, walidhamiria kumkomesha. Ndaze alifunga milango yake haraka na kuweka sawa kanga kiunoni tayari kwenda kumkabili mtoto wa mgomvi wake.

Wakiwa njiani kuelekea kwa bi Sadifa walikutana na mwanamke ambae alikuwa kwenye mwendo wa haraka kama kuna kitu ambacho anakiwahi, sura ya yule mwanamke haikua ngeni usoni mwao ila hawakujua wamewahi kuiona wapi.

"Mmh! mbona mwendo huu tena , heeeh huu mtaaa haujambo kwa hekaheka, ukute kuna mtu anakwenda kusutwa" Ndaze alimsindikiza mwanamke yule kwa maneno ya chini ambayo waliyasikia wao wenyewe tu.

***********

"Maumivu ya hizi ndoo nilizobeba hayafikii kamwe yale ninayoyasikia juu yako Baraka! Kwanini unakata tamaa mapema? Mamy alijisemea kwenye nafsi yake akiwa kabakia hatua chache kuufikia mlango wa kwao Baraka.

Mapigo ya moyo wake yalianza kubadili mdundo, kutoka kwenye udundaji wa kawaida kuusogelea ule wa haraka , taratibu aliiachia ndoo ya mkononi na kuishusha ile ya kichwani , pumzi nzito aliishusha baada ya kuutua mzigo ule ambao haukua kawaida yake kuubeba, masikio yake aliyategesha kwa lengo la kupata kusikia chochote ila aliduwazwa na ukimya, ukimya ulikuwa mkubwa mno kiasi cha kushindwa kuelewa chochote kinachoendelea ndani.

"Yaani hata sauti ya kijiko nisiisikie?Ila kama nina lengo la kuongea na Baraka kwanini nisiingie moja kwa moja? Alijiuliza Mamy huku akiufungua mlango kwa tahadhari kubwa.

Madumu ambayo yalibebwa na Baraka muda mfupi yalimsalimu mara tu baada ya kuingia, ila ukimya alioukuta ndani ulianza kumpa wasiwasi, hakua na budi zaidi ya kuongeza kasi ya utembeaji wake , masikio yake yalianza kusikia sauti ambazo hazikuwa na tafsiri nzuri kwenye ubongo wake, alitupilia mbali mawazo hayo na kuendelea kupiga hatua za ujasiri huku moyo wake ukiwa kwenye kasi ya ajabu, macho yalimtoka baada ya kushuhudia kile ambacho alikipinga kwenye akili yake.
"Mamaaaa.......!!!!! Mamy aliita kwa mshangao na kukaa chini bila ya kutegemea.......itaendeleaaaaaa
◇ Sehemu ya 18 ◇

Madumu ambayo yalibebwa na Baraka muda mfupi yalimsalimu mara tu baada ya kuingia, ila ukimya alioukuta ndani ulianza kumpa wasiwasi, hakua na budi zaidi ya kuongeza kasi ya utembeaji wake , masikio yake yalianza kusikia sauti ambazo hazikuwa na tafsiri nzuri kwenye ubongo wake, alitupilia mbali mawazo hayo na kuendelea kupiga hatua za ujasiri huku moyo wake ukiwa kwenye kasi ya ajabu, macho yalimtoka baada ya kushuhudia kile ambacho alikipinga kwenye akili yake.

"Mamaaaa.......!!!!! Mamy aliita kwa mshangao na kukaa chini bila ya kutegemea.

Sauti yake ilikwenda kuwatenganisha wale walioshikana mithili ya nyama na mfupa, bi Sadifa macho ya hasira yalimtoka baada ya kumuona Mamy mbele yake , hata yule mwanaume aliyekua kifuani mwake na yeye alihangaika kuvuta nguo zake zilizokua pembeni ili austiri mwili wake.

"Weeh mtoto ni adabu za wapi hizo kuingia majumbani kwa watu bila hodi ? Nilimkataza mimi Baraka kuniletea watu wa ovyo, ona sasaa.. ndio nini kuniharibia biashara yangu" alilalamika bi Sadifa huku na yeye akivuta shuka kuustiri mwili wake.

Mamy hakuwa na jibu lolote zaidi ya majuto, alijuta kuuvamia mtumbwi wa vibwengo, akiwa bado kaiziba sura yake ghafla kelele zilisikika mlangoni, aliyeingia na yeye hakutaka kubisha hodi zaidi ya kelele zake, macho yalimtoka mwanamke yule asiamini kuwa kile alichokifata ndio kakumbana nacho , haikuwa tu kwa upande wake bali hata yule mzee aliyekua akihangaika kufunga mkanda wa suruali yake alishangaa hadi suruali yenyewe kuporomoka magotini, ni aibu! Mambo hadharani.

