Maono ya Rais mama Samia kuhusu uwekezaji nchini kwenye nyuzi 360

Maono ya Rais mama Samia kuhusu uwekezaji nchini kwenye nyuzi 360

Tatizo kubwa la wabongo ni upeo mdogo wa kufikiri, hivi watu wanafikiri kuwa faida inayipatikanwa kwa wawekezaji ni kodi tu? au Ajira tu? nje ya hapo wanahisi hakuna faida ya uwepo wao. Hizi ni akili za karne zilizopita bado wabongo zimo vichwani mwao.
 
Ajira zipi sasa unazungumzia mkuu, maana bila sekta binafsi kukua hakuna ajira na hakuna ukuaji wa sekta binafsi bila uwekezaji.
Haya ndio madhara ya kupost mambo usiyokuwa na uwezo nayo kuyajadili,

Mara hii tu umeshasahau hata umetuandikia nini.
 
Ni huo wakati wa JK ambapo vijana wengi waliotoka chuo walikuwa wakiajiriwa, mishahara ya wafanyakazi ilikuwa ikiongezwa kila mwaka, miradi Mingi ya maendeleo kama shule, vyuo, barabara na madaraja ilifanyika na watu walikuwa na hela na kazi mitaani.

Hizo sera za huyo mpuuzi wenu magufuli zimesaidia nini maana kama kukopa tu, kwa miaka 5 amekopa kuliko alivyokopa JK kwa miaka 10??? Na watu wamekosa ajira kwa makampuni kufunga biashara na kuondoka, majobless wamejaa mitaani na wengi kugeuka wachuuzi ( machinga)
Hii analysis yako mbona inaangalia pande Moja tu?

Afu ujue unaongelea pindi wanafunzi wanamaliza chuo wachache Sana na Sasa Idadi iko zaidi ya hapo.
Then huangalii na priorities za wakati ule na wakati wa Hayati.

Lakini pia usisahau ni 2012 kipindi cha JK watu walijazana Taifa kwenye interview.

Tuendelee kuchapa kazi
 
Ni huo wakati wa JK ambapo vijana wengi waliotoka chuo walikuwa wakiajiriwa, mishahara ya wafanyakazi ilikuwa ikiongezwa kila mwaka, miradi Mingi ya maendeleo kama shule, vyuo, barabara na madaraja ilifanyika na watu walikuwa na hela na kazi mitaani.

Hizo sera za huyo mpuuzi wenu magufuli zimesaidia nini maana kama kukopa tu, kwa miaka 5 amekopa kuliko alivyokopa JK kwa miaka 10??? Na watu wamekosa ajira kwa makampuni kufunga biashara na kuondoka, majobless wamejaa mitaani na wengi kugeuka wachuuzi ( machinga)
Watu wanachukulia jumla jumla kuwa uwekezaji unaongeza ajira, lakini ukweli ni kuwa uwekezaji unaweza kusababisha ajira zipotee tena kwa maelfu. Ajira inaweza kuwa ya mshahara au ya kujiajiri mwenyewe. Sasa kama umejiajiri kihalali halafu kutokana na sera za serikali unalazimishwa kuachana na shughuli uliyokuwa umejiajiri, hapo uwekezaji huo na balaa. Huko vijijini mamilioni ya wakulima wamenyang’anywa ardhi zao ili tu kupisha hao wanaoitwa wawekezaji huku wakulima hao wakikejeliwa kuwa hawazalishi kwa tija na kuwa wawekezaji hao watawaajili. Binafsi nimebahatika kuzunguka sana maeneo ya vijijini kutokana na kazi niliyokuwa naifanya. Niliwahi kufika wilaya moja nikamkuta mtu ambaye alikuwa na ekari kumi na mbili, yeye alikopa power tiller Mfuko wa pembejeo (AGTIF) kwa lengo la kulima mpunga katika shamba lake hilo, wakati huo huo aliletwa mwekezaji tena toka nje ya nchi akapewa ardhi katika kata hiyo ilia alime mpunga, kilichofanyika ni kuwa mamlaka zilichukua ardhi ya wakulima wadogo wadogo katika vijiji vinavyomzunguka mwekezaji huo na kuunganisha ili kumpatia eneo la kutosha mwekezaji huo, hivyo kupelekea wananchi hao kukosa ardhi ya kulima akiwemo huyo aliyepoteza hekta 12. Sasa fikiria huo mkopo aliochukua AGTIF aliulipaje wakati tayari shamba alilotaka kuzalishia ambalo ni mali yake amenyang’anywa? Yaani uwanyang’anye ardhi wazawa na kuwafanya manamba katika ardhi yao hiyo hiyo! Ukienda njia ya Rufiji, utaona kuna mapori mengi sana kuzunhguka vijiji na unaweza kuzani kuwa kuna ardhi kubwa sana ya kulima, lakini ukweli ni kuwa ardhi yote hiyo wamepewa hao wanaoitwa wawekezaji na ardhi hiyo hata kuilima hawailimi lakini wakati huo huo wanavijiji waliokuwa wanaimiliki ardhi hiyo wanasumbuka kwa kukosa ardhi ya kulima. Huko nyuma kabla RUBADA haijavunjwa na JPM ilikuwa ndio Karl Peters wa Tanzania katika kunyang’anya ardhi na kuidalalia. Malaki ya hekta zimeondolewa mikononi mwa wakulima na kupewa wajanja kwa mgongo wa uwekezaji, Tena huko nyuma kuna watu walikuwa wanakuja bila hata senti tano lakini baada ya kupewa ardhi wanachukua hati wanaenda benki tena za ndani ya nchi na kukopa mamilioni ya pesa na kufanyia biashara zingine kama uagizaji wa mafuta.



Unalalamika kuwa wamachinga wamezidi, umachinga ,mwingine ni matokeo ya watu kupoteza ardhi zao sasa inabidi wafanye uchuuzi, bodaboda, umalaya, mama ntilie (sio kama nadharau kazi hizo la hasha) kwa sababu hizo sekta hazijai zinampokea yeyote anayekuja kujiunga nazo ingawa soko linakuwa halipanuki.

Pia watu wanasema wakati wa JK kulikuwa na pesa mtaani lakini hawajiulizi kuwa zilikuwa pesa halali? Wizi, ufisadi na ubadhirifu wa pesa za umma na uuzaji wa madawa ya kulevya ulichangia katika ukuaji uchumi, hivyo uchumi wa wakati huo haukuwa halisi. Wewe inaweza kuwa hukuwa unaiba lakini manufaa ya wizi yalikufikia kupitia mnyororo wa wizi. Mathalani afisa au mfanyabiashara akishahomola atakuja mtaani kwako na kukupa kazi ya kumjengea au utamuuzia nguo bei juu au atawahonga nyumba zake ndogo mamilioni hivyo watu wengine kunufaika kama vile saluni za urembo nk. Lakini vile vile kulikuwa na watu kibao wanaumia kwa kukosa dawa, pensheni, na huduma zingine sababu sehemu kubwa ya pesa imeibwa. Kwa sasa hata mambo yakilegezwa vipi pesa haziwezi kurudi kama wakati wa JK unless wizi/ufisadi urudi upya kwa kasi. Kuna afisa mmoja wa kawaida kabisa asiye na cheo ilikuwa kila mwisho wa wiki lazima aende kwa ndege kwao Mwanza na kurudi jumapili au jumatatu asubuhi ila wakati wa JPM alikuwa haendi licha ya kuwa kazi yake haikubadilika.

Kiwango cha ukopaji hakiwezi kulingana kwa kila Rais aliyetawala, lakini ni wazi marais wote watano walikopa ila JPM alipoingia alikuta deni kubwa tayari, ukopaji wake haukusababisha deni liwe kubwa, na hayo madeni ya nyuma yanaongezeka riba, hivyo unaweza kuona deni limeongezeka wakati wa JPM lakini sehemu kubwa ya ongezeko hilo ni riba za nyuma kuliko deni jipya. Ukitaka kukosoa hili chukua data kila Rais aliyeingia madarakani alikuta deni shilingi ngapi na alipoondoka aliacha shilingi ngapi.

Watu wamevamia mjadala na wakati hawaelewi undani wa mambo na vilevile chuki binafsi dhidi ya JPM.
 
Hii analysis yako mbona inaangalia pande Moja tu?

Afu ujue unaongelea pindi wanafunzi wanamaliza chuo wachache Sana na Sasa Idadi iko zaidi ya hapo.
Then huangalii na priorities za wakati ule na wakati wa Hayati.

Lakini pia usisahau ni 2012 kipindi cha JK watu walijazana Taifa kwenye interview.

Tuendelee kuchapa kazi
Kwenye Ile Interview ya Takukuru
 
Mkuu tumerudi tena kwenye nchi ya hoja kwa hoja. Kwa mkuu anayedhani ana hoja au ushuauri wa maana huu ndio wakati. Ambaye hatutumia wakati huu huenda asipate tena fursa ya kutoa hoja yake kwa ufasaha katika kipindi fulani na kubaki kulia lia.
Kinachonishangaza ni kuwa na nyie mlikuwa mnajua hatukuwa kwenye mwelekeo sahihi. Hilo tu ndilo linalonishangaza.
 
Watu wanachukulia jumla jumla kuwa uwekezaji unaongeza ajira, lakini ukweli ni kuwa uwekezaji unaweza kusababisha ajira zipotee tena kwa maelfu. Ajira inaweza kuwa ya mshahara au ya kujiajiri mwenyewe. Sasa kama umejiajiri kihalali halafu kutokana na sera za serikali unalazimishwa kuachana na shughuli uliyokuwa umejiajiri, hapo uwekezaji huo na balaa. Huko vijijini mamilioni ya wakulima wamenyang’anywa ardhi zao ili tu kupisha hao wanaoitwa wawekezaji huku wakulima hao wakikejeliwa kuwa hawazalishi kwa tija na kuwa wawekezaji hao watawaajili. Binafsi nimebahatika kuzunguka sana maeneo ya vijijini kutokana na kazi niliyokuwa naifanya. Niliwahi kufika wilaya moja nikamkuta mtu ambaye alikuwa na ekari kumi na mbili, yeye alikopa power tiller Mfuko wa pembejeo (AGTIF) kwa lengo la kulima mpunga katika shamba lake hilo, wakati huo huo aliletwa mwekezaji tena toka nje ya nchi akapewa ardhi katika kata hiyo ilia alime mpunga, kilichofanyika ni kuwa mamlaka zilichukua ardhi ya wakulima wadogo wadogo katika vijiji vinavyomzunguka mwekezaji huo na kuunganisha ili kumpatia eneo la kutosha mwekezaji huo, hivyo kupelekea wananchi hao kukosa ardhi ya kulima akiwemo huyo aliyepoteza hekta 12. Sasa fikiria huo mkopo aliochukua AGTIF aliulipaje wakati tayari shamba alilotaka kuzalishia ambalo ni mali yake amenyang’anywa? Yaani uwanyang’anye ardhi wazawa na kuwafanya manamba katika ardhi yao hiyo hiyo! Ukienda njia ya Rufiji, utaona kuna mapori mengi sana kuzunhguka vijiji na unaweza kuzani kuwa kuna ardhi kubwa sana ya kulima, lakini ukweli ni kuwa ardhi yote hiyo wamepewa hao wanaoitwa wawekezaji na ardhi hiyo hata kuilima hawailimi lakini wakati huo huo wanavijiji waliokuwa wanaimiliki ardhi hiyo wanasumbuka kwa kukosa ardhi ya kulima. Huko nyuma kabla RUBADA haijavunjwa na JPM ilikuwa ndio Karl Peters wa Tanzania katika kunyang’anya ardhi na kuidalalia. Malaki ya hekta zimeondolewa mikononi mwa wakulima na kupewa wajanja kwa mgongo wa uwekezaji, Tena huko nyuma kuna watu walikuwa wanakuja bila hata senti tano lakini baada ya kupewa ardhi wanachukua hati wanaenda benki tena za ndani ya nchi na kukopa mamilioni ya pesa na kufanyia biashara zingine kama uagizaji wa mafuta.



Unalalamika kuwa wamachinga wamezidi, umachinga ,mwingine ni matokeo ya watu kupoteza ardhi zao sasa inabidi wafanye uchuuzi, bodaboda, umalaya, mama ntilie (sio kama nadharau kazi hizo la hasha) kwa sababu hizo sekta hazijai zinampokea yeyote anayekuja kujiunga nazo ingawa soko linakuwa halipanuki.

Pia watu wanasema wakati wa JK kulikuwa na pesa mtaani lakini hawajiulizi kuwa zilikuwa pesa halali? Wizi, ufisadi na ubadhirifu wa pesa za umma na uuzaji wa madawa ya kulevya ulichangia katika ukuaji uchumi, hivyo uchumi wa wakati huo haukuwa halisi. Wewe inaweza kuwa hukuwa unaiba lakini manufaa ya wizi yalikufikia kupitia mnyororo wa wizi. Mathalani afisa au mfanyabiashara akishahomola atakuja mtaani kwako na kukupa kazi ya kumjengea au utamuuzia nguo bei juu au atawahonga nyumba zake ndogo mamilioni hivyo watu wengine kunufaika kama vile saluni za urembo nk. Lakini vile vile kulikuwa na watu kibao wanaumia kwa kukosa dawa, pensheni, na huduma zingine sababu sehemu kubwa ya pesa imeibwa. Kwa sasa hata mambo yakilegezwa vipi pesa haziwezi kurudi kama wakati wa JK unless wizi/ufisadi urudi upya kwa kasi. Kuna afisa mmoja wa kawaida kabisa asiye na cheo ilikuwa kila mwisho wa wiki lazima aende kwa ndege kwao Mwanza na kurudi jumapili au jumatatu asubuhi ila wakati wa JPM alikuwa haendi licha ya kuwa kazi yake haikubadilika.

Kiwango cha ukopaji hakiwezi kulingana kwa kila Rais aliyetawala, lakini ni wazi marais wote watano walikopa ila JPM alipoingia alikuta deni kubwa tayari, ukopaji wake haukusababisha deni liwe kubwa, na hayo madeni ya nyuma yanaongezeka riba, hivyo unaweza kuona deni limeongezeka wakati wa JPM lakini sehemu kubwa ya ongezeko hilo ni riba za nyuma kuliko deni jipya. Ukitaka kukosoa hili chukua data kila Rais aliyeingia madarakani alikuta deni shilingi ngapi na alipoondoka aliacha shilingi ngapi.

Watu wamevamia mjadala na wakati hawaelewi undani wa mambo na vilevile chuki binafsi dhidi ya JPM.
Mkuu rcm
RUBADA - Rufiji Basin Development Authority

Hii inahusikaje na kunyanganya Ardhi?
 
Wanapewa derivative right of occupancy ambayo inatosha kuwa collateral ukizingatia kwamba muda unakua ni 33,66 na 99 years.

Hakuna anayekataa investors kuja nchini ila swala hapa ni kuwa tunawakaribisha vipi, ukizingatia kwamba kuna ulazima wa kulinda ajira za vijana wetu kwani tusipozilinda tutawafanya kuwa manamba kwenye nchi yao na elimu yao itakua haina faida, tutatengeneza kizazi ambacho kimekandamizwa kwa muda na siku wakichoka hapata kalika hapa.

Kodi ni tamu ndio ila tusifanye hivyo at the expence of our national security.
Suala la kwanza kujiuliza hapa ili mada yako iwe fikirishi zaidi na kuweza kupata majibu sahihi kwa muktadha sahihi wa hoja yako naomba kuchagiza yafuatayo;

Moja, can a foreign investor own land in Tanzania!?

Mbili, can a foreign investor obtain right of occupancy and or derivative right of occupancy in Tanzania!?

Kama majibu yote yatakuwa ndio basi cha kujiuliza ni kwamba utaratibu upoje chini ya Kituo cha Uwekezaji?
 
Hivi huko si ndiyo tulikotoka na bado kodi ilikuwa 800m?
Umemjibu vizuri sana,huko ndipo tulipotoka,nakumbuka Muhongo alipigia debe vitalu wapewe wageni,ilikuwa kelele nchi nzima kwamba vitalu wapewe wazawa,leo tunataka kurudi kule tena

Nafikiri tunahitaji wawekezaji wa kuja kutoa elimu iliyo bora maana naona shida yetu ni Elimu basi🤣🤣🤣
 
Sio kila mwekezaji ni genuine ,

Wengine ni janja janja tu, wanakuja kwa malengo yaliyojificha moja wapo ikiwa kupata ardhi yetu ili wachukulie mikopo kwenye mabenki yao huko nje na kuendelea na mambo mengine

Tusipokua makini tunaweza kuta sehemu kubwa ya ardhi yetu ipo rehani kwenye mabenki ya nje hiyo ni threat kwa national security.
Nakumbuka kuhusu SGR Nape na yule mbunge wa Nzega mjini walisema inabidi tuwape wawekezaji,Magufuli akasema waleteni hata sasa hivi waje wajenge🤣🤣🤣,hakuna wawekezaji wa maana
 
Wakati wa JK huo si ndio ujinga uliokuwa unafanyika na kodi ilikuwa ni 800bn kwa mwezi wastani, SSH hana maoni, kodi lazima ikusanye kwa sheria kama anaona kodi ni kubwa abadilishe sheria, vinginevyo anatengeneza mazingira ya wafanyabiashara kukataa kulipa kodi halali kabisa.
Wewe inaelekea unataka watu waporwe hela zao kwa kisingizio cha ukusanyaji kodi
 
Mkuu rcm
RUBADA - Rufiji Basin Development Authority

Hii inahusikaje na kunyanganya Ardhi?
Kwa mujibu wa sheria iliyounda RUBADA, ardhi yote katika bonde la Kilombero iliwekwa chini ya RUBADA bila kujali kuwa kuna mamilioni ya watu kuanzia Kilombero hadi Rufiji walikuwa wanaishi na kumiliki maeneo hayo. Hivyo ilikuwa akitokea mwekezaji anahitaji sehemu yoyote ya ardhi RUBADA wanaitwaa ardhi hiyo toka kwa wananchi na kumuuzia/kumpa mwekezaji huyo bila kujali kuwa wananchi pia wanaihitaji ardh ihiyo wananchi watake wasitake.
 
Kwa akili yangu ndogo sina pingamizi wawekezaji wa nje kukaribishwa na kuwa na haki ya kuchagua waajiriwa wao wa kigeni kwenye key positions maana ndo wenye mali. Vibali via kz vitolewe kwa kuzingatia sheria ya Employment of non-citizens. Lakini kwa kutathmini nadhani tungeanza na meza ya majadiliano na EAC na SADC ili watanzania wawe na fursa anazotoa hapa nyumbani kwa wawekezaji wageni. South Africa 🇿🇦 tu tunaelewa jinsi zenophobia imewatesa ndugu zetu. Lazima tuelewe rules of the game giving and taking au watu wetu ndo wataumia.
 
Mh. Rais mama samia anaamini kwamba wawekezaji wakija kwa wingi nchini watachangia ukuaji wa uchumi kwa kasi ambapo kwa sasa kinachowakwamisha ni complications zisizo na ulazima, kodi zisizo rafiki na vibali vya kazi kwa wawekezaji.

Kuna watu wanajenga hoja kwamba mtizamo huu wa Mh.Rais utaikosesha nchi mapato na pia utoaji wa vibali vya kazi kwa wageni/ wawekezaji utaathiri ajira za wenyeji.

Naomba kujibu hoja hizi kulingana na ufahamu wangu na wengine wanaweza kuongezea.

Kuhusu kodi
1. Kampuni za kigeni zikiwekewa mazingira rafiki ya kuwekeza nchini, hata kama hazitozwi kodi kubwa katika hatua za awali, kutokana na operesheni zake, hatimaye kuna kodi za aina mbalimbali zitakuja kulipwa.

Kwa mfano, kampuni itaajiri watu kibao, watalipa PAYE, bidhaa zinazozalishwa zitalipiwa VAT, wafanyakazi wa kampuni watakuwa wanapata kipato ambapo watafanya manunuzi ya bidhaaa ambapo watakuwa wanalipa kodi kupitia manunuzi na.k

Hivyo hii itasaidia kukusanya kodi kidogo kidogo lakini kutoka kwenye vyanzo vingi hivyo kuwa na win win situation.

2. Wawekezaji wakiwa wengi kutakuwa na 'economic diversification' na hii itakuwa na positive multiple effects kwenye uchumi wetu.

3. Makampuni yatakayowekeza nchini yatauza bidhaa kwenye nchi nyingine pia, kwa hiyo watu watakuja hapa nchini kununua bidhaa wapeleke kwao. Kwa mfano makampuni ya china ya simu, magari na.k yakiwekeza tanzania yatauza africa nzima, hivyo badala ya wafanyabiashara wa kiafrika kwenda guanzhou, watajaa Tanzania na watalala kwenye mahoteli yetu na kununua matikiti yetu ya mkuranga. Tunapata pesa na kodi.

4. Watanzania kujifunza kutoka kwa wawekezaji. Haya makampuni yakija kwa wingi, tutapata fursa ya kujifunza teknologia n.k. wadogo zetu hawatahangaika sana kuzunguka kutafuta field atachement na lile tatizo la kuwa na na engineers wasioweza kutengeneza chochote kotokana na kusoma theories tu litapungua.

Kuhusu ajira.

1. Makampuni haya hayataajiri wageni tu bali pia wenyeji hasa kwenye nafasi za kazi za jumla kama uhasibu, manunuzi, utawala. Na.k top management pekee ndio watakuwa wenye kampuni au waliochaguliwa na wenye kampuni.

Hili ni muhimu kwa sababu zifuatazo

1. Hakuna mwekezaji yoyote makini anayeweza kukubali kumkabidhi kampuni mtu asiyemjua awe ndio mfanya maamuzi kwa mtaji wa mabilioni. Hata kama ni wewe huwezi kufanya hiyo labda kama una bet mtaji.

2. Waafrica wengi tuna kosa baadhi ya skills za msingi kwenye maeneo flani. Kwa mfano kwenye electronics, ukweli bado tuko nyuma sana na tuliwahi kuyauliza makampuni kadhaa ya electronics kwamba kwa nini wasiwekeze afrika kwa kuwa kuna soko kubwa? Jibu lilikuwa kwamba africa hakuna raslimaliwatu yenye skills nzuri kwenye electeonics na hawaruhusu wachina kuwekeza na kufanya wenyewe kwenye maeneo hayo.

3. Changamoto ya uaminifu. Moja ya shida kubwa inayotukabili wa Tanzania ni suala la uaminifu. Ni rahisi sana kupata mtu mwenye elimu, lakini kupata watu wa aminifu si jambo la kitoto. Kama huamini wekeza pesa mahali halafu weka mbongo azisimamie halafu ulete mrejesho. Kwa hiyo ni vigumu kumlazimisha mwekezaji kuweka meneja asiyemjua vizuri. Hata hivyo kwenye eneo hili bado tunayo fursa ya kujifanyia self improvement na kufanya vizuri.

Kwa ujumla kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji nchini kama alivyosema mh. Rais Samia kuna faida kwa pande zote na tunahitaji wawekezaji kuliko wanavyotuhitaji.

N.b: Mada hii inazungumzia wawekezaji toka nje.
Namba 3 hilo sio tatizo Tanzania tu bali ni africa nzima especially kusini mwa jangwa la sahara.

Ni kweli tunapaswa kujirekebisha au zitungwe sheria kali kwa ajili ya hii changamoto.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Sio kila mwekezaji ni genuine ,

Wengine ni janja janja tu, wanakuja kwa malengo yaliyojificha moja wapo ikiwa kupata ardhi yetu ili wachukulie mikopo kwenye mabenki yao huko nje na kuendelea na mambo mengine

Tusipokua makini tunaweza kuta sehemu kubwa ya ardhi yetu ipo rehani kwenye mabenki ya nje hiyo ni threat kwa national security.
Ukweli mtupu, suala hili watu wanalichukulia poa tu.
 
Mh. Rais mama samia anaamini kwamba wawekezaji wakija kwa wingi nchini watachangia ukuaji wa uchumi kwa kasi ambapo kwa sasa kinachowakwamisha ni complications zisizo na ulazima, kodi zisizo rafiki na vibali vya kazi kwa wawekezaji.

Kuna watu wanajenga hoja kwamba mtizamo huu wa Mh.Rais utaikosesha nchi mapato na pia utoaji wa vibali vya kazi kwa wageni/ wawekezaji utaathiri ajira za wenyeji.

Naomba kujibu hoja hizi kulingana na ufahamu wangu na wengine wanaweza kuongezea.

Kuhusu kodi
1. Kampuni za kigeni zikiwekewa mazingira rafiki ya kuwekeza nchini, hata kama hazitozwi kodi kubwa katika hatua za awali, kutokana na operesheni zake, hatimaye kuna kodi za aina mbalimbali zitakuja kulipwa.

Kwa mfano, kampuni itaajiri watu kibao, watalipa PAYE, bidhaa zinazozalishwa zitalipiwa VAT, wafanyakazi wa kampuni watakuwa wanapata kipato ambapo watafanya manunuzi ya bidhaaa ambapo watakuwa wanalipa kodi kupitia manunuzi na.k

Hivyo hii itasaidia kukusanya kodi kidogo kidogo lakini kutoka kwenye vyanzo vingi hivyo kuwa na win win situation.

2. Wawekezaji wakiwa wengi kutakuwa na 'economic diversification' na hii itakuwa na positive multiple effects kwenye uchumi wetu.

3. Makampuni yatakayowekeza nchini yatauza bidhaa kwenye nchi nyingine pia, kwa hiyo watu watakuja hapa nchini kununua bidhaa wapeleke kwao. Kwa mfano makampuni ya china ya simu, magari na.k yakiwekeza tanzania yatauza africa nzima, hivyo badala ya wafanyabiashara wa kiafrika kwenda guanzhou, watajaa Tanzania na watalala kwenye mahoteli yetu na kununua matikiti yetu ya mkuranga. Tunapata pesa na kodi.

4. Watanzania kujifunza kutoka kwa wawekezaji. Haya makampuni yakija kwa wingi, tutapata fursa ya kujifunza teknologia n.k. wadogo zetu hawatahangaika sana kuzunguka kutafuta field atachement na lile tatizo la kuwa na na engineers wasioweza kutengeneza chochote kotokana na kusoma theories tu litapungua.

Kuhusu ajira.

1. Makampuni haya hayataajiri wageni tu bali pia wenyeji hasa kwenye nafasi za kazi za jumla kama uhasibu, manunuzi, utawala. Na.k top management pekee ndio watakuwa wenye kampuni au waliochaguliwa na wenye kampuni.

Hili ni muhimu kwa sababu zifuatazo

1. Hakuna mwekezaji yoyote makini anayeweza kukubali kumkabidhi kampuni mtu asiyemjua awe ndio mfanya maamuzi kwa mtaji wa mabilioni. Hata kama ni wewe huwezi kufanya hiyo labda kama una bet mtaji.

