Pre GE2025 Mapendekezo ya CHADEMA juu ya Miswada ya Sheria za Uchaguzi ambayo Kamati ya Bunge inazuia yasisomwe Bungeni

Pre GE2025 Mapendekezo ya CHADEMA juu ya Miswada ya Sheria za Uchaguzi ambayo Kamati ya Bunge inazuia yasisomwe Bungeni

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Nataka unijibu je unaona sahihi na unaunga mkono kwa kila jimbo kuwe na wabunge wawili?
Cdm wanataka sera ya majimbo, unajua mfumo wao utafanya vipi kazi? Au unatumia mapendekezo ya cdm kwa mfumo wa kiccm? Je wakipunguza mishahara na muda wa vikao vya bunge? Jitahidi kutokutumia mtazamo wako kwenye mifumo ya wengine. Kwa taarifa yako watapunguza sana matumizi yasiyo na tija ya serekali.
 
Chadema inastahili pongezi
Tangu zoezi la kukusanya maoni lianze, maoni ya Chadema ndio the most exhaustive na bango kitita lake ndilo bango kitita kubwa kuliko michango yoyote!.

P
Hata hicho kipengele cha 5 cha kila jimbo kuwa na wabunge 2 wa kike na kiume? Unajua idadi ya wabunge itafika hata 700 kama hilo litapita? 300 tu hawa asilimia 90 hakuna wanachofanya sasa kumbe wanataka waongezwe wafike hata 700?
Ama kweli hii nchi kukombolewa ni miaka 100 au 300 ijayo
 
Pendekezo moja kati ya arobaini, umelishikia bango. Wao wameleta solution kwa issue ya viti maalumu. Hatuwezi kuendelea kulipa wabunge wa dezo.
Ni la hovyo.........
Huwezi mtu ukakaa ukawaza kuongeza idadi ya wabunge.
Inashtua kidogo.
 
CHADEMA hawajasema wanataka vikao vya bunge vipunguzwe wala malipo yapunguzwe. Wamesema, kwenye submission yao ya John Mnyika leo, wanataka kila jimbo liwe na wabunge wawili wa kuchaguliwa, mmoja mwanamke mmoja mwanamme.

Kwa hio, kwa mapendekezo ya CHADEMA, bunge hili la sasa la watu 400 linaenda kuwa na watu 800!

Tuwe na Rais wa kike na kiume basi! Na diwani mwanamke na mwanamke. Mana tunatafuta jozi za wawili wawili wa kwenda kuchumbiana kwenye vikao!

Ni mtu gani mwenye akili kichwani, wa chama cha upinzani cha nchi ya dunia ya tatu, ya watu masikini wa kutupwa, wachafu wenye njaa, wanaoshindia mihogo na maji machafu ya mitoni, biashara za masinia ya ndizi vichwani, boda boda na mama ntilie, anaependekeza kuongeza gharama za kutajirisha viongozi ???
Haki hata mimi hili limenishangaza sana. Yani wabunge ina maana watafika hata 800. Sijui hili linasaidia vipi mwananchi. Yani eti akiwepo wabunge wa kike na kiume so hoja zitakuwa zikiwasilishwa kijinsia au...
Na hapa unaona watu wanasema maoni safi.

Hii nchi watu wanaleta ushabiki kisiasa tu na ndio maana adui mkubwa wa nchi hii ni ujinga si kitu kingine. Ujinga ni mtaji wa wanasiasa na unawafanya wazidi kutajirika
 
Cdm wanataka sera ya majimbo, unajua mfumo wao utafanya vipi kazi? Au unatumia mapendekezo ya cdm kwa mfumo wa kiccm? Je wakipunguza mishahara na muda wa vikao vya bunge? Jitahidi kutokutumia mtazamo wako kwenye mifumo ya wengine. Kwa taarifa yako watapunguza sana matumizi yasiyo na tija ya serekali.
Jibu hoja kulingana na hoja iliyopo mezani kwa sasa. Kinachoendelea na kujadiliwa kwa sasa siyo habari za utawala wa majimbo. Hoja ni juu ya kuwa na wabunge wawili katika kila jimbo.je unakubaliana na huo ujinga?
 
Hapo kwenye wabunge wawili kwa Jimbo kwa maoni yangu ni Big no, mengine safi.
 
