Mambo muhimu niliyojifunza katika maisha yangu ya kuajiriwa

Mambo muhimu niliyojifunza katika maisha yangu ya kuajiriwa

Dah big sijawasiliana nae kitambo sana nadhani last time ilikuwa 2016, kwa sasa sijui yupo wapi
Mkuu
Ni kwamba kazi umekosa kabisa au ndio vile unapata lakini unaona maslahi hayaendani na hadhi yako?

Vipi,hujafikiria kuhusu kujiajiri?

Na kabla la ngekewa kukudondokea kwa Dr KJ, naamini ulikuwa unapambana huku na kule..

Je ni mbinu zipi ulizokuwa ujazitumia nyingine za kutafuta kazi?
Na vipi zile mbinu hujazitumia tena kwa wakati huu kipindi huna kazi?

...
Upande mwingine ningependa kuuliza kuhusu internships zilizopo kwenye hayo mashirika .
Kuna graduates wengi sana fresh from school..hawana experience ya aina yoyote,vipi je,wanayo nafasi ya kuweza kupata hizo nafasi?
Na kama ni ndiyo..je,Ni watu wa namna gani(vigezo) mliokuwa mhafanya nao hizo internship.
Hii inaweza kuwa msaada kwa namna moja ama nyingine kwa fresh graduates....hata pia experienced jobless graduate km Mimi.
 
EPISODE 9: Umeshawahi wahi kufanya kazi ambayo mda wote unakuwa bize kazini? Work-life balance is a must if don’t wish to go insane.
Baada ya kumaliza ile tripu ya Tabora na Kigoma salama at least nilikuwa nimeboresha uzoefu wa kazi za field kwenye hii ofisi mpya. Kumbuka kwamba nilibaki peke yangu baada ya kukubaliana na dadaB arudi home ila kutokana na kumsoma kwa mda mfupi na kuunganisha na uzoefu wangu wa kule kwa Dr KJ kazi ikawa rahisi sana kwangu. Hapo ndipo nikajua kwa nini waajiri wengi sikuhizi they prefer job experience than grade A academic certificates.

Nikarudi ofisini salama na kwa kushirikiana na dadaB tukasubb report pale na maisha mengine yakaendelea. Baada ya muda na mimi nikawa ni among senior officers pale hata nikawa trusted kuwa-mentor the new employees maswala ya kazi. Anyway it was good experience kwa kweli na niliinjoi sana kazi yangu.

Uzuri wa ile kazi ilikuwa ni kusafiri kitu ambacho nilikuja kugundua kumbe mimi napenda sana kusafiri tena hususani safari za mikoa ya mbali na vijijini nilikuwa napenda sana. Unajua kwenye kusafiri sio tu kuenjoy zile moments za kuwa kwenye gari au flight lakini inasaidia kuexplore new opportunitis na kuongexza network yako na watu tofauti tofauti unaokutana nao. Sasa pale ofisini ilikuwa ukikaa sana hujasafiri basi ni mwezi na nusu au miwili. Lakini kikawaida ilikuwa kila mwezi lazima mtu usafiri walau kwa si chini ya wiki, yaani safari ilikuwa ni lazima kulingana na nature ya kazi hususani kwenye idara yetu. Mimi ilifikia wakati mpaka nikawa nawatania watu kwamba sitakuja kuoa au kuruhusu mke wangu afanye kazi pale ofsini maana ndoa inaweza ikayumba hahaahaa sababu watu kila mara wapo safarini na hivyo mke anaweza kushindwa kutimiza majukumu ya nyumbani vizuri (jokes) with that job nilisafiri kila wilaya unayoijua wewe hapa Tanzania zilikzokuwepo kipindi kile. Utanitajia wapi nisipajue mimi.

Ofisi ilikuwa inakufacilitate kila kitu ukiwa safarini ili uweze kuendelea na majukumu yako ya kazi hata ukiwa nje ya ofisi. Mfano vitendea kazi bora kabisa laptops, vimodem kwa ajili ya internet vyenye unlimited bando nk. Kwanza ilikuwa ni marufuku staff kupanda mabasi haya abiria is either usafiri kwa gari ya ofisi sehemu ambako hakuna viwanja vya ndege au ukodi gari hata ktoka dar mpaka ifakara endapo usafiri wa ndege haupo na magari ya ofisi yapo na shughuli nyingine. Na ilikuwa lazima ulale sehemu yenye hadhi ya juu kulingana na eneo ulilopo ili kuwezesha usalama wako na pia mazingira rafiki ya kuendelea kupiga mzigo. Kifupi ilikuwa ukisafiri unasafiri na dawati lako maana kwa necha ya kazi ilikuwa huwezi kumuachia mtu akushikie shughuli zako maana utamuonea tuu, labda kama mtu ni mgonjwa, amefiwa au likizo za uzazi ilikuwa inaeleweka ila sio safari. Ukisafiri utawezeshwa kila kitu kusafiri na majukumu yako, hakuna kumuachia mtu ofsini.

Kwahiyo life pale ofsini ilikuwa ni mshike mshike, bize mda wote. Mtu kwenda weekend job au kuchelewa kutoka mpka saa tatu usiku ilikuwa ni kawaida sana. Yaani ilikuwa ukiangalia vimeo ulivyonavyo kwenye meza yako unajikuta tuu wenyewe kwa hiari yako jumamosi au jumapili unaingia job walau kwa masaa manne ukapunguze vimeo. Au mara kwa mara unatoka ofsini saa mbili au tatu usiku.

Mfano mimi kwenye portifolio yangu nikajikuta nina kama zaidi ya NGOs 700 ya kuzisimamia. Yaani hapo uhakikishe wameleta report zao za fedha na miradi, report zimekaa sawa, uindize report kwenye system tena kwa kuzitranlate kwa kingereza, kuhakikisha umewatumia fedha za quarter nyingine baada ya kujiridhisha na report ya fedha. Kisha uhakikishe uhakikishe hizo NGOs umezitembelea ili kwenda kuzikagua huko field kama wanatekeleza miradi sawa sawa au wapo wrong ili uwaelekeze. Wakati huo huo uhakikishe unatrain waliokosa funding ili nao wapate fedha maana ofisi ile ilikuwa na wafadhili wengi waliokuwa wanaweka fedha zao ili ziende kwa wadau huko mikoani, kwahiyo mnajikuta mna fedha lakini wanaopata ni wachache so in order to maintain reputation ya ofisi kwa donors ilikuwa ni lazima kwenda huko na huko mikoani kuwafundisha watu jinsi ya kuomba na kupata ruzuku kutoka kwetu kulingana na vigezo vetu ndio mana tukawa tunapokea hata proposal za Kiswahili ilimradi kutombagua mtu.

Sasa kwenye mazingira kama hayo unafanyaje? Watu tulikuwa bize muda wote ukiangalia kazi ni nyingi mpaka unatamani siku ingekuwa na masaa 30 walau unaweza kupata muda mzuri wa kupumzika. Kiukweli kuna watu ambaop hawakuwa na shida sana na kazi waliacha asee. Pia ukiachana na sababu za integrity kuachishwa kazi kama mshikaji wangu Big lakini wengi pia walitimuliwa sababu ya performance issue, hawakuweza kwenda speed ya ofisi. Na katika vitu ambavyo menejiment ilikuwa haiwezi kukuvumilia ni malalamiko kutoka kwa grantees kwamba umewaomba rushwa au umewacheleweshea fedha zao, hapo ulikuwa hueleweki. Kwahiyo unachotakiwa kufanya grantee akileta report yake leo baada ya wiki uwe umeshaireview na kuprocess fedha zake. Hata system ilikuwa inakukumbusha kwamba report ipo due hivyo unatakiwa kuishughulikia. Sasa mtu unasimamia miradi zaidi ya 500 what do you expect. Usipokuwa smart and organized unakuwa chizi. Work-life balance ni kama haikuwepo pale ofsini.

