Mambo ya kwa Babu LOLIONDO

Najaribu kuwaza,itakuwa vipi babu akisema hakuna kikombe mpaka lugha ya taifa ibadilishwe toka kiswahili na kuwa kinyakyusa?
 

Mkuu hapo kwenye red tukipaweka sawa unaweza kubadili mtazamo. Mathayo 7 : 16 inasema "mtawatambua kwa matunda yao" na si matendo. Matunda ni outcome. Sasa hebu pima matunda ya babu baada ya watu kubwia hicho kikombe. Kuna mabadiliko yoyote katika roho zao?

Zamani Mungu alikuwa hekaluni katika sanduku la agano. Na waisraeli iliwapasa kwenda huko kwa ajili ya kuomba toba. Lakini tangu kufa kwa Yesu Kristu na pazia kupasuka, Mungu hakai katika majengo achia mbali kwenye kikombe cha babu, bali anakaa mioyoni mwa watu waaminio. Iweje basi pale mimi ninapoamini nisiweze kutengeneza hiyo dawa na kunywa na kyponywa mpaka niende Yerusalem (kwa babu) tena anichotee mwenyewe (kama kuhani mkuu alivyofanya kwa ajili ya dhambi za wengine). Tena basi hilo neno analodai babu linaponywa halimo ndani ya dawa hiyo kwa vile mpaka babu akuchotee mwenyewe ndipo upokee uponyaji. hiyo nguvu ya uponyaji iko mkononi mwa babu.

My bible is my yard stick.
 
Uislamu upo wazi hauna löngolongo umekamilika na walishasema BABU "NO". Tatizo ukiristo haujakamilika ndo maana babu kajitokeza kila mtu anaongea lwake leo kakobe, kesho pengo mara upako hakuna dira kabisa.

Tofauti na ukristo uislam una-reinforce statements zake kwa jambia.
 
Na kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe mbele za mungu sku hiyo inakuja!!! kama huamini kaa kimyaaa! Mungu anatenda
 
.
Hapo itakuwa nami nitamimina Roho wangu, watoto wenu wake kwa waume watatabiri, wazee wenu wataota ndoto na vijana wenu wataona maono.
Miss Jude, hili ni Neno la Mungu? Au labda kutakuwa na uchakachuaji?
.

1Yohana 4:1-3,15 "Wapenzi msiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, ya kwamba zimetokana na Mungu kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.
 
Mimi sipo hapa kumtetea babu wala Mungu wa babu. Ninachofahamu mimi ni kwamba Mungu hahitaji wanadamu wamtetee bali hujitetea mwenyewe. Pamoja na hoja nyingi ambazo zimeshatolewa na watu kuhusu kile kinachoendelea kwa babu, tena kuna wengine wamezungumza wakijibu maswali yote yaliyoinuka kuihusu tiba ya babu kwa hoja zilizoenda shule, bado wengine wanainuka na kuanzisha tread za kuuliza yale yale ambayo yashajibiwa. Nimefikia mahali pa kujishuku kwamba huenda sisi wana Jf, kiwango chetu cha ukichaa kiko juu.
Nasema hivyo kwa sababu ikiwa mtu anauliza maswali hapa jamvini na anamtaka babu ajibu hoja zake kibiblia kama kweli katumwa na Mungu. Hivi ni kweli huyu mtu anaamini kwamba babu anamda wa kufungua jf, ili ajibu hoja zake? Kwa jinsi babu alivyotingwa na kazi yake huanza kutoa tiba 06 hrs to 21hrs kabla ya kulala?
Ninachoona cha wale wote wanaompinga babu hawajawa na hoja za nguvu kwa upande wa imani. Maana hata ukirudi nyuma hakuna yeyote katika manabii wa Mungu aliwahi kukubalika na watu wa wakati wake. Hata yesu mwenyewe walimtuhumu kwamba alikuwa akiwaponya watu kwa nguvu za belzebuli. Na nashindwa kupata jibu ni kwa nini watu hasa wale wa kidini wanampa shetani mamlaka kubwa kuliko Muumba ambaye ni mmiliki wa viumbe vyote. Sasa waulize hawa wanaomtilia shaka babu na kutaka wale waliokunywa dawa wathibitishwe na daktari, sikatai jambo hilo ila wasiwasi wangu mimi kwa hawa watu kama wanae mtu hata mmoja aliyakuwa mgonjwa na baada ya kumwombea akapona na doctor akawapa ushahidi wa uthibitisho wa uponyaji. Sana sana watakuambia tulikemea pepo likatoka na hivyo daktari hawezi kuthibitisha pepo.
Mleta hoja pia anapotosha maandiko ili kukidhi matakwa yake anaposoma matay 24:24 na kueleza kwamba nabii wa uongo watadanganya hata wateule. Kinachomaanishwa kwenye huu mstari ni kwamba mteule hadanganyiki!! Mstari unasema watawadanganya yamkini hata wateule. Hiyo YAMKINI inasimama ikiwa na maana kama INGELIWEZEKANA wateule wangedanganyika. Sasa yamaanisha hawadanganyiki.
Kuhusu huduma kutolewa bure kile kiasi mgonjwa anachotoa pale kwa babu ni kama sadaka tu. Ndodi anatibu sukari kwa sh. 3m.
Tusijipotoshe wenyewe lazima tuwaze nje ya box, Yuda msaliti tunaambiwa alikuwa mweka hazina, hizo pesa alizokuwa akiweka kuna biashara gani mitume waliokuwa wakiifanya?
Kila jambo liwe. kwa jina la Yesu haina maana zaidi kilitamka jina mdomoni zaidi ya kuliishi yaani maisha yaliyomkiri Yesu na matendo yako popote watu humshuhudia Yesu ndani mwako.
 
Naamini kabisa ile tiba ya Babu wa Loliondo ni Damu ya Yesu. Period!

Kwanini?

Kwa sababu,
1. Ukinywa tu kazi inaanza papo hapo kuanzia pale kichwani kwenye ubongo hukoo puani kwenye macho sijui kushuka hadi kifuani na kwenda sehemu zingine za mwili hadi kwenye unyayo!

2. Ule mitishamba ukitengeneza wewe mwenyewe ni sumu inayoweza kuua, lkn kwa tiba ile ya Babu ni salama maana imeguzwa na kuwa Damu ya Yesu kabisa na mtu akiinywa hadhuriki hata kidogo.

Damu ya Yesu idumu Milele na Milele. Amen.
 

.
Nimefurahi kwa jibu lako na hasa kwenye eneo la "TABIA" naamini sana katika tabia. Tabia hunena makuu kuliko matendo au maneno. Tabia haitengenezwi bila mateso, na tabia ni ushindi sio kipawa.
Ukiona nguvu yoyote katika utendaji bila tabia ni ya kwa shetani. Ila nguvu na tabia vyafaa kutawala kama Bwana wetu Yesu alivyoshinda na kuketi katika kiti cha enzi cha baba.
Miss judi, je unao ushahidi wa utumishi wa mchungaji wa liliondo kwamba aliwahi kuanguka alipojaribiwa katika huduma yake, ili iwe kwamba ni mtu asiye na tabia ya utauwa(kiungu)?
.
 
Mkuu umetibiwa ugonjwa gani ukapona?maana ile si kinga!tujuze after check up hospital
 
Angeimwaga tu, angeshangaa wote wanasepa!
 
duuuuu inaonekna umesha pata kikombe mkubwa unavyo piga promo mpaka tuna ogopa>>>>>>>>>>>>>>.
 
nice joke but amwage dawa ipi? Kuna aina ngapi za dozi pale?

Good reasoning, halafu ingemsaidia nn kugawa foleni wakati wagonjwa wote angewatibu yeye mwenyewe, the joke is note well constructed namshauri mtunzi ai edit kisha atutumie hiyo edited version.
 
jamani nyoka si ni mdudu mbaya na mungu aliweka adui kati yake na mwanadamu lakini mnakumbuka mungu aliwambia watu tazameni ile nyoka ya shaba nanyi amtakufa na ikawa hivyo mdudu ambaye ni adui kwa wanadamu akageuka kuwa tiba basi tuamini dawa ya babu ni uponyaji tosha toka kwa yesu kwa sababu kageuza sumu kuwa tiba
 
du nimemkubali babu hiyo katoa kali ya mwaka kwani kila mtu aenda adai ana kisukari heko babu:angry:
 
Mkuu inaelekea ulikipokea kikombe ukiwa katika hali ya fulu kujiachia.
Heri wewe uliyeamini hata maradhi yako yakakuacha, kuliko wale wataalamu wa mashaka na kuhoji.
Hata Yesu angelikuwepo wakati wetu huu katika mwili wangehoji juu ya mamlaka yake, wakitaka kujua ni kwa nini amemfufua lazaro kutoka wafu huku akiacha kufanya hivyo pia kwa baba yake wa kufikia Yusufu?
Hawataki kujisalimisha katika mawazo ya Mungu bali wanamlazimisha ajisalimishe katika mawazo yao.
Kamwe haitakaa iwe hivyo banaa!!!
.
 
Hii lazima ucheke hata kama umenuna! Sasa Ilikuwaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…