Mambo matatu Muhimu kabla hatujamsahau Hayati Dkt. Magufuli

Mambo matatu Muhimu kabla hatujamsahau Hayati Dkt. Magufuli

Unaandika ujinga na bado unajiaminisha una akili, aliyekuroga kafa, Go figure
Muda mwingine ni ngumu sana kujipima uwezo wako wa kufikiri hivyo haina haja ya kubishana .
 
Hayati JPM kama angaliweza kutii sheria na katiba kwa kuzingatia masuala muhimu ya kiutu na kidemokrasia, utawala wake ungaliweza kuweka alama muhimu sana katika historia ya nchi yetu. Uthubutu wake wa kufanya maamuzi magumu ili kulinda rasilimali za nchi yetu na kwa maslahi mapana ya nchi yetu ni sifa kubwa ambayo alikuwa nayo.

Kurudisha nidhamu ya utendaji na ufanisi katika ofisi za umma pia ni kongole nyingine kwake. Kukemea kwa uwazi vitendo vya rushwa, uonevu na ukandamizaji wa kimatabaka pia ilikuwa ni "credit" nyingine kwake. Na hata pia uthubutu wake wa kuanzisha ama kuendeleza miradi mikubwa ya kimkakati kama vile mradi wa umeme wa bwawa la Nyerere.

Taifa linapaswa kuwa na "succession plan" na kuanza kuandaa viongozi waliopo ili waje kuwa baadaye viongozi wazuri hapo baadaye. Wananchi wengi hawatamani kuwa na Rais aina ya JPM kutokana na mabaya yake, ila wanatamani kuwa na Rais kama yeye kutokana na mazuri yake.

Kama tunataka kiongozi mwenye haiba ya JPM kwa upande wa mazuri yake, yaani mwenye uthubutu wa kufanya maamuzi magumu, na watu wakatambua kuwa yupo "serious" na hata kuupelekea umma kutii kwa dhati, basi naweza kuwataja Tundu Lissu ama Mwigulu Nchemba, pengine pia yupo Kassim Majaliwa.

Hawa ni watu ambao wanaweza kuanza kuandaliwa ili kama wakifanikiwa kushika uongozi wa juu wa nchi wasigeuke kuwa viongozi katili na madikteta. Kama ni uthubutu wa kukemea, kuamua na kufanya maamuzi magumu hii sifa wote wanayo.
Mwigulu huyo ni katili mwandamizi
 
Tanesco wana kiwanda cha mita?
Mbona kampuni za simu hazigawi bure simu?
Hapa mkuu hujaelewa nini maana ya matumizi mtaji( capital expenditure ) na matumizi yasiyo mtaji (Revenue expenditure).Nguzo,meter,waya nk vinapaswa kugharimiwa na Serikali ( kupitia Tanesco) kwa kuwa ndio vinavyowezesha kazi ya kuwaunganishia wateja wengine wengi zaidi (na hivyo kuongeza mapato ya Tanesco )-hii ndo capital expenditure kwao, hivyo inabidi wakakope au wafanye vyovyote ili wapate mtaji, wauendeleze na kufanya biashara yao iwe endelevu.Sisi watumiaji wa umeme tuendelee kulipa bili ipasavyo ( na hivi kuna LUKU ndo kabisa hakuna anaekubali kulala giza eti kisa umeme umeisha!-nasi tutapambana mpaka uwe unawaka kila tunapouhitaji)-Hii ni Revenue expenditure ambayo tabia yake kuu ni kujirudiarudia(tunanunua umeme kila siku,wiki,mwezi nk) ila nguzo au mita ni Mara moja tu.SHIDA HAPA bila kupepesa macho ni kwamba hawa TANESCO hawana mshindani ndio TATIZO kubwa.Sheria zibadilike ili kuwepo na ushimdani katika uzalishaji na usambazaji wa umeme.Mfano mzuri ni kampuni za simu za mkononi(wateja tunaenjoy kwa kuchagua kampuni unayoona inakidhi unachokitaka).
 
Hayati JPM kama angaliweza kutii sheria na katiba kwa kuzingatia masuala muhimu ya kiutu na kidemokrasia, utawala wake ungaliweza kuweka alama muhimu sana katika historia ya nchi yetu. Uthubutu wake wa kufanya maamuzi magumu ili kulinda rasilimali za nchi yetu na kwa maslahi mapana ya nchi yetu ni sifa kubwa ambayo alikuwa nayo.

Kurudisha nidhamu ya utendaji na ufanisi katika ofisi za umma pia ni kongole nyingine kwake. Kukemea kwa uwazi vitendo vya rushwa, uonevu na ukandamizaji wa kimatabaka pia ilikuwa ni "credit" nyingine kwake. Na hata pia uthubutu wake wa kuanzisha ama kuendeleza miradi mikubwa ya kimkakati kama vile mradi wa umeme wa bwawa la Nyerere.

Taifa linapaswa kuwa na "succession plan" na kuanza kuandaa viongozi waliopo ili waje kuwa baadaye viongozi wazuri hapo baadaye. Wananchi wengi hawatamani kuwa na Rais aina ya JPM kutokana na mabaya yake, ila wanatamani kuwa na Rais kama yeye kutokana na mazuri yake.

Kama tunataka kiongozi mwenye haiba ya JPM kwa upande wa mazuri yake, yaani mwenye uthubutu wa kufanya maamuzi magumu, na watu wakatambua kuwa yupo "serious" na hata kuupelekea umma kutii kwa dhati, basi naweza kuwataja Tundu Lissu ama Mwigulu Nchemba, pengine pia yupo Kassim Majaliwa.

Hawa ni watu ambao wanaweza kuanza kuandaliwa ili kama wakifanikiwa kushika uongozi wa juu wa nchi wasigeuke kuwa viongozi katili na madikteta. Kama ni uthubutu wa kukemea, kuamua na kufanya maamuzi magumu hii sifa wote wanayo.
Tatizo katiba tuliyo nayo ni mbovu hata angeifuata bado ingempa madaraka makubwa mno
 
Nimeamini mtu asipokuwepo ndo thamani yake inaonekana. Kuna vitu sikuvipenda enzi ya Magufuli. Ila Magufuli ni bora kuliko aliyepo. Hivi huyu mama hajui hata wananchi wanyonge wanahali gani. Zaidi ya kuweka tozo na kupanda ndege Zanzibar Dodoma Dar es salaam and the vice-versa .
Aa wapi hiyo thaman mnaona nyie tu
 
Katika Nchi ambayo Viongozi wanajipimia kama hii Tanzania ya Sasa tunahitaji vitu vitatu :-

1. Katiba Mpya ,tunahitaji katiba inayong'ata ili viongozi na wananchi waheshimu madaraka.

2. Chama kimoja (ingawa linaendana na katiba),Tanzania bado ni nchi changa kuwa na mfumo wa vyama vingi hivyo tunahitaji chama imara kimoja. Mfano Nchi ina changamoto nyingi Rais yuko bize Kutatua changamoto za wananchi kiongozi wa Upinzaniyuko Mwanza anaorganise issue kubwa kama ya kudai katiba mpya ,nchi haiwezi kwenda hivyo.

3. Tunamuhitaji Mao Zedong. Itachukua Muda kwa watu wengi kuja kuamini kwamba JPM alikuwa mzalendo wa kweli pamoja na mapungufu yake ,ni ngumu kuendesha nchi kama Tanzia ukacheka na watu na mambo yakaenda,Na sio kwamba aliua upinzani ni ukweli usipingika bado Hatujafikia kuhitaji vyama vingi.

Rais Samia Suluhu Hassan ni rais Mzuri ana mipango mizuri ,tatizo Moja kubwa Anatafuta hela nyingi na kwa kuwakamua Wananchi kisha Watu wachache wanatafuna pesa na nyingine ndio zinaenda kwenye eneo husika .Mama kama ataweza thibiti Upotevu wa Hela kuna uwezekano mkubwa baada ya miaka 5 tutakuwa Mbali sana.
Mbona jpm tumeshamsahau kitambo sana. Bora hata kashasha anakumbukwa
 
Tanesco wana kiwanda cha mita?
Mbona kampuni za simu hazigawi bure simu?
Je kabla kampuni ya simu haijasambaza huduma za mtandao wake, huwa wanamlazimisha mteja alipie gharama za minara?

Hata kama kampuni za simu zinawauzia watu simu, hizo simu si zinakuwa mali ya mteja?
 
Kwasababu Magufuli aliwaondoa kwenye baraza kwa chuki zake binafsi sivyo, kwa mama samia naye aendeleze chuki zile zile

Sio chuki binafsi..dharau za kupitiliza kwa hao vijana ndio jamaa akawaweka pembeni huwezi kumwambia mzee sisi ndio tumekuweka hapo…hayati umwambie hivyo akuchekee…
 
Ni vile uchaguzi wa haki na uwazi ccm haishindi hata sekunde moja ila kwa ile style ya kina Nape na jamaa zake watashinda tu, uchaguzi ukifika BiM ataendelea kuwa rais ila siyo rais wa watanzania kwa uchaguzi sababu mpaka sasa dalili zinaonyesha hali tete kutokea huku mtaani.
 
Ni vile uchaguzi wa haki na uwazi ccm haishindi hata sekunde moja ila kwa ile style ya kina Nape na jamaa zake watashinda tu, uchaguzi ukifika BiM ataendelea kuwa rais ila siyo rais wa watanzania kwa uchaguzi sababu mpaka sasa dalili zinaonyesha hali tete kutokea huku mtaani.
Hali ya uchumi ni mbaya hakuna unaloshika linakwenda.
 
Lete Ushaidi kuwa huyo mungu wenu magufuli miradi yote alikuwa ashailipia hela? Huyo sindio alikuwa anawadanganya mazuzu Kama wewe kuwa miradi yote anajenga kwa fedha za ndani!
Mtamkumbuka tu siku moja
 
Tanesco wana kiwanda cha mita?
Mbona kampuni za simu hazigawi bure simu?
Yes hazigawi simu bure...bt simu ni mali ya mteja au ya kampuni za simu?

Kwa mfano wako huu inamaanisha kua Nguzo na mita zilipaswa kua mali ya Mteja, je ndivyo ilivyo?
 
Back
Top Bottom