"Mwalimu Swami!! Alijiuliza Mamy kwa mshangao huku macho yake yakitua kwa mara nyingine kwa mzee ambae alikua mbele yake , alichoka baada ya kushuhudia sehemu nyeti za mzee yule kwa mara nyingine.

"Huwezi hata kushikilia nguo zako kama ulivyoshindwa kuzihimili hisia zako! Mwanaume huna aibu hata kidogo wewe, upewe nini uridhike? Nini umekosa kwangu hadi kuhangaika na watu kama hawa? Mtamu sana huyu eeeh....basi utabaki na yeye na utanipa talaka yangu niondoke zangu, nimechoka kufuga kunguru" kwa hasira mwanamke yule aliropoka asijali hata uwepo wa mwanafunzi wake.

"Hivi Sadifa lini utaziachia ndoa za watu? Nilikuwa nasikia tu ila leo yamenikuta, Kitu gani unataka kutoka kwa mume wangu? Mwambie akuoe basi nijue tupo wawili kuliko hivi unavyonifanyia, unataka sote tuwe kama wewe!!! Sadifa nakuua leo kwa mikono yangu yaani sitajali chochote " baada ya kauli hizo Mwalimu Swami alimsogelea bi Sadifa pale chini na kuanza kumshushushia mvua ya ngumi huku machozi yakimtoka.

Mzee aliacha kufunga mkanda kwa mara nyingine na kumfuata mkewe ambae alikuwa juu ya mwili wa bi Sadifa akitembeza kipigo, Mamy na yeye uvumilivu ulimshinda ingawa hakuwa na nguvu ya kupambana nao ila roho ya imani ya kumsaidia bi Sadifa mama mkwe wake ilimvaa, alijivika ujasiri na kusogea hadi walipokua, alisaidiana na yule mzee kumtoa Mwalimu Swami mwilini kwa bi Sadifa na hilo walifanikiwa japo ilikuwa kwa tabu , Mamy alimfuata bi Sadifa kwa lengo la kumstiri mwili wake ila alishtukia akivutwa na kutupwa pembeni, alipotaka kumjua nani aliyemvuta alishangaa kumuona mamaake eneo lile.

"Mamaaa!! Aliita kwa mshangao ila aliitikiwa kwa kofi takatifu la uso.

Wote macho yao yalitua kwa mama yule ambae hawakujua alifikaje, Mamy na yeye alibaki akiugulia maumivu hapo ndipo alipokumbuka kuwa kwao aliondoka bila kuaga tena muda mrefu umepita.

"Nataka kijana wako akae mbali na mwanangu na endapo nitakuta mabadiliko yoyote kwenye mwili wa binti yangu tofauti na nilivyomzaa , nakuapia umalaya wenu mtakwenda kuufanyia mahabusu" bi Huba alisema hayo kwa hasira .

"Lakini mam......."Kabla hajamaliza kauli yake alistukia kofi zito likitua kwa mara nyingine kwenye shavu lake.

"Usinitibue....haya ndio madhara ya kukuamini ma kukusikiliza, JIULIZE imekuharibu hadi uhuru niliokupa unautumia vibaya, twendeeee!!!! Alifoka bi Huba.

"Mimi siondoki hadi nijuwe Baraka yupo wapi? Siondoki ili niujue na usalama wa huyu Mama, ulinifunza kusaidia watu na wala sio kukandamiza" Mamy alimjibu mamaake majibu ambayo kila mmoja yalinshangaza.


Wakiwa kwenye mshangao huo viumbe viwili vipya viliwasili kwenye mjengo, naam sio wengine ni Masha na Ndaze. Walioingia walitazamana kwa macho ya kulikoni huku nyuso zao zikionekana kufurahia tukio lile, tayari walijua kilichojiri kutokana na picha waliyoikuta.

"Huyu si yule mwanamke tuliepishana nae njiani akiwa na kasi ya 4G? Kwa sauti ya chini Masha alimuuliza Ndaze akimuelekeza kwa kidole sehemu ambayo mwanamke yule alijikunja, pembeni alikuwepo mumewe akihangaika kufunga suruali yake.

"Ni yeye huyoo! Muone anavyolia masikini, Sadifa mbaya" alijibu Ndaze huku akimtazama Sadifa kwa jicho la chuki maana hata na yeye yaliwahi kumkuta.

