Maono ya Ujerumani Kuhusu Afrika Kabla ya 1884

Maono ya Ujerumani Kuhusu Afrika Kabla ya 1884

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,048
Reaction score
22,790
Sote tunaelewa kuwa mkutano wa Berlin wa mwaka 1984 ndio ulioigawa Afrika kuwa katika mipaka tuliyo nayo leo. Mkutano huo uliitishwa na Otto von Bismarck ili kuigawa Afrika miongoni mwa mataifa ya Ulaya ambayo tayari yalikuwa yana infleunce Afrika kwa nia ya kuondoa conflicts. Ujerumani ilikuwa na influence katika sehemu tatu: Cameroon, Namibia na hapa kwetu Deutsch-Ostafrika.

Nia kuu ya Bismark ilikuwa ni kuigawa sehemu ya Afrika kusini mwa jangwa la Sahara katika vipande vinavyoanzia bahari ya Atlantic na kuishia bahari ya Hindi. Plani yake ilikuwa ni kuwa kuanzia Cameroon hadi Zanzibar ingekuwa nchi moja chini ya Ujerumani, halafu kuanzia Congo Brazaville hadi Msumbiji ya kasikazini ingekuwa nchi moja chini ya Ubelgiji, na kuanzia Angola hadi Mozambique ingekuwa nchi moja chini ya Ureno, halafu sehemu nyingine yote ya kusini mwa Afrika ingebaki chini ya Uingereza. Kwa plani hiyo Ramani ya Africa leo hii ingekuwa hivi:

1629757338078.png


Plani hiyo haikukubaliwa na mataifa mengine ya Ulaya hasa Mfalme Leopord wa Ubeligiji hakutaka kupoteza sehemu ya Kongo ambayo alikuwa amejimilikisha yeye binafsi, na halafu kukawa na ubishi mwingine kuhusu mgawanyo ambao ungeiweka Kenya, Uganda, sehemu ya kaskazini mwa Kongo, Central African Republic, Chad na na Nigeria chini ya mamlaka moja. Ukawa mvutano mkali kati ya Uingereza na Ufaransa. Mwingereza hakutaka kupoteza Uganda kwa vile ndicho chanzo cha mto Nile, na Mfaransa naye hakutaka kupoteza kipande chochote cha Afrika kwani kama plani hiyo ingeendelea, mfaransa angebaki mikono mitupu.

Halafu snag nyingine ikawa ni kuwa Waingereza nao hawakutaka kupoteza sehemu ya Zambia na Zimbabwe kwa vile ilikuwa inamilikiwa na kampuni ya Rhodes ambayo ilikuwa imeanzisha migodi kule. Kwa hiyo plani nzima ya Bismarck ikafeli, ndipo wakaamua kukata vipande vipande tuvionavyo leo. Hata hivyo Bismarck hakutaka kusindwa kirahisi, badala yake akaishawishi Uingereza ikubali kuchukua visiwa vya Zanzibar ili wabadilishane na visiwa vya Heligoland, na vile vile wabadilishe mpaka wa Namibia ili ufikie mto Zambezi, akijua kuwa kwa kutumia mto Zambezi angeweza kufikia bahari ya Hindi kirahisi bila kuzunguka Cape of Good Hope. Kwa hiyo Mpaka wa Nambia ukabidilishwa na kuwa na kale kasehemu kembamba kanakofikia mto Zambezi kama ionekanvyo kwenye ramani hapa.

1629758320475.png


Wakati huo Uingereza ilikuwa inajua kuwa mto Zambezi hauwezi kutumika kwa usafiri wa meli kwa vile kulikuwa na Victoria falls mpakani mwa Zambia na Zimbabwe, ila wakawakubalia wajerumani haraka haraka kusudi wabaki na umiliki Kenya, Uganda, Zambia na Zimbabwe ambazo walikuwa na hatari ya kupoteza kwenye mkutano huo.

Sijui kama plani ya Bismarck ingefanikiwa huenda siku moja tungetawaliwa na Paul Biya, au Mobutu au Ngueso. Vile vile watu maarufu kama Roger Milla, Diblo Dibala, Abeti Maskini na Ndungidi wangekuwa watu wetu.
 
Natamani angebakia Mjerumani kututawala badala ya Muingereza, maana tungenyooka kisawasawa.

Katika kipindi kifupi alichotawala alifanya mambo mengi ya kuijenga Tanganyika ukilinganisha na Muingereza. Pia ukifanya uzembe kama vile kuchelewa kazini ilikuwa ni viboko 11 bila utani. Kwa hivyo nina imani tungekuwa na discipline ya kutosha.

Nikiiangalia Namibia ilivyokuwa jangwa lakini maendeleo yake ni makubwa kuliko sisi tuliokuwa na resources tele tele.
 
