Mambo ya kuzingatia uwapo safarini

Mambo ya kuzingatia uwapo safarini

Mbna upande wa kure-play msg inazingua hapa forum? Shughulikieni hili linakera
 
Hivi kwann kuna kuwa na wadada wa hivi?! Me hii huwa nakutana nayo sana kwenye daladala, unakutana na mdada ananuka jasho la kichwa balaa yaani harufu ambayo ni kali kuvumilia.

Mara nyingi huwa ni kipindi cha jua kali. Au mvua imnyeshee halafu jua liwake muda huo huo.
Uchafu tu
 
Msafiri kafiri. Nimewahi safiri bila nauli kwenye treni (Kuzamia bafeti) toka Mpanda mpaka Tabora. Katika kubadili badili siti na harakati za kukwepa msako nikajikuta nipo siti moja na mdada ana watoto watatu wadogo, hakunisemesha njia nzima na ikaonekana uwepo wangu ni kero kwake. Chuma ikabuma (iliharibika) porini siku mbili mimi nilikuwa na mikate bofro mbili na maji makubwa chupa mbili maana najua kadhia ya treni zetu za mkoloni.
Basi nikagawa mkate mmoja, nikamwambia awape watoto wapoze njaa baada ya kuona kaishiwa misosi maji na majuisi juisi yake ambayo njia nzima alikuwa anakula peke yake na wanae.
Tulikaa pale siku mbili na mimi nilikuwa na simu ya Nokia inakaa na chaji wiki, akaniomba simu awasiliane na watu wake maana yake iliisha chaji nikamwambia mimi sina mawasiliano hivyo nikatoa laini yangu akaweka ya kwake na simu yangu ikawa kama yake.
Kichwa kilikuja asubuhu tukaendelea na safari mpaka Tabora. Tumefika Tabora stendi yule sister akanipa laki moja kama shukrani na asante kibao basi sikuchujua hata namba nikajikataa zangu kiroho safi bandidu mie.
Toka hapo nilijifunza kuwa mwema na mkarimu safarini mpaka leo hii. Hii ilikuwa 2011.
 
Najijua nilivyo ndo mana nakwambia hivyo
Kimasihara siliwi mkuu
Ova🤣🤣🤣🤣
.... ndio maana nasema tunza akiba ya maneno mkuu, watoto ni kwa vile hawapost ila nao wanaongoza kwa kula kimasikhara... itakuja kukukuta tu hata ya mtoto.
 
1. Salimia unayemkuta kwenye siti maana hujui ya baadae. Inakera hukusalimia halafu baadae unaanza kuuliza "Eti hapa tumefika wapi?" 🙄🙄🙄

2. Kuwa mstaarabu unapoingia kwenye basi hasa kama tayari unajua siti yako haina haja ya kugombania mlangoni.

3. Sikiliza nyimbo na video za kwenye simu yako kwa kutumia earphones kwani kinachokufurahisha wewe kwa mwingine yawezekana ni kero.

4. Usiongee na simu kwa sauti kubwa hasa mambo yako binafsi kwani hakuna anayehitaji kujua mambo yako.

5. Kuwa mwangalifu unaposinzia epuka kumlalia jirani yako unaposinzia. Sambamba na hilo soma gazeti lako kwa uangalifu sio unalitandaza hadi linagusa pua ya mwenzako.

6. Usilazimishe kuchungulia dirishani kila mara wakati umekaa siti ya katikati, hiyo ni kero kwa aliyekaa dirishani.

7. Kama unasafiri na watoto wakatie siti yao isiwe kero kwa jirani yako. Unasafiri na watoto watatu kwenye siti moja ni kero kwa jirani yako na kwa watoto.

8. Usipake pafyumu kali za kukereketa wenzio. Sambamba na hilo piga mswaki vizuri ni kero kukaa na abiria anayenuka mdomo hasa anapokusemesha.

9. Msome abiria uliyekaa naye kama hapendi kusemeshwa usimsemeshe semeshe, mwache, wengine wana mambo yao kichwani, wengine wanaenda kwenye misiba, wengine wamefukuzwa na waume zao huko walikotoka, sio kila mtu anapenda kuongea safarini.

10. Kama unajijua una tatizo la kutapika safarini jiandae mapema kwa kuwa na vifaa vya kukusaidia kwenye hali hiyo.

Ongezea la kwako hapo kama unalo.
Mabasi yenye muziki, mhudumu /konda au dereva wasifungulie mziki sauti kubwa mno kana kwamba humo ndani ni Bar. Wazingatie kwamba kila abiria ana mambo yake kichwani yaliyomfanya asafiri na sio kuja kusikiliza muziki kwenye gari lao.
Ila No 1,3,4,8 na 9 nimezipenda sana. Hongera mkuu.
 
Yani ndio Bus linatoka mule Mbezi Louis kuitafuta Morogoro road, mama na mtoto waliokaa pembeni yangu wote kwa pamoja wakaanza kutapika. Dakika sifuri tu nimepakwa matapishi dadek.

Sijawahi kusafiri kwa raha mimi.

Enzi za Mohammed trans, natoka kanda ya ziwa kuitafuta Dar. Kuna wabibi ndani ya bus wanasafiri na wajukuu wao wadogo sana kiumri. Mmoja kati yao akaachia uharo kwenye corridor zile za katikati ya siti. Bus zima tulitafutana kwa hiyo harufu yake!

Mara nyingine tena natoka Dar kwenda Kanda ya Ziwa, ndani kuna familia ya hawa ndugu zetu wasukuma. Yani mmoja amekaa siti ya nyuma kabisa, anapiga story na mwenzie aliekaa siti ya katikati ya Bus. Walipanda na ndoo ndogo ya maji ya kunywa, wanachota kwa kikombe then wanapasiana kutoka nyuma mpaka katikati. Siku hiyo kabila lote la wasukuma lilinikwaza!

Mara ya mwisho nimepanda Bus, siti ya pembeni akakaa mzee mmoja hivi. Asee mzee alikua ananuka tumbaku sijawahi ona. Kila watu wakishuka kula na kuchimba dawa, yeye anashuka kuvuta tumbaku zake. Nilifika kwa tabu sana wakuu!
Hao wasukuma ndio kiboko 😂😂ndoo ya maji
 
Ndio maana huwa napenda nikisafiri na basi yaani safari inapoanza tu mi nishagida pombe kitambo. Hapo simsumbui mtu mwanzo mpaka mwisho wa safari. Nishawahi kulala kabisa kwenye siti za nyuma kuanzia Manyoni hadi Mbezi.
 
Siku iyo niko Moro msamvu mida ya saa 4 usiku Nasubiri usafiri wa kwenda Dar ikaingia New Force ya kutoka Sumbawanga ilijaa ila nikapanda ivyoivyo, sasa nikawa nimesimama.

Sasa karibu na kwenye siti niliosimama kulikuwa na mkaka anachati na mke wake, mke wake akawa anamwambia mumewe umeme nyumbani kwao umekatika, basi mwanaume akamjibu, kwahiyo leo tunatom**na kwenye giza?!! Nikashindwa kuvumilia nikacheka yule kaka akanigeukia tukaaangaliana wote tukaanza kucheka teena [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom