Mambo muhimu ya kufanya pindi tu unapopokea taarifa za msiba wa mzazi wako au ndugu yako wa karibu

Mambo muhimu ya kufanya pindi tu unapopokea taarifa za msiba wa mzazi wako au ndugu yako wa karibu

Juzi napokea taarifa dada yangu amepata ajali amepoteza fahamu wamempeleka hospitali yawezekana hata amepoteza uhai!!!!!!! Nikakata simu nikwamuomba MUNGU nikamwambia MUNGU kama YESU KRISTO alikufa msalabani na akafufuka akaushinda umauti na huyu dada anyanyuke hata sasa AMENI.

Nikampigia simu shemeji ananiambia nipo nae namrudisha nyumbani jion nampigia dada anasema ameanza na mazoezi.

Nimeamini Ukiomba kwa imani lolote linakuwa.
Hakika Mungu alikuongoza katika hilo. Ki ukweli pamoja na kwamba kufiwa kuna umma, lakini kuwa mstahamilivu na jasiri katika kupokea taarifa za kutisha namna hii humsaidia mtu kupata muda wa kufanya maombi fulan ambayo baadae huwa na msaada mkubwa kwa muombaji.
 
We umeongelea mambo ya kiroho. Yapo ya kimwili au kidunia. Ukifiwa usipipoteze mwelekeo.
Kwanza funga milango watu wakusanyike nje au kibarazani.

Pili usilielie, angalia nyendo za ndugu zako maana wengine wanatumika kipindi cha msiba kufanya hujuma kwenye familia.

Tatu kama eneo lako kuna utaratibu wa kuendesha misiba na jumuia, ukoo, vyama vya kuzikana n.k waachie wafanye majukumu yao.

Nne hakikisha wasichana na aki na mama wa ndani wanakuwa sehemu moja usiku na mchana ili wasifanye uchafu kipindi cha msiba.
Hahaha huu nao ni ushauri mzuri wa kuzingatia. Ubarikiwe sana mkuu kwa ushauri ulioshiba.
 
Ushauri mzuri ktk kipindi kigumu, ila sijui kwenye item 4 kutumia muda mwingi kumuombea marehemu alazwe pema una tumia reference ya imani ipi? Nasema hivi kwakuwa baadhi ya imani say wakristo, wewe mwenyewe ukiwa hai kwa matendo yako ndio utakua unajiamulia uende wapi Bwana akikutwaa!

Naamanisha ibada tunayofanyia wafu ni utaratibu na utu kufanya hivyo otherwise haibadili hatma yako ie. Chapter yako inakua closed kwa namna ulivyoishi.

Yote kwa yote, umefanya vizuri kushauri namna ya kujipanga msiba unapotokea ukizingatia KIFO HAKIZOELEKI!
Kweli mkuu, kwanza nafikiri imani zote zinashauri mtu kufanya ibada mwenyewe akiwa hai, kuliko kutegemea kuombewa baada ya kifo.

Ndio maana hata waislam wanasisitiza mtu uswali kabla haujaswaliwa. Lakini pia hii haiondoi ile nafasi ya kumuomba Mungu amsamehe marehemu madhambi yake nk. Maana hatuwezi kujua pengine Mungu ataweza kutumia maombi ya waombaji wema kumsamehe marehemu.

So hiyo namba 4 ni moja kati ya njia ya kumfariji mfiwa. Kwani hakuna mtu ambae hupenda kuona ndugu yake anaenda mahali pabaya huko mbinguni.
Japo mtu anaweza kujua kwamba baba yake, mama yake, mke au mume wake alikuwa haendi kanisani wala msikitini lkn akifanya maombi huhisi faraja kwamba anakuwa amemsaidia ndugu yake kuepukana na adhabu ya Mungu huko alipokwenda.
 
Kiuhalisia ukifiwa haya mambo hayapo
Inategemea mtu na mtu. Ya kwa wengine obvious inaweza kuwa ngumu kwa muda ule anaopewa taarifa kutokana na uzito wa msiba. Lkn baada ya kutulia kama dakika 5 hivi akili kidogo inarudi mahala pake na muhusika anaanza kufanya haya niliyoyaandika. Soma comment namb #18 utaelewa mkuu.
 
Leo nimemkumbuka baba yangu hadi chozi kukaribia kunitoka alafu nakutana na mada kama hii.