Sote tunaelewa kuwa mkutano wa Berlin wa mwaka 1984 ndio ulioigawa Afrika kuwa katika mipaka tuliyo nayo leo. Mkutano huo uliitishwa na Otto von Bismarck ili kuigawa Afrika miongoni mwa mataifa ya Ulaya ambayo tayari yalikuwa yana infleunce Afrika kwa nia ya kuondoa conflicts. Ujerumani ilikuwa na influence katika sehemu tatu: Cameroon, Namibia na hapa kwetu Deutsch-Ostafrika.

Nia kuu ya Bismark ilikuwa ni kuigawa sehemu ya Afrika kusini mwa jangwa la Sahara katika vipande vinavyoanzia bahari ya Atlantic na kuishia bahari ya Hindi. Plani yake ilikuwa ni kuwa kuanzia Cameroon hadi Zanzibar ingekuwa nchi moja chini ya Ujerumani, halafu kuanzia Congo Brazaville hadi Msumbiji ya kasikazini ingekuwa nchi moja chini ya Ubelgiji, na kuanzia Angola hadi Mozambique ingekuwa nchi moja chini ya Ureno, halafu sehemu nyingine yote ya kusini mwa Afrika ingebaki chini ya Uingereza.

Plani hiyo haikukubaliwa na mataifa mengine ya Ulaya hasa Mfalme Leopord wa Ubeligiji hakutaka kupoteza sehemu ya Kongo
Asante kwa kutueleza mawazo yako lakini naomba uniruhusu kupinga mawazo kadhaa:
1. Mkutano wa Berlin wa 1885 haukugawa Afrika. Ugawaji huo uliwahi kuanza kidogo kabla na hasa kufuata baada ya mkutano. Uliweka kanuni kadhaa zilizolenga kupunguza hatari ya ugomvi kati nchi za Ulaya wakati zikikutana kwenye bara la Afrika. Kwa njia hiyo mkutano uliandaa ugawaji wa Afrika.

2. Kuhusu habari za kimsingi soma hapa: Mkutano wa Berlin wa 1885 - Wikipedia, kamusi elezo huru, hasa kifungu kuhusu "Maazimio". Maazimio ya mkutano ka Kiingereza utapata hapa kama pdf: https://loveman.sdsu.edu/docs/1885GeneralActBerlinConference.pdf, pia hapa ikifupishwa kidogo: (1885) General Act of the Conference of Berlin •.

3. Bismarck (mkuu wa serikali ya Ujerumani) hakuwa na mipango yoyote kuhusu Afrika. Mwanzoni alikataa majaribio ya kuunda koloni za Kijerumani. Baadaye alikasirika juu ya Waingereza na Wafaransa jinsi walivyojaribu kugawa maeneo ya Afrika ya Magharibi kwa ajili ya wafanya biashara yao wakibagua wafanya biashara Wajerumani, hivyo kwenye mwaka 1884 alikubali mikataba ifanywe na machifu na wafalme huko Togo, Kamerun na Namibia. Karl Peters, alipoelekea Afrika ya Mashariki kwa shabaha ya kuunda koloni, alionywa rasmi na serikali ya Bismark asiendelee. (Peters aliporudi baada ya mkutano na karatasi za mikataba na machifu wa Tanganyika, Bismarck alisitasita kuikubali hadi Peters alitishia angetafuta kibali cha mfalme wa Ubelgiji...)

3. Mara utaratibu ulikubaliwa katika maazimio ya mkutano wa Berlin kuhusu namna ya kutwaa maeneo katika Afrika, mashindano yalianza haraka sana (scramble for Afrika) kujipatia kipande...
 
Waafrika tunaonewa na kila jamii makima sisi.[emoji23][emoji23]



Lunatic [emoji2957][emoji2957][emoji2957]
 
Asante kwa kutueleza mawazo yako lakini naomba uniruhusu kupinga mawazo kadhaa:
1. Mkutano wa Berlin wa 1885 haukugawa Afrika. Ugawaji huo uliwahi kuanza kidogo kabla na hasa kufuata baada ya mkutano. Uliweka kanuni kadhaa zilizolenga kupunguza hatari ya ugomvi kati nchi za Ulaya wakati zikikutana kwenye bara la Afrika. Kwa njia hiyo mkutano uliandaa ugawaji wa Afrika.

2. Kuhusu habari za kimsingi soma hapa: Mkutano wa Berlin wa 1885 - Wikipedia, kamusi elezo huru, hasa kifungu kuhusu "Maazimio". Maazimio ya mkutano ka Kiingereza utapata hapa kama pdf: https://loveman.sdsu.edu/docs/1885GeneralActBerlinConference.pdf, pia hapa ikifupishwa kidogo: (1885) General Act of the Conference of Berlin •.