Kwenye mapendekezo hayo Unapata picha gani?
CHADEMA ni walafi tu wa madaraka, hawana nia ya kweli kulikomboa taifa hili kutoka kwenye makucha ya CCM.
Ni another monster in making.
 
Yani CHADEMA mnapendekeza bunge liwe double the size, mna akili vichwani kweli nyinyi ?????

Eti kila jimbo lipige kura kwa mwanamke na kwa mwanamme. Kwani wanaenda kuchumbiana mle bungeni ????

Basi na kila wizara tuwe na waziri mwanamke na mwanamme!

Every freaking where, tuwe na pair za kijinsia! Na Mwenyekiti wa CHADEMA tupate na mwanamke pia, kum-pair na Mbowe!

Wretchedly poor third world coutry mnafikiria ku double the legislature?

Most imbecilic proposition in political history of the world
Jinga kabisa wewe. Soma uelewe. Viti maalum vya wanawake vinafutwa! Badala yaek wanawake wapigiwe kura....
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nimesoma mapendekezo ya CHADEMA yaliyowasilishwa mbele ya kamati ya Bunge neno kwa neno, msitari kwa msitari na kifungu kwa kifungu.nimesoma kuanzia mwanzo hadi mwisho kwa kuwa mimi siyo mvivu katika kusoma na huwezi ukanificha jambo kwa kuliweka kwenye maandishi kwa matarajio kwamba sitasoma.

Ili andiko langu lisiwe refu sana basi Leo nitawapitisha katika hoja namba tano inayohusu aina ya wabunge na hoja namba nane inayohusu muundo wa tume na mapendekezo waliyopendekeza CHADEMA.

Ndugu zangu Watanzania imenisikitisha sana tena sana kunihuzunisha, kunishangaza, kuniduwaza, kunisononesha,kunipa mawazo, kunistajaabisha, kunipa maswali yasiyo koma niliposoma mapendekezo ya CHADEMA katika aina ya wabunge katika hoja yao namba tano.

Kwamba sasa CHADEMA wanapendekeza kuwa katika kila jimbo kuwe na wabunge wawili wawili watakaochaguliwa na wananchi kwa kufuata jinsia na makundi, yaani kutakuwa na mgombea mwanamke na mwanaume katika kila jimbo la uchaguzi ambapo mwanaume atapigiwa kura na wanaume tu na mwanamke naye atapigiwa kura na wanawake wenzake. halafu hapo hapo mwisho wa siku baada ya kumaliza uchaguzi mkuu CHADEMA wanataka na kupendekeza tena kuwe na wabunge wa viti maalum wasiopungua 30% ndani ya bunge letu.

Pia kwanini kuwe na viti maalumu tena wakati tayari mmeshapendekeza na kutaka kuwa kila jimbo lazima awepo mwanamke? Sasa hao viti maalum wanaingia kufanya nini tena bungeni? Kwani nini yalikuwa madhumuni ya kuanzisha viti maalumu? Si yalikuwa ni kuleta usawa wa kijinsia? Sasa kama mmependekeza kuwepo mwanamke kila jimbo halafu unataka tena viti maalum vya nini ? Hivi CHADEMA mna akili kweli ninyi?

Hivi nani aliyependekeza ujinga huu ndani ya CHADEMA? Kwa faida ya nani? Kwa jasho la nani ? Kwanini CHADEMA wanataka kutubebesha mzigo Watanzania walipa kodi? Kwanini wanaangalia maslahi yao na matumbo yao na kutusahau wananchi walipa kodi? Kwanini wanataka pesa zote na makusanyo yote ya nchi yaelekezwe katika kulipa mishahara na marupurupu ya wabunge? Kwanini tuache kufanya maendeleo na tujikite katika kulipa mishahara na kuwalea na kuwatunza wabunge kwa jasho letu? Yaani badala ya kufikiri namna ya kupunguza gharama wao wanaongeza gharama? Yaani jimbo liwe na wabunge wawili ? Halafu tena baadaye mpewe tena viti maalumu?

Hivi kwanini ninyi CHADEMA mbatupatia saba hasira na kichefuchefu Watanzania? Kwanini mnatia kinyaa? Hivi kama hamna hoja kwa nini msikae kimya? Hivi huu ndio ujinga na uhayawani mliokuwa mmekalia siku zote mnaujadili kwa ajili ya maslahi ya mimatumbo yenu kuijaza? Tutakuja kula kwenye matumbo yenu? Mtatuwekea bomba la chakula kutoka kwenye matumbo yenu? Yaani sisi tuhenyeke halafu ninyi mnataka kujiwekea uchochoro wa kutafuna pesa za nchi? Mna akili kweli ninyi?

