Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
kwa mawazo yangu na uelewa wangu mkuu nakuomba rudi kwa walim chambua alaf wape nafasi uone kama watakuangusha.wengine hawa utawatumbua mpaka mwisho hawataacha kwasababu hawafwati maadil kama walimu.muone Mh wazir mkuu anavyofanya kaz.ametoka wap.lione hilo .

NAWAKILISHA
 
Nadhani mheshimiwa una haja ya kuwachunguza baadhi ya walimu wenye sifa stahiki uwape wadhifa fulani ndani ya wilaya mbalimbali na mikoa kwani kada hii wana maadili ya kutosha na wanaheshimu majukumu.

Hawa unaowatoa sehemu mbalimbali ufisadi, wizi na kukosa uadilifu hakutaisha. Yaani hata miezi 3 haijaisha Bukoba wameiba. Mwalimu anaweza kufanya kazi ya ukuu wa idara kwa mshahara huo huo aliozea na akapiga kazi.

Ila endelea kutumbua mpaka mwisho heshima irudi.
 
Mheshimiwa sitachoka kukuunga mkono kwa juhudi kubwa unazofanya kuijenga Tanzania mpya.lakini ombi hawa unaowatumbua hakikisha unasimamisha mishahara yao ili walipwe watu wanaofanya kazi kwa moyo na uadilifu vinginevyo hao ni hewa namishahara wanyopewa ndiyo inayoharibu utaratibu wako kwa war umishi wengine.tumbua hao
 
Mh. Rais Salamu Kwako.

Mh. Rais naomba uiagize Mifuko ya jamii au uombe msaada nje ya nchi hususani CUBA au Korea Kusini watujengee Viwanda vya Dawa Za binadamu, hii itasaidia kupunguza serikali kutumia fedha nyingi sana za kigeni kuagiza dawa nje au kununua Dawa toka nje ya nchi, Wanaweza kujenga kiwanda kimoja kikubwa sana Afrika mashariki na kati kitakachozalisha dawa za kutosha na za aina mbalimbali hasa kwa magonjwa ambayo ni sugu nchini.


Mh. Rais Kwa nini usiombe msaada wa ujenzi wa mitambo ya kusafishia mafuta ya petrol na Diesel ili Uganda ikianza kusafirisha mafuta yake tuingie nayo mkataba ili tuwe tunayasafisha hapa hapa ya kwetu na kuwaachia mengine hao wasafirishaji, hii itatusaidia kupunguza gharama za kuyaagiza tena hayo mafuta toka nje ya nchi, na mitambo hii itatusadia sisi wenyewe baada ya kuanza kuchimba mafuta yetu na kuyasafishia hapa hapa na kuyauza ndani na nje ya nchi hasa majirani zetu.

Mh. Rais, Omba tena msaada au serikali ijenge yenyewe Hospitali kama ya Muhimbili-Mloganzila katika kanda mbali mbali hasa Mwanza, Mbeya, Arusha Dodoma na Tanga.


Mh. Rais Nina Imani na wewe sana, na ni matumaini yangu kuwa Imani huzaa Imani, Hongera kwa ununuzi wa ndege, sisi tunaoona mbali tunajua umuhimu wa ndege hizi nchini.
 
Mh rais kwanza Napenda kukupongeza kwa Kazi nZuri Na jitihada zako ambazo zinaanza kuzaa matunda, songa mbele maana tunakuombea pamoja Na changamoto hizo tutafika. Lengo la kuandika andiko hili Ni kukushauri Na kukuunga mkono juu ya sikitiko lako juu ya upotoshaji mitandaoni.