3. Bismarck (mkuu wa serikali ya Ujerumani) hakuwa na mipango yoyote kuhusu Afrika. Mwanzoni alikataa majaribio ya kuunda koloni za Kijerumani. Baadaye alikasirika juu ya Waingereza na Wafaransa jinsi walivyojaribu kugawa maeneo ya Afrika ya Magharibi kwa ajili ya wafanya biashara yao wakibagua wafanya biashara Wajerumani, hivyo kwenye mwaka 1884 alikubali mikataba ifanywe na machifu na wafalme huko Togo, Kamerun na Namibia. Karl Peters, alipoelekea Afrika ya Mashariki kwa shabaha ya kuunda koloni, alionywa rasmi na serikali ya Bismark asiendelee. (Peters aliporudi baada ya mkutano na karatasi za mikataba na machifu wa Tanganyika, Bismarck alisitasita kuikubali hadi Peters alitishia angetafuta kibali cha mfalme wa Ubelgiji...)

3. Mara utaratibu ulikubaliwa katika maazimio ya mkutano wa Berlin kuhusu namna ya kutwaa maeneo katika Afrika, mashindano yalianza haraka sana (scramble for Afrika) kujipatia kipande...
1. Mkutano wa Berlin kuhusu Africa ni historia inayojulika duniani kote; uliitishwa na Bismarck kwa kushirikiana na mflame wa Ureno. Wote walitaka himayo zao zianzie bahari ya Atlantic mpaka Bahari ya Hindi. Mreno aunganishe Angola na Msubiji, na Mjerumani naye unganise Cameroon na Deutsch-Ostafrika. Wengine ndio waliokataa wazo hilo; hata hivyo wakakubaliana kuwa matumizi ya maji ya mto Kongo iwa ni halali kwa mataifa yote
2. Ingawa tayari Africa ilishavamiwa, hakukuwa na mipaka inayotambulika, ni kutokana na mkutano ule ndipo wakaigawa afrika katika mipaka inayotambulika karibu mpaka leo. Karl Peters alikuja kwetu kabla ya mkutano huo wa Berlin, na wakati huo tayari Ujerumani ilishaichukua Namibia, na Kamerun, na ilikuwa mbioni mbioni kuichukua nchi yetu. Tunamjua karl Peters zaid kwa ajili ya mikataba yake, lakini kulikuwa na contingent kubwa la wajerumani waliokujan kufanya exploration na kuikamata nchi. Ingechukuliwa bila hata kuwapo kwa mikataba ya akina mangungo.
3. Siyo kwamba baada ya mkutano ndipo waliopanza mashindano ya kuivamia Afrika, Mwaka 1884 tayari eneo lote la Africa lilikuwa limeshavamiwa na wazungu isipokuwa Ethiopia tu; mkutano wa berlini ndio ulioweka mipaka
4. mambo mengine naona unaongelea maazimio ya mkutano huo baada ya kukataa maoni ya Bismark kuhusu mipaka itakayowezesha nchi kuwa na access na Bahari ya Atlantic na Bahari ya Hindi kwa eneo la kusini mwa sahara.
5. Ni kutokana na kushindikana kwa plani hiyo ndipo Ramani ya Namibia ikachorwa vile ili Ujerumani iweze kuwa na access na bahari ya Hindi kupitia mto Zamabezi.

Usipokubaliana na facts hizo, fine.
 
Tulitaka kuiua mipaka hii kwa njia yetu ya kuwaunganisha vijana wetu kupitia Sanaa, wakatuhujumu. Unaikumbuka "Kora Africa"?
Ili tamasha ilikuaje likapotea
Lilikua likifanyika sun city sa nakumbuka
 
1. Mkutano wa Berlin kuhusu Africa ni historia inayojulika duniani kote; uliitishwa na Bismarck kwa kushirikiana na mflame wa Ureno. Wote walitaka himayo zao zianzie bahari ya Atlantic mpaka Bahari ya Hindi. Mreno aunganishe Angola na Msubiji, na Mjerumani naye unganise Cameroon na Deutsch-Ostafrika. Wengine ndio waliokataa wazo hilo; hata hivyo wakakubaliana kuwa matumizi ya maji ya mto Kongo iwa ni halali kwa mataifa yote
2. Ingawa tayari Africa ilishavamiwa, hakukuwa na mipaka inayotambulika, ni kutokana na mkutano ule ndipo wakaigawa afrika katika mipaka inayotambulika karibu mpaka leo. Karl Peters alikuja kwetu kabla ya mkutano huo wa Berlin, na wakati huo tayari Ujerumani ilishaichukua Namibia, na Kamerun, na ilikuwa mbioni mbioni kuichukua nchi yetu. Tunamjua karl Peters zaid kwa ajili ya mikataba yake, lakini kulikuwa na contingent kubwa la wajerumani waliokujan kufanya exploration na kuikamata nchi. Ingechukuliwa bila hata kuwapo kwa mikataba ya akina mangungo.
3. Siyo kwamba baada ya mkutano ndipo waliopanza mashindano ya kuivamia Afrika, Mwaka 1884 tayari eneo lote la Africa lilikuwa limeshavamiwa na wazungu isipokuwa Ethiopia tu; mkutano wa berlini ndio ulioweka mipaka
4. mambo mengine naona unaongelea maazimio ya mkutano huo baada ya kukataa maoni ya Bismark kuhusu mipaka itakayowezesha nchi kuwa na access na Bahari ya Atlantic na Bahari ya Hindi kwa eneo la kusini mwa sahara.
5. Ni kutokana na kushindikana kwa plani hiyo ndipo Ramani ya Namibia ikachorwa vile ili Ujerumani iweze kuwa na access na bahari ya Hindi kupitia mto Zamabezi.

