Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Awape posho walimu wote si wakuu wa shule tu kama ilivyoanza kufanyika sasa hivi analeta ubaguzi na chuki kwani wakuu hawana kazi zaidi ya kukaa ofisini, walimu wa kawaida ndio wanaofundisha morali ya walimu inashuka na matokeo yake yatakuwa mabaya
Hilo nalo Neno.kila mtumishi ni muhimu kuwa motivated kwa njia moja au nyingine.
 
Mimi nitamuomba aseme neno moja tuu
"Nimeguswa na tetemeko la ardhi Bukoba, Poleni! "
Na roho yangu itapona! .
Pasco
Kamanda,Neno ulilolitabiri limetoka kama mada yako ilivyosema unapokuwa mjeda wa akiba.
 
Ndugu wananchi, nimeyasikia na nitayafanyia kazi "naahidi sitowaangusha" 🙂
 
Poleni sana Wananyamongo kweli picha tu zinatoa ujumbe na nazikumbuka sana.

Wanaoratibu Ahadi za Mh RAIS Ujumbe wenu huo ktk kupanga Utekelezaji wake.

Wananyamongo wanawakumbusha Ahadi ya Mh Rais
 
Na Ahadi ni Deni lazima utimize
kipindi cha uchaguzi, zile nyimbo zilikuwa na maana sanaa, "mmeipenda wenyewe, chaguo lenu wenyewe....." nadhani hapo melody imekujia malizia mwenyewe

na hii "sisiem ni ile ile oooh ni ile ile" 🙂
 
Lugha ya staha plse jamani
 
AAche kusimanga wananchi na kuwatukana huku wakiwa na majonzi kama hawezi aachie ngazi hakulazimishwa aliomba mwenyewe
 
Urais ni cheo cha msimu miaka 5 au 10 co mingi huwezi jua ya kesho,ishi vizuri na watu,pia mchezo wa siasa hautaki hasira.
 
MH RAIS AKIKUPA NAFASI YA KUONGEA NAE LEO JAPO KWA DAKIKA MOJA TU,

JE UTAMWAMBIA NINI? PAMOJA NA...PONGEZI,USHAURI HATA MAOMBI n.k

Angalizo..maneno ya staha ni muhimu.
Nitamwambia aendelee na msimamo wake huo huo km hakuna shughuli za siasa hadi 2020, hakuna bunge kuonyeshwa "live", hakuna maandamano, hakuna kuhudhuria mikutano ya UN, AU, SADC na kadhalika maana ataokoa gharama nyingi. Kwa ufupi nitamwambia azidi kukaza bolt kila mahali ili fadha ya walipa kodi isipotee bure.
 
Ujumbe mzuri ktk kupiga hatua na kulisaidia Taifa.umefika kwa wahusika.thanks
 
1. Aangalie jinsi ya kukuza ajira kwa vijana kupitia bank ya kilimo. Mfano, badala ya bank kuendelea kuomba cashflow za mradi, dhamana nk wawe na utaratibu wa kusimamia miradi ya vijana wenye uhitaji wa mkopo kwa kuwapatia mtaalam wa fani husika kuanzia mwanzo wa mradi mpaka unasimama. Vile vile wawe na utaratibu wa kulipa fedha za mahitaji moja kwa moja kwa supplier au vibarua nk.....hapa bank itawezesha ajira kwa mwenye shamba na yule afisa mradi anaesimamia.
.2. Atoe muundo wa serikali
 
OMBI LANGU KWA MHESHIMIWA RAIS WETU DKT MAGUFULI KUHUSU MIKATABA MIBOVU YA MADINI.

Kwanza napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa Dkt John Pombe Magufuli kwa kazi nzito na kubwa ya kufumua mfumo aliokuta na kutengeneza mfumo mpya unaoendana na matakwa yetu wananchi ya muda mrefu. Mheshimiwa Rais amejitahidi sana kutumbua majipu na kuziba mirija ya ufujaji wa mali za umma,watu waliokuwa wanakwepa kodi katika awamu hii wamedhibitiwa kwelikweli, hilo ni jambo zuri sana kwani limepelekea mapato ya serikali kuongeza maradufu ukilinganisha na awamu zilizopita.Pamoja na kufunua mifumo mbalimbali na kukutana na uozo mbalimbali Raisi wetu hajasita kuchukua hatua ndio maana nampongeza kwa hilo.

Jambo la pili, Namuomba sana Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa Dkt John Pombe Magufuli sasa ajielekeze katika kufumua mikataba yote ya madini ambayo ilikwisha kusainiwa nyuma, kwani mikataba hiyo ni yakinyonyaji na imekuwa inalikosesha taifa letu mapato mengi sana.Nchi yetu imebarikiwa sana na Mwenyezi Mungu, haipendezi hata kidogo serikali kuendelea kuongeza kodi kwa wananchi wanyonge huku madini yetu yakiachwa vilevile. Katika bajeti iliyosomwa na serikali mwaka huu binafsi sijaona ongezeko la kodi katika sekta ya madini. Namuomba sana Mheshimiwa Rais wetu sasa anze kutumbua majipu yote yaliyopo katika madini yetu,kwani huku ndiko kuna ufisadi mkubwa sana na serikali yetu kupitia kwenye madini ndiko inakoibiwa sana. Ninapendekeza katika mikataba ya madini watanzania tunufaike kwa 60% huku wawekezaji wao wachukue 40% ya mapato yanayotokana na madini kwa mwezi nasio kama sasa ambapo sisi ni 4% tu ndio tunanufaika huku wawekezaji wao wakichukua 96%,ndio maana nasema hii mikataba ni yakinyonyaji sana.Haiwezekani kabsa madini ni yakwetu ila kwa sababu wao wawekezaji wanamitambo ya kisasa ya kuchimbia madini yetu ndio wachukue 96% huku sisi tukiachiwa 4% ya mapato yatokanayo na madini kwa mwezi. Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa Dkt John Pombe Magufuli, ninakuomba ufumue mikataba yote ya madini ili tuanze upya.. Kutokana na mikataba mibovu ndio maana sekta ya madini imekuwa inachangia mapato kwa kiasi kidogo sana ukilinganisha na sekta ya utalii ambayo ndio inaongoza kwa kuchangia pato kubwa la taifa kwa mwaka.

Mwisho, namuomba sana Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa Dkt John Pombe Magufuli asijekuogopa kwa hili la kufumua na kusuka upya mikataba yote ya madini kwani Watanzania wazalendo tuko nae bega kwa bega tunamuombea sana.

Mungu ibariki Tanzania.
Mungu mbariki Mheshimiwa Rais wetu Dkt Magufuli na viongozi wengine wa serikali pamoja na watanzania wote wapenda amani na maendeleo. Amen!!!.


Wako,
Abel Magembe Lugimba.
Mbunge wa Akiba-Jimbo la Kalambo,Rukwa (2020-2025).
 
Ninawasiwasi na waliostructure JD ya Rais wa Tz make vitu muhimu kama kuangalia mikataba mibovu ni kimya tu
 
Siku Magufuli akiwagusa wawekezaji wa madini Tanzania haitokuwa na muda na kuwa kama Congo. Magufuli ni kikatuni lakini hao jamaa ndio Wahuni.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…