Uchungu wa kufiwa unatofautiana ndugu, na mbinu za kumfariji mfiwa pia haziwezi kuwa sawa
Ya ni kweli kabisa mkuu, ila inategemea mtu na mtu.
 
Habari zenu wana JF wenzangu

Bila kupoteza muda ndugu zangu inajulikana wazi kuwa kila binadamu yupo hapa duniani kwa siku zake maalum za kuishi, na baada ya siku hizo kuisha atakufa na kurudi kule alipotokea.

Sasa basi.. ingawa kifo kipo lakini hakuna anaependa kufa au kufiwa. Hii ni kwa sababu kwanza ukishakufa haurudi kuwa hai, pili hakuna anaejua kwa macho yake mwenyewe kwamba baada ya kufa anakwenda wapi, tatu dini zimekuwa zikitueleza kuhusu adhabu iliyopo mbele yetu baada ya vifo vyetu kutokana na matendo yetu.

Kwa vile hakuna binadamu aliekamilika, kwahiyo kila mmoja wetu anajiona ana makosa mbele ya Mungu, hivyo kuogopa kufa mapema na kwenda kukutana na adhabu zake.

Halikadhalika pia hakuna anaependa kufiwa. Hii ni kwa sababu mfiwa anajua kwamba huyo baba yake, mama yake, mtoto wake au ndugu yake aliefariki hatopata tena chance ya kuonana nae katika maisha ya duniani. Yani ndio unakuwa mwisho wao kuongea pamoja, kucheka pamoja, kuishi pamoja, kusaidiana, kupendana, kuonana nk.
Hivyo basi mfiwa huumia kwa namna ambavyo alimpenda au kuwa na ukaribu na marehemu.

Maumivu ya kufiwa, au kufa kwa yule anaekiona kifo chake huwa ni makubwa sana. Mfano mama anapoona kwamba ugonjwa alionao hauwezi kupona, na pengine anakaribia kufa huku akiwaacha watoto wake wakiwa bado wadogo mno wenye kumuhitaji na kuhitaji malezi yake, ni lazima ataumia sana tena sana ila hatokuwa na la kufanya zaidi ya kuomba dua Mungu amsaidie kumlelea watoto wake kupitia mtu fulani, (labda bibi, mamdogo, shangazi nk) pindi tu atapochukua roho yake.

Mimi nimesha experience kufiwa na mzazi ambae tulimpenda sana, na yeye alitupenda mno watoto wake. So i know how it feel kuondokewa ghafla au hata kwa maradhi na mzazi au ndugu, lakini kuna njia ambayo ukiitumia kipindi cha msiba huo mzito itakusaidia kwa kiwango fulani kupunguza maumivu utayopata wewe mfiwa.

Je unatakiwa ufanyaje baada ya kushuhudia kwa macho yako kifo cha baba yako, mama yako, au ndugu yako, au pengine kuletewa habari za kifo chake.

1) Jambo la kwanza kama ni Mkristo unatakiwa hapo hapo useme ama kwa hakika bwana wewe ndio ametoa na wewe ndio umetwaa, jina lako lenye nguvu kuliko majina yote lihimidiwe daima milele AMEN

Kama ni Muislamu unatakiwa kusema Inna lillah Wainna Illayhi rajiun (Hakika sisi wote ni wa kwako Mola wetu mtukufu, na kwako wewe Mola wetu mtukufu sisi sote tutarejea)

Kwa wale wasiofatilia kauli hizi za dini unaweza kusema sisi tulimpenda, lakini wewe Mungu ndio umempenda zaidi.

Hii itakupa faraja kubwa mfiwa kwani itambidi ukubaliane na ukweli kwamba Mungu mwenyewe ameamua kuchukua kilicho chake, kwahiyo huna budi kukubaliana na hali hiyo hata kama hukutarajia au kupendezewa nacho.

2) Jambo la pili unatakiwa umuombe Mungu kwa imani yako akuongoze katika kipindi hiki kigumu kwako, lakini pia akupe subira na ustahamilifu, na pia kukuepusha na kufuru. Hii ni kwa sababu kuna baadhi ya watu wakifiwa na watu wao wa karibu huluzi fasta control na kupelekea wengine kukufuru Mungu kwamba "kwanini umemchukua mama yangu tu na sio mama wa kina Nusrat, Jessica, Abdallah, John nk" sijui "nimekukosea nini Mungu hadi kunipa msiba huu mzito ambao unajua kabisa siwezi kuubeba", "Eeh Mungu wangu kwanini umemchukua mwanangu mkubwa ambae ndio alikuwa tegemeo langu, je maisha yangu yatakuaje baada ya kumchukua mwanangu huyu mwenye msaada mkubwa kwangu nk. Yani inafika kipindi mtu anasahau kwamba kila kiumbe hapa duniani ni cha Mungu, kwahiyo hakuna mwenye uwezo au ruhusa ya kumzuia kukichukua, iwe leo, kesho au siku yoyote aitakayo yeye muumbaji.
Kumbuka Mungu huwa hakosei na wala haonei. Kila analofanya limekamilika tangu enzi na enzi.

3) Jambo la tatu ni kumuomba Mungu akupe muongozo wa maisha yako mapya ambayo utaishi bila kuwa karibu na yule alieondoka.

4) Jambo la nne tumia muda mwingi kumuombea marehemu ili apate makazi mema au Mungu aipokee roho yake na kuiweka katika roho za walio wema.

Kifupi ya kwangu ni hayo tu, ila kama kuna mungine anayo ya zaidi ya haya basi ruhusa kuyaorodhesha hapo chini kwenye comments.

Hii ni kwa wale tunaoamini uwepo wa Mungu, bila kujali dini ya mtu. Ila wasioamini uwepo wa Mungu naomba wasome tu lakini wasiandike chochote kuharibu uzi huu.

Karibuni ndugu zangu.
Nakataa kukubaliana na ww moja kwa moja japo umeshauri vtu vya msingi,ndugu kumbuka tone ya msiba hubadilika kulingana na mambo yanavoendelea Mara tu baada ya kupokea taarifa,kwnz Ni taarifa mbaya ambazo huwez kuzibadili ili walau ziwe Ni jokes,waweza yazingatia hayo uloyashauri ila ikafika mda wa kuaga Mara ya mwisho tone ikabadilika akili zinakuja kurud unajikuta wodini,au Ile umejitahd kuicontrol mood ila wafiwa wenzio wakakuaminisha through body language kuwa wanaumia Sana Sana,pengine Ni wadogo zako au mama yako/baba yako napo mood ikakudrive harshly,kumbuka hayo yote huja mfiwa akiwa kwny hali mbaya Sana mentally and emotionally,hapa ndipo nyimbo za faraja na maneno mazuri mtu huhisi km ana kupigiwa kelele flan hv,acha tuuu,RIP daddy
 
Inategemea mtu na mtu. Ya kwa wengine obvious inaweza kuwa ngumu kwa muda ule anaopewa taarifa kutokana na uzito wa msiba. Lkn baada ya kutulia kama dakika 5 hivi akili kidogo inarudi mahala pake na muhusika anaanza kufanya haya niliyoyaandika. Soma comment namb #18 utaelewa mkuu.
Kufuata hayo mambo ukifiwa??
Labda msiba tu msiba
Sio msiba unaohusu damu yako
Ila pia watu tunatofautiana moyo na viwango vya mqpenzi
 
Nakataa kukubaliana na ww moja kwa moja japo umeshauri vtu vya msingi,ndugu kumbuka tone ya msiba hubadilika kulingana na mambo yanavoendelea Mara tu baada ya kupokea taarifa,kwnz Ni taarifa mbaya ambazo huwez kuzibadili ili walau ziwe Ni jokes,waweza yazingatia hayo uloyashauri ila ikafika mda wa kuaga Mara ya mwisho tone ikabadilika akili zinakuja kurud unajikuta wodini,au Ile umejitahd kuicontrol mood ila wafiwa wenzio wakakuaminisha through body language kuwa wanaumia Sana Sana,pengine Ni wadogo zako au mama yako/baba yako napo mood ikakudrive harshly,kumbuka hayo yote huja mfiwa akiwa kwny hali mbaya Sana mentally and emotionally,hapa ndipo nyimbo za faraja na maneno mazuri mtu huhisi km ana kupigiwa kelele flan hv,acha tuuu,RIP daddy
Ni kweli mkuu kuondokewa kuna uma, na hata mimi yalinikuta mwaka mmoja tu uliyopita tena nikiwa nje ya nchi. Kama hautojali sogea kidogo hapo juu kwenye post namb #18 nimeeleza hali ilivyokuwa.

Hakika ni uchungu lkn kuna njia ukikumbuka kuzitumia za kumtegemea Mungu kwa kile kilichotokea, basi Mungu huyo huyo atakusaidia kukupa faraja fulan ambayo hakuna mtu yeyote atakaeweza kukupa.

RIP kwa wazazi wetu wote waliotangulia mbele ya haki.
 
Wewe kariri tu kifo ni tukio la kawaida la asili. Hakuna anaeishi milele.
Mkuu hata ukariri vipi hili swala moja wapo likikufika, ukariri wako utakutoka kwa muda. Yani angalau baada ya dakika kadhaa ndo akili itakaa sawa na kukupa uhalisia kwamba kweli kufa kupo na wote tutakufa.
 
Kufuata hayo mambo ukifiwa??
Labda msiba tu msiba
Sio msiba unaohusu damu yako
Ila pia watu tunatofautiana moyo na viwango vya mqpenzi
Yah ni kweli inategemea mtu na mtu, lkn pia ni neema fulan kama ukiwa unapenda kumuomba Mungu akuongoze kwenye hayo pindi tu unapopokea habari ya msiba wa mtu wako wa karibu.
 
Hapo kwenye namba 4 huwa ni faraja tu za huku duniani kuwekana sawa kisaikolojia, hakuna kitu utafanya kumshawishi Mungu mtu akishamaliza safari yake!
Soma Ebr 9:27
 
Hapo kwenye namba 4 huwa ni faraja tu za huku duniani kuwekana sawa kisaikolojia, hakuna kitu utafanya kumshawishi Mungu mtu akishamaliza safari yake!
Soma Ebr 9:27
Yah ni kweli kabisa, ila si kuna ile kufarijiana kama ulivyosema mkuu.
 
Habari zenu wana JF wenzangu

Bila kupoteza muda ndugu zangu inajulikana wazi kuwa kila binadamu yupo hapa duniani kwa siku zake maalum za kuishi, na baada ya siku hizo kuisha atakufa na kurudi kule alipotokea.

Sasa basi.. ingawa kifo kipo lakini hakuna anaependa kufa au kufiwa. Hii ni kwa sababu kwanza ukishakufa haurudi kuwa hai, pili hakuna anaejua kwa macho yake mwenyewe kwamba baada ya kufa anakwenda wapi, tatu dini zimekuwa zikitueleza kuhusu adhabu iliyopo mbele yetu baada ya vifo vyetu kutokana na matendo yetu.

Kwa vile hakuna binadamu aliekamilika, kwahiyo kila mmoja wetu anajiona ana makosa mbele ya Mungu, hivyo kuogopa kufa mapema na kwenda kukutana na adhabu zake.

Halikadhalika pia hakuna anaependa kufiwa. Hii ni kwa sababu mfiwa anajua kwamba huyo baba yake, mama yake, mtoto wake au ndugu yake aliefariki hatopata tena chance ya kuonana nae katika maisha ya duniani. Yani ndio unakuwa mwisho wao kuongea pamoja, kucheka pamoja, kuishi pamoja, kusaidiana, kupendana, kuonana nk.
Hivyo basi mfiwa huumia kwa namna ambavyo alimpenda au kuwa na ukaribu na marehemu.

Maumivu ya kufiwa, au kufa kwa yule anaekiona kifo chake huwa ni makubwa sana. Mfano mama anapoona kwamba ugonjwa alionao hauwezi kupona, na pengine anakaribia kufa huku akiwaacha watoto wake wakiwa bado wadogo mno wenye kumuhitaji na kuhitaji malezi yake, ni lazima ataumia sana tena sana ila hatokuwa na la kufanya zaidi ya kuomba dua Mungu amsaidie kumlelea watoto wake kupitia mtu fulani, (labda bibi, mamdogo, shangazi nk) pindi tu atapochukua roho yake.

Mimi nimesha experience kufiwa na mzazi ambae tulimpenda sana, na yeye alitupenda mno watoto wake. So i know how it feel kuondokewa ghafla au hata kwa maradhi na mzazi au ndugu, lakini kuna njia ambayo ukiitumia kipindi cha msiba huo mzito itakusaidia kwa kiwango fulani kupunguza maumivu utayopata wewe mfiwa.

Je unatakiwa ufanyaje baada ya kushuhudia kwa macho yako kifo cha baba yako, mama yako, au ndugu yako, au pengine kuletewa habari za kifo chake.