Usipokubaliana na facts hizo, fine.
Ndugu, kile kitu unachoita "fact" hakipatikani kwa kusema au kutaka. "Facts" zako hazipo. Nimeshakupatia matini ya maazimo ya Mkutano wa Berlin. Ndani yake hakuna ugawaji wa maeneo maalum (isipokuwa kuhusu Kongo).
Kuhusu siasa ya Ujerumani mambo ni wazi. Nchi hiyo iliteleza katika ukoloni wake bila mpango wowote. Kulikwa na mataifa yaliyotaka koloni kimsingi kama jambo la heshima la kitaifa (UIifaransa na Italia) au koloni maalumu tu (Uingereza), ama wakiona faida au kwa kuzuia wengine wasipate. Ujerumani ilipata koloni zake bila mpango.
Ona hapa hitimisho ya siasa ya Bismarck katika miaka kabla ya mkutano wa Berlin: "Bismarck had opposed colonial acquisitions, arguing that the burden of obtaining, maintaining, and defending such possessions would outweigh any potential benefit. He felt that colonies did not pay for themselves, that the German formal bureaucratic system would not work well in the easy-going tropics, and that the diplomatic disputes colonies brought would distract Germany from its central interest, Europe itself."
Hapa maneno ya Bismarck mwenyewe 1884: " I have not abandoned my former aversion to colonies .. which make a strip of land their foundation, and then seek to draw emigrants, appoint officials, and establish garrisons. This mode of colonization may be good for other countries, but it is not practicable for us. I do not believe that colonial projects can be artificially established" (chanzo hapa)
Kuanzia 1883 Bismarck alibadilika akikasirika kuhusu mapatano ya Uingereza na Ufaransa katika Afrika ya Magharibi walipolenga kugawana nafasi kati ya wafanyabiashara yao akiona wanaonea wafanyabiashara Wajerumani. Hapo alikubali 1884 kuidhinisha mikataba kati ya makampuni ya Kijerumani na wafalme au machifu huko Togo, Kamerun, Namibia na Papua Guinea Mpya. Aliamini angeweza kutoa waraka wa ulinzi halafu kuwaachia wafanyabiashara waendeshe maeneo hayo wenyewe. Hakutaka kutuma askari ng'ambo, aliamini nchi ingepata faida ya kibiashara bila hatua hiyo. Hii ni sababu kwamba koloni za Ujerumani hazikuitwa "koloni" bali "maeneo ya kulindwa" (Schutzgebiete), na pia jeshi la kikoloni likaitwa "Schutztruppe" (jeshi la ulinzi). Ingawa hali halisi zilikuwa koloni.

Wakati Peters alipoondoka kuelekea Afrika ya Mashariki alionywa rasmi na serikali ya Bismarck kuwa hawezi kutegemea ulinzi wa Ujerumani. Peters mwenyewe alilalamika katika kitabu juuy a maisha yake "Niliposafiri 1884 pamoja na wenzangu kwenda Zanzibar, serikali ya Kijerumani haikutaka kusikia habari za koloni katika Afrika ya Mashariki ikajaribu yote yaliyowezekana kutuzuia". (Chanzo: Karl Peters: Die Gründung von Deutsch-Ostafrika.« Hamburg, Rüsch'sche Verlagsbuchhandlung 1906, online hapa).
Bismarck alibadilika msimamo kwa sababu 2: 1) aliona katika uchaguzi uliokaribia, vyama vilivyopigania ukoloni vitaongezeka nguvu, ata vihitaji; 2) Peters alitisha kama serikali yake isingekubali "mikataba" yake, angejiunga na mfalme wa Ubelgiji. Basi Peters alipata waraka wa ulinzi kutoka serikali iliokuwa msingi wa koloni ya baadaye.