" Lakini hapa sielewi ujuwe kuhusu huyu mtoto wa kuitwa Mamy! Mmmh mamaake atamla nyama leo maana sio kwa kumkuta kwenye hili danguro" Masha aliongea baada ya kuona Mamy akivutwa na mamaake ili watoke nje ila mtoto aligoma.

"Hahaaaaa mtoto kazi imemkolea utafikiri ni rahisi kutokaa!! Maneno hayo ya Ndaze yalikwenda kuzidisha hasira kwa bi Huba.

Kishindo na kelele moja kubwa ndio ambayo ilimshtua kila mmoja aliyekuwa eneo lile, masikio yao waliyatega ili waweze kusikia sauti ile kwa mara nyingine ila ukimya bado ulitawala masikioni mwao, walipokosa majibu walianza kuitafsiri sauti ile ya nani na imetoka wapi?

"Barakaaa!!! Hatimae Mamy na bi Sadifa walitamka hilo jina kwa wakati mmoja.

Bi Huba na wengine ambao walikua eneo lile walikosa cha kuzungumza, macho ya kila mmoja wao yalihamia kwa wale ambao walitamka jina la Baraka, wa kwanza kuelekea ilipotoka sauti ile ni Mamy huku akizidi kuwaacha walimshangaa midomo wazi , mshangao mkubwa ulimkumba baada ya kufika chumbani kwa Baraka na kuushuhudia mwili wa Baraka ukiwa chini sakafuni , sio hivyo tu mwili huo ulikua umezamishwa kisu katikati ya tumbo huku damu zikianza kutoka, kwa haraka mno Mamy aliusogelea mwili ule ambao uhai wake ulikua unaelekea mwisho, hakujali nyuma yake kulikua na akina nani alichoamua yeye ni kumkumbatia na kuanza kumtazama usoni kwa hisia.

"Baraka ......kwanini umeamua hivi? Nitaambatana na nani kuelekea kwenye safari yetu ? Nani atanishika mkono? Nani atanisomesha B wangu? Kwanini iwe mapema hivi? " Mamy aliongea hayo kwa sauti ya kilio na machozi yakiwa mashavuni mwake.

"Mamy...... nisamehe sana , nimechoka kiasi ambacho siwezi tena kuendelea kuvumilia haya!! .....kkoooh ... kkoh..., moyo hauhimili tena haya, miaka yote 13 sikuwahi kupata amani ya moyo zaidi ya fukuto la maumivu lililourarua moyo wangu....wacha niwaachie dunia yenu" Baraka aliongea kwa uchungu na tabu mno huku kikohozi kikimuandama, kila neno ambalo alilitamka lilikua ni mwiba kwenye moyo wa Mamy.

Kumbe haikua hivyo tu, hata wale ambao walikua ukumbini basi walisogea chumbani na kuyasikia maneno ya Baraka, mamaake ambae na yeye alikua pembeni akilia alijikuta akikosa hata nguvu ya kuusogelea mwili wa kijana wake, Mamy na Baraka walihisi uwepo wa watu ila hawakuwapa kipaumbele hata kidogo.

"Mamy nina furaha kubwa mno kuona naondoka duniani ukiwa mbele yangu, ni wewe pekee ambae uliikubali hali yangu, ni wewe pekee ambae ulininyanyua pale nilipoanguka , ni wewe pekee ambae hukuwahi kujali nipoje na wala familia yangu ina kitu gani, nakuona mbali sana Mamy, ipiganie ile ndoto yetu tuliyoota pamoja, yapiganie maisha ya watoto wengine waliokata tamaa kama mimi, Mamy...... NAKUPENDA......." ingawa alizungumza kwa tabu ila ujumbe alihakikisha unafika kwa mlengwa kabla hajaiacha dunia.

Muda wa pumzi za kijana Baraka kutamba kwenye sayari ya dunia uliishia tamani, alitulia tuli huku mkono wake mmoja ukiwa umeshikilia kisu na mwengine ukiwa shavuni kwa kipenzi chake, uso wa Mamy tayari ulivimba kwa kilio , maumivu ambayo aliyasikia yalikua hayana mfano, alihangaika kumuamsha Baraka ambae tayari pumzi ilikata , akiwa kwenye huzuni ghafla aliona kitu ambacho kilimshangaza ..........itaendeleaaaaaa
 
*******

◇ Sehemu ya 19 ◇

Muda wa pumzi za kijana Baraka kutamba kwenye sayari ya dunia ulifikia tamati, alitulia tuli huku mkono wake mmoja ukiwa umeshikamana na mkono wa Mamy, uso wa Mamy tayari ulivimba kwa kilio cha kimyakimya , maumivu ambayo aliyasikia yalikua hayana mfano, alihangaika kumuamsha Baraka ambae tayari pumzi ilikata , aliamua kupeleka macho yake pembeni ili aubadilishe ukweli ila alikutana na kitu ambacho kilimshangaza .

