Mambo madogo ambayo Wanandoa ama Wapenzi wanaoishi Pamoja wakifanya yanaweza kuzalisha migogoro kwenye mahusiano

Mambo madogo ambayo Wanandoa ama Wapenzi wanaoishi Pamoja wakifanya yanaweza kuzalisha migogoro kwenye mahusiano

yes yes no mara waaaaa nyie tupendeni tu babuuuuu,,tumeumbwa kwaajili yenu😌
Hakika Mjukuu, maisha yafaa nini bila ninyi.

Mimi nikiambiwa chagua fedha ama ninyi, nitachagua ninyi 😜
 
Hakika Mjukuu, maisha yafaa nini bila ninyi.

Mimi nikiambiwa chagua fedha ama ninyi, nitachagua ninyi 😜
Sasa wewe utaishi maisha marefu yenye furaha 🤣🤣🤣 sio watu humu wanajitia ushababi wanashindana na mwanamke 😅😅 they will end up be miserable in their whole life. Maisha/kuishi na watu ni michezo ya akili sio miguvu na ujuaji.
 
Jambo la kushauriwa na mke lina element nyingi za interest zake binafsi.
Sidhani kama ni sahihi, mpe nafasi mshauriane ukiona anachokushauri hujakipenda mpe facts kwanini unakataa Ushauri wake.

Lakini haifai Mipango yenu ya maendeleo ya familia usimshirikishe Mkeo badala yake ukamshirikishe mtu baki.
 
Sasa wewe utaishi maisha marefu yenye furaha 🤣🤣🤣 sio watu humu wanajitia ushababi wanashindana na mwanamke 😅😅 they will end up be miserable in their whole life. Maisha/kuishi na watu ni michezo ya akili sio miguvu na ujuaji.
Na iwe hivyo Mkuu, maisha yenyewe ndiyo haya haya

Let's enjoy it to the fullest 🤗
 
Sidhani kama ni sahihi, mpe nafasi mshauriane ukiona anachokushauri hujakipeda mpe facts kwanini unakataa Ushauri wake.

Lakini haifai Mipango yenu ya maendeleo ya familia usimshirikishe Mkeo badala yake ukamshirikishe mtu baki.
Mke mshirikishe ila kuwa makini na ushauri anaokupa.
 
Babuuuu babuuuuu hapa umenipiga kamba nzito sana
Hahaha...............huamini Mjukuu?😅

ukija kunisalimia Mwezi December, niletee hela halafu uniambie nichague ukae Siku zote 28 za Likizo ama unipe hela za Kiko uondoke baada ya Siku 1.

Nitakwambia usinipe hela ya Kiko ila ukae na Mimi Babu yenu Mwezi mzima 😜
 
Mke mshirikishe ila kuwa makini na ushauri anaokupa.
Ni sahihi Mkuu, naunga mkono hoja yako

Ni lazima kuchuja Ushauri unaopewa

Kumbuka kisa cha kwenye Biblia, kuhusu Mke wa mfalme kudai zawadi ya kichwa cha mtume Yohana badala ya zawadi nyinginezo ya dhahabu n.k
 
Hahaha...............huamini Mjukuu?😅

ukija kunisalimia Mwezi December, niletee hela halafu uniambie nichague ukae Siku zote 28 za Likizo ama unipe hela za Kiko uondoke baada ya Siku 1.

Nitakwambia usinipe hela ya Kiko ila ukae na Mimi Babu yenu Mwezi mzima 😜
babu unazeeka ila swaga zinazid kurudi ujanani,🙄we mzee weweeee
 
Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la wandoa wapya ama Wapenzi waliokuwa wakiishi pamoja Kwa muda mrefu kuingia Kwenye migogoro na hatimaye Ndoa zao kuvunjika ama wakati mwingine uchumba wao wa muda mrefu kuvunjika.

Tukiwa kama Wazazi ama watu tulioishi na kupitia mahusiano tunaweza kuwa na cha kuwafunza Vijana wetu wanaotarajia kuingia Kwenye maisha ya Ndoa ama Wapenzi wapya ili kuwasaidia kupunguza migogoro isiyo ya lazima kwenye maisha yao ya mahusiano.