Kuna maneno ya Bismarck aliyosema 1888 yanayoonyesha hakuwa na raha kuhusu koloni; aliombwa kuingilia katika katika vurugu ya Emin Pasha pale Sudan Kusini. Alijibu: "Ramani yako ya Afrika ni ya kuvutia sana. Lakini ramani yangu ya Afrika iko Ulaya. Ufaransa iko upande wa kushoto, Urusi upande wa kulia, katikati tuko sisi".

Sasa nimeleta ushahidi mara mbili katika maneno ya wenyewe kwamba hapakuwa na mpango wa kuunda koloni kubwa ya Kijerumani jinsi uzlivyodai.
Basi lete ushahidi wako!!!
 
Ndugu, kile kitu unachoita "fact" hakipatikani kwa kusema au kutaka. "Facts" zako hazipo. Nimeshakupatia matini ya maazimo ya Mkutano wa Berlin. Ndani yake hakuna ugawaji wa maeneo maalum (isipokuwa kuhusu Kongo).
Kuhusu siasa ya Ujerumani mambo ni wazi. Nchi hiyo iliteleza katika ukoloni wake bila mpango wowote. Kulikwa na mataifa yaliyotaka koloni kimsingi kama jambo la heshima la kitaifa (UIifaransa na Italia) au koloni maalumu tu (Uingereza), ama wakiona faida au kwa kuzuia wengine wasipate. Ujerumani ilipata koloni zake bila mpango.
Ona hapa hitimisho ya siasa ya Bismarck katika miaka kabla ya mkutano wa Berlin: "Bismarck had opposed colonial acquisitions, arguing that the burden of obtaining, maintaining, and defending such possessions would outweigh any potential benefit. He felt that colonies did not pay for themselves, that the German formal bureaucratic system would not work well in the easy-going tropics, and that the diplomatic disputes colonies brought would distract Germany from its central interest, Europe itself."
Hapa maneno ya Bismarck mwenyewe 1884: " I have not abandoned my former aversion to colonies .. which make a strip of land their foundation, and then seek to draw emigrants, appoint officials, and establish garrisons. This mode of colonization may be good for other countries, but it is not practicable for us. I do not believe that colonial projects can be artificially established" (chanzo hapa)
Kuanzia 1883 Bismarck alibadilika akikasirika kuhusu mapatano ya Uingereza na Ufaransa katika Afrika ya Magharibi walipolenga kugawana nafasi kati ya wafanyabiashara yao akiona wanaonea wafanyabiashara Wajerumani. Hapo alikubali 1884 kuidhinisha mikataba kati ya makampuni ya Kijerumani na wafalme au machifu huko Togo, Kamerun, Namibia na Papua Guinea Mpya. Aliamini angeweza kutoa waraka wa ulinzi halafu kuwaachia wafanyabiashara waendeshe maeneo hayo wenyewe. Hakutaka kutuma askari ng'ambo, aliamini nchi ingepata faida ya kibiashara bila hatua hiyo. Hii ni sababu kwamba koloni za Ujerumani hazikuitwa "koloni" bali "maeneo ya kulindwa" (Schutzgebiete), na pia jeshi la kikoloni likaitwa "Schutztruppe" (jeshi la ulinzi). Ingawa hali halisi zilikuwa koloni.

Wakati Peters alipoondoka kuelekea Afrika ya Mashariki alionywa rasmi na serikali ya Bismarck kuwa hawezi kutegemea ulinzi wa Ujerumani. Peters mwenyewe alilalamika katika kitabu juuy a maisha yake "Niliposafiri 1884 pamoja na wenzangu kwenda Zanzibar, serikali ya Kijerumani haikutaka kusikia habari za koloni katika Afrika ya Mashariki ikajaribu yote yaliyowezekana kutuzuia". (Chanzo: Karl Peters: Die Gründung von Deutsch-Ostafrika.« Hamburg, Rüsch'sche Verlagsbuchhandlung 1906, online hapa).
Bismarck alibadilika msimamo kwa sababu 2: 1) aliona katika uchaguzi uliokaribia, vyama vilivyopigania ukoloni vitaongezeka nguvu, ata vihitaji; 2) Peters alitisha kama serikali yake isingekubali "mikataba" yake, angejiunga na mfalme wa Ubelgiji. Basi Peters alipata waraka wa ulinzi kutoka serikali iliokuwa msingi wa koloni ya baadaye.

Kuna maneno ya Bismarck aliyosema 1888 yanayoonyesha hakuwa na raha kuhusu koloni; aliombwa kuingilia katika katika vurugu ya Emin Pasha pale Sudan Kusini. Alijibu: "Ramani yako ya Afrika ni ya kuvutia sana. Lakini ramani yangu ya Afrika iko Ulaya. Ufaransa iko upande wa kushoto, Urusi upande wa kulia, katikati tuko sisi".

