Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Mh Raisi mama Samia anasema takukuru waangalie Kama kuna kesi za kubumba bumba wasizipeleke mahakamani

Zinaichafua serekali hongera mama kwa kutambua"wanyonge walikuwa Wana nyongwa kweli"

Kesi nyingi ni zao la kujipendekeza so dhani hata Kama hayati alikuwa anafurahia
Kwa hiyo maneno y kigogo mnayaleta huku kutuchambulia siasa!? [emoji848]
 
Mishahara duni, vyeo havipandi.

Mkiajiliwa na mikopo yenu hiyo si mtaishia kazini siku ya kuripot tu
Bora ajira zitolewe,kuliko kua nje ya ajira.
Atoe ajira na kabla ya kutoa,TAMISEMI waangaliwe,wamefanya hovyo kwenye ajira zilizopita za walimu.Haiwezekani uajiri waliomaliza 2018 ukawaacha wa 2015,2016,2017 na wote wana sifa zilezile,siyo fair.
 
Yaani Meko ameacha upuuzi ktk mfumo wa Ajira. Badala ya ku ajiri yeye anafanya internal TRANSFERS
 
Mh Raisi mama Samia anasema takukuru waangalie Kama kuna kesi za kubumba bumba wasizipeleke mahakamani

Zinaichafua serekali hongera mama kwa kutambua"wanyonge walikuwa Wana nyongwa kweli"

Kesi nyingi ni zao la kujipendekeza so dhani hata Kama hayati alikuwa anafurahia
Kuna yule alikuwa Mtendaji Mkuu wa RAHCO, Benhadard Tito. Yuko lupango kwa mwaka karibia tano sasa.
KOSA?
Alimpa ukweli Magufuli juu ya reli ya majaribio iliyoasisiwa na Kikwete na Samwel Sitta.

Seth na Rugemalila,
Wengi tu ambao kesi hazina mbele wala nyuma.
 
Mheshimiwa rais,

Vijana tuliohitimu vyuo toka mwaka 2015 tuna hali ngumu sana mtaani.

Hima,tunaomba utuangalie(sana) sisi vijana tuliohitimu vyuo toka mwaka 2015 kwani tunateseka katika nchi yetu wenyewe.

Kumbuka tumeandaliwa katika mazingira ya kutegemea kuajiriwa.
Lakini toka mwaka 2015 tumewekwa kando kwa sababu lukuki zikiwemo;
UHAKIKI WA WATUMISHI,KUJENGA MIUNDOMBINU KWANZA na KUUNDA UPYA MFUMO WA AJIRA.

Sasa mama,tunaomba katika utawala wako utupe jicho la kulia.
Halafu pia uone kama ni watoto wako hawa wanaohangaika.

Mungu amekuweka wewe kwenye urais kwa makusudi mengi likiwemo hili suala la ajira.

Basi tunaomba uteekeleze mipango ya Mungu.


NB: Ukimaliza hili,fumuafumua kitu kiitwacho "HESLB".Ni chukizo.
Hivi nyinyi hamuelewi selikali haina hela, subirini kidogo tungeneze mambo yakae sawa
 
Mh Raisi mama Samia anasema takukuru waangalie Kama kuna kesi za kubumba bumba wasizipeleke mahakamani

Zinaichafua serekali hongera mama kwa kutambua"wanyonge walikuwa Wana nyongwa kweli"

Kesi nyingi ni zao la kujipendekeza so dhani hata Kama hayati alikuwa anafurahia
Mungu anijalie afya njema
 
Mh Raisi mama Samia anasema takukuru waangalie Kama kuna kesi za kubumba bumba wasizipeleke mahakamani

Zinaichafua serekali hongera mama kwa kutambua"wanyonge walikuwa Wana nyongwa kweli"

Kesi nyingi ni zao la kujipendekeza so dhani hata Kama hayati alikuwa anafurahia
HAKI HUINUA TAIFA

Asante sana Mh Raisi Mama Samia Suluhu Hassan.

Tunakuombea. Endelea hivihivi. Mungu akubariki.
 
Kwa muda sasa, udhibiti wa mada hapa JF umekuwa ukiongezaka kupita kiasi na kuondoa kabisa maana ya slogan inayotumiwa na huu mtandao( inafahamika kwa member humu).

Inafika hatua mtu unaandika mada huku unajiuliza hii mada itabaki au itafutwa. Tumefika hatua mbaya.

Sasa leo nimelata mada ya kuwashauri Mama Samia ateua IGP,CDF na Boss wa TISS kutoka Zanzibar eti nayo imeondolewa. This is too much!
Ushauri wako ni fyongo. Ni uchochezi. Hauna mantiki. Wamefanya vizuri kuuondoa. Wako sahihi.
 
Nimependa Rais wetu mpya kupunguza ushabiki kwenye mambo, kuhimiza uwazi zaidi wa report za matumizi, kujali zaidi mifumo.