Nakumbuka kuna new employee ndio alikuwa ameajiriwa ana kama mwezi tuu akapiga chini kazi bila kupata kazi nyingine. Yule jamaa alivoajiriwa pale alikuwa amebakiza kama mwezi hivi afunge ndoa. Basi ameingia pale ofsini amekutana na mshike mshike wa kaxi na hakuna ugeni, kwani ugeni ulikuwa mwisho wiki ya kwanza. Sasa yule bwana harusi inaonekana maswala ya kushughulikia maandalizi ya harusi yake alikuwa anayasimamia yeye mwenyewe kwa kiasi kikubawa sijui hata kama alikuwa na kamati yule bwana maana simu yake ilikuwa bize sana na kila kitu anaulizwa yeye. Basi pale mjengoni tukamchangia kama kawaida tena mzigi wa kutosha tuu na kutokana na maandalizi yake akaruhusiwa awe anafanya kazi nusu siku.

Lakini tulikuwa tunabaki na bwana harusi mpaka usiku maana naona alikuwa akiangalia haoni pa kutokea lazima abaki ofsini kupunguza majukumu. Sasa sisi tulikuwa tunafanya kazi kwenye pool ambapo wote mnaonana na kusikilizana. Sasa kuna siku kazi zimepamba moto, basi simu ya bwana harusi ikawa inaita sana akawa hapokei. Mdada mmoja akamwambia bwana harusi pokea simu inaita basi akapokea nadhani sijui kuchanganyikiwa au vipi akaamkia “shikamoo”, sijui akajibiwa nini tukamsikia anasema “mdau nimekwambia atakuja mtu huko huko kuwatembelea wiki ijayo atawasaidia”. Sijui akajibiwa nini akamwambia yule mpigaji simu “ongea na huyu mwenzangu atakuasaidia” akawa amempa yule dada aliyemwambia apokee simu ili aongee na simu yake.

Yule dada akachukua simu akijua anaongea na grantee ii amsaidie bwana harusi kutatua changamoto yake akamuuliza mpigaji una shida gani nikusaidie? Akajibiwa mimi ni mchumba wake na ni mke mtarajiwa wa huyo mwenye simu lakini naona ananiambia vitu ambavyo ambavyo sivielewi, je yuko sawa kwani maana kuna vitu nataka kumwambia kuhusu gauni la harusi. Ndio yule dada kumwambia bwana harusi wewe anayepiga simu ni mkeo sio grantee hebu toka nje ukaongee naye. Aisee ofisi nzima tulibusrst kwa kucheka. Yaani bwana harusi alivurugwa na kazi mpaka akawa amesahau sauti ya mkewe mtarajiwa. Lakini pia inaonekana sijui alivurugwa kiasi gani mpaka akawa anaongelea maswala ya kazi wakati bi harusi anaongelea maswala ya gauni. Ikabidi atoke nje akaongee na mkewe badae akarudi.

Basi harusi ikapita lakini baada ya wiki kama tatu hivi bwana harusi akaandika barua ya kuacha kazi. Sasa HR hakutaka kuiprocess moja kwa moja akawa anamtaka kwanza afikirie mara mbili mbili uamuzi wake labda kama ni ishu ya maslahi na amepata sehemu nzuri zaidi. Basi HR akatufata watu ambao aliona kidogo tupo karibu na bwana harusi ili tuongee naye. Bwana harusi wala hakuficha akatuchana live japo hajapata kazi sehemu nyingine ila mazingira ya kazi pale yamemshinda maana yalikuwa ni busy mno with less work-life balance. Tuakajaribu kumsihi pale avumilie atazoea tuu akagoma kabisa. Jamaa etu mmoja akasema jamani tumuacheni huyu ni mtu mzima anajua analolifanya. Mimi nikaongezea nikasema tena huyu muhehe wa Iringa huko tusije tumalazimisha akajinyongea ofsini halafu ikawa balaa jingine. Basi bwana harusi akaresign kama alivyopanga, mhehe yule ni kweli alikuwa hana kazi maana baada ya hapo vilianzan vizinga kwa sana na tuu vile mkewe alikuwa karibu anajifungua basi alikuwa na uhitaji sana wa pesa. Kwa sisi washkaji zake tulimbusti tulivyoweza lakini nilijifunza kuna watu wana maamuzi magumu na misimamo asee. Unaachaje kazi huna kazi?

Nakumbuka tulimfikishia HR sababu za kwanini yule bwana harusi ameacha kazi na uzuri au ubaya kwenye taarifa za ofisi ya HR waligundua wengi tuu walionekana hawakuwa na performace nzuri kwa sababu hawakuwa na muda wa kutosha wa kuopumzika. So ikawekwa mikakati pale ili kuboresha work-life balance kwa wafanyakazi. Hata menejiment walikuwa wanajua kwamba work-life balance was essential for promoting employee well-being, maintaining job satisfaction, preventing burnout, and creating a positive and productive work environment. Ignoring work-life balance can have adverse effects on individuals and organizations alike, impacting health, relationships, and overall job performance.

Mikakati iliyowekwa ni pamoja na kuongeza wafanyakazi, kwa hiyo ikatafutwa ofisi nyingine yenye uwezxo wa kuaccommodate wafanyakazi wengi zaidi lakini pia likizo ilikuwa ni lazima. Maana before hapo likizo ilikuwa ni optional kwamba mtu unaweza ukalipwa pesa ule mda wa likizo ili uendelee kupiga mzigo, na kwa jinsi kazi zilivokuwa nyingi mtu aliona bora auze baadi ya siku za likizo ili apunguze kazi huku akipokea mshiko. Hii hata mimi nikifanya sana. Basi maisha baada ya hapo yaliendelea kama kawaida na kiukweli work load ilikuwa imepungua sana na tulifanya kazi kwa utulivu na ufanisi mkubwa.

Wadau wangu nilifanya kazi pale kwa miaka mi4 before I shifted to another organization. Based on my job responsibilities as a Program Officer - grants, I have developed a diverse set of skills as followas
  1. Grant Management: Demonstrated ability to review, assess, and select grant applications in accordance with established procedures and regulations.​
  2. Communication Skills: Regularly communicated with grant applicants regarding the status of their applications, ensuring accurate and timely information.​
  3. Training and Facilitation: Organized and facilitated training sessions on project and financial management for CSOs/NGOs/partners nationwide.​
  4. Supervision and Leadership: Successfully supervised over 100 grantees annually in various sectors, including governance, youth, human rights, gender & women empowerment, health and disability.​
  5. Capacity Development: Designed and conducted capacity development sessions for grantees, covering project management, financial management, project monitoring and evaluation, and project report writing.​
  6. Partnership Management: Worked closely with local partners to identify and address capacity gaps in project grants management.​
  7. Monitoring and Evaluation: Conducted field visits to assess and monitor project implementation performance and collect success stories from partners.​
  8. Flexibility and Adaptability: Ensured flexibility and high quality of capacity development support provided to partners.​
  9. Report Writing: Prepared periodic reports for management purposes and other stakeholders.​
  10. Stakeholder Engagement: Collaborated with various stakeholders, including CSOs, CBOs, FBOs, and NGOs, throughout the grant management process.​
  11. Project Implementation Oversight: Monitored and assessed project implementation to ensure alignment with goals and objectives.​
  12. Time Management: Successfully handled multiple responsibilities and tasks within deadlines.​
  13. Analytical Skills: Evaluated grant applications, monitored project performance, and prepared reports, demonstrating strong analytical abilities.​
Nipeni connection wadau

Tukutane next episode
Aisee kweli maisha hayako fair …mtu kama huyu anakosaje kazi kisa hana connection na madini yote haya? Mkuu bila shaka utapata kazi soon kipawa hiki kisipotee bure
 
EPISODE 10: Get ready for unexpected

Story Interlude…….

Before sijaendelea na stori yangu naomba kusema hili. Kuna baadhi ya watu wananiuliza hapa jukwaani na wengine kunijia PM kutaka kujua kwamba inaonekana niliwahi kupata pesa nyingi kwanini sikufikiria au sifikirii kujiajiri? Najua wapo wengine wengi ambao wanajiuliza hilo swali ila wameamua tu kupita kimya kimya.