Sasa nimeleta ushahidi mara mbili katika maneno ya wenyewe kwamba hapakuwa na mpango wa kuunda koloni kubwa ya Kijerumani jinsi uzlivyodai.
Basi lete ushahidi wako!!!
Siyo mahala pa kubishana hapa kwa kunganisha statements ambazo nyingine unaziweka out of context. Nitakutafutia kitabu kinachoonyesha kuwa mwanzo halisi wa hiyo inayoitwa Berlin Conference ilikuwa ni nia ya mfalme wa wa Ureno kutaka kuunganisha Mozambique na Angola. Akamshawishi Chancellor wa Ujerumani kuwa kwa vile Leopold wa Ubelgiji ameashachukua eneo kubwa la Kongo na kuna hatari akaendelea kuchukua zaidi, hivyo kuna haja ya kukaa na kufanya utaratibu wa kugawana bila kukwaruzana. Wakati huo Karl peters alishamwambia Chancellor kuwa anataka kuchukuka sehemu ya kwetu hii na sehemu ya Uganda na ameshaongea na watawala wa huko na kupata mikataba nao (hiyo ikiwa ni before the conference). Chancellor alimkatalia, ndipo Karl akamtishia Chancellor huyo kuwa asipomkubalia basi atagawa maeneo hayo kwa Leopold. Hali hiyo pamoja na ushauri aliokuwa amepata kutoka kwa mfalme wa ureno ndiyo ilisababisha Chancellor atake kuichukua nchi yetu kwa nguvu kutoka kwa Karl akitaka aunganishe nchi yetu na Kamerun ambayo walikuwa nayo kwa muda mrefu; uunganishaji wa namibia na nchi yetu haukuwa alternative kwani plani hiyo ingeingiliana na plan ya rafiki yake Mfalme wa ureno.

Sijakukatalia conclusions unazoleta kwani ziko documented kwenye mkataba huo, lakini hujanieletea chimbuko la mkutano wenyewe hadi kufikia mktaba huo. Walikaa Berlin kwa miezi mitatu mfululizo, sasa kama jambo lenyewe lingekuwa ni mktaba huo tu nawe unaamini kuwa kweli ingewachukua miezi mitatu kweli kukubaliana hayo. Kulikuwa na mambo contentious sana yaliyojadiliwa kuhusu hiyo mipaka ndipo wakaamua kufikia consesus unayosoma. Nitakutafutia kitabu hicho usome mwenyewe nikikipata. nadhani kilikuwa kinaitwa jina kama "Behind Bismarck's Berlin Conference on Africa" ingawaje sasa hivi sikumbuki sawasawa.
Nadhani Library ya stanforn wana old copy ya kitabu hicho.

Nadhani kitabu hicho ni hiki; ingawa sina uhakika sana ila title yake inaelekea kufanana kwa kuweka uzito mwa mkutano mikononi mwa Bismarck

1629851793638.png
 
Hawa watu walishaona mbali sana kabla yetu na hata leo hii wanafanya mambo kwa akili sana
 
Sote tunaelewa kuwa mkutano wa Berlin wa mwaka 1984 ndio ulioigawa Afrika kuwa katika mipaka tuliyo nayo leo. Mkutano huo uliitishwa na Otto von Bismarck ili kuigawa Afrika miongoni mwa mataifa ya Ulaya ambayo tayari yalikuwa yana infleunce Afrika kwa nia ya kuondoa conflicts. Ujerumani ilikuwa na influence katika sehemu tatu: Cameroon, Namibia na hapa kwetu Deutsch-Ostafrika.

Nia kuu ya Bismark ilikuwa ni kuigawa sehemu ya Afrika kusini mwa jangwa la Sahara katika vipande vinavyoanzia bahari ya Atlantic na kuishia bahari ya Hindi. Plani yake ilikuwa ni kuwa kuanzia Cameroon hadi Zanzibar ingekuwa nchi moja chini ya Ujerumani, halafu kuanzia Congo Brazaville hadi Msumbiji ya kasikazini ingekuwa nchi moja chini ya Ubelgiji, na kuanzia Angola hadi Mozambique ingekuwa nchi moja chini ya Ureno, halafu sehemu nyingine yote ya kusini mwa Afrika ingebaki chini ya Uingereza. Kwa plani hiyo Ramani ya Africa leo hii ingekuwa hivi:



Plani hiyo haikukubaliwa na mataifa mengine ya Ulaya hasa Mfalme Leopord wa Ubeligiji hakutaka kupoteza sehemu ya Kongo ambayo alikuwa amejimilikisha yeye binafsi, na halafu kukawa na ubishi mwingine kuhusu mgawanyo ambao ungeiweka Kenya, Uganda, sehemu ya kaskazini mwa Kongo, Central African Republic, Chad na na Nigeria chini ya mamlaka moja. Ukawa mvutano mkali kati ya Uingereza na Ufaransa. Mwingereza hakutaka kupoteza Uganda kwa vile ndicho chanzo cha mto Nile, na Mfaransa naye hakutaka kupoteza kipande chochote cha Afrika kwani kama plani hiyo ingeendelea, mfaransa angebaki mikono mitupu.

Halafu snag nyingine ikawa ni kuwa Waingereza nao hawakutaka kupoteza sehemu ya Zambia na Zimbabwe kwa vile ilikuwa inamilikiwa na kampuni ya Rhodes ambayo ilikuwa imeanzisha migodi kule. Kwa hiyo plani nzima ya Bismarck ikafeli, ndipo wakaamua kukata vipande vipande tuvionavyo leo. Hata hivyo Bismarck hakutaka kusindwa kirahisi, badala yake akaishawishi Uingereza ikubali kuchukua visiwa vya Zanzibar ili wabadilishane na visiwa vya Heligoland, na vile vile wabadilishe mpaka wa Namibia ili ufikie mto Zambezi, akijua kuwa kwa kutumia mto Zambezi angeweza kufikia bahari ya Hindi kirahisi bila kuzunguka Cape of Good Hope. Kwa hiyo Mpaka wa Nambia ukabidilishwa na kuwa na kale kasehemu kembamba kanakofikia mto Zambezi kama ionekanvyo kwenye ramani hapa.

View attachment 1905496

Wakati huo Uingereza ilikuwa inajua kuwa mto Zambezi hauwezi kutumika kwa usafiri wa meli kwa vile kulikuwa na Victoria falls mpakani mwa Zambia na Zimbabwe, ila wakawakubalia wajerumani haraka haraka kusudi wabaki na umiliki Kenya, Uganda, Zambia na Zimbabwe ambazo walikuwa na hatari ya kupoteza kwenye mkutano huo.

Sijui kama plani ya Bismarck ingefanikiwa huenda siku moja tungetawaliwa na Paul Biya, au Mobutu au Ngueso. Vile vile watu maarufu kama Roger Milla, Diblo Dibala, Abeti Maskini na Ndungidi wangekuwa watu wetu.
Britain alianza mchakato wa kuitawala Dunia yote tangu 1497 na alianza kuitawala baadhi ya sehemu za bahari huko ulaya kasoro Spain na Portugal walioanza kuexplore nje ya maeneo yao

Yaani inakadiriwa kuwa Robo ya dunia hawa Waingereza walimiliki yaani 25% au zaidi...kote Afrika, Asia, America na visiwa vya kutosha. Na msemo wao wa

'' Always the sun sets on British Empire''

Waingereza waliwaambia Wahindi na Wachina kuwa popote jua linapomulika mjue ni mali ya Uingereza, aliyekuja kufuta hii kauli ni Mfalme Francisco wa Hispania na kusema

'' I will never let the sun sets in British Empire''
 
Britain alianza mchakato wa kuitawala Dunia yote tangu 1497 na alianza kuitawala baadhi ya sehemu za bahari huko ulaya kasoro Spain na Portugal walioanza kuexplore nje ya maeneo yao

Yaani inakadiriwa kuwa Robo ya dunia hawa Waingereza walimiliki yaani 25% au zaidi...kote Afrika, Asia, America na visiwa vya kutosha. Na msemo wao wa

'' Always the sun sets on British Empire''

Waingereza waliwaambia Wahindi na Wachina kuwa popote jua linapomulika mjue ni mali ya Uingereza, aliyekuja kufuta hii kauli ni Mfalme Francisco wa Hispania na kusema

'' I will never let the sun sets in British Empire''
Wachina wanataka kuanza kurudia usemi huo leo. Wameshachukua karibu Africa yote, sehemu kadhaa za Asia na America ya kusini. Sasa hivi wanataka kuichukua Afghanstani pia.
 