Ushauri wangu Ni mfupi kuwa dawa ya Moto Ni Moto Na kwamba ili kukabiliana Na upotoshaji huu , dawa sio kuizuia Bali kuwawezesha wafanyakazi wa serikali kukabiliana Na upotoshaji huu kwa kuwa tayari kueneza ukweli kupitia mitandao hiyo hiyo . Kwa kuanzia kila msemaji Au afisa Habari wa wizara Na vitengo vya serikali afundishwe namna bora ya kutumia mitandao hiyo . Pili iwepo sera ya matumizi bora ya mitandao ya kijamii kwa kila kitengo cha serikali Na Tatu TCRA waongezewe uwezo wa kushughulikia wahalifu wa mitandaoni kwa kupewa mafunzo zaidi...

Wadau tuongezee....

Moderators: please Naomba msiunganishe uzi huu Na mwwingine .
 
Katika utendaji kazi sehemu yoyote ile hapokosi unafiki, ghiliba, usaliti na uchonganishi wa aina yoyote ile. Na haya yote yanatokea pindi pale mtu anafanya kazi ktk misingi mema, mazingira mazuri ambayo yanatetea kundi la watu fulani ambao kwa namna moja ama nyengine. Watu ambao watakuwa wanakupinga na kukusema vibaya ni wale watu ambao umegusa maslahi yao, watatumia ushawishi mkubwa, fitna nyingi, uchonganishi na uchochezi wa hali ya huu ili wakugombanishe na boss wako.

Lakini kitu kikubwa unatakiwa unatakiwa usirudi nyuma katika kutetea maslahi ya watu wako Bali unatakiwa kuongeza nguvu na spidi ili ulete haki na usawa kwa RAIA wote bila kuwaogopa hao wachonganishi kwani ukirudi nyuma utageuka jiwe.

Najua hadi dakika hii hawajaelewa nini namaanisha lakini endelea kuniazima sikio lako utanifahamu vizuri. Kipindi cha nyuma cha uongozi wa hayati Mwalimu Julius kambarage Nyerere wakati akihutubia mkutano mmoja hivi aliwahi kutoa hadithi Fulani. Hadithi ile ilikuwa hivi " kulikuwa na msichana mzuri sana mmoja katika kijiji fulani, wanaume wengi walivutika na ile uzuri wake na wakataka wampose. Binti huyu alikuwa anaishi mlimani lakini mpaka ufike kule alipo kuna vikwazo na masharti.

Waliojitokeza kwenda kumposa yule binti walikutana na bibi kizee, bibi huyu alikua anamuuliza kila mmoja utaweza kufika kule mlimani? Kuna kelele nyingi na za kutisha na unatakiwa wakati unaenda ukisikia hizi kelele usiangalie pembeni wala nyuma, ukigeuka nyuma au pembeni utakuwa jiwe.

Watu wengi walipopewa haya maagizo yaliwashinda kwani kadri walipokuwa wanamkaribia yule binti mrembo kelele zilikuwa nyingi na vishindo vikubwa wakisema huyoo huyoo mchinje mchinje. Kutokana na kelele kuwa nyingi wakawa wanageuka nyuma na kuwa mawe. Basi lile eneo la mlimani lilikuwa na mawe madogomadogo mengi sana ambao ni watu.

Siku moja kijana mmoja mdogo sana alijitoa mhanga kwenda kule mlimani kwa yule binti. Kulikuwa na vitisho vingi sana lakini yule kijana hakuangalia nyuma wala pembeni na kufanikiwa kumfikia yule binti "

Dhima ya hadithi hii ni kwamba tusiwe waoga kma tumeamua kufanya jambo fulani. Lengo langu ni kumuomba na kumsihi Mh Rais john pombe magufuli asikubali kugeuka jiwe, nadhani sasa mmeanza kupata lengo la hadithi na ninachokimaamisha.

Mh JPM ana nia ya dhati na thabiti katika kuwatumikia wananchi, ana nia na lengo la kupigania haki za wanyonge na kuwaepusha watanzania kutoka katika dhuluma, unyonyaji na ufisadi kutoka kwa baadhi ya watu wasiokuwa na nia njema na taifa hili. Wanapiga kelele nyingi,vishindo vingi ilikumkwamisha Rais wetu mpendwa ili nae ageuke Jiwe. Wakisikia Rais kafanya mazuri wanapinga,akinunua ndege wanapinga,akihakiki wafanyakazi hewa wanapinga,akitumbua wazembe na wapiga dili wanapinga lengo ni kumkwamisha Rais wetu ili nae ageuke jiwe.