2. Waafrica wengi tuna kosa baadhi ya skills za msingi kwenye maeneo flani. Kwa mfano kwenye electronics, ukweli bado tuko nyuma sana na tuliwahi kuyauliza makampuni kadhaa ya electronics kwamba kwa nini wasiwekeze afrika kwa kuwa kuna soko kubwa? Jibu lilikuwa kwamba africa hakuna raslimaliwatu yenye skills nzuri kwenye electeonics na hawaruhusu wachina kuwekeza na kufanya wenyewe kwenye maeneo hayo.

3. Changamoto ya uaminifu. Moja ya shida kubwa inayotukabili wa Tanzania ni suala la uaminifu. Ni rahisi sana kupata mtu mwenye elimu, lakini kupata watu wa aminifu si jambo la kitoto. Kama huamini wekeza pesa mahali halafu weka mbongo azisimamie halafu ulete mrejesho. Kwa hiyo ni vigumu kumlazimisha mwekezaji kuweka meneja asiyemjua vizuri. Hata hivyo kwenye eneo hili bado tunayo fursa ya kujifanyia self improvement na kufanya vizuri.

Kwa ujumla kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji nchini kama alivyosema mh. Rais Samia kuna faida kwa pande zote na tunahitaji wawekezaji kuliko wanavyotuhitaji.

N.b: Mada hii inazungumzia wawekezaji toka nje.

Hapo kwenye kwenye ajira kama watakwenda kwa utaratibu wa Mama alivyosema wa muwekezaji kuja au kuleta watu awatakao kwa sababu yeye ndio mwenye hela basi usitegemee kuna mtanzania atapewa ajira kwenye hizo nafasi!
Huo utaratibu wa mwekezaji kuja kufanya atakavyo haupo nchi yeyote duniani!
 
Kwa mujibu wa sheria iliyounda RUBADA, ardhi yote katika bonde la Kilombero iliwekwa chini ya RUBADA bila kujali kuwa kuna mamilioni ya watu kuanzia Kilombero hadi Rufiji walikuwa wanaishi na kumiliki maeneo hayo. Hivyo ilikuwa akitokea mwekezaji anahitaji sehemu yoyote ya ardhi RUBADA wanaitwaa ardhi hiyo toka kwa wananchi na kumuuzia/kumpa mwekezaji huyo bila kujali kuwa wananchi pia wanaihitaji ardh ihiyo wananchi watake wasitake.
Mkuu
Sio Kwamba Ardhi iliwekwa RUBADA kwa ajili ya kulinda mazingira ya maji na sio kwa ajili ya kupewa wawekezaji

Maana hizi Authority za mamlaka za Maji hazitofautiani katika mambo ya ardhi ,
 
Kwa akili yangu ndogo sina pingamizi wawekezaji wa nje kukaribishwa na kuwa na haki ya kuchagua waajiriwa wao wa kigeni kwenye key positions maana ndo wenye mali. Vibali via kz vitolewe kwa kuzingatia sheria ya Employment of non-citizens. Lakini kwa kutathmini nadhani tungeanza na meza ya majadiliano na EAC na SADC ili watanzania wawe na fursa anazotoa hapa nyumbani kwa wawekezaji wageni. South Africa [emoji1221] tu tunaelewa jinsi zenophobia imewatesa ndugu zetu. Lazima tuelewe rules of the game giving and taking au watu wetu ndo wataumia.
Dada Theodora
How can u relate zenophobia na vibali vya kazi? Sio Kwamba Soko la ajira linaongozwa na competitive ya labour force sio upendeleo??
 
Hapo kwenye kwenye ajira kama watakwenda kwa utaratibu wa Mama alivyosema wa muwekezaji kuja au kuleta watu awatakao kwa sababu yeye ndio mwenye hela basi usitegemee kuna mtanzania atapewa ajira kwenye hizo nafasi!
Huo utaratibu wa mwekezaji kuja kufanya atakavyo haupo nchi yeyote duniani!
Aliyesema aje afanye "atakavyo" nani?
 
Back
Top Bottom