Siyo mahala pa kubishana hapa kwa kunganisha statements ambazo nyingine unaziweka out of context. Nitakutafutia kitabu kinachoonyesha kuwa mwanzo halisi wa hiyo inayoitwa Berlin Conference ilikuwa ni nia ya mfalme wa wa Ureno kutaka kuunganisha Mozambique na Angola. Akamshawishi Chancellor wa Ujerumani kuwa kwa vile Leopold wa Ubelgiji ameashachukua eneo kubwa la Kongo na kuna hatari akaendelea kuchukua zaidi, hivyo kuna haja ya kukaa na kufanya utaratibu wa kugawana bila kukwaruzana. Wakati huo Karl peters alishamwambia Chancellor kuwa anataka kuchukuka sehemu ya kwetu hii na sehemu ya Uganda na ameshaongea na watawala wa huko na kupata mikataba nao (hiyo ikiwa ni before the conference). Chancellor alimkatalia, ndipo Karl akamtishia Chancellor huyo kuwa asipomkubalia basi atagawa maeneo hayo kwa Leopold. Hali hiyo pamoja na ushauri aliokuwa amepata kutoka kwa mfalme wa ureno ndiyo ilisababisha Chancellor atake kuichukua nchi yetu kwa nguvu kutoka kwa Karl akitaka aunganishe nchi yetu na Kamerun ambayo walikuwa nayo kwa muda mrefu; uunganishaji wa namibia na nchi yetu haukuwa alternative kwani plani hiyo ingeingiliana na plan ya rafiki yake Mfalme wa ureno.

Sijakukatalia conclusions unazoleta kwani ziko documented kwenye mkataba huo, lakini hujanieletea chimbuko la mkutano wenyewe hadi kufikia mktaba huo. Walikaa Berlin kwa miezi mitatu mfululizo, sasa kama jambo lenyewe lingekuwa ni mktaba huo tu nawe unaamini kuwa kweli ingewachukua miezi mitatu kweli kukubaliana hayo. Kulikuwa na mambo contentious sana yaliyojadiliwa kuhusu hiyo mipaka ndipo wakaamua kufikia consesus unayosoma. Nitakutafutia kitabu hicho usome mwenyewe nikikipata. nadhani kilikuwa kinaitwa jina kama "Behind Bismarck's Berlin Conference on Africa" ingawaje sasa hivi sikumbuki sawasawa.
Nadhani Library ya stanforn wana old copy ya kitabu hicho.

Nadhani kitabu hicho ni hiki; ingawa sina uhakika sana ila title yake inaelekea kufanana kwa kuweka uzito mwa mkutano mikononi mwa Bismarck
Kaka umeleta maneno mengi lakini hujaleta chanzo chochote kuthibitisha madai yako. Kutaja jina la kitabu fulani haina maana. (utaratibu ni nukuu, chanzo, pamoja na ukurasa unaorejelea).
Bismarck aliitisha mkutano baada ya kuelewana na Ufaransa; kinyume Ureno pamoja na Uingereza walijaribu kuzuia upanuzi wa maeneo ya mfalme Leopold na Ufaransa kwa kudai eti kuna haki ya Ureno juu ya pwani lote la Kongo. Leopold alimwomba Bismarck kuingia. Bismarck aliona nafasi ya kuchukua kazi ya mpatanishi mwema baina ya nchi nyingine akatuma mwaliko kwa mkutano.
Ukitaka kujisomea online, hapa hitimisho zuri la mwanahistoria Mchina: Wang Shih-tsung: The Conference of Berlin and British ‘New’ Imperialism, 1884-85

Sijaweza kuangalia kitabu unachotaja lakini nimepata ukaguzi wake katika makala ya mwanahistoria Mwingereza, ona chini kuhusu Bismarck na Afrika:
1629877149274.png

Chganzo: Bismarck and the German Interest in East Africa, 1884-1885, H. P. Meritt, The Historical Journal, Vol. 21, No. 1 (Mar., 1978), pp. 97

Hitimisho kwa jumla hapa, katika ukurasa kwa walimu wa historia

Germany and the Desire for Colonies

Despite German Chancellor Otto Von Bismarck’s opposition to overseas colonies, pressure from the German people to establish colonies for international prestige led to a significant empire during the Scramble for Africa.

Learning Objectives​

Analyze Germany’s efforts to obtain more influence in various areas of the globe

Key Takeaways​

Key Points​

  • Prior to German unification in 1871, most of the focus of German foreign policy was on issues internal to the state and its European neighbors.
  • This pragmatic attitude was mainly supported by the leading political figure of the time, Otto von Bismarck, a major force behind unification.
  • Bismarck disliked colonialism but reluctantly built an overseas empire when it was demanded by both elite and mass opinion.
  • The attitude toward colonialism shifted again during the reign of Kaiser Wilhelm II, who espoused a Weltpolitik foreign policy that emphasized aggressive diplomacy, the acquisition of overseas colonies, and the development of a large navy.
  • The rise of German imperialism and colonialism coincided with the latter stages of the ” Scramble for Africa ” during which enterprising German individuals, rather than government entities, competed with other already established colonies and colonialist entrepreneurs.
  • German colonies comprised territory that makes up 22 countries today, mostly in Africa, including Nigeria, Ghana, and Uganda.
  • Germany lost control of its colonial empire at the beginning of World War I when its colonies were seized by its enemies in the first weeks of the war.
    Chanzo: German Imperalism | Boundless World History
 
Back
Top Bottom