Sasa ipo hivi, kwanza kabisa katika watu ambao wanaoamini katika “be employed with a plan B” mimi ni mmoja wao. Siwezi kuzungumzia hapa kuhusu kushika pesa au kutoshika pesa lakini nitazungumzia mtazamo na uzoefu wangu katika hiyo be employed with a plan B. Kipindi nipo ajira tofauti tofauti nilishajaribu sana hizo plan B, kwamba kutengeneza kipato nje ya kazi yangu. Kama nilivoeleza na nitakavyoendelea kuelezea huko mbele kazi zangu kwa asilimia 60 zilikuwa ni za kusafiri safari sana, So fursa niliyoiona kwanza kwa haraka ni kulima kwa kukodisha au kununua mashamba huko vijijini. Naweza kusema nimelimisha sana mazao tofauti tofauti lakini kwakweli kazi ya kulima au kulimisha inataka kwanza usimamizi wa madhubuti sana. Sasa kwangu mimi ilikuwa ngumu sana kwa sababu leo nipo kesho sipo unaacha wasimamizi unaowaamini kule shamba lkn mwisho wa siku hasara tuu.

Lakini pia nilijaribu baadhi ya biashara kwa hapa mjini lakini pia usimamizi ulinigharimu. Kingine nilichogundua asee hakuna mtu anafanikiwa kwa kusomea au kuiga kuwa mfanyabiashara isipokuwa bishara ni inner motive ambayo mtu anakuwa nayo. Labda mtu akose option kabisa ya kuajiriwa ndio anaweza akaforce akawa mfanya biashara mzuri maana hana option.

Ukiwa na inner motive ya kufanya biashara hakuna kitakachokuzuia hata kusafiri kikazi hakuwezi kuwa tatizo sana lakini kwa mimi vingi nilivyojaribu vilikufa au ilikuwa ni loss tuu. Kwahiyo kama wewe umejaaliwa hiyo inner motive na umeajiriwa unaweza kuwa na mafanikio sana kwa sababu kipato unachopata kwenye kuajiriwa kinabust biashara zakko.

Kwahiyo ndugu zangu this is not an excuse lakini tunakumbushana tu binadamu tumeumbwa tofauti sana lakini pia tumelelewa kwenye mazingira tofauti. Nyie wenyewe mashahidi, hata humu ndani kuna nyuzi zinaanzishwa mtu ana milioni 100 lkni hajui afanye biashara gani wakati huo huo kuna watu wana nyuzi humu wanatafuta laki2 mtaji ili waimplement project zao watoboe maisha. Pia Hapa JF nyuzi kibao zimeanzishwa kushangaa hao viongozi wanaotuimbia mahuburi kila siku watu wafikirie kujiajiri na wakati wenyewe wakitumbuliwa hawajiari ila wanatega kunyenyekea teuzi zingine. Hapo utaona kwamba sio kwamba watu hawajui umuhimu wa kuwa na plan B lkini ile inner motive ni tatizo. Ni mtazamo tuu huu jamani. Kwa hiyo wandugu bado natafuta ajira hahahaa

OK, The chill time's interlude done, let's switch it up and get down to business. Nilisema hapo juu expect the unexpected eeh? Yes, ujue kwenye haya maisha sometimes mtu unakuwa unapanga mipango yako na kuwa namategemeo makubwa sana lakini unachokuja kukutana ni kinyume kabisa na matarajio yako. Wewe unapanga hili lakini unapigwa na kitu kizito ambacho huku tarajia kabisa.

Kama nilivodokeza huko juu kwenye maelezo yangu kwamba pale ofsini ukifauru probation unapewa mkataba wa miaka miwili ambao unaweza kurenewkila baada ya miaka miwili kulingana na uhitaji wa ofisi. Mashirika mengi tu haya makubwa yasiyo ya kiserikali wanafanya hivi hata haya international. Na kwa taratibu za pale ofisini ilikuwa ukifauru kurenew mkataba mara mbili yaani ufanye nao kazi kwa miaka minne na kuendelea huwa wanakupa zawadi nzuri tuu ya fedha nadhani ilikuwa ni motivation ya kuwafanya watu wabaki pale kwa muda mrefu japo kutimuana kulikua nje nje kama usipoenda sawa na taratibu za ofisi.

Basi mimi nashukuru Mungu nilipiga mzigo kwa muda wa miaka minne yaani nilifanikiwa kurenew mkataba mara moja. Sasa kuna kipindi nikaona huku kwenye ma NGO ni kama job security inakuwa ndogo sana, maana unaweza mwenyewe ukajidamka asubuhi, ukanyoosha, ukafika job ukakuta barua kutoka kwa HR kwamba kazi basi. Kwahiyo nikaanza kufikiria kutafuta kazi serkalini kwa kuamini kwamba kule kuna pensionable employment yaani ajira ya kudumu. Halafu yale mazingira very hectic ya kazi nikawa naona kama watu wa government wanakula sana shushu basi nikawa nawatamani sana. Maana mtu unakosa hata muda wa kusimamia mambo yako muhimu hata ujenzi unawea ukajikuta kwa sehemu kubwa ubawaacha mafundi wanajenga bila uwepo wako. Basi bhana Kwa kuwa sikuwa na presha basi nikawa natafuta kazi huku sina haraka kihivyo nikawa navizia zile nafasi ambazo naona nazihitaji ndio naaply.

Mungu wa mbinguni asivyo Athumani na wala haishi Kigamboni, ikatokea kwamba miezi miwili kabla ya kurenew mkataba wangu yaani nimalize miaka minne ili kama menejiment wataridhika na mimi basi nindelee nitimize miaka sita nikapata mchongo serikalini tena kwenye hizi idara ambazo zinajiendesha zenyewe mfano wa TRA, TPDC, TCRA, TBS, BRELA etc. Kuna moja hapo ndio nilipata tena ilikuwa ni kitengo cha elimu kwa umma ni shavu ambalo lilikuwa na safari nyingi maana ilikuwa ni kuzunguka mikoani kuelimisha watu maswala yanayohusiana na idara husika. Kwakweli ilikuwa na nafasi nzuri sana ambayo sikujiuliza mara mbili.

Nikaitaarfu menejimenti kwamba sitarenew tena mkataba. Nakumbuka line meneja wangu alisikitika sana maana mimi nilikuwa ni kati ya majembe yake aliyokuwa anayategemea katika kurescue challenged situation. Hapa nimekumbuka ishu moja nakumbuka kuna siku nililala au nilitoka ofsini saa kumi alfajiri kisa kurescue situation.

Ilikuwa hivi, boss kubwa la pale ofsini alienda Canada kweny meeting na donors sasa kwa kuwa ile ofisi yetu ilikuwa ni moja ya shirika linalofanya vizuri basi wakamwalika boss kubwa aende huko kutoa presentation namna gani tuanvofanya kazi mpaka kutoa matokeo makubwa. Sasa boss kubwa yeye alikuwa amejiandaa zile issue strategic zaidi kumbe wale donors walikuwa wanataka vitu ambavyo kwa boss kubwa vilikuwa ni minor sana nap engine vingempa shida kuvijibia kikamilifu labda kama angesoma maripoti ya miaka ya nyuma.

Sasa alipomaliza presentation yake inaonekana nwakamshooti maswali ambayo yalihitaji zaidi mtu anaeenda sana field ili kutoa majibu ya uhakika. Bosikubwa akamcheki line meneja kama vipi amwandalie baadhi ya majibu. Sasa muda huo ilikuwa ni muda wa kama saa moja ousiku watu ndio tunajiandaa kutoka ofsini na wengine wameshaondoka. Nadhani kwa kule Canada ilikuwa ndio asubuhi watu ndio wanaaza majukumu yao ya kikazi. Mara line manager akanipa simu niongee na bosskubwa jamaa akanielekeza pale ishu anazozitaka nimwandalie then nimtumie kwa email. Mimi nikamtumia fasta nikawa naondoka. Wakati nimshafika nje ya ofisi mara naona bosskubwa ananipigia wasapu kupokea ananiomba nimtafutie tena baadi ya taarifa. Nikalaani sana kwanini nilikuwa hewani wasapu hahaaa ila nikageuza sikuwa na jinsi. Sasa ile nitumie taarifa hii mara ile ikawa haiishi uzuri zile data mimi nilikuwa nazo. Basi nikamwambia bosskubwa kama vipi waniunge mimi kwa skype nikiwa pale ofsini ili tusaidie kuwajibu. Boss kubwa akaniuliza kama nina uhakika sita mwangusha, nikamwambia kwani hizo info si ndio mimi ambazo ninampatia, lakini nikashindwa tu kumwambia mbona wewe unajikanyaga kanyaga tuu huko hahaha. (Jokes, ofcourse I respect the na amekuwa role model wangu sana na alishalamba uteuzi serikalini mda mrefu tuu) kwenye ministerial level)

Basi akanicoonect pale yale majamaa meupe yakaanza kunishoot maswali pale nikawa nawajibu, wakawa wanataka kueleshwa kwa undani sana maana walikuwa ni wawakilishi wa wafadhili ambao ilikuwa walete mpunga mrafu sana ofisini. Basi pale nikajikuta naenda nao mpaka session yote aliyopangiwa bosskubwa ni kama bosskubwa alitumia akili kuwaambia kuwa kuna ofisa alimwandaa kutoka Tanzania (yaani mimi eti) kushiriki ule mkutano kwani alitaka kuonyesha pale ofsini tunacollective working style, basi ile pia ilimpa crediti sana. Basi mimi nikajikuta natoka pale saa nane yaani kama inaenda inaenda saa kumi. Uzuri ile ofisi ilikuwa karibu na breakpoint pale posta basi mda wa wao wakibreak kula mimi naingizia zangu breakpint nagonga msosi. Basi mwisho bosskubwa akanipa likizo ya sikumbili nipumzike kufidia ile kazi ya kutoboza usiku.

Basi wakati naaga menejiment wakanishawishi sana nibaki lakini ikashindikana na nikawapa sababu naenda serikalini basi ikabidi tuu waelewe na kunitakia kila lenye heri. Kwakuwa nilimaliza miaka mine pale basi nikapewa mshiko wangu wa pongezi na wiki ya mwisho wakandaa farewell cake tukatata pale ofisi nzima then nikamalizia vimeo vyangu kisha nikakabidhi ofisi nikaondoka kuanza majukumu mapaya.

Sasa kule serikalini baada ya kupokea offer letter kilichobaki ni kusaini tu mkataba. Kwa kuwa tulikuwa watu kama 10 hivi tuliopata ajira pale kwenye hiyo position ilibidi tusubiriane ili wote tuanze siku moja. Kwa hiyo mimi tangu nilipoacha kazi nilikuwa na kama mwezi mmoja hivi wa kupumzika ndio nikaanze kazi serikalini. Niliona afadhali na nilifurahi kupata hilo gap kwa sababu huo muda niliutumia kupumzika na familia nyumbani kwa sababu kipindi hicho ndio kwanza nilikuwa nimetoka kuoa na nina katoto ka kwanza. Basi maisha yakawa poa tuu huku nikiendelea kusikilizie muda ufike nikaanze mzigo serikalini.

Sasa kipindi kile ilikuwa ndio kipindi Magufuli ameingia ofisini, nadhani wote mnakumbuka speed aliyoingia nayo madarakani. Advertise ya kwanza Mkurugenzi wa ile idara ambayo nilipata kazi akatumbuliwa. Hiyo haikuwa big ishu kwangu sana maana ilikuwa hainiathiri moja kwa moja. Advertise ya pili mzee baba akastopisha ajira zote mpya serikalini until further directives. Hapo ndo nilipopigwa na kitu kizito, askwambie mtu ile taarifa uliifurahia au kuona ya kawaida kama tu ilikuwa haikugusi moja kwa moja ila kwa sisi ambao ilitugusa asee!!!

Sasa nikajipa moyo sisi tayari tunaofa letter so itakuwa haituhusu. Nikatamani kuwapigia wengine ambaop nao walikuwa wamepata iyo kazi lakini binafsi nikawa siwajui kwani nilisikia tu pale idarani wanasema nitakuwa na wenzangu wengine kama 10 hivyo tunasubiriana ili tuanze wote pamoja. Basi nikatimba pale idarani kwenda kuulizia mstakabalim utakuweje. Niliulizwa tuu umekuja na ile barua ya ofa? Nikajibu ndio, wakaniambia iache hapo kwa sekretari mpaka utakapopewa taarifa nyingine kwa muda ule maelekezo yalikwa ndio hayo. Daa pale pale nihisi nguvu zinaniishia lkn nikajikaza basi nikaiacha ile barua pale kwa secretary lakini nikaitoa kopi, na nikamuomba namba yule sekretari ili niwe nafatilia. Katika kipindi ambacho nilikuwa nafatilia taarifa ya nabari basi ni kipindi kile maana nilikuwa nataka kujua mzee baba ataruhusu lini kuendelea na michakato ya ajira pale ilipoishia.

Hahaaa ni kama ilikuwa kusubiria mawe yanayochemshwa eti yataiva, mzee baba alikaza. Nilikuwa nampigia simu yule sekretari wa pale serikalini kufatilia maendeleo nadhani mpaka alinichoka maana kuna siku akaniambia kaka sasa naona tu nikutafutie namba ya katibu wa ikulu ili uwe unampigia mwenyewe moja kwa moja. Dah nikaona hapa nishachokwa sasa, lakini nikasema hata kama ningekuwa mimi ningefanyaje. Kwakweli Nilikuwa frustrategy sana kipindi hiki ila sikujilaumu kuacha kazi kule nilikokuwepo maana sikukurupuka ni vile mipango imekwenda ndivyo sivyo. Basi ikabidi nikubaliane na hali halisi. Siku moja line manager akanipigia simu kuniuliza kama lile sekeseke limenikuta na mimi nikamweleza pale na mimi miongoni mwao akaishia tu kuniambia yaani mwezi uliofata tu baada ya mimi kuondoka walikuwa wameshapata mtu mwingine. Nilichomwambia tu asjali ila nitamweka awe referee wangu kwenye CV yangu maana niko mbioni sasa kutafuta sehemu ningine.

Hivi ndivyo ilivyokuwa na msala wangu wa kuhamia serikalini. Hapo nilijifunza kitu kikubwa sana wakati mungine sio kila plan unayoitegemea inakuja kama ilivyo, therefore, you better get ready for the unexpeceted outcomes. Ila badae nikaja kumwelewa na nikamkubali sana Rais Magufuli, ilikuwa ni nadra sana kutomfatilia hotuba zake kwenye vyombo vya habari labda niwe sina nafasi.

Muendelezo soma Mambo muhimu niliyojifunza katika maisha yangu ya kuajiriwa.
 
Mkuu
Ni kwamba kazi umekosa kabisa au ndio vile unapata lakini unaona maslahi hayaendani na hadhi yako?

Vipi,hujafikiria kuhusu kujiajiri?

Na kabla la ngekewa kukudondokea kwa Dr KJ, naamini ulikuwa unapambana huku na kule..

Je ni mbinu zipi ulizokuwa ujazitumia nyingine za kutafuta kazi?
Na vipi zile mbinu hujazitumia tena kwa wakati huu kipindi huna kazi?

...
Upande mwingine ningependa kuuliza kuhusu internships zilizopo kwenye hayo mashirika .
Kuna graduates wengi sana fresh from school..hawana experience ya aina yoyote,vipi je,wanayo nafasi ya kuweza kupata hizo nafasi?
Na kama ni ndiyo..je,Ni watu wa namna gani(vigezo) mliokuwa mhafanya nao hizo internship.
Hii inaweza kuwa msaada kwa namna moja ama nyingine kwa fresh graduates....hata pia experienced jobless graduate km Mimi.
Mkuu Saint Anne kuhusu kujiajiri nimetoa ufafanuzi kwenye episode namba 10.

Labda nikujibu kuhusu internship positions kwenye mashirika. Kama unavyoona kwenye stori yangu nina uzoefu sana wa kufanya na NGOs za Tanzania. Kuhusu internship binafsi sijaona zikiwa zinatangazwa publicly hata kwa mashirika niliyowahi kufanya nayo kazi yote local na international internship vacancies zinakuwa zinatangazwa internally only kulingana na mahitaji ya ofisi.

Mnaweza tu mkaambiwa idara ya uhasibu abahitaji intern kama mtu anamjua mtu amlete au idara ya utawala inahitaji reception wa muda kwahiyo mara nyingi kwa uzoefu wangu hivyo ndio vigezo yaani KUJUANA, I am sory to say that lakini ndio uhalisia. Na mara nyingi interns wana nafasi kubwa ya kuajiriwa endapo wataonyesha kuwajibika vizuri huko maofisi.
 
Mkuu Saint Anne kuhusu kujiajiri nimetoa ufafanuzi kwenye episode namba 10.

Labda nikujibu kuhusu internship positions kwenye mashirika. Kama unavyoona kwenye stori yangu nina uzoefu sana wa kufanya na NGOs za Tanzania. Kuhusu internship binafsi sijaona zikiwa zinatangazwa publicly hata kwa mashirika niliyowahi kufanya nayo kazi yote local na international internship vacancies zinakuwa zinatangazwa internally only kulingana na mahitaji ya ofisi.

Mnaweza tu mkaambiwa idara ya uhasibu abahitaji intern kama mtu anamjua mtu amlete au idara ya utawala inahitaji reception wa muda kwahiyo mara nyingi kwa uzoefu wangu hivyo ndio vigezo yaani KUJUANA, I am sory to say that lakini ndio uhalisia. Na mara nyingi interns wana nafasi kubwa ya kuajiriwa endapo wataonyesha kuwajibika vizuri huko maofisi.
Nimekuelewa sana Mkuu..
Hiyo paragraph ya mwisho nimekuelewa.


Kuna mahala nilikaribia kupata internship(Kuna mtu alinistua akaniambia kama nipo free niende ni mwezi mmoja)..lakini kukawa na mgongano wa kimaslahi baina ya Mtu aliyetaka niende,na yule ambaye nilitakiwa nikafanye naye kazi nikienda(alikuwa na mtu wake..
Mwisho wa siku tukaamua kuacha tu maana ningefanya kazi katika mazingira magumu.


Nakusubiri upate Mkuu,hizi walizotangaza wewe hukosi..
Ukipata usinisahau kwenye internship.



Ngoja nisome sasa episode Yako ya 10.
 
EPISODE 10: Get ready for unexpected

Story Interlude…….

Before sijaendelea na stori yangu naomba kusema hili. Kuna baadhi ya watu wananiuliza hapa jukwaani na wengine kunijia PM kutaka kujua kwamba inaonekana niliwahi kupata pesa nyingi kwanini sikufikiria au sifikirii kujiajiri? Najua wapo wengine wengi ambao wanajiuliza hilo swali ila wameamua tu kupita kimya kimya.

Sasa ipo hivi, kwanza kabisa katika watu ambao wanaoamini katika “be employed with a plan B” mimi ni mmoja wao. Siwezi kuzungumzia hapa kuhusu kushika pesa au kutoshika pesa lakini nitazungumzia mtazamo na uzoefu wangu katika hiyo be employed with a plan B. Kipindi nipo ajira tofauti tofauti nilishajaribu sana hizo plan B, kwamba kutengeneza kipato nje ya kazi yangu. Kama nilivoeleza na nitakavyoendelea kuelezea huko mbele kazi zangu kwa asilimia 60 zilikuwa ni za kusafiri safari sana, So fursa niliyoiona kwanza kwa haraka ni kulima kwa kukodisha au kununua mashamba huko vijijini. Naweza kusema nimelimisha sana mazao tofauti tofauti lakini kwakweli kazi ya kulima au kulimisha inataka kwanza usimamizi wa madhubuti sana. Sasa kwangu mimi ilikuwa ngumu sana kwa sababu leo nipo kesho sipo unaacha wasimamizi unaowaamini kule shamba lkn mwisho wa siku hasara tuu.

Lakini pia nilijaribu baadhi ya biashara kwa hapa mjini lakini pia usimamizi ulinigharimu. Kingine nilichogundua asee hakuna mtu anafanikiwa kwa kusomea au kuiga kuwa mfanyabiashara isipokuwa bishara ni inner motive ambayo mtu anakuwa nayo. Labda mtu akose option kabisa ya kuajiriwa ndio anaweza akaforce akawa mfanya biashara mzuri maana hana option.

Ukiwa na inner motive ya kufanya biashara hakuna kitakachokuzuia hata kusafiri kikazi hakuwezi kuwa tatizo sana lakini kwa mimi vingi nilivyojaribu vilikufa au ilikuwa ni loss tuu. Kwahiyo kama wewe umejaaliwa hiyo inner motive na umeajiriwa unaweza kuwa na mafanikio sana kwa sababu kipato unachopata kwenye kuajiriwa kinabust biashara zakko.

Kwahiyo ndugu zangu this is not an excuse lakini tunakumbushana tu binadamu tumeumbwa tofauti sana lakini pia tumelelewa kwenye mazingira tofauti. Nyie wenyewe mashahidi, hata humu ndani kuna nyuzi zinaanzishwa mtu ana milioni 100 lkni hajui afanye biashara gani wakati huo huo kuna watu wana nyuzi humu wanatafuta laki2 mtaji ili waimplement project zao watoboe maisha. Pia Hapa JF nyuzi kibao zimeanzishwa kushangaa hao viongozi wanaotuimbia mahuburi kila siku watu wafikirie kujiajiri na wakati wenyewe wakitumbuliwa hawajiari ila wanatega kunyenyekea teuzi zingine. Hapo utaona kwamba sio kwamba watu hawajui umuhimu wa kuwa na plan B lkini ile inner motive ni tatizo. Ni mtazamo tuu huu jamani. Kwa hiyo wandugu bado natafuta ajira hahahaa

OK, The chill time's interlude done, let's switch it up and get down to business. Nilisema hapo juu expect the unexpected eeh? Yes, ujue kwenye haya maisha sometimes mtu unakuwa unapanga mipango yako na kuwa namategemeo makubwa sana lakini unachokuja kukutana ni kinyume kabisa na matarajio yako. Wewe unapanga hili lakini unapigwa na kitu kizito ambacho huku tarajia kabisa.

Kama nilivodokeza huko juu kwenye maelezo yangu kwamba pale ofsini ukifauru probation unapewa mkataba wa miaka miwili ambao unaweza kurenewkila baada ya miaka miwili kulingana na uhitaji wa ofisi. Mashirika mengi tu haya makubwa yasiyo ya kiserikali wanafanya hivi hata haya international. Na kwa taratibu za pale ofisini ilikuwa ukifauru kurenew mkataba mara mbili yaani ufanye nao kazi kwa miaka minne na kuendelea huwa wanakupa zawadi nzuri tuu ya fedha nadhani ilikuwa ni motivation ya kuwafanya watu wabaki pale kwa muda mrefu japo kutimuana kulikua nje nje kama usipoenda sawa na taratibu za ofisi.

Basi mimi nashukuru Mungu nilipiga mzigo kwa muda wa miaka minne yaani nilifanikiwa kurenew mkataba mara moja. Sasa kuna kipindi nikaona huku kwenye ma NGO ni kama job security inakuwa ndogo sana, maana unaweza mwenyewe ukajidamka asubuhi, ukanyoosha, ukafika job ukakuta barua kutoka kwa HR kwamba kazi basi. Kwahiyo nikaanza kufikiria kutafuta kazi serkalini kwa kuamini kwamba kule kuna pensionable employment yaani ajira ya kudumu. Halafu yale mazingira very hectic ya kazi nikawa naona kama watu wa government wanakula sana shushu basi nikawa nawatamani sana. Maana mtu unakosa hata muda wa kusimamia mambo yako muhimu hata ujenzi unawea ukajikuta kwa sehemu kubwa ubawaacha mafundi wanajenga bila uwepo wako. Basi bhana Kwa kuwa sikuwa na presha basi nikawa natafuta kazi huku sina haraka kihivyo nikawa navizia zile nafasi ambazo naona nazihitaji ndio naaply.

Mungu wa mbinguni asivyo Athumani na wala haishi Kigamboni, ikatokea kwamba miezi miwili kabla ya kurenew mkataba wangu yaani nimalize miaka minne ili kama menejiment wataridhika na mimi basi nindelee nitimize miaka sita nikapata mchongo serikalini tena kwenye hizi idara ambazo zinajiendesha zenyewe mfano wa TRA, TPDC, TCRA, TBS, BRELA etc. Kuna moja hapo ndio nilipata tena ilikuwa ni kitengo cha elimu kwa umma ni shavu ambalo lilikuwa na safari nyingi maana ilikuwa ni kuzunguka mikoani kuelimisha watu maswala yanayohusiana na idara husika. Kwakweli ilikuwa na nafasi nzuri sana ambayo sikujiuliza mara mbili.

Nikaitaarfu menejimenti kwamba sitarenew tena mkataba. Nakumbuka line meneja wangu alisikitika sana maana mimi nilikuwa ni kati ya majembe yake aliyokuwa anayategemea katika kurescue challenged situation. Hapa nimekumbuka ishu moja nakumbuka kuna siku nililala au nilitoka ofsini saa kumi alfajiri kisa kurescue situation.

Ilikuwa hivi, boss kubwa la pale ofsini alienda Canada kweny meeting na donors sasa kwa kuwa ile ofisi yetu ilikuwa ni moja ya shirika linalofanya vizuri basi wakamwalika boss kubwa aende huko kutoa presentation namna gani tuanvofanya kazi mpaka kutoa matokeo makubwa. Sasa boss kubwa yeye alikuwa amejiandaa zile issue strategic zaidi kumbe wale donors walikuwa wanataka vitu ambavyo kwa boss kubwa vilikuwa ni minor sana nap engine vingempa shida kuvijibia kikamilifu labda kama angesoma maripoti ya miaka ya nyuma.

Sasa alipomaliza presentation yake inaonekana nwakamshooti maswali ambayo yalihitaji zaidi mtu anaeenda sana field ili kutoa majibu ya uhakika. Bosikubwa akamcheki line meneja kama vipi amwandalie baadhi ya majibu. Sasa muda huo ilikuwa ni muda wa kama saa moja ousiku watu ndio tunajiandaa kutoka ofsini na wengine wameshaondoka. Nadhani kwa kule Canada ilikuwa ndio asubuhi watu ndio wanaaza majukumu yao ya kikazi. Mara line manager akanipa simu niongee na bosskubwa jamaa akanielekeza pale ishu anazozitaka nimwandalie then nimtumie kwa email. Mimi nikamtumia fasta nikawa naondoka. Wakati nimshafika nje ya ofisi mara naona bosskubwa ananipigia wasapu kupokea ananiomba nimtafutie tena baadi ya taarifa. Nikalaani sana kwanini nilikuwa hewani wasapu hahaaa ila nikageuza sikuwa na jinsi. Sasa ile nitumie taarifa hii mara ile ikawa haiishi uzuri zile data mimi nilikuwa nazo. Basi nikamwambia bosskubwa kama vipi waniunge mimi kwa skype nikiwa pale ofsini ili tusaidie kuwajibu. Boss kubwa akaniuliza kama nina uhakika sita mwangusha, nikamwambia kwani hizo info si ndio mimi ambazo ninampatia, lakini nikashindwa tu kumwambia mbona wewe unajikanyaga kanyaga tuu huko hahaha. (Jokes, ofcourse I respect the na amekuwa role model wangu sana na alishalamba uteuzi serikalini mda mrefu tuu) kwenye ministerial level)

Basi akanicoonect pale yale majamaa meupe yakaanza kunishoot maswali pale nikawa nawajibu, wakawa wanataka kueleshwa kwa undani sana maana walikuwa ni wawakilishi wa wafadhili ambao ilikuwa walete mpunga mrafu sana ofisini. Basi pale nikajikuta naenda nao mpaka session yote aliyopangiwa bosskubwa ni kama bosskubwa alitumia akili kuwaambia kuwa kuna ofisa alimwandaa kutoka Tanzania (yaani mimi eti) kushiriki ule mkutano kwani alitaka kuonyesha pale ofsini tunacollective working style, basi ile pia ilimpa crediti sana. Basi mimi nikajikuta natoka pale saa nane yaani kama inaenda inaenda saa kumi. Uzuri ile ofisi ilikuwa karibu na breakpoint pale posta basi mda wa wao wakibreak kula mimi naingizia zangu breakpint nagonga msosi. Basi mwisho bosskubwa akanipa likizo ya sikumbili nipumzike kufidia ile kazi ya kutoboza usiku.

Basi wakati naaga menejiment wakanishawishi sana nibaki lakini ikashindikana na nikawapa sababu naenda serikalini basi ikabidi tuu waelewe na kunitakia kila lenye heri. Kwakuwa nilimaliza miaka mine pale basi nikapewa mshiko wangu wa pongezi na wiki ya mwisho wakandaa farewell cake tukatata pale ofisi nzima then nikamalizia vimeo vyangu kisha nikakabidhi ofisi nikaondoka kuanza majukumu mapaya.

Sasa kule serikalini baada ya kupokea offer letter kilichobaki ni kusaini tu mkataba. Kwa kuwa tulikuwa watu kama 10 hivi tuliopata ajira pale kwenye hiyo position ilibidi tusubiriane ili wote tuanze siku moja. Kwa hiyo mimi tangu nilipoacha kazi nilikuwa na kama mwezi mmoja hivi wa kupumzika ndio nikaanze kazi serikalini. Niliona afadhali na nilifurahi kupata hilo gap kwa sababu huo muda niliutumia kupumzika na familia nyumbani kwa sababu kipindi hicho ndio kwanza nilikuwa nimetoka kuoa na nina katoto ka kwanza. Basi maisha yakawa poa tuu huku nikiendelea kusikilizie muda ufike nikaanze mzigo serikalini.

Sasa kipindi kile ilikuwa ndio kipindi Magufuli ameingia ofisini, nadhani wote mnakumbuka speed aliyoingia nayo madarakani. Advertise ya kwanza Mkurugenzi wa ile idara ambayo nilipata kazi akatumbuliwa. Hiyo haikuwa big ishu kwangu sana maana ilikuwa hainiathiri moja kwa moja. Advertise ya pili mzee baba akastopisha ajira zote mpya serikalini until further directives. Hapo ndo nilipopigwa na kitu kizito, askwambie mtu ile taarifa uliifurahia au kuona ya kawaida kama tu ilikuwa haikugusi moja kwa moja ila kwa sisi ambao ilitugusa asee!!!

Sasa nikajipa moyo sisi tayari tunaofa letter so itakuwa haituhusu. Nikatamani kuwapigia wengine ambaop nao walikuwa wamepata iyo kazi lakini binafsi nikawa siwajui kwani nilisikia tu pale idarani wanasema nitakuwa na wenzangu wengine kama 10 hivyo tunasubiriana ili tuanze wote pamoja. Basi nikatimba pale idarani kwenda kuulizia mstakabalim utakuweje. Niliulizwa tuu umekuja na ile barua ya ofa? Nikajibu ndio, wakaniambia iache hapo kwa sekretari mpaka utakapopewa taarifa nyingine kwa muda ule maelekezo yalikwa ndio hayo. Daa pale pale nihisi nguvu zinaniishia lkn nikajikaza basi nikaiacha ile barua pale kwa secretary lakini nikaitoa kopi, na nikamuomba namba yule sekretari ili niwe nafatilia. Katika kipindi ambacho nilikuwa nafatilia taarifa ya nabari basi ni kipindi kile maana nilikuwa nataka kujua mzee baba ataruhusu lini kuendelea na michakato ya ajira pale ilipoishia.

Hahaaa ni kama ilikuwa kusubiria mawe yanayochemshwa eti yataiva, mzee baba alikaza. Nilikuwa nampigia simu yule sekretari wa pale serikalini kufatilia maendeleo nadhani mpaka alinichoka maana kuna siku akaniambia kaka sasa naona tu nikutafutie namba ya katibu wa ikulu ili uwe unampigia mwenyewe moja kwa moja. Dah nikaona hapa nishachokwa sasa, lakini nikasema hata kama ningekuwa mimi ningefanyaje. Kwakweli Nilikuwa frustrategy sana kipindi hiki ila sikujilaumu kuacha kazi kule nilikokuwepo maana sikukurupuka ni vile mipango imekwenda ndivyo sivyo. Basi ikabidi nikubaliane na hali halisi. Siku moja line manager akanipigia simu kuniuliza kama lile sekeseke limenikuta na mimi nikamweleza pale na mimi miongoni mwao akaishia tu kuniambia yaani mwezi uliofata tu baada ya mimi kuondoka walikuwa wameshapata mtu mwingine. Nilichomwambia tu asjali ila nitamweka awe referee wangu kwenye CV yangu maana niko mbioni sasa kutafuta sehemu ningine.

Hivi ndivyo ilivyokuwa na msala wangu wa kuhamia serikalini. Hapo nilijifunza kitu kikubwa sana wakati mungine sio kila plan unayoitegemea inakuja kama ilivyo, therefore, you better get ready for the unexpeceted outcomes. Ila badae nikaja kumwelewa na nikamkubali sana Rais Magufuli, ilikuwa ni nadra sana kutomfatilia hotuba zake kwenye vyombo vya habari labda niwe sina nafasi.

See you to the next episode tuone ilikuwaje. Thank you.
Kuhusu biashara umeongea ukweli kabisa
Biashara inahitaji moyo wa chuma.


Na hata huo moyo wa chuma na hiyo inner motive,bado Kuna siku utakosa,biashara Ina faida na hasara,,panda Shuka.
Si nyepesi kama watu wengi wanavyoongeal..hata tunaosimamia wenyewe show bado mambo ni magumu .



Kuhusu msala wa ajira serikalini aiseee inahuzunisha sana🥺
Nimejikuta naumia, ningekuwa mimi nahisi ningepata depression.
Mbaya zaidi ndio muda una familia aisee 🙌

Mungu atakupa tena Mkuu.
 
EPISODE 10: Get ready for unexpected

Story Interlude…….

Before sijaendelea na stori yangu naomba kusema hili. Kuna baadhi ya watu wananiuliza hapa jukwaani na wengine kunijia PM kutaka kujua kwamba inaonekana niliwahi kupata pesa nyingi kwanini sikufikiria au sifikirii kujiajiri? Najua wapo wengine wengi ambao wanajiuliza hilo swali ila wameamua tu kupita kimya kimya.

Sasa ipo hivi, kwanza kabisa katika watu ambao wanaoamini katika “be employed with a plan B” mimi ni mmoja wao. Siwezi kuzungumzia hapa kuhusu kushika pesa au kutoshika pesa lakini nitazungumzia mtazamo na uzoefu wangu katika hiyo be employed with a plan B. Kipindi nipo ajira tofauti tofauti nilishajaribu sana hizo plan B, kwamba kutengeneza kipato nje ya kazi yangu. Kama nilivoeleza na nitakavyoendelea kuelezea huko mbele kazi zangu kwa asilimia 60 zilikuwa ni za kusafiri safari sana, So fursa niliyoiona kwanza kwa haraka ni kulima kwa kukodisha au kununua mashamba huko vijijini. Naweza kusema nimelimisha sana mazao tofauti tofauti lakini kwakweli kazi ya kulima au kulimisha inataka kwanza usimamizi wa madhubuti sana. Sasa kwangu mimi ilikuwa ngumu sana kwa sababu leo nipo kesho sipo unaacha wasimamizi unaowaamini kule shamba lkn mwisho wa siku hasara tuu.

Lakini pia nilijaribu baadhi ya biashara kwa hapa mjini lakini pia usimamizi ulinigharimu. Kingine nilichogundua asee hakuna mtu anafanikiwa kwa kusomea au kuiga kuwa mfanyabiashara isipokuwa bishara ni inner motive ambayo mtu anakuwa nayo. Labda mtu akose option kabisa ya kuajiriwa ndio anaweza akaforce akawa mfanya biashara mzuri maana hana option.

Ukiwa na inner motive ya kufanya biashara hakuna kitakachokuzuia hata kusafiri kikazi hakuwezi kuwa tatizo sana lakini kwa mimi vingi nilivyojaribu vilikufa au ilikuwa ni loss tuu. Kwahiyo kama wewe umejaaliwa hiyo inner motive na umeajiriwa unaweza kuwa na mafanikio sana kwa sababu kipato unachopata kwenye kuajiriwa kinabust biashara zakko.

Kwahiyo ndugu zangu this is not an excuse lakini tunakumbushana tu binadamu tumeumbwa tofauti sana lakini pia tumelelewa kwenye mazingira tofauti. Nyie wenyewe mashahidi, hata humu ndani kuna nyuzi zinaanzishwa mtu ana milioni 100 lkni hajui afanye biashara gani wakati huo huo kuna watu wana nyuzi humu wanatafuta laki2 mtaji ili waimplement project zao watoboe maisha. Pia Hapa JF nyuzi kibao zimeanzishwa kushangaa hao viongozi wanaotuimbia mahuburi kila siku watu wafikirie kujiajiri na wakati wenyewe wakitumbuliwa hawajiari ila wanatega kunyenyekea teuzi zingine. Hapo utaona kwamba sio kwamba watu hawajui umuhimu wa kuwa na plan B lkini ile inner motive ni tatizo. Ni mtazamo tuu huu jamani. Kwa hiyo wandugu bado natafuta ajira hahahaa

OK, The chill time's interlude done, let's switch it up and get down to business. Nilisema hapo juu expect the unexpected eeh? Yes, ujue kwenye haya maisha sometimes mtu unakuwa unapanga mipango yako na kuwa namategemeo makubwa sana lakini unachokuja kukutana ni kinyume kabisa na matarajio yako. Wewe unapanga hili lakini unapigwa na kitu kizito ambacho huku tarajia kabisa.

Kama nilivodokeza huko juu kwenye maelezo yangu kwamba pale ofsini ukifauru probation unapewa mkataba wa miaka miwili ambao unaweza kurenewkila baada ya miaka miwili kulingana na uhitaji wa ofisi. Mashirika mengi tu haya makubwa yasiyo ya kiserikali wanafanya hivi hata haya international. Na kwa taratibu za pale ofisini ilikuwa ukifauru kurenew mkataba mara mbili yaani ufanye nao kazi kwa miaka minne na kuendelea huwa wanakupa zawadi nzuri tuu ya fedha nadhani ilikuwa ni motivation ya kuwafanya watu wabaki pale kwa muda mrefu japo kutimuana kulikua nje nje kama usipoenda sawa na taratibu za ofisi.

Basi mimi nashukuru Mungu nilipiga mzigo kwa muda wa miaka minne yaani nilifanikiwa kurenew mkataba mara moja. Sasa kuna kipindi nikaona huku kwenye ma NGO ni kama job security inakuwa ndogo sana, maana unaweza mwenyewe ukajidamka asubuhi, ukanyoosha, ukafika job ukakuta barua kutoka kwa HR kwamba kazi basi. Kwahiyo nikaanza kufikiria kutafuta kazi serkalini kwa kuamini kwamba kule kuna pensionable employment yaani ajira ya kudumu. Halafu yale mazingira very hectic ya kazi nikawa naona kama watu wa government wanakula sana shushu basi nikawa nawatamani sana. Maana mtu unakosa hata muda wa kusimamia mambo yako muhimu hata ujenzi unawea ukajikuta kwa sehemu kubwa ubawaacha mafundi wanajenga bila uwepo wako. Basi bhana Kwa kuwa sikuwa na presha basi nikawa natafuta kazi huku sina haraka kihivyo nikawa navizia zile nafasi ambazo naona nazihitaji ndio naaply.

Mungu wa mbinguni asivyo Athumani na wala haishi Kigamboni, ikatokea kwamba miezi miwili kabla ya kurenew mkataba wangu yaani nimalize miaka minne ili kama menejiment wataridhika na mimi basi nindelee nitimize miaka sita nikapata mchongo serikalini tena kwenye hizi idara ambazo zinajiendesha zenyewe mfano wa TRA, TPDC, TCRA, TBS, BRELA etc. Kuna moja hapo ndio nilipata tena ilikuwa ni kitengo cha elimu kwa umma ni shavu ambalo lilikuwa na safari nyingi maana ilikuwa ni kuzunguka mikoani kuelimisha watu maswala yanayohusiana na idara husika. Kwakweli ilikuwa na nafasi nzuri sana ambayo sikujiuliza mara mbili.

Nikaitaarfu menejimenti kwamba sitarenew tena mkataba. Nakumbuka line meneja wangu alisikitika sana maana mimi nilikuwa ni kati ya majembe yake aliyokuwa anayategemea katika kurescue challenged situation. Hapa nimekumbuka ishu moja nakumbuka kuna siku nililala au nilitoka ofsini saa kumi alfajiri kisa kurescue situation.

Ilikuwa hivi, boss kubwa la pale ofsini alienda Canada kweny meeting na donors sasa kwa kuwa ile ofisi yetu ilikuwa ni moja ya shirika linalofanya vizuri basi wakamwalika boss kubwa aende huko kutoa presentation namna gani tuanvofanya kazi mpaka kutoa matokeo makubwa. Sasa boss kubwa yeye alikuwa amejiandaa zile issue strategic zaidi kumbe wale donors walikuwa wanataka vitu ambavyo kwa boss kubwa vilikuwa ni minor sana nap engine vingempa shida kuvijibia kikamilifu labda kama angesoma maripoti ya miaka ya nyuma.