Hakujali kabisa uwepo wa watu waliokua nyuma yake, ila alichokifanya yeye ni kutaka kuhakikisha kile ambacho amekiona, alijitahidi kuusogeza mkono wake hadi sehemu ambayo kulikua na stuli chakavu iliyoanguka huku madaftari mengi yakiwa pembeni pamoja na mapande ya viyoo , hapo ndio aligundua kua mshindo ambao waliusikia ulitokana na anachokiona , kwa umakini huku mikono yake ikitetema aliinyanyua karatasi ambayo ilikua juu ya madaftari huku vioo vidogo vidogo vikiwa juu yake, maandishi makubwa juu yaliyokolezewa wino wa rangi nyekundu yalisomeka BARUA KWA MAMA yalimstaajabisha, Mmh ...BARUA KWA MAMA ? Alijiuliza Mamy nafsini mwake.

Aliitazama vyema karatasi ile na kujihakikishia kua ule ulikua ni mwandiko wa kipenzi chake, hakuona vyema ujumbe ule kuusoma yeye ikiwa mlengwa alikuwepo, kwa hatua za kiuchovu alimsogelea bi.Sadifa ambae muda huo alijiinamia akilia, Mamy alichuchumaa na kumshika bega.

"Mama, nadhani haya ni mavuno ya kile ambacho tulikipanda na kukipalilia siku za nyuma, hatupaswi kulia kwa maana machozi hayana msaada tena , bila ya shaka huu ni ujumbe wako" Mamy alizungumza kwa hisia na upole , alimkabidhi mama Baraka karatasi ambayo hakuna ambae alijua kilichoandikwa , kwa mwendo wa maumivu na uchovu Mamy alijikokota na kutoka kwenye chumba kile.

Bi Sadifa alilia baada ya kuona maandishi makubwa juu ya karatasi ile, hata maneno ya Mamy yalimchoma kiasi ambacho alishindwa kuisoma na kubaki nayo mkononi, alimtazama Mamy ambae alikua anaishia kutoka nje, kwa muda ule hakuna aliyethubutu kumwambia chochote zaidi ya mamaake bi.Huba kumfuata nyuma.


Mume wa mwalimu Swami na yeye aliikimbia aibu , tokea watu walipoingia chumbani kwa Baraka yeye tayari alikula nyayo, ingawa mwalimu Swami alikua na maumivu ya kumfumania mumewe ila hayakufikia maumivu ya kifo cha mwanafunzi wake Baraka, aliumia kuona mtaji mkubwa ambao ungezalisha biashara yenye tija mbeleni umejifilisi , mwalimu Swami alimsogelea bi. Sadifa aliyekua akilia huku karatasi ikiwa mkononi mwake , Ndaze na Masha walikua pembeni wakichukua kila hatua za tukio .....kwao wao ilikua ni furaha kuona adui yao akiteseka.

"Sadifa , sifikirii kama unapaswa kumwaga machozi kiasi hiki, wewe muda huu unatakiwa ufurahi kwa vile hiki kiumbe hakitashuhudia maovu yako tena, najua kuwa hata ule uchungu wa kufiliwa na mtoto basi huna kabisa ila tu unajitafuta, Sadifa...hii laana haitakuacha salama, umepoteza taa ambayo ingekusaidia vyema kumurika siku za mbele, kwaheri" mwalimu Swami aliongea hayo huku machozi yakimtoka , hakuona sababu ya kubaki pale hivyo alitafuta njia mikono yake ikiishia kufuta machozi.

"Mpanda ovyo hula ovyo" hii ilikua ni kauli iliyotamkwa kwa dharau kutoka kwa Masha .

" Ulisahau kua dunia ni mti mkavu na kiumbe hupaswi kuuelemea hata kidogo , umelikoroga Sadifa jiandae kulinywa" Ndase na yeye hakua nyuma kutoa ya moyoni, alipomaliza alimshika mkono shogaake na wao wakatoka nje huku wakicheka.

Sadifa alilia kama mtoto baada ya kuona kila mtu aliondoka, alisikitika kuona akibaki pekee kwenye jambo zito kama hilo, kila alipotaka kumtazama kijana wake nafsi yake ilimsuta, aliishia kutazama barua ambayo ilikua mkononi mwake, nguvu za kusoma hakua nazo angewezaje ? alihisi kuwehuka hadi kufikia hatua ya kupiga kelele ambazo zilikwenda kuwashtua majirani.

