nzalendo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 12,106
- 12,916
Hii ni kwa ufupi juu ya mambo mbali mbali tunayokutana nayo toka enzi mpaka leo hii.....Mengine hudhaniwa ni ya kutunga mengine yanahusishwa na uchawi na ushirikina hasa kwenye makampuni ......
Basi hapa nitakuwa nampeni stori tofauti tofauti juu ya vituko na mambo ambayo si ya kawaida sana katika ulimwengu huuu.
Miaka mingi imepita tulikuwa tunasafiri kuelekea Mpanda tuna lori limekula nundu ya kutosha mixer vipeto ..unajua njaa tena.....sasa njia tuliyopita ni ya Manyoni halafu unakata kushoto kuelekea Rungwa kisha unakata kulia kuitafuta KItunda....hapa tulipishana na basi la SABENA linatoka Tabora kueleke Mbeya hii njia kwa miaka hiyo ni njia dume kwelikweli na tulikuwa tunapita nyakati za kiangazi...aidha tulikuwa tunatembea na kila kitu muhimu kwa dharura ya aina yoyote ile.....
Kwa kifupi kuna pori linaitwa Mpembampazi hapo kuna Simba wakubwa kuliko simba wote niliokwisha kuwaona pia kuna Twiga weupe....anyway .......ilikuwa majira ya kama saa kumi na mbili jioni hivi machine inaunguruma mdogo mdogo taa nilikuwa nimewasha ingawa giza lilikuwa sio zito bado kulikuwa na mwanga.....zingatia ni ndani ya msitu(pori ) nene.....mara taa za gari zikawa zinajiwasha na kujizima zenyewe kama vile zimechanganyikiwa...halafu gari likazima ghafla....kwenye gari tulikuwa watu sita..mmoja kwenye kiti kushoto..... wawili kitanda cha chini...... na wawili kitanda cha juu.....wote tukawa kimya tunatafakari....kujaribu kupiga starter hata switch on haionyeshi.....tukawa kimya kama dk. moja hivi.....mara ukapita upepo wa baridiii upepo mkali kiasi halafu kimyaaa......mara tukasikia mlia shwaa shwaaa shwaa shwaaa kama vile kuna kitu kinaji buruza....
Kuangalia mbele tulishuhudia nyoka mweupe kama maziwa hana madoa doa ni mweupe tuu unene wake ni kama sadolin yaani diameter yake.....halafu kakatiza barabara kwa mbele....wote tuko kimya tunamuangalia tu....kichwa kikapotelea chakani lakini kiwiliwili bado kinakatiza barabarani....,,na mlio shwaa shwaa shwaaa.....duuuh...sasa cha ajabu zaidi mkiani alikuwa anawaka taa...taa ya rangi ya blue..na ina mwanga wa kutosha.....yaani mkia wake ulisimama juu kama mkia wa ng'e..halafu kwa juu kuna kama kakikombe ndio kuna kama jiwe hivi ndio linalotoa huo mwanga........bahati mbaya zamani hizo tulikuwa hatutembei na kamera.....
kwa kifupi baada ya joka kupotelea kichakani gari lilikubali kuwaka na tukaendelea na safari...sasa baada ya kufika Mpanda tukawahadithia jambo tulilolishuhudia......wakafurahi sana wakatukaribisha sehemu fulani kuna wazee wanakunywa pombe za kienyeji...walituhoji na kupata uhakika kabisa kwamba huyo nyoka wanamfahamu na kumuona ni bahati kubwa sana na huonekana mara moja baada muda mrefu sana na lile jiwe linalowaka taa ni jamii ya LULU....
.....ITAENDELEA>>>>>>>>
Basi hapa nitakuwa nampeni stori tofauti tofauti juu ya vituko na mambo ambayo si ya kawaida sana katika ulimwengu huuu.
Miaka mingi imepita tulikuwa tunasafiri kuelekea Mpanda tuna lori limekula nundu ya kutosha mixer vipeto ..unajua njaa tena.....sasa njia tuliyopita ni ya Manyoni halafu unakata kushoto kuelekea Rungwa kisha unakata kulia kuitafuta KItunda....hapa tulipishana na basi la SABENA linatoka Tabora kueleke Mbeya hii njia kwa miaka hiyo ni njia dume kwelikweli na tulikuwa tunapita nyakati za kiangazi...aidha tulikuwa tunatembea na kila kitu muhimu kwa dharura ya aina yoyote ile.....
Kwa kifupi kuna pori linaitwa Mpembampazi hapo kuna Simba wakubwa kuliko simba wote niliokwisha kuwaona pia kuna Twiga weupe....anyway .......ilikuwa majira ya kama saa kumi na mbili jioni hivi machine inaunguruma mdogo mdogo taa nilikuwa nimewasha ingawa giza lilikuwa sio zito bado kulikuwa na mwanga.....zingatia ni ndani ya msitu(pori ) nene.....mara taa za gari zikawa zinajiwasha na kujizima zenyewe kama vile zimechanganyikiwa...halafu gari likazima ghafla....kwenye gari tulikuwa watu sita..mmoja kwenye kiti kushoto..... wawili kitanda cha chini...... na wawili kitanda cha juu.....wote tukawa kimya tunatafakari....kujaribu kupiga starter hata switch on haionyeshi.....tukawa kimya kama dk. moja hivi.....mara ukapita upepo wa baridiii upepo mkali kiasi halafu kimyaaa......mara tukasikia mlia shwaa shwaaa shwaa shwaaa kama vile kuna kitu kinaji buruza....
Kuangalia mbele tulishuhudia nyoka mweupe kama maziwa hana madoa doa ni mweupe tuu unene wake ni kama sadolin yaani diameter yake.....halafu kakatiza barabara kwa mbele....wote tuko kimya tunamuangalia tu....kichwa kikapotelea chakani lakini kiwiliwili bado kinakatiza barabarani....,,na mlio shwaa shwaa shwaaa.....duuuh...sasa cha ajabu zaidi mkiani alikuwa anawaka taa...taa ya rangi ya blue..na ina mwanga wa kutosha.....yaani mkia wake ulisimama juu kama mkia wa ng'e..halafu kwa juu kuna kama kakikombe ndio kuna kama jiwe hivi ndio linalotoa huo mwanga........bahati mbaya zamani hizo tulikuwa hatutembei na kamera.....
kwa kifupi baada ya joka kupotelea kichakani gari lilikubali kuwaka na tukaendelea na safari...sasa baada ya kufika Mpanda tukawahadithia jambo tulilolishuhudia......wakafurahi sana wakatukaribisha sehemu fulani kuna wazee wanakunywa pombe za kienyeji...walituhoji na kupata uhakika kabisa kwamba huyo nyoka wanamfahamu na kumuona ni bahati kubwa sana na huonekana mara moja baada muda mrefu sana na lile jiwe linalowaka taa ni jamii ya LULU....
.....ITAENDELEA>>>>>>>>