1) Jambo la kwanza kama ni Mkristo unatakiwa hapo hapo useme ama kwa hakika bwana wewe ndio ametoa na wewe ndio umetwaa, jina lako lenye nguvu kuliko majina yote lihimidiwe daima milele AMEN

Kama ni Muislamu unatakiwa kusema Inna lillah Wainna Illayhi rajiun (Hakika sisi wote ni wa kwako Mola wetu mtukufu, na kwako wewe Mola wetu mtukufu sisi sote tutarejea)

Kwa wale wasiofatilia kauli hizi za dini unaweza kusema sisi tulimpenda, lakini wewe Mungu ndio umempenda zaidi.

Hii itakupa faraja kubwa mfiwa kwani itambidi ukubaliane na ukweli kwamba Mungu mwenyewe ameamua kuchukua kilicho chake, kwahiyo huna budi kukubaliana na hali hiyo hata kama hukutarajia au kupendezewa nacho.

2) Jambo la pili unatakiwa umuombe Mungu kwa imani yako akuongoze katika kipindi hiki kigumu kwako, lakini pia akupe subira na ustahamilifu, na pia kukuepusha na kufuru. Hii ni kwa sababu kuna baadhi ya watu wakifiwa na watu wao wa karibu huluzi fasta control na kupelekea wengine kukufuru Mungu kwamba "kwanini umemchukua mama yangu tu na sio mama wa kina Nusrat, Jessica, Abdallah, John nk" sijui "nimekukosea nini Mungu hadi kunipa msiba huu mzito ambao unajua kabisa siwezi kuubeba", "Eeh Mungu wangu kwanini umemchukua mwanangu mkubwa ambae ndio alikuwa tegemeo langu, je maisha yangu yatakuaje baada ya kumchukua mwanangu huyu mwenye msaada mkubwa kwangu nk. Yani inafika kipindi mtu anasahau kwamba kila kiumbe hapa duniani ni cha Mungu, kwahiyo hakuna mwenye uwezo au ruhusa ya kumzuia kukichukua, iwe leo, kesho au siku yoyote aitakayo yeye muumbaji.
Kumbuka Mungu huwa hakosei na wala haonei. Kila analofanya limekamilika tangu enzi na enzi.

3) Jambo la tatu ni kumuomba Mungu akupe muongozo wa maisha yako mapya ambayo utaishi bila kuwa karibu na yule alieondoka.

4) Jambo la nne tumia muda mwingi kumuombea marehemu ili apate makazi mema au Mungu aipokee roho yake na kuiweka katika roho za walio wema.

Kifupi ya kwangu ni hayo tu, ila kama kuna mungine anayo ya zaidi ya haya basi ruhusa kuyaorodhesha hapo chini kwenye comments.

Hii ni kwa wale tunaoamini uwepo wa Mungu, bila kujali dini ya mtu. Ila wasioamini uwepo wa Mungu naomba wasome tu lakini wasiandike chochote kuharibu uzi huu.

Karibuni ndugu zangu.
Huu ushauli ni mzuli japo ni mgumu kuutekeleza pindi unapoletewa taarifa ya msiba wa mtu wako wa karibu
 
Huu ushauli ni mzuli japo ni mgumu kuutekeleza pindi unapoletewa taarifa ya msiba wa mtu wako wa karibu
Ndo mana tukasema inategemea na mtu. Ila ukiwa unamuomba Mungu kwamba siku likitokea tukio la aina hiyo akuongoze katika haya manne, basi uwezekano wa kuyafanya kupitia Mungu upo.
 
Ushauri mzuri ktk kipindi kigumu, ila sijui kwenye item 4 kutumia muda mwingi kumuombea marehemu alazwe pema una tumia reference ya imani ipi? Nasema hivi kwakuwa baadhi ya imani say wakristo, wewe mwenyewe ukiwa hai kwa matendo yako ndio utakua unajiamulia uende wapi Bwana akikutwaa!

Naamanisha ibada tunayofanyia wafu ni utaratibu na utu kufanya hivyo otherwise haibadili hatma yako ie. Chapter yako inakua closed kwa namna ulivyoishi.

Yote kwa yote, umefanya vizuri kushauri namna ya kujipanga msiba unapotokea ukizingatia KIFO HAKIZOELEKI!
Hili suala limekaa kiimani sana Kumuombea marehemu apumzike salama..hii naona haina mantiki yoyote
 
Back
Top Bottom