Mamlaka zijitahidi kuzuia wananchi wasigeuke kuwa " Wananchi wenye hasira Kali"

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
Salaam, Shalom!!

Mahusiano ya Dola na wananchi yanatakiwa kuwa sawa na mahusiano ya kipofu na Mwizi anayekula Kwa kificho na kipofu, Si vyema kukosea na kumshika mkono akastuka.

Watu wanapotea na kutekwa hadharani viongozi kimya, unyanyasaji Kwa wasio HAKI sasa haujifichi, wananchi wanachokozwa hapo.

Sasa wananchi wamefika hatua ya kutafuta namna ya kujilinda wao wenyewe ilhali KAZI ya Serikali ni kuuhakikishia umma ulinzi.

Wananchi wanapoungana Kwa nguvu ya asili Kwa hasira na visasi huitwa " Wana chi wenye hasira Kali". Hawa hawazuiliki.

Sijawahi ona au kusikia popote Duniani wananchi wenye hasira Kali wakipelekwa court, ni kama vile wao wakishahukumu inatosha. Nadhani ndio Hasa Nia ya kuzuia mikusanyiko isiyo na kibali Cha polisi Ili kuwazuia watu Hawa wasigeuke kuwa " wananchi wenye hasira Kali".

Angalizo: Wananchi wasichokozwe, HAKI itendeke Kwa wote, wasijepandwa na hasira Kisha kugeuka kuwa " Wananchi wenye hasira Kali ".

Ubarikiwe Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿.
 
Wewe waache waote mapembe ya Kiburi cha mamlaka waje waone hasira za wafu zitakavyowanyeshea. Ikifikia hatua hiyo hakuna cha jeshi wala polisi wala usalama wa Taifa wa kuwasaidia.
Ni kama vile viongozi wamepigwa upofu wasione hatari iliyoko mbele yetu.

Ubarikiwe sana Mzee Warioba.
 
Hii kwa sasa ni kama sikio la kufa.......
 
Njia sahihi ni kuanza kupigania na kupata uhuru upya. 1. Kudai uwepo wa Tanganyika iwe ndani au nje ya Muungano. 2 kuandika Katiba mpya au kuhuisha Katiba ya Warioba. 3. Kufanya kura ya maamuzi kuhusu uwepo au kutokuwepo Muungano kabla kuingia kwenye Federation ya Africa Mashariki. 4. Kuweka Tume huru ya uchaguzi itakayohusika na michakato ya kupata viongozi wa nchi, wabunge na wakuu wa Idara wizara na makampuni.
 
Kweli kabisa.

Suluhu ni kupata

"Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote "
 
Sikiliza Mkuu. Unapokuwa na mti wa matunda yenye sumu nyumbani kwako ambapo watoto wanaweza kula na kufa, dawa sio kusema wazazi waangalie watoto wasile matunda haya yana sumu. Suluhisho lipo katika kuuondoa mti wenye sumu.

Sasa kama serikali haitaki kuondoa mti wenye sumu, tufanyeje? Wapigwe tu wafe.
 
Usihofu hao waliokamatwa tegeta watatolewa mfano ambaye kila anaependa kula ugali mtaani atajifunza kwa kuona.

Nakwambia watachofanywa hao jamaa hakuna mtu atashambulia mtumishi wa serikali tena.
 
Wapigwe wafe kina nani?

Hawa polisi, wafanya KAZI TRA, serikalini, USALAMA, viongozi nk nk ni ndugu zetu pia, ni Watanzania.

Tunahitaji kuhakikisha Damu isiyo na hatia ya mtz yeyote haimwagiki.
 
Reactions: Ame
Dhuluma na uovu vikizidi hofu ya kifo huondoka na watu wanaamua kutumia njia yoyote ile katika kudai au kupigania haki zao.
 
Muliro anajaribu kutisha wananchi ,kama hao wahuni wakija bila kufuata procedures wataitiwa watekaji tu...Haiwezekani Land Crusier ije kunipiga block halafu kizembe tu nisarende nope lazima nipige yowe la WATEKAJI.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…