Maono ya Rais mama Samia kuhusu uwekezaji nchini kwenye nyuzi 360

Maono ya Rais mama Samia kuhusu uwekezaji nchini kwenye nyuzi 360

Dada Theodora
How can u relate zenophobia na vibali vya kazi? Sio Kwamba Soko la ajira linaongozwa na competitive ya labour force sio upendeleo??
Ni twin issues. Angalia utoaji wa vibali vya kz SA ni strict mno na ndo maana wageni wengi wanafanya kz kinyemela hasa pale ni informal sector. Zenophobia prescribes on their issuance of workpermits na wanasema kabisa wageni wanachukua kz zao. Lkn ukienda kusoma SA utapata kibali kusoma lkn parttime job ngumu sana.

SA wanautaratibu wa kutoa takwimu mara kwa mara za ajira za wazawa - blacks, colored, white, disabled, gay etc
 
Ni twin issues. Angalia utoaji wa vibali vya kz SA ni strict mno na ndo maana wageni wengi wanafanya kz kinyemela hasa pale ni informal sector. Zenophobia prescribes on their issuance of workpermits na wanasema kabisa wageni wanachukua kz zao. Lkn ukienda kusoma SA utapata kibali kusoma lkn parttime job ngumu sana.

SA wanautaratibu wa kutoa takwimu mara kwa mara za ajira za wazawa - blacks, colored, white, disabled, gay etc
Ila Nadhani suala la SA ni controversial katika Zenophobia na vibali vya kazi. Kuna vitu vya kujiuliza je watu wetu hapa mfumo wa elimu unawafanya waajirike?
 
Mkuu
Sio Kwamba Ardhi iliwekwa RUBADA kwa ajili ya kulinda mazingira ya maji na sio kwa ajili ya kupewa wawekezaji

Maana hizi Authority za mamlaka za Maji hazitofautiani katika mambo ya ardhi ,
Usichanganye mamlaka za mabonde ya maji anbazo ziko nane: kazi zake ni kulinda vyanzo vya maji, kutoa vibali vya matumizi ya maji mfano unataka kuchimba kisima, kufanya kilimo cha umwagiliaji. RUBADA iliundwa kwa ajili ya kuendeleza bonde la mto Rufiji kuanzia mto Ruaha kule kilombero mto rufiji hadi unaooingia baharini na kazi yske ilikuwa kutafuta hao wanaiitwa wawekezaji kwa ajili ya kulitumia bonde kulima mazao. Hivyo walipokuwa wakienda kwa wananchi walikuwa wanaenda kibabe na kwa vitisho kuwa sheria inasrma wao ndio wamiliki wa bonde hilo bila kujali watu wameishi maeneo hayo tangu karne kadhaa nyuma. Kwa kweli kuna wananchi wameumizwa sana kwa kunyang"anywa ardhi maeneo hayo. Ukitaka ushahidi ju ya hili soma ripoti za HAKIARDHI ( Ngo) baadhi zinapatikana mtandaoni.

Nakumbuka mkurugenzi wake mmoja hapa mwishoni mwishoni alikuwa anakabiliwa na mashtaka ya kuchukua rushwa ili kuwapa ardhi hao wawekezaji hasa ya Rufiji.
 
Ila Nadhani suala la SA ni controversial katika Zenophobia na vibali vya kazi. Kuna vitu vya kujiuliza je watu wetu hapa mfumo wa elimu unawafanya waajirike?
Elimu yetu ina mapungufu tena siyo madogo lakini informal sector si wanajiajiri? Hizo fursa hasa ndo shida huko. Kwetu hata vibali vya kz wanapewa expatriate salonists lkn huko aisee, ni shida.
 
Mh. Rais mama samia anaamini kwamba wawekezaji wakija kwa wingi nchini watachangia ukuaji wa uchumi kwa kasi ambapo kwa sasa kinachowakwamisha ni complications zisizo na ulazima, kodi zisizo rafiki na vibali vya kazi kwa wawekezaji.

Kuna watu wanajenga hoja kwamba mtizamo huu wa Mh.Rais utaikosesha nchi mapato na pia utoaji wa vibali vya kazi kwa wageni/ wawekezaji utaathiri ajira za wenyeji.

Naomba kujibu hoja hizi kulingana na ufahamu wangu na wengine wanaweza kuongezea.

Kuhusu kodi
1. Kampuni za kigeni zikiwekewa mazingira rafiki ya kuwekeza nchini, hata kama hazitozwi kodi kubwa katika hatua za awali, kutokana na operesheni zake, hatimaye kuna kodi za aina mbalimbali zitakuja kulipwa.

Kwa mfano, kampuni itaajiri watu kibao, watalipa PAYE, bidhaa zinazozalishwa zitalipiwa VAT, wafanyakazi wa kampuni watakuwa wanapata kipato ambapo watafanya manunuzi ya bidhaaa ambapo watakuwa wanalipa kodi kupitia manunuzi na.k

Hivyo hii itasaidia kukusanya kodi kidogo kidogo lakini kutoka kwenye vyanzo vingi hivyo kuwa na win win situation.

2. Wawekezaji wakiwa wengi kutakuwa na 'economic diversification' na hii itakuwa na positive multiple effects kwenye uchumi wetu.

3. Makampuni yatakayowekeza nchini yatauza bidhaa kwenye nchi nyingine pia, kwa hiyo watu watakuja hapa nchini kununua bidhaa wapeleke kwao. Kwa mfano makampuni ya china ya simu, magari na.k yakiwekeza tanzania yatauza africa nzima, hivyo badala ya wafanyabiashara wa kiafrika kwenda guanzhou, watajaa Tanzania na watalala kwenye mahoteli yetu na kununua matikiti yetu ya mkuranga. Tunapata pesa na kodi.

4. Watanzania kujifunza kutoka kwa wawekezaji. Haya makampuni yakija kwa wingi, tutapata fursa ya kujifunza teknologia n.k. wadogo zetu hawatahangaika sana kuzunguka kutafuta field atachement na lile tatizo la kuwa na na engineers wasioweza kutengeneza chochote kotokana na kusoma theories tu litapungua.

Kuhusu ajira.

1. Makampuni haya hayataajiri wageni tu bali pia wenyeji hasa kwenye nafasi za kazi za jumla kama uhasibu, manunuzi, utawala. Na.k top management pekee ndio watakuwa wenye kampuni au waliochaguliwa na wenye kampuni.

Hili ni muhimu kwa sababu zifuatazo

1. Hakuna mwekezaji yoyote makini anayeweza kukubali kumkabidhi kampuni mtu asiyemjua awe ndio mfanya maamuzi kwa mtaji wa mabilioni. Hata kama ni wewe huwezi kufanya hiyo labda kama una bet mtaji.

2. Waafrica wengi tuna kosa baadhi ya skills za msingi kwenye maeneo flani. Kwa mfano kwenye electronics, ukweli bado tuko nyuma sana na tuliwahi kuyauliza makampuni kadhaa ya electronics kwamba kwa nini wasiwekeze afrika kwa kuwa kuna soko kubwa? Jibu lilikuwa kwamba africa hakuna raslimaliwatu yenye skills nzuri kwenye electeonics na hawaruhusu wachina kuwekeza na kufanya wenyewe kwenye maeneo hayo.

3. Changamoto ya uaminifu. Moja ya shida kubwa inayotukabili wa Tanzania ni suala la uaminifu. Ni rahisi sana kupata mtu mwenye elimu, lakini kupata watu wa aminifu si jambo la kitoto. Kama huamini wekeza pesa mahali halafu weka mbongo azisimamie halafu ulete mrejesho. Kwa hiyo ni vigumu kumlazimisha mwekezaji kuweka meneja asiyemjua vizuri. Hata hivyo kwenye eneo hili bado tunayo fursa ya kujifanyia self improvement na kufanya vizuri.

Kwa ujumla kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji nchini kama alivyosema mh. Rais Samia kuna faida kwa pande zote na tunahitaji wawekezaji kuliko wanavyotuhitaji.

N.b: Mada hii inazungumzia wawekezaji toka nje.
Mkuu nakubaliana na wew kwa asilimia kubwa sana,
Ishu kubwa ni kuwaruhusu hawa wawekezaji wa njee, ndo wana mitaji mikubwa na wana skill ya business

Sent using Jamii Forums mobile app
 
JK aliziacha Halmashauri kukusanya mapato zenyewe na kukipangia miradi ya maenseleo kwenye maeneo yao.

Magufuri mapato yake yalichanganya mpaka fedha za Halmashauri ndiyo maana unaona ziko juu kidogo. Halafu mipango ikapangwa kutokea Serikali Kuu.

Hapo ndiyo utakuta kwenu mliokusanya fedha nyingi hamna barabara wakati Chato kwenye makusanyo madogo wanajengewa Airport
Baada ya Halmashauri kujipangia maendeleo gani zilifanya?
Je anaenda kubadili sheria za kodi au maneno ya kisiasa tu sheria ni zile zile?
 
Usichanganye mamlaka za mabonde ya maji anbazo ziko nane: kazi zake ni kulinda vyanzo vya maji, kutoa vibali vya matumizi ya maji mfano unataka kuchimba kisima, kufanya kilimo cha umwagiliaji. RUBADA iliundwa kwa ajili ya kuendeleza bonde la mto Rufiji kuanzia mto Ruaha kule kilombero mto rufiji hadi unaooingia baharini na kazi yske ilikuwa kutafuta hao wanaiitwa wawekezaji kwa ajili ya kulitumia bonde kulima mazao. Hivyo walipokuwa wakienda kwa wananchi walikuwa wanaenda kibabe na kwa vitisho kuwa sheria inasrma wao ndio wamiliki wa bonde hilo bila kujali watu wameishi maeneo hayo tangu karne kadhaa nyuma. Kwa kweli kuna wananchi wameumizwa sana kwa kunyang"anywa ardhi maeneo hayo. Ukitaka ushahidi ju ya hili soma ripoti za HAKIARDHI ( Ngo) baadhi zinapatikana mtandaoni.

Nakumbuka mkurugenzi wake mmoja hapa mwishoni mwishoni alikuwa anakabiliwa na mashtaka ya kuchukua rushwa ili kuwapa ardhi hao wawekezaji hasa ya Rufiji.
Nakumbuka haki ardhi walikumbwa Sana na hili since 2013....ukisoma majarida yao utapata maarifa
 
Elimu yetu ina mapungufu tena siyo madogo lakini informal sector si wanajiajiri? Hizo fursa hasa ndo shida huko. Kwetu hata vibali vya kz wanapewa expatriate salonists lkn huko aisee, ni shida.
Lakini Hoja yako nikuwa lazima tulinde ajira za ndani lakini lazima policy ziendane na soko linasemaje au Sio Dada Theodora
 
Lakini Hoja yako nikuwa lazima tulinde ajira za ndani lakini lazima policy ziendane na soko linasemaje au Sio Dada Theodora
On Point. Na tuko tayari kudialogue na nchi nyingine majirani kwenye labour's market policies for symbiotic relations.
 
On Point. Na tuko tayari kudialogue na nchi nyingine majirani kwenye labour's market policies for symbiotic relations.
Lakini Diplomasia ya uchumi ni muhimu sana angalia mipaka ya Tanzania na kenya kaskazini juu ya mahindi.
 
Baada ya Halmashauri kujipangia maendeleo gani zilifanya?
Je anaenda kubadili sheria za kodi au maneno ya kisiasa tu sheria ni zile zile?
Rudi kijijini kwako kaangalie yaliyofanyika kabla ya 2015
 
Wakati wa mkapa, mwinyi na Nyerere ilikuwa inakusanywa kiasi gani kwa kila mmoja wao kwa mwezi
Wakati wa JK huo si ndio ujinga uliokuwa unafanyika na kodi ilikuwa ni 800bn kwa mwezi wastani, SSH hana maoni, kodi lazima ikusanye kwa sheria kama anaona kodi ni kubwa abadilishe sheria, vinginevyo anatengeneza mazingira ya wafanyabiashara kukataa kulipa kodi halali kabisa.
 
Leo, Mh. Rais amekutana na Wawekezaji kutoka China ambao wameahidi kufanya uwekezaji mkubwa Tanzania kwa kufungua Industrial parks na kuwekeza kwenye kutengeneza Magari, Simu na Madawa Miongozi mwa mambo mengine.

Siku chache zilizopita tulishauri wawekezaji hasa kutoka China washawishiwe kuwekeza nchi hasa kwenye maeneo hayo hapo juu halafu wafanyabiasha kutoka nchi nyingine za kiafrika waje kununilia Tanzania badala ya kwenda China ambapo tutapata faida za aina nyingi.

Tunampongeza Mhe. Rais kwa hatua hii ambayo itasaidia kuzalisha ajira kwa vijana na tunamuombea kila la heri.
 
Mh. Rais mama samia anaamini kwamba wawekezaji wakija kwa wingi nchini watachangia ukuaji wa uchumi kwa kasi ambapo kwa sasa kinachowakwamisha ni complications zisizo na ulazima, kodi zisizo rafiki na vibali vya kazi kwa wawekezaji.

Kuna watu wanajenga hoja kwamba mtizamo huu wa Mh.Rais utaikosesha nchi mapato na pia utoaji wa vibali vya kazi kwa wageni/ wawekezaji utaathiri ajira za wenyeji.

Naomba kujibu hoja hizi kulingana na ufahamu wangu na wengine wanaweza kuongezea.

Kuhusu kodi
1. Kampuni za kigeni zikiwekewa mazingira rafiki ya kuwekeza nchini, hata kama hazitozwi kodi kubwa katika hatua za awali, kutokana na operesheni zake, hatimaye kuna kodi za aina mbalimbali zitakuja kulipwa.

Kwa mfano, kampuni itaajiri watu kibao, watalipa PAYE, bidhaa zinazozalishwa zitalipiwa VAT, wafanyakazi wa kampuni watakuwa wanapata kipato ambapo watafanya manunuzi ya bidhaaa ambapo watakuwa wanalipa kodi kupitia manunuzi na.k

Hivyo hii itasaidia kukusanya kodi kidogo kidogo lakini kutoka kwenye vyanzo vingi hivyo kuwa na win win situation.

2. Wawekezaji wakiwa wengi kutakuwa na 'economic diversification' na hii itakuwa na positive multiple effects kwenye uchumi wetu.

3. Makampuni yatakayowekeza nchini yatauza bidhaa kwenye nchi nyingine pia, kwa hiyo watu watakuja hapa nchini kununua bidhaa wapeleke kwao. Kwa mfano makampuni ya china ya simu, magari na.k yakiwekeza tanzania yatauza africa nzima, hivyo badala ya wafanyabiashara wa kiafrika kwenda guanzhou, watajaa Tanzania na watalala kwenye mahoteli yetu na kununua matikiti yetu ya mkuranga. Tunapata pesa na kodi.

4. Watanzania kujifunza kutoka kwa wawekezaji. Haya makampuni yakija kwa wingi, tutapata fursa ya kujifunza teknologia n.k. wadogo zetu hawatahangaika sana kuzunguka kutafuta field atachement na lile tatizo la kuwa na na engineers wasioweza kutengeneza chochote kotokana na kusoma theories tu litapungua.

Kuhusu ajira.

1. Makampuni haya hayataajiri wageni tu bali pia wenyeji hasa kwenye nafasi za kazi za jumla kama uhasibu, manunuzi, utawala. Na.k top management pekee ndio watakuwa wenye kampuni au waliochaguliwa na wenye kampuni.

Hili ni muhimu kwa sababu zifuatazo

1. Hakuna mwekezaji yoyote makini anayeweza kukubali kumkabidhi kampuni mtu asiyemjua awe ndio mfanya maamuzi kwa mtaji wa mabilioni. Hata kama ni wewe huwezi kufanya hiyo labda kama una bet mtaji.

2. Waafrica wengi tuna kosa baadhi ya skills za msingi kwenye maeneo flani. Kwa mfano kwenye electronics, ukweli bado tuko nyuma sana na tuliwahi kuyauliza makampuni kadhaa ya electronics kwamba kwa nini wasiwekeze afrika kwa kuwa kuna soko kubwa? Jibu lilikuwa kwamba africa hakuna raslimaliwatu yenye skills nzuri kwenye electeonics na hawaruhusu wachina kuwekeza na kufanya wenyewe kwenye maeneo hayo.

3. Changamoto ya uaminifu. Moja ya shida kubwa inayotukabili wa Tanzania ni suala la uaminifu. Ni rahisi sana kupata mtu mwenye elimu, lakini kupata watu wa aminifu si jambo la kitoto. Kama huamini wekeza pesa mahali halafu weka mbongo azisimamie halafu ulete mrejesho. Kwa hiyo ni vigumu kumlazimisha mwekezaji kuweka meneja asiyemjua vizuri. Hata hivyo kwenye eneo hili bado tunayo fursa ya kujifanyia self improvement na kufanya vizuri.

Kwa ujumla kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji nchini kama alivyosema mh. Rais Samia kuna faida kwa pande zote na tunahitaji wawekezaji kuliko wanavyotuhitaji.

N.b: Mada hii inazungumzia wawekezaji toka nje.
Wakati wa Jakaya wawekezaji walikuwa kibao ,tulipata nini?,acheni masihara na hii nchi,sana tutarudi kuwa shamba la bibi tu.

Bila kukazia suala la mikataba kwa umakini dhidi ya wawekezaji kwa taifa na kukusanya kodi bila mzaha kama alivyofanya hayati Magufuli ni bure tu.
Mfano kampuni ya Barrick Gold Mine na kina Acasia walikuwepo ,hatukupata kodi stahiki na walikuwa wakipora tu,usishangae kampuni zikajaa kodi usizione
 
JK aliziacha Halmashauri kukusanya mapato zenyewe na kukipangia miradi ya maenseleo kwenye maeneo yao.

Magufuri mapato yake yalichanganya mpaka fedha za Halmashauri ndiyo maana unaona ziko juu kidogo. Halafu mipango ikapangwa kutokea Serikali Kuu.

Hapo ndiyo utakuta kwenu mliokusanya fedha nyingi hamna barabara wakati Chato kwenye makusanyo madogo wanajengewa Airport
Miradi gani ya maana halimashauri hizo zilifanya ?,ebho !,
Magufuli ndani ya muda mfupi tu tumeona matokeo ,
Kipindi cha Jakaya halishauri gani zilifanya miradi ya maana ?,acheni ujinga
 
Wakati wa Jakaya wawekezaji walikuwa kibao ,tulipata nini?,acheni masihara na hii nchi,sana tutarudi kuwa shamba la bibi tu.

Bila kukazia suala la mikataba kwa umakini dhidi ya wawekezaji kwa taifa na kukusanya kodi bila mzaha kama alivyofanya hayati Magufuli ni bure tu.
Mfano kampuni ya Barrick Gold Mine na kina Acasia walikuwepo ,hatukupata kodi stahiki na walikuwa wakipora tu,usishangae kampuni zikajaa kodi usizione
Mkuu, ungesoma kwanza hoja zilizotolewa kwenye bandiko la msingi ndio uchangie. Majibu ya maswali yako yote yalishajibiwa kwenye post Na. 1.

Pia ni ajabu kama wewe huoni umuhimu wa kukuza uwekezaji na kukua kwa uchumi. Nadhani ni suala la uelewa tu.
 
Miradi gani ya maana halimashauri hizo zilifanya ?,ebho !,
Magufuli ndani ya muda mfupi tu tumeona matokeo ,
Kipindi cha Jakaya halishauri gani zilifanya miradi ya maana ?,acheni ujinga
Kwa namna unavyoandika kama bata anakunya, inaonekana kabisa wewe siyo mtu MAKINI. Kuendelea na mjadala huu na wewe tutakuwa tunakuumiza bure.

Tafuta majukwa ya darasa la 7, Ila hapa siyo pako
 
Back
Top Bottom