Kwa maoni yangu, yafuatayo hapa chini ni baadhi ya mambo madogo dogo ambayo ukifanya yanaweza kuzalisha migogoro isiyo ya lazima Kwa wapenzi ama Wanandoa watarajiwa;

Mosi, Kutokula Chakula kilichoandaliwa na Mke wako/Mpenzi wako.
Kuna baadhi ya Wanaume wenzetu, kupitia mizunguko waifanyayo Mchana kutwa, huwapelekea wakati mwingine kula huko huko, hivyo wanapokuwa wamerudi nyumbani kwao kushindwa kula chakula kilichoandaliwa na Mke/Mpenzi wake. Jambo hili halina afya kabisa kwenye maisha yenu ya Ndoa na mapenzi, hata kama ulilazimika kula huko Mtaani, hakikisha unaacha sehemu ya kula chakula alichokuandalia Mkeo/mpenzi wako.

Pili, Kunyoa mavuzi kabla ya kusafiri ama ukiwa huko huko safarini.
Kufanya hivyo kuna mjengea mwenzako taswira ya kuhisi kwamba uendapo unaenda kuchekupa ama ukiwa huko huko safarini ulichepuka ndiyo maana umerudi umeshanyolewa huko Ikulu ndogo.

Tatu, Kupunguza ghafla idadi ya round Kwa Mkeo ama Mpenzi wako mara baada ya kurudi kutoka safari, hii moja Kwa moja mpenzi wako atahisi ulipotoka umetumika sana, hivyo nguvu wamekumaliza.

Nne, Kutoa manii(shahawa) kidogo mara baada ya kurudi safari yako ya kikazi.
Unapokuwa haujashiriki ngono muda mrefu iwe Siku 3,4 ama Wiki ukikutana na Mkeo/mpenzi wako lazima utakojoa manii nzito nzito, iwapo utakuwa umetumika Siku kadhaa nyuma kabla ya kurudi nyumbani, Mkeo anaweza kujua hivyo kuzalisha migogoro isiyo ya lazima.
Ndiyo maana Wazee wenu badala ya kunywa soda tunaagiza Korosho ama Karanga mbichi ili kufukia mashimo mashimo ya njiani.

Tano, Kuchati na simu muda mwingi wa Usiku unapokuwa nyumbani na familia.
Hii hata kama Mkeo/Mpenzi wako hana D mbili lakini atahisi unamchepuko wako unaochati nao muda huo.

Sita, kwenda kuangalia Mpira kwenye Mabaa wakati nyumbani umefunga DStv/Azam Tv.
Hata kama hajawahi kukwambia, lakini jambo hili lazima linamkera mwenzako, na kuna Siku litawaletea migogoro isiyo ya lazima.

Saba, Kucheza Vikoba ama kukopa Mikopo mbalimbali pasipo kumshirikisha Mume wako.
wapo baadhi ya Wanandoa/Wapenzi wanakopa fedha/Vyombo pasipo kumshirikisha Mume wake, Mume anakuja kujua baada ya Mke kufatwa na kudaiwa yeye akiwepo ama wakati mwingine kutumia fedha aliyoachiwa ya Matumizi kulipa madeni kisha familia kushindwa kula Siku hiyo.

Haya ni baadhi ya mambo madogo dogo ambayo yanamkera mwenzi wako na wakati mwingine ndiyo chanzo cha migogoro mingi katika Ndoa na maisha mengi ya mahusiano.

Yapo mengine mengi ambayo mnahisi yatakuwa ndiyo chanzo cha hiyo migogoro katika mahusiano yetu.

Tunaweza kusaidiana kushea ili kuwasaidia Wanandoa wapya ama Wapenzi watarajiwa.
Naam!!
 
Ujumbe mzuri Sana
Kama wanaume watakuwa n mambo haya ndo nying zitadumu na mahusiano mengi yatadumu
 
Back
Top Bottom