Mambo ambayo watanzania wengi mpaka wasomi wanayaongea kana kwamba wana ushahidi nayo kwa 100% wakati huenda sio kweli hata kidogo..

Kumbe hupingi kama hayo mambo yanaweza kuwa kweli. Basi yaache hivyo hivyo. By the way mbona ni namba 7 tu ndio ya uongo hapo?
Sijakataa kwamba yasemwayo huenda yapo ila kitu kama huna ushahidi nacho kwanini ukikomalie kuaminisha watu kana kwamba ulikiona??
mb
 
Na maofisa wenzako wanakujua ni mmbeya kwahiyo huwa wanajadili ujinga ukiwepo ila ukitoka tu ndio wanajadili Madili ya hela
 
Bivi na wewe ni afisa au ofisa
 
Aise umenichekesha sana this is funny ila akili zetu watanzania wakati mwingine, yani kwa umbeya na porojo tupo vizuri kwa kweli
 
5 na 6 kuna uwezekano mkubwa ni ukweli
Mh embu acheni uzuzu sasa ajifiche kwa kitu gani, kwani angekuwa hai kama mamlaka zimeamua asifanywe chochote nini mtafanya
Dpp ana final say nani ashtakiwe na nani asishtakiwe kwa maslahi ya nchi
Kuna mambo mangapi ya ajabu yamefanyika nchi hii na wote tumekaa kimya
 
Mimi ndiyo maana sitaki kusafiri kwenda nchi za watu kwenda kutafuta maisha nakomaa hapa hapa kwa sababu ma zero brain wengi hapa nchini ni mtaji mkubwa kwa kutusua maisha kwa mwenye akili
 
Hapo kwenye Corona na Jiwe ✅
 
9.Ukisomesha mtoto wako shule ya English Medium, atakuja kuwa Doctor, Engineer, Pilot au Mwanasheria
 
Yote hayaumizi zana ila hiyo namba nne hapo aisee ramli chonganishi
 
9. Huwi tajiri mpaka uwe mchawi. Pia huwezi kufanikiwa katika kuchimba madini mpaka uwe mchawi.

10. Mwenge kuhusishwa na Imani za kishirikina. Na kiongozi wa mbio za mwenge lazima afe siku chache tu baada ya kukimbiza mwenye.

11. Kilimanjaro na baadhi sehemu za nchi hazikupaswa kuwa sehemu ya Tanganyika. Mwl. Nyerere alifanya ujanja kuzileta Tanganyika.

12. Wachina hujenga usiku Kwa sababu za kishirikina.

13. Fimbo ya Mwl. Nyerere ilikuwa Inampa taarifa juu ya matukio ya mbele katika muda, kama vile ajari, hivyo Mwl. Alichukuwa tahadhari kabla ya kwenda sehemu fulani au kufanya jambo fulani.
 
14. Mwalimu Nyerere alikataa kumpa mkono malkia Elizabeth wa Uingereza badala yake akampa kifimbo ashike kwa sababu malkia alivaa "Gloves" kama ishara hataki ashikane mkono na mtu mweusi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…