Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Maji bado ni tatizo kubwa nchini. Suluhu ni kuimarisha hiyo wizara na kuwajibisha wazembe...
 
Eti ivunjwe...hahaaaaa, we sema ipewe kipaumbele tu, maji ni hitaji muhimu sana kwa maisha, na kila nchi dunia nzima ina wizara ya maji kwa taarifa yako.
 
Umesoma wapi?
Mto Nile unaanzia Jinja nchini Uganda ila Bonde lake linaanzia sehemu nyingi ikwemo Tanzania, Burundi, Rwanda, Kenya, DRC na kwingine.

Ukishataja Ziwa Victoria huna haja ya kutaja Mto Nile. Katika Tanzania hatuna jina linaloitwa mto Nile ila tuna Taasisi ya Kimataifa inayosimamia Bonde la Mto Nile ambapo Ziwa Victoria ni sehemu ya Bonde hilo.
 
Mto Nile unaanzia Jinja nchini Uganda ila Bonde lake linaanzia sehemu nyingi ikwemo Tanzania, Burundi, Rwanda, Kenya, DRC na kwingine.

Ukishataja Ziwa Victoria huna haja ya kutaja Mto Nile. Katika Tanzania hatuna jina linaloitwa mto Nile ila tuna Taasisi ya Kimataifa inayosimamia Bonde la Mto Nile ambapo Ziwa Victoria ni sehemu ya Bonde hilo.

Kwaiyo inamaanisha kuna source ya mto nile na pia kuna uwezo wakutafuta chanzo cha maji pale?
 
Ishu ni kwa serikali kuipa kipaumbele kwa kuwapa bajeti ya kutosha kufanya uwekezaji wa kutosha. Je unafahamu mitambo ya Ruvu Juu na Ruvu Chini ilijengwa lini?
 
The Nile has two major tributaries, the White Nile and Blue Nile. The White Nile is considered to be the headwaters and primary stream of the Nile itself. The Blue Nile, however, is the source of most of the water and silt. The White Nile is longer and rises in the Great Lakes region of central Africa, with the most distant source still undetermined but located in either Rwanda or Burundi. It flows north through Tanzania, Lake Victoria, Uganda and South Sudan.
 
Wizara imelala sana. Huku iringa gharama ya kuunganisha maji ni kubwa kuliko umeme. Wizi mtupuu idara ya maji iringa na wizara ipo
 
Kwa taarifa yako Mto Nile unaanzia ziwa victoria ndani ya nchi ya Uganda. Acha ubishi soma
mto nile unaanzia rwanda, burundi na congo kijeografia hakuna mto unao anzia ziwani. maji ya mto kagera yanayopita ziwa victoria haya changanyiki na maji ya ziwani yana pita ziwani kama mto
 
Nchi yoyote inayotaka kuendelea lazima iwe na dira ya maendeleo, uongozi mzuri na watu wazalendo kwa taifa lao. Taifa letu kwa muda mrefu limekua tegemezi kwenye jumuiya za kimataifa na kwa kiasi kikubwa tegemezi kwenye bajeti ya maendeleo. Tanzania imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi na amani surprisingly hatua za maendeleo zimekua hazilingani na mibaraka hii aliyotupatia mwenyezi Mungu.


Nchi nyingi za Afrika ikiwamo Tanzania zimekua zikilalamikiwa kwa kuendekeza anasa na matumizi yasiyokua ya lazima., matumizi makubwa ya serikali yasiyoendana na ukuaji wa uchumi na uhalisia wa hali ya kiuchumi ni moja ya mambo yanayorudisha nyuma maendeleo ya nchi kwa pesa nyingi za serikali kwenda kwenye matumizi yasiyo ya lazima na pesa kidogo kuelekezwa kwenye shughuli za maendeleo.

Tunaitaji Tanzania yenye viongozi wazalendo na wenye uchungu wa kuona nchi yao inabiga hatua za maendeleo. Mh. Dr, John Pombe Magufuli toka achaguliwe kuwa Rais ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameonyesha dhamira ya dhati ya kubadili mwelekeo wa Taifa letu kwa kubana matumizi. Maamuzi mbalimbali aliyoyafanya toka aingie Ikulu ya Tanzania ni yamuelekeo wa kizalendo na yakupigia mfano. Kwa mfano, kusitisha safari za nje, kuelekeza pesa za sherehe za wabunge kwenda kununua vitanda katika hospitali ya muhimbili, yote haya ni maamuzi ya kizalendo. Baadhi ya watanzania wamekua wakipuuza juhudi hizi, kwa mtu mwenye kulipenda taifa lake hana budi kumuunga mkono Rais wetu ili aweze kufanya maamuzi makubwa zaidi kama vile kufumua sheria ya manunuzi ambayo imekua chanzo cha kupoteza mapato makubwa ya serikali na kudhibiti rushwa.


Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Mbariki Rais wetu.
 
Mahakama ya ufisadi ianze na zike billion zilizolipwa makandarasi hewa wizara ya Ujenzi, kivuko feki cha 1978 kwa billion 8 , mabehewa mabovu, wezi wa Escrow, EPA
 
NINA HAKI YA KUTOA MAONI KWA DR.JOHN POMBE MAGUFULI RAIS WA JMT AWAMU YA TANO.

