Mambo mawili yaliyonishangaza Tanga

Mambo mawili yaliyonishangaza Tanga

Ulifata nini kwamgwe? Uliingilia michungwani? Vipi ulipita Ngojoro, Kambini je?
Sasa ngoja nikufungue.
kile kijiji ndio kilikua cha kibiashara enzi hizoo.Kilikua na utajiri mkubwa uliotokana na kiwanda cha kuchakata mkonge tunakiita Korona. Kipo mbele kidogo kuna kota za kambi.
Palizaa matajiri wakubwa tu wa Tanga mfano Sefu Mwarabu aliyekua anamiliki mabasi ya Zafanana.
Pia kulikua na utajiri wa kikoloni aka Rupia watu washatoka sana pale.
Kule mkundi ulifika? Kuna kisima cha kijerumani kina maajabu, wwakati wa mvua (masika) maji hupungua lakini wakati wa ukame (kiangazi) maji hujaa na kumwagika.
Siku nyingine ukija kwamgwe aka Bondo niambie nikutembeze nikuonyeshe maeneo ya historia.
 
Ndugu mtembezi, almost Tanzania yote iko hivyo tembea ujionee,
Mwaka 2014 niliwahi kwenda Itirima Simiyu aisee siyo mchezo
 
Huko Tanga ni mbali mkuu, juzi nilkua naangalia ITV kipindi cha ripoti maalumu nililia mkuu. Katikati ya jiji la Dodoma ambako ni makao makuu ya nchi na imejengwa Ikulu kuna watu ni maskini wa kutupwa maana tukisema uwazike utakua umewapandisha hadhi. Hapo Dodoma kuna soko la Msalato, wakazi wa jiji wanaenda kuoteza mabaki ya mifupa ya nyama kwa ajiri ya mlo.!!!!
Acha kuleta uwongo unamdanganya nani ambaye hajafika Dodoma...soko la nyama la msalato machinjio yapo palepale kwa nyuma hatua chache tu sasa utasemaje wanakula mabaki ya mifupa😀😀
 
Acha kuleta uwongo unamdanganya nani ambaye hajafika Dodoma...soko la nyama la msalato machinjio yapo palepale kwa nyuma hatua chache tu sasa utasemaje wanakula mabaki ya mifupa[emoji3][emoji3]
Mkuu nimetoa reference!! Ni kipindi cha week cha Ripoti Maalumu cha ITV, ingia YOUTUBE uone maajabu!! Watoto wanaokota mifupa ilitupwa chini na kuanza kula palepale nyingine wanaweka kwenye mifuko wanapeleka nyumbani kupika. Mwandishi kaenda nao mpaka home wakamwonyesha wanavyopika. Kuna mwanasaikolojia mmoja aliojiwa akasema huu ni zaidi ya unyama kwani hata mbwa ambaye ni well trained hawezi kula mabaki ya mifupa

itv njoo mtusaidie link
 
Habari zenu wana JF,

Wiki moja iliyopita nilifanikiwa kusafiri kutoka mkoani Arusha hadi mkoani Tanga hasa katika wilaya ya Handeni vijijini. Kwakweli tembea uone. Nilipofika Handeni vijijini kuna kijiji kinaitwa (Kwamgwe) nilishangazwa na mambo makubwa mawili. Mambo gani hayo?

Jambo la kwanza ni umasikini wa kutupwa, yaani watu waishio Handeni vijijini hasa katika kijiji hicho ni fukara sana. Mfano nyumba nyingi ni za miti iliyokandikwa na udongo na juu zimeezekwa kwa nyasi. Asilimia 97 ya watu waishio katika kijiji hicho nilichokitaja wanaishi hivyo. Kiufupi Maisha yao ni mabaya sana.

Nimefanikiwa kutembea maeneo mengi nchini na kuoña umasikini ambao tumeuzoea, kama vile nyumba duni zilizojengwa na matofali ya udongo pamoja na kuezekwa na bati za kawaida lakini kule Handeni vijijini nyumba za miti ndio nyingi na nyingi zimeezekwa kwa nyasi.

Baadae nilijiuliza maswali mwenyewe kwamba kwamba familia za kule hazina kipato cha kuwasaidi kufyatua matofali ya tope au ndio wameamua tu kuishi hivyo?

