Mandela halisi aliuwawa na makaburu huyu ni feki

Mandela halisi aliuwawa na makaburu huyu ni feki

Inavyosemekana katika mitaa ya weusi waliokata tamaa pale SA, wanaamini mandela halisi alishafia jela (walimuua kwa siri) na makaburu wakatafuta mtu aliye shabihiana naye waka mtrain kwa kipindi kirefu kumwakilisha mandela halisi! wanachodai ni. ...pointi kubwa juu ya dai hili ni 1/.kuwa kunatofauti kubwa ya kifalsafa kati ya mandela aliyeingia gerezani na mandela aliyetoka gerezani. 2/.Mandela aliyetoka gerezani alifika kijijini kwao mara chache sana, ila hakuweza kupaform baadhi ya ceremonial rituals. 3/. Hakuweza kukutana kimwili na mke wake winnie ambaye angeweza kugundua tofauti za mwilini, na mazingira yalishaandaliwa yaliyopelekea kuvunjika kwa uhusiano huo! 4/ mateso ya jela za makaburu hasa kwa wapigania uhuru kama mandela na Salomon malhangu, ni vigumu kutoka jela na kuwa na afya na uwezo wakuishi na kufikia umri aliofikia 'mzee madiba'! wengi waliuwawa jela 5/. ANC ya mandela aliyetoka gerezani haikuwa na mwelekeo wa ukombozi wa weusi .............

acha kuwapotosha watu angalia kwenye red hapo


attachment.php
 
...mmmh!...maneno iko mingi saaana...hivi kumbe mtu unayemwona kuna uwezekano mkubwa akawa sio yule unayemtazama!!??...
 
Nitakuwa mtu wa mwisho kuamini habari kama hii....

Huwa kinachonisikitisha ni jinsi ambavyo Mandela na Winie walishindwa kuishi pamoja kwa raha na amani baada ya kupambana pamoja....

Mambo mengine tuyaache yalivyo kwani ukiamua kufuata maneno ya mitaani hata mzazi wako mwenyewe unaweza kumkana!!

Ndugu yanguwe,wanaume ni wale wale hata kama ni Mandela! Kama Winnie ndiye angekuwa mfungwa Huyo babu angemsubiri? si angeoa kabisa! si afadhari Winnie alikuwa anaiba, kitu kinachofanywa hata na watu walio kwenye ndoa hai bila mtu hata kuwa safari.
Kama alijua kusamehe na ku reconcile alishindwa nini hapo? basi tu kamba hukatikia pabovu, alikuwa anatafuta sababu ya kumwoa Graca.

Nani ana bisha???
 
Kama watu wanabadilisha jinsia ya uume kua ya kike ije iwe sauti upo dunia ya 7 nini
 
Umenikumbusha Landlord wangu wa zamani Anaitwa Konkod baharia mstaafu hapo maeneo ya kijitonyama karibu na Grand Villa hotel alikuwa na tabia ukiwa unalipa kodi anataka na namba za mke/mume kama hujaoa Gf/Bf wako aziandike kwenye diary ni lazima! Sasa ikitokea siku umefanya Double allocation lazima atengeneze bomu anampigie jamaa aje la sivyo umnunulie pombe!pombe yenyewe anamix Penaso na Banana basi analewa siku 3 kikweli he was fun!
Aliuza nyumba akahamia mwananyamala akawa na wapangaji kama 7 hivi mmojawapo Ben kinyaiya alikuja pewa notice kisa eti mtoto wake wa kiume ameanza kupaka carolite anamuiga Beny hivyo sio role model mzuri kwa mwanae.
Wenye nyumba wana hilaa.
 
Acha hiyo maneno mbovumbovu
Miaka yote leo ndiyo wanasema haya ?

Acha upandikizi wako Mkuu mleta mada.

Mtu akifariki ndo mambo yake mengi ya siri hujulikana alichoandika huyu jamaa kinaweza kikawa kweli haswa hili suala la kutokulala na Winnie baada ya kutoka gerezani. Lakini tusisahau kuwa kadri umri wa binadamu unavyoongezeka ndo busara huwa kubwa, labda yule arrogant Mandela wa 1962 alibadilika baada ya kifungo kirefu na umri kuwa mkubwa. Hata hapa Tanzania Nyerere yule wa miaka ya 1960s ukisikiliza hotuba zake na ushauri na misimamo yake ni tofauti na yule wa miaka ya 1990s
 
Mkuu SLAA ANAWEZA naona leo umeamua kuja na mada yenye akili, vipi hapo mbozi wazima?

Back to topic:
Nakuunga mkono kwa 100% kuwa huyu ni Mandela feki na si yule tuliyemfahamu hapo mwanzo kupitia maandishi na vitabu vya kihistoria.

Mandela ulimjulia wapi wewe mkaazi wa Mbwinde,Punguzeni porojo zenu za vilingeni!
 
Ndugu yanguwe,wanaume ni wale wale hata kama ni Mandela! Kama Winnie ndiye angekuwa mfungwa Huyo babu angemsubiri? si angeoa kabisa! si afadhari Winnie alikuwa anaiba, kitu kinachofanywa hata na watu walio kwenye ndoa hai bila mtu hata kuwa safari.
Kama alijua kusamehe na ku reconcile alishindwa nini hapo? basi tu kamba hukatikia pabovu, alikuwa anatafuta sababu ya kumwoa Graca.

Nani ana bisha???

Sina proof ya kuuunga mkono au kukupinga kati ya hayo uliyoyasema; siyo kuhusu wanaume kwa ujumla wao bali kuhusu Mzee Madiba...

Ila ninalojua kuwa reunion ya couples ambazo zimetenganishwa kwa muda mrefu ni jambo gumu sana. Ni mtihani wa aina yake!

Hata hivyo, mimi nasikitika kwa sababu ninegefurahi kama wangeweza kuishi pamoja kwani walipambana pamoja.

Mambo ya kuibiana sitaki kuyaongelea kwa sasa, kwani hawa jamaa walipitia maisha magumu sana!

Babu DC!!
 

hiyo makitu nilikunywa siku moja nilivobadili daladala ya tabata kwenda ya feri sikuwa najuwa; nilivoshuka feri sikuwa najuwa, nilivoingia kwenye pantoni sikuwa najuwa. nilijitambuwa baada ya kufika kigambonino baada ya kupigwa na upepo wa bahari.
 
acha kuwapotosha watu angalia kwenye red hapo


attachment.php

Pia nasikia alikuwa na alama kwenye mguu alipoumizwa wakati wanacheza na wenzake mchezo wa kuchapana fimbo...

Hizi hadithi nyingine hata huwezi kujua kama zinatungwa na binadamu...
 
...mmmh!...maneno iko mingi sana...hivi kumbe mtu unaemwona kuna uwezekano mkubwa akawa sio yule unayemtazama au kumwangalia!?...hapa inabidi kutafuta tofauti ya mbili mara mbili na mbili jumlisha na mbili,ukipata jibu itakuwia raisi kujua nini kilitangulia kati kuku na yai...

wewe sasa ndio umenichanganya kabisa ... yani baada ya kufuata misemo yako hapo juu nimejikuta sasa hata huyo aliyefungwa sio mwenyewe.

Bora nisichukue lolote toka kwy uzi huu nibakie na kile nilichokikuta toka kwy historia.
 
Maneno ya mtaani ndo chimbuko la facts ijapo siwezi kuyaamini haya ila kila kitu kinawezekana na hata hizi sifa za wazungu kwa Mandera kimsingi zinaniacha inspired kutaka kujua zaidi

Ipo siku ukweli utadhihiri wenyewe.
 
Back
Top Bottom