Nadhani mnaijua vyema Jiulize kwa hekaheka yaani kelele moja tu ya bi .Sadifa ilikijaza chumba cha Baraka kwa umati wa watu , walioshika na kutikisha vichwa vyao kwa huzuni walikuwepo , hata wale ambao waliziba midomo yao kwa viganja vya mikono pia walijaa, haikushangaza wengine nyuso zao kuonekana kujaa nuru ya tabasamu, kila mmoja na namna yake alivyochukulia tukio lile .

Bi Mwinde aliusogelea mwili wa Baraka na kuustiri kwa kitenge chake ambacho alikifungua kichwani kwake , kile kisu ambacho kilizama tumboni hakuthubutu kukishika, baada ya hapo alimsogelea bi Sadifa ambae hadi muda huo hakuna aliyekwenda kumpa maneno ya faraja zaidi ya lawama, alimtazama kwa jicho kali huku ndita zikijengeka usoni mwake.

" Wapiganapo fahari wawili ziumiazo ni nyasi, Sadifa nilikwambia mapema kuhusu hili ila ulidharau, ona leo hii kilichotokea hata ulimwengu wenyewe unakucheka , unashindwa hata kumtazama eeeh? Nitamzika Baraka kwa vile nilimpokea wakati wa kuja duniani " bi Mwinde aliongea kwa uchungu na hasira huku akitoa simu kumpigia Mwenyekiti wa mtaa.

"Najua ulimwengu na vilivyomo vinanilaani ila ningefanya nini? Yote haya kayataka Mshirazi........" Bi Sadifa alitamani kujitetea ila aliishia njiani kwa kilio.

"Sadifa......Siku zote nakwambia ya kwamba kila mtu dunia hii huyaharibu maisha yake kwa mikonoye , hukutakiwa kabisa kumfikiria yule aliyekuangusha ila ulitakiwa uangalie nini ambacho alikuachia, Baraka umemkatisha ndoto zake, Baraka umemkosesha haki zake za msingi nyingi mno, Baraka umemuumiza na Baraka huyuhuyu umemuua kwa tabia zako" alilalamika bi Mwinde machozi yakimtoka.

"Niueni na mimi? Niue bi Mwinde? Kwanini lawama zote kwangu? Mnakijua alichonifanyia Mshirazi? Yeye ndie sababu ya yote haya.... " alilalamika bi Sadifa huku akilia kwa hasira.

"Sitakuua mimi Sadifa ila matendo yako ndio yataamua khatma ya maisha yako, hukupaswa kuyakumbatia na kuyaweka kifuani yale yaliyokuumiza badala yake ulitakiwa kuyashusha na kuyafukia kabisa, siku zote makosa ndio hutufunza mwananguu!!" Bi Mwinde alizidi kutoa lawama.

Bi. Sadifa alizidi kulia kama mtoto kutokana lawama za bi. Mwinde, ghafla simu ya bi Mwinde iliita na kumfanya atoke nje , bi .Sadifa aliitumianafasi hiyo kusota kwa tabu hadi alipoufikia mwili wa Baraka, hata kama ulifunikwa ila aliutazama kwa masikitiko na kuanza kuikunjua karatasi ambayo ilikua mikononi mwake, kishingo upande alianza kusoma maandishi ambayo yaliandikwa.

BARUA KWA MAMA.
Mama..
Wino na karatasi havitoshi kueleza yale machungu ninayohisi moyoni mwangu ila wacha nijaribu kuyaeleza kwa uchache , machozi yangu yaangukayo humu yatatosha kukuonyesha jinsi gani naumia kuandika haya, naelewa kua hukuwahi kunipenda tokea pale nilipoonyesha dalili za kuja duniani ila hukua na njia kwa vile Mungu mwenyewe kataka iwe.

Niliumia kuona watoto wenzangu wakiwa wenye furaha na wazazi wao, uliniachia kiulizo...kwanini isiwe mimi? Sio wewe mamaangu wala yule nisiyemtambua hadi kufa kwangu, yawezekana ungenikutanisha au kunieleza chochote kuhusu yeye basi ingepunguza robo ya kiu yangu, Mama....ingawa sioni ladha ya utamu kila nitamkapo jina hili ila sikuacha kukuita, watoto wenzangu wananidharau sababu ikiwa ni matendo yako kwangu na kwa jamii iliyokuzunguka.

Nilitamani niwe mbele yako nikuelezae haya ila hukuwahi kunipa hiyo nafasi, na hiyo nafasi ningeipata saa ngapi ikiwa masikio na mdomo wako vimezowea kunitamkia maneno makali yenye kuchoma, mama kama ni furaha basi leo unatakiwa kufurahi maana naondoka kwenye sayari hii, hukuwahi kunipa nafasi ya kua mtoto wako ila ulinifanya kua mtu baki ambae sikuwa na msaada wowote kwako, achilia msaada hata ile thamani ya utoto kwako pia sikuona kabisa.

Mama nakuachia ulimwengu wako, tamba uwezavyo , nimechoka kuwekwa lawamani, nimechoka kushuhudia matendo yako, nimechoka kudharauliwa na kutukanwa. Ukitaka nipumzike kwa amani waeleze wana Jiulize kilichokufanya ukawa na maisha haya.

Ikikupendeza pia ....mpe salamu zangu Mamy mwambie NAMPENDA ❤️........itaendeleaaaaaa

Naam hii ndio barua aliyoacha Baraka kwenda kwa mamaake, jee? Bi Sadifa atawaambia wana Jiulize kilichomfanya kuwa alivyo? Tukutane sehemu ya mwisho ya simulizi hii.


◇ Sehemu ya 20 ◇

Aliporudi tu aliamua kujifungia chumbani kwake na kulia kwa sauti, hata baba yake alimshangaa maana alimpita ukumbini bila kumsemesha chochote, kwa vile yeye alifika mwanzo kabla ya mamaake basi hakutaka kuzungumza na yeyote , dakika chache bi Huba na yeye alifika akiwa haihai hali ambayo ilizidi kumchanganya babaake Mamy, wote walikisogelea chumba cha binti yao na kuanza kugonga mlango bila mafanikio yoyote, ni sauti ya kilio pekee ndio walifanikiwa kuisikia.

"Kuna nini? Mbona siwaelewi!! Aliuliza babaake Mamy kwa hofu huku akimtazama mkewe aliyeonekana kuchanganyikiwa, hakupewa jibu lililoeleweka hali ambayo ilimzidishia wasiwasi.

Ilipita robo saa nzima chumba kikiwa kimya hata kilio kama kile cha awali hawakusikia, hofu juu ya binti yao iliongezeka , lakini kwa vile walikua pembeni ya mlango basi waliamua kugonga tena ila hakuna walichoambulia zaidi ya ukimya , juhudi na maneno mazuri yenye ushawishi ziligonga mwamba hadi kufikia uamuzi ya kuvunjwa mlango.

Sauti ya kilio kikali kutoka kwa mama mzazi ndio ilisikika, kwa mwendo wa haraka mikono ikiwa mdomoni alimfuata Mamy aliyekua chini huku mapovu yakimtoka mdomoni na kifungashio chenye picha ya panya kikiwa kando yake, muonekamo wake ulidhihirisha kua roho yake tayari iliachana na kiwiliwili, hakua na nguvu ya kulia tena zaidi ya kutulia tuli kama sanamu lililokosa mteja huku machozi yakimtiririka.

Baba wa Mamy alimtazama kwa uchungu bintie ambae hakuonyesha dalili za uhai, roho ilimuuma kuona mtoto wake wa pekee akipoteza uhai kwa namna ile, viulizo vingi vilikua kichwani mwake asijue nini kimemfika mwanawe, alimsogelea na kumkumbatia mkewe ili watiane ujasiri wa kukabiliana na kile ambacho wanakiona, hawakutamani iwe hata ndoto maana sio tukio zuri, alijaribu kumtazama na kumchunguza bintie kwa mara nyingine pengine kunaweza kua na mabadiliko ila alibahatika kuona karatasi ambayo bila shaka ilikua na ujumbe, taratibu aliichukua huku mikono ikitetema na jasho jembamba la vidole likimtoka.

KWENU WAZAZI...

Mnisamehe kwa hili licha ya kwamba litawaumiza, kama ndege wafananao hutua tawi moja basi naamini huu ni mti ambao tumeuchagua mimi na Baraka, yawezekana mti huu ukawa na kivuli kitakachotufanya tupumzike kwa amani, naamini pia tutakua na maisha bora zaidi ya haya tuliyoyaishi hapa, hata ndoto zetu naamini tutazitimiza kwa maana tulikua na imani sawa, siwezi kusoma bila uwepo wa Baraka na wala siwezi kupiga hatua yoyote pasipo na Baraka.

Najua kwamba mlinipenda sana wazazi wangu na kila ambacho nilikitaka mulinipa kwa wakati , ila hamkufanikiwa kunitendea jambo moja tu, hili jambo ndio limewapeleka mukanikosa leo hii, WAZAZI WANGU hamkuziheshimu hisia zangu wala hamkuwahi kulitilia maanani lile lililonitatiza....au ndio tunaishi kwenye dunia ya KILA MTU ABEBE MSALABA WAKE? Na ile zama ya MTOTO WA MWENZIO NI WAKO tukaifukia ardhini! Imeniumiza mno na moyo wangu haukuridhishwa na maamuzi ya Baraka na hii yote imetokana na jamii yetu jinsi inavyotuchukulia sisi watoto.

Kama kizuri kinaundwa basi naamini matendo ya mama Baraka yangebadilika, Kila kitu kina chimbuko lake hatukutakiwa kumhukumu hadi kizazi chake, hata wewe MAMA mwishoni ulidiriki kunivua imani uliyonivisha miaka mingi, uliwaamini wao kuliko mimi mwanao? Uliwasikiliza wao kuliko mimi? Unakijua alichokitaka mwalimu Mkandarasi kwangu? Mmmmh sina mengi nawaachia JIULIZE yenu iliyojaa uozo .
Mamy Baraka..... ❤️

"Mke wangu nilikwambia zamani kuhusu huyu mtoto ona sasa....tumempoteza kwa uzembe wako , kwanini mambo yote haya yanatokea unakua kimya? Ona sasa ...faida yake nini? huyu mwalimu Mkandarasi kafanya nini kwa binti yangu? Aliuliza baba wa Mamy kwa hasira.

Bi.Huba alibaki kulia asijue cha kujibu baada ya kuona hasira za wazi kwa mumewe, alitamani kusema kitu ila mdomo bado ulikua mzito mno, machozi ndio ambayo yalizungumza kile anachokisikia moyoni mwake, hata mumewe aligundua hilo ila hakua na cha kufanya.

***************

Kama hatua ndefu hutumika kufupisha mwendo basi Baraka na Mamy waliamua kuyafupisha maisha yao, familia ya Mamy ililazimika kuungana na familia ya Baraka lengo ikiwa ni kukienzi kile ambacho watoto wao walikiacha. Wote wawili walizikwa sehemu moja na kila ambae alifika msibani kwao basi hakuacha kuangusha chozi. Ilihuzunisha ila hakuwepo ambae angekua na uwezo wa kubadili ukweli.

Baada ya mazishi kumalizika Sadifa aliomba muda wa kuzungumza machache kabla ya watu kutawanyika, kila mmoja masikio yake aliyategesha kwa lengo la kutaka kusikia nini kitakachosemwa, hii aliifanya kwa lengo la kutimiza alichotakiwa kufanya na kijana wake.

"Najua nimewakosea wengi Jiulize hii, hata wale niliowaumiza na kuwavunja moyo ni wengi ila kamwe hamkunilipa ubaya , wote mumeungana na mimi kumstiri mwanangu, Nimejifunza kua ubaya haulipwi kwa ubaya japo kua sikulitilia maanani hapo mwanzo na haya ndio madhara yake, sikupaswa kumchukia na kumkomoa kijana wangu Baraka sababu ikiwa ni matendo ya uovu kwa babaake, alinitendea mengi Mshirazi......." aliongea Sadifa kwa upole na kusita kidogo kuacha machozi yaanguke, hata watu wa Jiulize walisimamisha masikio yao ili wasipitwe na neno.

"Nadhani wengi wenu hakuna asiyemjua Mshirazi, ingawa alikuja kama Mkandarasi wa soko kuu la Jiulize ila mapenzi kati yetu yaliingilia kazi yake, sikutazama alipotoka wala ukoo wake ila niliangalia uzuri na maokoto, mazima nilizama na kujiachia kwake, Mshirazi alinipa kila nilichotaka tena kwa wakati sahihi, Jiulize hii ndio ilimbadilisha Mshirazi wangu maana baada yamimi kuonekana nang'aa basi na wengine walitamani, badala ya kuwa wangu Mshirazi alikua pata sote, tuligombana kiasi ambacho ilipelekea kuachana, hakuniacha mtupu ila aniachia ....." kilio ndio kilisitisha simulizi ya bi.Sadifa na kufanya wengine wabaki wakimtazama.