Mfano Rais kujua kuwa mifumo sita tofauti ya ukusanyaji wa kodi ni njia mbaya tunatakiwa kuwa na mfumo mmoja ni wazo zuri na inaonyesha uzoefu wake wa kufanya kazi mashirika makubwa ya kimataifa na kuwa na mifumo imara.
Naona mawaziri wanaogopa maana hakuna ushabiki
 

Attachments

  • IMG_3582.MP4
    1.1 MB
Wapo wanaouliza kama Mama Samia ataweza ?, Mimi nauliza nini kipimo cha kuweza?

Kwa mtazamo wangu huenda mengi aliyofanya mtangulizi wake ningeweza kusema aliweza kama angekuwa mtendaji (Waziri Mkuu) lakini alifeli kama Rais...

Kwahio Je akiendelea kubana uhuru wa habari, kutoipa fursa separation of power ifanye kazi, kuanzisha miradi bila upembuzi yakinifu na kuwashirikisha wadau, kufanya kazi zote peke yake..., kutofuata mifumo na kuwaacha wachuuzi kila mahali kwa kisingizio ni wanyonge na ni wapiga kura.., Je atakuwa ameweza ?

Kwangu mimi kipimo cha kuweza ni kuwaunganisha watanzania wote, kufuata sheria na haki (kama kuna sheria mbovu ifutwe/ibadilishwe) kuchagua watendaji wazuri na kuwaacha wafanye kazi na kusikiliza ushauri na maoni ya wadau..., kuacha taasisi zifanye kazi zao na sio baadhi ya watu..., kuwa Rais wa Watanzania na sio wa Chama...

Tofauti na hapo anaweza kuonekana ameweza kwa jicho la Propaganda ila kwa kazi ya Urais inavyotaka akawa amefeli...
 
Mh. Rais aunde timu (think-tank) mahsusi ya wataalam watakaomsadia katika sekta zote kubwa nchini kubwa zaidi CAGs wote wastaafu wawepo kwenye timu. Itasaidia sana yeye kama ovwrseer wa nchi kupata kuwa proactive na kuwa na mielekeo mizuri ya ki-nchi nyakati zote.
 
Mabadiliko ni lazima ili kazi nzuri ifanyike. Mbona tokea uchaguliwe mheshimiwa hatujaona mabadiliko yeyote makubwa ya cabinet yako? Kiongozi yeyote anahitaji upinzani wa ideas, lakini sio upinzani wa vitendo. Manake watu wanaokataa kutekeleza agenda iliyoamuliwa na wote, wanastahili kupigwa chini. Lakini kama mtu ana wazo zuri zaidi la kutekeleza jambo ni lazima asikilizwe.

Kuna watu wanaompinga Mhe SS kivitendo tayari tena bila sababu yoyote ya msingi isipokuwa ni kutokana na kwamba yeye ni mwanamke. Kama mimi ningekuwa Mhe. SS, ningefuta watu kama hao wote na haijalishi kuwa ni mawaziri, wakuu wa mikoa au wakuu wa majeshi. Kama ni watu ambao hawana ideas nzuri zaidi na wana mipango ya kuvuruga uongozi wangu just because mimi ni mwanamke, wangetambua nguvu yangu ya kalamu kama Rais wa Jamhuri. Mheshimiwa SS, tunataka kuona uongozi imara, na tafadhali anza na hili. Hauhitaji Yes Men, lakini pia hauhitaji wavurugaji ambao hawana wazo wala neno ila wanakupinga tu sababu ya jinsia yako. Nasisitiza!!
 
yaaani vikirudi tu hivyo tutabak hapahapa kwa miaka 50 ijayo.nchi inaongozwa kisayans.ukiruhusu hayo unayoyatka itakua kazi kila siku majukwaaan na matumbo.we need kaz hapa kazi tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hayo yameruhusiwa kikatiba na ikatungwa sheria yake. Labda umshauri afute lakini chochote kilichopo kikatiba in sheria. Na kiongozi mzuri ni yule anaye zingatia katiba na sheria kama JPJM alivunja katiba hatakiwi kumwiga
 
Kwa heshima zote naomba uupokee ushauri huu ukiona ni vema. Ninajua kuna wasaidizi wako wengi humu mitandaoni esp babalao JF.

USHAURI: Uza ndege zote, pesa itakayoatikana anzisha kilimo cha umwagiliaji. (Biashara ya usafiri wa anga achia sekta binafsi, wawekee mazingira rafiki ya biashara kisha wewe (serikali) utakuwa ni mkusanyaji wa kodi. Katika hilo uboreshe viwanja vya ndege). Anzisha irrigation system schemes za uhakika. Tuanzishe plantations za mazao mbalimbali ambapo tutaweza kupata malighafi kwa ajili ya viwanda vyetu na tutauza mazao mengine nchi za nje kisha tutapata fedha za kigeni. Ardhi nzuri ya kutosha yenye rutuba tunayo, maji tunayo. Mungu ametujalia haya.

Duniani kote mapinduzi ya viwanda yalitokea baada ya mapinduzi ya kilimo. Kilimo na viwanda vitakuwa ni mwarobani wa tatizo la ukosefu wa ajira.

Usiogope kuona tofauti na mtangulizi wako. Sio dhambi kuona tofauti na aliyekutangulia.

Bila unafiki naomba kuwasilisha.


YESU NI BWANA NA MWOKOZI!
 
Back
Top Bottom