Kwamba tuwe na wabunge wengi kuliko hata uingereza? Nani kasema na kwa hoja ipi na kwa utafiti upi na kwa ushahidi upi na kwa mifano ya wapi na kwa misingi ipi na kwa vigezo vipi na kwa namna gani? wingi wa wabunge katika jimbo moja kunachochea maendeleo katika jimbo? na vipi mbunge mmoja hawezi kuleta maendeleo katika jimbo mpaka wawe wawili? Kwa nini pesa za kumhudumia mbunge wa pili kuanzia mshahara,pesa ya usafiri au gari,posho za kikao,safari,kamati,kiinua mgongo zisipelekwe katika jimbo husika kuchochea maendeleo ya wananchi?

Kwanza kwanini mnataka mlete ubaguzi katika kupiga kura? Kwa kuwa pendekezo lenyewe ni la kibaguzi tu.utaanzaje kusema kila jinsia impigie mtu wa jinsia yake? Siyo ubaguzi huu? Siyo kuvunja umoja, mshikamano, upendo na nguvu katika majimbo na hatimaye Taifa zima kwa ujumla wake na hivyo kuzorotesha maendeleo katika majimbo na Taifa zima kwa ujumla wake?

Kwanini mnakuwa walafi sana na wenye uchu wa madaraka ninyi CHADEMA? Kwanini siku zote mnajifikiria matumbo yenu na familia zenu pekee? Mmegikiria kuwaza maisha ya watanzania na vipato vyao? Mngewaza maisha ya watanzania mngeanzia wapi kupendekeza ujinga wa namna hiyo?

Kwa hakika mlaaniwe kabisa ninyi mliokosa akili za kutambua maisha ya watanzania na vipato vyao na uzalendo kwa Taifa letu .Mungu awaalaani na kuwapiga upofu katika kila kitu. Nawaombea mpigwe pigo kama la 2020 msiwepo kabisa Bungeni ,maana hamna faida yoyote ile zaidi ya kujali matumbo yenu na maslahi yenu na kuja kuleta vibuli mtaani mkishavimbwiwa kodi zetu kama ambavyo mmekuwa mkitutukana kama alivyo fanya Godbless Lema kwa kusema kazi ya bodaboda ni ya laana.

Nitaendelea kuchambua hoja namba nane katika uzi mwingine.

Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Tuondolee ujuha wako hapa
 
Kwamba Chadema wanataka bungeni kuwe na wabunge wanawake na wanaume kwa kila jimbo?

Kama kweli wamependekeza hivi, wamekosea, tena wamekosea sana, sijajua kama kuna sehemu kwenye mapendekezo yao wameweka namna ya kupunguza mishahara na marupurupu ya wabunge.

Lakini kama hawajagusa hapo, halafu wakataka wawepo wabunge wa jinsia mbili kwa kila jimbo, plus viti maalum, Chadema wamefeli, watu tunazungumzia kupunguza gharama, iweje wao waongeze gharama?

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Jibu hoja kulingana na hoja iliyopo mezani kwa sasa. Kinachoendelea na kujadiliwa kwa sasa siyo habari za utawala wa majimbo. Hoja ni juu ya kuwa na wabunge wawili katika kila jimbo.je unakubaliana na huo ujinga?
Don't be naive, tazama kwenye kichwa Cha Uzi wako pale juu, Kuna popote umesema wabunge wawili Kila Jimbo, au umejitia hasira na mapendekezo ya cdm na hoja za kuokoteza?
 
Yani CHADEMA mnapendekeza bunge liwe double the size, mna akili vichwani kweli nyinyi ?????

Eti kila jimbo lipige kura kwa mwanamke na kwa mwanamme. Kwani wanaenda kuchumbiana mle bungeni ????

Basi na kila wizara tuwe na waziri mwanamke na mwanamme!

Every freaking where, tuwe na pair za kijinsia! Na Mwenyekiti wa CHADEMA tupate na mwanamke pia, kum-pair na Mbowe!

Wretchedly poor third world coutry mnafikiria ku double the legislature?

Most imbecilic proposition in political history of the world
Point.
 
Back
Top Bottom