Jambo la pili lililonishangaza Uziguani nadhani litakuwa ni sehemu ya mila za watu wa huko (Wazigua).J ambo Hilo ni kutembea peku peku tena umbali mrefu. Wazigua wa Handeni vijijini wanapenda sana kutembea peku peku kwa watu wa rika lote iwe vijana, watu wazima, au wazee.

Mfano wakati nafika huko lilikuwa ni kipindi cha mvua sasa nikawa naona tu watu wakikanyaga tu matope peku peku wakiwa wanaenda katika shughuli zao mbalimbali. Karibu na wewe kama una chochote cha kuchangia.
Huko ndio kwa kina mwana FA na lulu diva hata kwao kupo hivyo hvyo ila mashauzi mengi mjini.
 
Jimbo linaloongozwa na CCM na Juma Aweso Waziri wa Maji.

Handeni wananchi wote ni CCM ili ujue na ujifunze madhara ya CCM kujikita mahali
Aweso kwao ni pangani huko ni kwa kina mwana FA
 
Na ndiyo mvaa bendera ya taifa shingoni anataka wapewe TIN namba.
 
Napapenda Tanga ila asilimia kubwa ya watu wakule wamezidi uvivu,umwinyi na mambo ya ushirikina,we cheki barabara tu yakuwasaidia wenyewe walikua wanagoma isijengwe haha sehemu itakua na maendeleo kweli
 
Handeni kuna umaskini wa kutupa kweli wala si uongo.

Sijui tunatokaje hapo.

Nimeshangaa nilipoenda Lushoto walau kule sijaona Nyumba ya nyasi, sijaona mwenda pekupeku.
 
Huko Tanga ni mbali mkuu, juzi nilkua naangalia ITV kipindi cha ripoti maalumu nililia mkuu. Katikati ya jiji la Dodoma ambako ni makao makuu ya nchi na imejengwa Ikulu kuna watu ni maskini wa kutupwa maana tukisema uwazike utakua umewapandisha hadhi. Hapo Dodoma kuna soko la Msalato, wakazi wa jiji wanaenda kuoteza mabaki ya mifupa ya nyama kwa ajiri ya mlo.!!!!
Dah nmeiona hii ITV aisee watu n maskin
 
Nyinyi na report zenu za NBS mnautaja mkoa wa kagera kuwa ndo maskini zaidi kisa unachangia pato dogo la taifa kuliko population yake....

Lakini Tazama maisha ya vijijini kagera....
Kwa kagera ukiiacha biharamuro na Ngara vijijini watu wana maisha bora kabisa na decent hasa vijiji vya wahaya na wanyambo

Hakafu unakuta mtu wa Tanga anasema wahaya wahaya[emoji23][emoji23]
Screenshot_20230516-000822.jpg
Screenshot_20230521-192417.jpg
Screenshot_20230516-001447.jpg
Screenshot_20230516-001220.jpg
Screenshot_20230516-001157.jpg
1684185512175.jpg


Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Sehemu yoyote wanayoendekeza uchawi kuliko chochote hapawezi kuwa na maendeleo daima. Handeni ni nyumbani kabisa, mimi ni Mzigua lakini sijawahi kukanyaga ardhi yake na sitathubutu kwenda, nisamehewe kama nafanya makosa.
 
Sehemu yoyote wanayoendekeza uchawi kuliko chochote hapawezi kuwa na maendeleo daima. Handeni ni nyumbani kabisa, mimi ni Mzigua lakini sijawahi kukanyaga ardhi yake na sitathubutu kwenda, nisamehewe kama nafanya makosa.

Usiende mkuu Njoo nikuuzie ukoo upate na kiamba huku mgombani
 
Acha kuleta uwongo unamdanganya nani ambaye hajafika Dodoma...soko la nyama la msalato machinjio yapo palepale kwa nyuma hatua chache tu sasa utasemaje wanakula mabaki ya mifupa[emoji3][emoji3]
We Mgogo masario sijui masare ya chama njoo uwaulize watu wenye TV sio unaleta umatonya hapa
Dah nmeiona hii ITV aisee watu n maskin
Huyo mgogo alikua anabisha anafunika kombe na mwanaharamu hapiti. Mpe story kidogo
 
Back
Top Bottom