Ombi langu kwa Mh Rais usikubali kugeuka jiwe kwa kelele za wabaya wasio na nia njema na thabiti kwa taifa letu, sisi wengine tupo nyuma yako kwa kila jambo. Kama ulikuwa unatumia spidi ndogo katika kuendesha nchi, ongeza mara mbili yake na wala usimuogope mtu kwani wewe ndo Nyerere, Nkurumah na Mandela uliyebakia Africa.

Prof Otieno Lumumba wa Kenya University alishawahi kusema "People are saying Nyerere is dead, but for me Nyerere is still alive, Nyerere is alive in Magufuli. What Magufuli is doing is what Nyerere did in his era, so I see Nyerere, Nkrumah and Madiba in Magufuli".

Please Rais usikubali kugeuka jiwe, watanzania tuko nyuma yako.

Na Fumbwe Rashidi Ngassa
 
..Japo sijaelewa Maana Ya Ghiliba Mpka sasa Ivi ILA Point nmeipata,Uko sawa Mkuu!!
 
Hulka yako Naona haitofautiana na Donald Trump, ukifikiria kila tatizo solution yake ni papo kwa papo . Ndio Maana Bi Hilary Clinton alimwambia Trump kwamba waliweza kupata maktaba wanuklia na Iran bila kurusha kombora au kupigana kwa ufupi. Sasa mwache Raisi afanye kazi yake hujui kinacho endelea kwa sasa kuhusiana na Hilo Jambo kisheria, kiu tawala n.k lakini huku mtaani tuona miundo mbinu inavyo wekwa sawa kurahisisha shughuli zetu.
 
MH.Rais wa JMT Dr.John Pombe Joseph Magufuri .hawezi kuwa sawa Mwl.nyerere . kwasababu.wanatofautiana vitu. 1.Rais JPM anaupinzani mkali tofauti na Nyerere 2.Wananchi wengi walikuwa wamechoka chama tawala 3.Rais JPM analiongoza taifa wakati idadi wasomi kumbwa,watu wengi ,wakosoaji watakuwa wengi 4.Rais JPM anakazi kubwa kubadilishi kupeleke misingi imara,nidhamu,kuheshiana ,haki kwa kila mtu 5.Rais JPM anania ya kutaka kuepeleka nchi katka uchumi wa kati ,viwanda, tayari anaanda mazingira 6.Rais JPM anapenda Tanzania au taifa mzalendo kupigania taifa zaidi tofauti Nyerere alipenda watu taifa , 7.Rais JPM anapenda maendeleo ya vitu(material) au taifa ,maendeleo wa nchi serikali iwe na hela .kuliko maendeleo watu(taifa kwanza watu wafuate) 8.Rais JPM anajali masikini,wanyonge,wasionacha ni mtetezi wa wengi 9.mwisho niseme watanzania kulio wengi masikini Mungu ajibu maombi yetu ametulekea rais tuliemtaka JPM
 
MIMI HUWA NASEMA MAGUFULI AKIONGEA KUNA WATU HUWA WANAMEZA VIDONGE VYA PRESHA KABLA YA SPEECH ZAKE.
 
Rais anasema tuwe wazalendo kwa kusifia vya kwetu,hii ni ngumu sana kwa sababu hivyo vitu anavyotaka tujivunie vingi ni vibovu na vya hovyo ingawa ni vya serikali. Hii haihitaji mganga ili kujua kua shule hospitali pamoja na mashirika mbalimbali ya binafsi ni bora mara dufu kuliko ya serikali. Kwani uzalendo ni kusifia k2 chako hata kama cha hovyo?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom