Mange Kimambi amuomba wakili Albert Msando akamtoe Wema Sepetu

Mange Kimambi amuomba wakili Albert Msando akamtoe Wema Sepetu

Hivi kutumia madawa ya kulevya ni makosa kisheria?
Na kama anasemekana anauza amekutwa na uthibisho?
Mtu anaitwa kuhojiwa kwa tuhuma za kutumia madawa ya kulevya? Like serious?

Hata wale madon wa unga huwezi kuwaita kuwahoji kisha ukawatia hatiani bila uthibitisho.

Makonda hajui anachokifanya
Period
Kukutwa na uthibitisho ni jambo lingine,hata hivyo makonda hawapeleki mahakamani, hao wanaitwa ili kuhojiwa, katika mahojiano hao watatoa leads za kama wao wanahusika au wanaweza help kujua wahusika, nadhani Mr makonda anafanya kazi nzuri kama mwenyekiti ya kamati ya usalama(m), kumbuka hiyo sio Kesi bado!
 
Soma sheria uelewe, polisi wanaweza kukuita na kukuhoji kwa chochote wanachohisi umekwenda kinyume na sheria na ni wajibu wako kutoa maelezo na hata kama huna hatia bado unawajibika kutoa maelezo.
Kuhojiwa sio hukumu na unaweza kuachiwa watakapojiridhisha kwamba sio mhusika na hawawajibiki kukulipa chochote.
Suala hapa ni kuwaachia polisi wahoji na kujiridhisha kama ni kweli wanahusika na kuuza au kutumia unga.

Biashara ya unga huwa inafanyika kwa siri sana mimi na wewe hatuwezi kusema kwamba Wema anahusika au hausiki.
Tusihoji kwa kuwa tunamapenzi na wema bali tusubili nini kitaendelea baada ya kuhojiwa.
Mange Kimambi yuko US hajui maisha ya kila siku ya watu huku ameandika kwa mapenzi yake kwa Wema
Waambie hao...
 
aiseee IDX ni nooomaaa...wanakuchunguza for ten yrs mpk wanapata ushahidi!!
Kumbe na wewe ni mfuatiliaji. Uwa nikitazama idx nawaza watu wengi tz watakuwa wanafungwa kimakosa ama kuna watu wengine wanauawa lakini wauaji wapo wanadunda.
mfano tajiri mke wake akikutwa kafa ndani siyo rahisi polisi kumchunguza mume wakati wao wanakwanbia first suspect ni partner wa marehemu akifa mtu aliye katika mahusiano
 
MIJITU inamtetea wema utadhani wanamjua kmbe wanamuona insta
Wewe nae naimani utulize akili
1. Utamuitaje binadamu mwenzio "mijitu"
2. Tunachozungumza ni busara ya kiongozi, ni vizuri kuweka issue public kwanza kabla ya kuhukumu
3. Ajifunze asikurupuke, criminal case sio suala la kukurupuka kwani ukimuharibia mtu sifa akikugeuka utalipia hadi senti ya mwisho.
4 . kumbe hata wewe unaita watu mijitu kaa chonjo.
 
Alichosema makonda ni wanasemekana na haijathibitika so ni haki yake kuwakata ili kuwahoj nankupata ukwel akiwa kama mwenyekit wa kamat ya ulinz na usalama

Ni tuhuma tu
Kuhoji ni sawa ila kuendeleA kuwashikilia pasi ushahidi ni dhulma
Mange kimambi" mkuu wananchi tunaomba uchukue kesi ya Wema probono.
Tena sio kumtoa ndani tu, tunaomba umfunze Makonda adabu by during him and the city for defamation wamlipe Wema mabilioni kama Yale Togo waliambiwa walipe....

Please please Albert tunaomba, Wema kutoka ndani sio solution kabisa, wameshamwalibia maisha yake, hawezi kufanya Kazi na kampuni yoyote ile kubwa,

Please please tunakuomba au kama vipi tujichange tukulipe".
Hadi sasa wasanii walioitwa kuhojiwa bado wanashikiliwa na jeshi la polisi
 
Alichosema makonda ni wanasemekana na haijathibitika so ni haki yake kuwakata ili kuwahoj nankupata ukwel akiwa kama mwenyekit wa kamat ya ulinz na usalama

Ni tuhuma tu

Makonda yupo sahihi.
Kwaninni kosa kuhoji mtu?Hata wewe unaweza fananishwa na gaidi,ukawekwa ndani ukikutwa si wewe unaachiwa!

Kesi ya kudai fidia kwa malice prosecution ina ingridients zake,kwanza lazma kesi iishe,iwe upande wako hiyo hukumu,etc!

Makonda piga kazi wacha kelele za chura zilie,jiwe limempata mtu gizani.

Yani Eti msanii anatoa wimbo mmoja,nahamia Mbezi,anaendesha Prado,anafanya shopping Dubai na Uturuki,anafanya Besdei ya Milioni 10 na kushoneshea mashosti nguo za party,hapana,Hii ni dharau kwa JPM na Makonda ambaye ni rais wa Dar es salaam!
 
Hakuna mtz mwenye akili isipokuwa sisi wachache, kila MTU lazima aisome namba, muda Wa kula bata walikula, wanadhani hakunaga msotoo?!,
 
Sula la hili liko kisiasa zaidi nawatu kujipatia umaarufu wa kisiasa mwisho wa siku mtanambia
 
Polisi na intelijensia ya Tz inavyofanya kazi inaniacha hoi.
Sijui kwakuwa niko addicted na IDx kwa kuona wenzetu wanavyofanya kazi.
Wenzetu hawawezi kumhold mtu kama hawana ushahidi wa uhakika uwe wa kimazingira au vithibitisho juu ya kosa analotuhumiwa.
Atahojiwa kama hawana hivyo vitu watamuacha waendelee kumpeleleza taratibu.
Wenzetu mtu kuitwa polisi akahojiwe ni hiari kwenda ama kutokwenda na akifika anaweza akatae kujibu chochote mpaka awepo mwanasheria wake.
Akigoma kwenda basi watatafuta sababu ya kumkamata mfano avunje sheria ya barabara akamatwe apelekwe polisi hapo watamhoji juu ya mahojiano pia ya kosa wanalohisi katenda awali kama hawana ushahidi.
Makonda anachofanya kiko sawa ila ninahisi kuna haki za watu/watuhumiwa hazizingatiwi yani sheria inawekwa pembeni mtu anafanya anavyohisi mwenyewe
Usizoee vya kuiga kwa 'wenzetu', hao unaoita wenzako hawako level sawa na wewe, jitahidi kuona wewe na uhalisia Wa maisha ya tz,sio story za kucompare, unawezaje kulinganisha vitu hiviii?!!!!,
 
Hivi kutumia madawa ya kulevya ni makosa kisheria?
Na kama anasemekana anauza amekutwa na uthibisho?
Mtu anaitwa kuhojiwa kwa tuhuma za kutumia madawa ya kulevya? Like serious?

Hata wale madon wa unga huwezi kuwaita kuwahoji kisha ukawatia hatiani bila uthibitisho.

Makonda hajui anachokifanya
Period
Kwani Wema ameshitakiwa au ameshutumiwa? Ifike mahala tutofautishe hivi vitu. Alaf kwani walitakiwa wahojiwe wapi ili ionekane ni sahihi? Club, hotel au majumbani kwao?
 
Usizoee vya kuiga kwa 'wenzetu', hao unaoita wenzako hawako level sawa na wewe, jitahidi kuona wewe na uhalisia Wa maisha ya tz,sio story za kucompare, unawezaje kulinganisha vitu hiviii?!!!!,
Nachoongelea hapa ni mbinu na weledi wa kufanya upelelezi bila kutumia nguvu.
Nitakupa mfano mmoja.
Kuna mdada mumewe alipotea tu from no where na yeye ndiye alitoa taarifa polisi.
baada ya kuwa na suspects wengi sana lakini hakuna hata mmoja aliyeonekana kuwa na clue iliyowasaidia kujua kilichompata yule mme wa huyo dada.
ikabidi waanze kumchunguza yule dada. Walikuwa wanamuita na kumhoji mara kadhaa then wanamuacha sababu alikuwa suspect ila hawakuwa na ushahidi. So wakaanza fuatilia nyendo zake wakagundua toka mmewe apotee anapenda kwenda sehemu flan km kama tatu toka nyumbani kwake kwenye shamba la farasi Na ameshaenda huko mara tatu.
Ikabidi waende wakakuta hakuna dalili yoyote mbaya mle ndani kulikuwa na big pond wakamfuata kumuuliza kinachompeleka kule akawambia kuwa lile shamba la rafiki wa familia yao na uwa wanaruhusiwa kuingia so uwa anaenda relax ana mawazo juu ya mmewe.
polisi bado walikuwa na mashaka wakamuacha, kesho yake polis mmoja akamfuata kazini yule dada akamwambia tumeamua kutafta kama labda mwili wa marehemu umetupwa majini tunataka pia tuka search ile pond unakoendaga.
lengo alitaka kuona reaction yake dada alipanic gafla akamwambia nna kazi tutaongea baadae akaondoka hiyo ilikuwa green light kwa polis.
kumbe dada alipotoka pale akakimbia kuelekea kule kuhamisha mwili na polis nao wakamfuatilia anataka kuingia wako anawaona akagairi akarudi home wao wakaleta team wakasearch pond wakapata mwili the next thing mwenyewe aliconfess.
nachojaribu kukuonyesha ni kwamba japo walimsuspect lakini hawakutumia nguvu bali akili na yeye mwenyewe aliyewaongoza kuwapeleka kwenye ushahidi may be wangemhold angegoma kusema maana hawakuwa na ushahidi juu yake.
sasa naongelea technics za polisi wetu
 
Acheni ushabiki usio na maana, mnashabikia wasanii mkifikiri wao ni malaika hawawezi fanya makosa, hamjui kuwa wengine huwa wanatumia kivuli cha umaarufu kufanya mambo maovu. kama kweli mna huruma mbona hamna hata mmoja anaye zungumzia askari walio tajwa kujiusisha na ngada mmebaki kuzungumzia wasanii heti wamechafuliwa majina askari walio simamishwa kazi hamuwaoni mnawaona tu wakina wema. acheni kufanya mambo kwa ushabiki.
 
Back
Top Bottom