Sasa alipomaliza presentation yake inaonekana nwakamshooti maswali ambayo yalihitaji zaidi mtu anaeenda sana field ili kutoa majibu ya uhakika. Bosikubwa akamcheki line meneja kama vipi amwandalie baadhi ya majibu. Sasa muda huo ilikuwa ni muda wa kama saa moja ousiku watu ndio tunajiandaa kutoka ofsini na wengine wameshaondoka. Nadhani kwa kule Canada ilikuwa ndio asubuhi watu ndio wanaaza majukumu yao ya kikazi. Mara line manager akanipa simu niongee na bosskubwa jamaa akanielekeza pale ishu anazozitaka nimwandalie then nimtumie kwa email. Mimi nikamtumia fasta nikawa naondoka. Wakati nimshafika nje ya ofisi mara naona bosskubwa ananipigia wasapu kupokea ananiomba nimtafutie tena baadi ya taarifa. Nikalaani sana kwanini nilikuwa hewani wasapu hahaaa ila nikageuza sikuwa na jinsi. Sasa ile nitumie taarifa hii mara ile ikawa haiishi uzuri zile data mimi nilikuwa nazo. Basi nikamwambia bosskubwa kama vipi waniunge mimi kwa skype nikiwa pale ofsini ili tusaidie kuwajibu. Boss kubwa akaniuliza kama nina uhakika sita mwangusha, nikamwambia kwani hizo info si ndio mimi ambazo ninampatia, lakini nikashindwa tu kumwambia mbona wewe unajikanyaga kanyaga tuu huko hahaha. (Jokes, ofcourse I respect the na amekuwa role model wangu sana na alishalamba uteuzi serikalini mda mrefu tuu) kwenye ministerial level)

Basi akanicoonect pale yale majamaa meupe yakaanza kunishoot maswali pale nikawa nawajibu, wakawa wanataka kueleshwa kwa undani sana maana walikuwa ni wawakilishi wa wafadhili ambao ilikuwa walete mpunga mrafu sana ofisini. Basi pale nikajikuta naenda nao mpaka session yote aliyopangiwa bosskubwa ni kama bosskubwa alitumia akili kuwaambia kuwa kuna ofisa alimwandaa kutoka Tanzania (yaani mimi eti) kushiriki ule mkutano kwani alitaka kuonyesha pale ofsini tunacollective working style, basi ile pia ilimpa crediti sana. Basi mimi nikajikuta natoka pale saa nane yaani kama inaenda inaenda saa kumi. Uzuri ile ofisi ilikuwa karibu na breakpoint pale posta basi mda wa wao wakibreak kula mimi naingizia zangu breakpint nagonga msosi. Basi mwisho bosskubwa akanipa likizo ya sikumbili nipumzike kufidia ile kazi ya kutoboza usiku.

Basi wakati naaga menejiment wakanishawishi sana nibaki lakini ikashindikana na nikawapa sababu naenda serikalini basi ikabidi tuu waelewe na kunitakia kila lenye heri. Kwakuwa nilimaliza miaka mine pale basi nikapewa mshiko wangu wa pongezi na wiki ya mwisho wakandaa farewell cake tukatata pale ofisi nzima then nikamalizia vimeo vyangu kisha nikakabidhi ofisi nikaondoka kuanza majukumu mapaya.

Sasa kule serikalini baada ya kupokea offer letter kilichobaki ni kusaini tu mkataba. Kwa kuwa tulikuwa watu kama 10 hivi tuliopata ajira pale kwenye hiyo position ilibidi tusubiriane ili wote tuanze siku moja. Kwa hiyo mimi tangu nilipoacha kazi nilikuwa na kama mwezi mmoja hivi wa kupumzika ndio nikaanze kazi serikalini. Niliona afadhali na nilifurahi kupata hilo gap kwa sababu huo muda niliutumia kupumzika na familia nyumbani kwa sababu kipindi hicho ndio kwanza nilikuwa nimetoka kuoa na nina katoto ka kwanza. Basi maisha yakawa poa tuu huku nikiendelea kusikilizie muda ufike nikaanze mzigo serikalini.

Sasa kipindi kile ilikuwa ndio kipindi Magufuli ameingia ofisini, nadhani wote mnakumbuka speed aliyoingia nayo madarakani. Advertise ya kwanza Mkurugenzi wa ile idara ambayo nilipata kazi akatumbuliwa. Hiyo haikuwa big ishu kwangu sana maana ilikuwa hainiathiri moja kwa moja. Advertise ya pili mzee baba akastopisha ajira zote mpya serikalini until further directives. Hapo ndo nilipopigwa na kitu kizito, askwambie mtu ile taarifa uliifurahia au kuona ya kawaida kama tu ilikuwa haikugusi moja kwa moja ila kwa sisi ambao ilitugusa asee!!!

Sasa nikajipa moyo sisi tayari tunaofa letter so itakuwa haituhusu. Nikatamani kuwapigia wengine ambaop nao walikuwa wamepata iyo kazi lakini binafsi nikawa siwajui kwani nilisikia tu pale idarani wanasema nitakuwa na wenzangu wengine kama 10 hivyo tunasubiriana ili tuanze wote pamoja. Basi nikatimba pale idarani kwenda kuulizia mstakabalim utakuweje. Niliulizwa tuu umekuja na ile barua ya ofa? Nikajibu ndio, wakaniambia iache hapo kwa sekretari mpaka utakapopewa taarifa nyingine kwa muda ule maelekezo yalikwa ndio hayo. Daa pale pale nihisi nguvu zinaniishia lkn nikajikaza basi nikaiacha ile barua pale kwa secretary lakini nikaitoa kopi, na nikamuomba namba yule sekretari ili niwe nafatilia. Katika kipindi ambacho nilikuwa nafatilia taarifa ya nabari basi ni kipindi kile maana nilikuwa nataka kujua mzee baba ataruhusu lini kuendelea na michakato ya ajira pale ilipoishia.

Hahaaa ni kama ilikuwa kusubiria mawe yanayochemshwa eti yataiva, mzee baba alikaza. Nilikuwa nampigia simu yule sekretari wa pale serikalini kufatilia maendeleo nadhani mpaka alinichoka maana kuna siku akaniambia kaka sasa naona tu nikutafutie namba ya katibu wa ikulu ili uwe unampigia mwenyewe moja kwa moja. Dah nikaona hapa nishachokwa sasa, lakini nikasema hata kama ningekuwa mimi ningefanyaje. Kwakweli Nilikuwa frustrategy sana kipindi hiki ila sikujilaumu kuacha kazi kule nilikokuwepo maana sikukurupuka ni vile mipango imekwenda ndivyo sivyo. Basi ikabidi nikubaliane na hali halisi. Siku moja line manager akanipigia simu kuniuliza kama lile sekeseke limenikuta na mimi nikamweleza pale na mimi miongoni mwao akaishia tu kuniambia yaani mwezi uliofata tu baada ya mimi kuondoka walikuwa wameshapata mtu mwingine. Nilichomwambia tu asjali ila nitamweka awe referee wangu kwenye CV yangu maana niko mbioni sasa kutafuta sehemu ningine.

Hivi ndivyo ilivyokuwa na msala wangu wa kuhamia serikalini. Hapo nilijifunza kitu kikubwa sana wakati mungine sio kila plan unayoitegemea inakuja kama ilivyo, therefore, you better get ready for the unexpeceted outcomes. Ila badae nikaja kumwelewa na nikamkubali sana Rais Magufuli, ilikuwa ni nadra sana kutomfatilia hotuba zake kwenye vyombo vya habari labda niwe sina nafasi.

See you to the next episode tuone ilikuwaje. Thank you.
Ume nikumbusha mbali mkuuu mambo za meza kupinduka, kazi tuliwahi pata taasisi Fulani ya serikali tulingia Kwa maelekezo project ilikuwa kama pailot tukaona tume tusua aseeee tukapewa mikataba baada ya muda watu walimtisha boss juu ya hiyo project kumbe walikuwa wameandaa watu wao ,boss akazama king tukala za uso mkataba ukasitishwa wajuba tukakaa benchi shushu ilikuwa tamu sana.
 
Back
Top Bottom