" Siku ya mwanzo kujigundua kua ni mjamzito nilifurahi mno, nilifurahi baada ya kuona nakwenda kuongeza familia baada ya wazazi wangu kufariki, niliamini kua hii ni Baraka , hata sikumchukia Mshirazi maana nilikua nampenda sana hivyo niliamini kaniachia kumbukumbu tamu mbeleni, sikuamini mimi sikuamini........kumbe Mshirazi alianiachia gonjwa hatari , ugonjwa ambao ulikwenda kuibomoa furaha yangu na kuijenga chuki moyoni mwangu......" kilio chake kilichobeba kwikwi kilizidi kuwaumiza waliokua wanamsikiliza .


"Chuki yangu na Baraka ilianzia hapa, nilijaribu mara nyingi kuuharibu ujauzito wake ila uligoma , hata nilipomzaa nilitaka kumdhuru ila bi.Mwinde alimsogelea na kumkinga, ilipita mwezi sikuwa nimempa jina ila bi.Mwinde alimpatia jina la Baraka, Mshirazi kayaharibu maisha yangu,Jiulize ilinipeperushia furaha yangu kwanini na wao nisiwaumize? Nilijiapiza na nyinyi lazima muumie, nisameheni kwa kuwaenezea ugonjwa, hata ukaribu wa Mamy na Baraka sikuutaka kwa sababu niliona mwenyewe namna ambavyo Mamy alimpenda kwa dhati Baraka, nihukumuni ikiwa mnahisi kuna adhabu inanifaa" alimalizia bi Sadifa huku mtandio wake wote ukirowana machozi na kamasi.


Kila aliyejijua mumewe au mwanaume wake kaangukia mikononi mwa bi Sadifa basi alilia kwa uchungu, mwalimu Swami, Ndaze na wengine wengi walibaki wakigaragara chini na kumlaani vilivyo bi.Sadifa, walikua wanaamini kuwa kivyovyote vile na wao wameathirika, makaburini palikua hapatoshi, kumbe Mkandarasi alikiwa pembeni bwana! Hata yeye alijikuta akiumia maana aliwahi kutembea na bi.Sadifa bila kutumia kinga yoyote , mamaake Mamy alibahatika kumuona mwalimu Mkandarasi akiwa kwenye sura ya taharuki, kwa hasira alimsogelea na kuanza kumkunja huku akimtupia maneno.


"Mwalimu mpumbavu sana wewe!! Hivi unajua jamii na serikali yetu inakuaminii kiasi gani? Kwanini umeondoa vazi la heshima ambalo umevishwa, bila ya shaka hii simulizi ya Sadifa imekugusa eeeh!! Sijui umetembea na wanafunzi wangapi ila najua umeharibu sana....chuki yako kimahusiano ndio imesababisha nishindwe kuwa upande wa mwanangu...aaaaagggh" alilalamika na kulia mamaake Mamy huku bado akiwa kamshikilia shati mwalimu Mkandarasi na kumtikisa.

Hata baba mzazi wa Mamy alimsogelea na kuanza kumtupia lawama, alimtaka akiri hadharani makosa yake kabla hawajaamua kumuadhibu, Angefanya nini mwalimu wa watu? Aliweka bayana kila uovu alioufanya kwa wanafunzi wake, alikubali pia alikua mbioni kumvaa Mamy ambae alikua mgumu. Alikiri kila uovu na njia alizotumia kumuweka matatani Baraka, mwisho aliwataka wanafunzi wa kike wakachunguzwe afya zao ili wazijue hali zao, wanafunzi wengi ambao walihudhuria mazishi walilia baada ya kusikia hayo.

Kwa vile mwenyekiti akikuwepo basi alipiga simu polisi na mwalimu Mkandarasi akawekwa chini ya ulinzi. Kesi dhidi yake ilifunguliwa, ushahidi ulikusanywa kwa wanafunzi wengi ma kuhukumiwa kifungo cha maisha.

Kila siku zilivyosogea ndivyo hali ya bi.Sadifa ilizidi kudumaa, hakua na mpangilio mzuri wa kula wala kufanya chochote, kifo cha Mamy na Baraka kilimuumiza sana , mwisho wa siku mawazo yalimuandana na kuamua kujiua kwa kujichoma kisu na kuacha ujumbe ambao ulisomeka👇

KWENU WAZAZI:
NI JUKUMU LETU SOTE KUWALINDA NA KUWATUNZA WATOTO WETU, WANAPITIA MAMBO MENGI MAZITO WAKIWA SHULENI NA MITAANI, VITA KATI YA MAMA NA BABA AU FAMILIA VISIMHUKUMU MTOTO.TUWATUNZE MAANA WAO NDIO HAZINA YETU.

MWISHO..
 
Back
Top Bottom