Ninaomba kutoa angalizo kwa Mh.Dr.John Pombe Magufuli katika kipindi cha miaka 5 atakachokuwa akiongoza JMT.
1. Ni vyema akaepuka watu wachonganishi watakaomchonganisha na Watendaji wake kwa manufaa ya watu hao.Kwa kutumia vyombo vya dola na utashi wake kama Rais ni vyema akachuja kila taarifa atakayopewa kabla ya kuchukua maamuzi stahiki.Kama ilivyokuwa wakati wa Kampeni,watu wengi watajisogeza kwake kwa njia ya kumpa ushauri katika mambo mbalimbali.
2. Ni vyema akatafakari sana katika uteuzi wa Watendaji atakao ufanya maana hao ndio watakuwa wafuatiliaji wa shughuli zake za kila siku.Kama kuna mahalia mbapo JPM anapaswa kuwa makini ni katika teuzi mbalimbali atakazozifanya.Asifanye uteuzi wenye nia ya kulipa fadhila.Bali weledi na uchapakazi pamoja na uaminifu katika utendaji wa kazi.
3. Ni vyema JPM akashughulikia kwa moyo wake wote suala la Zanzibar kabla hali ya amani haijavurugika ZAIDI.Mshindi halali atangazwe na kazi iendelee.Imani kwamba CUF watavunja Muungano si ya kujenga na Imani kwamba CCM pekee ndiyo yenye kuleta amani na utulivu si hoja makini na jadidi.
4. Ni vyema akaweka mikakati thabiti ya kushughulikia ahadi lukuki alizoziahidi ili imani ya Wananchi kwake na kwa Chama chake irudi na Maisha ya Wananchi yawe bora zaidi.Watangilizi wake hawakutimiza ahadi zao lukuki walizotoa kwa mbwembwe majukwaani.
5. Ni vyema akaepuka kuongozwa na watangulizi wake ambao kwa nguvu kubwa walimbeba na kumweka madarakani.Akumbuke yeye ndiye rais wa JMT na watangulizi wake walikwisha maliza vipindi vyao.
6. Ni vyema akafanya kazi na makundi yote hususani vyama pinzani na wanaharakati wapenda maendeleo.Kushinda uchaguzi sio kushinda kila kitu.Hata walioshindwa wanaweza kupewa ushirikiano kwa ajli ya kuleta maendeleo yanayohitajika.
7. Ni vyema harakati za kufufua Viwanda vilivyokuwa vimebinafsishwa na kutelekezwa ama kubadilishwa kuwa magodauni ziendane na kuboresha upatikanaji wa uhakika wa nishati ya umeme pamoja na kuondoa Michango lukuki inayoitwa ya kisheria katika Viwanda hivyo kama OSHA,FIRE RESCUE,NEMC,VIPIMO,MAJI,TBS,LESENI,CESS ZA VIJIJI,MITAA NA WILAYA,NK.Hizi zote huwa ni kero kwa Wenye viwanda.Pia ni vyema soko la ndani la bidhaa husika lilindwe kwa ajili ya kuhakikisha bidhaa hizo zinauzwa na tija kupatikana.
8. Ni vyema akaondoa kabisa kodi katika pembejeo za kilimo kama matrekta, mbolea, powertiller, mbegu bora n.k.Jitihada za kuboresha sekta ya Kilimo ziwe za dhati na zenye tija na wala sio blah blah.
9. Ni vyema suala la Bunge kuwa la mipasho badala ya chombo cha kutunga sheria na kujadili matatizo ya wananchi likemewe kwa sauti kuu na yeye awe mfano bora wa kulisimamia hilo.Jambo baya katika hotuba yake alisisitiza hilo na papo hapo yeye mwenyewe akatoa mipasho kwa kuwaita wapinzani ?watoto?
10. Ajira kwa vijana ni bomu hatari.Ni lazima tatizo hili litatuliwe kwa jitihada kubwa kwa kufufua viwanda na kuimarisha kilimo sambamba na kukomesha ajira za upendeleo.
Haya ni maoni yangu binafsi, hata hivyo michango kwa wengine ni muhimu kwa nia ya kutupeleka katika maisha bora zaidi.Aidha kutofautiana mitizamo ni chanzo cha Maarifa mengine.

Bunge si mali ya Rais,hapaswi hata kwa sekunde moja kuliingilia. Ule ni Mhimili Huru, kama ilivyo Executive na Judiciary. Bunge ndilo lenye wajibu wa kuisimamia Serikali,ila si Serikali kulisimamia Bunge! Jukumu ulilompa unamwonea tu.
 
Inakuaje mfanya kazi aliyeamua kutumia pikipiki kama usafiri wake wa kumuwahisha kazini aambiwe akate kibari cha kuingia mjini.mfano mimi nina barua inayoonyesha kuwa ni mfanyakazi nimeajiriwa na pikipiki ninayotumia ni kwa ajili ya kuwahi kazini lakini wakamataji hawataki kuelewa .
 
Lipia kwanza hiyo pikipiki yako kodi kama kuna MTU atakusumbua
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom