Mapigano kati ya Israel na Palestina yalianza tangu enzi za vita kati ya Mfalme Daud Muisrael na Goliati Mfilisti (Mpalestina)

Mapigano kati ya Israel na Palestina yalianza tangu enzi za vita kati ya Mfalme Daud Muisrael na Goliati Mfilisti (Mpalestina)

Miaka ya nyuma kabla ya kuzaliwa Kristo (BC) kulitokea mapigano kati ya Waisrael na Wakaanani ambao ndio wenyeji wa eneo hilo wa kabila la Wafilisti ambao ndio Wapalestina wa sasa

Waisrael walikuwa wakiaminika kuwa ni wacha Mungu na Wafilisti walidaiwa kuwa wapagani kwa wakati huo

Katika vita hiyo nabii Daudi alipambana Goliati ambaye alikuwa Mfilisti na Daudi kufanikiwa kumuua Goliati kwa kumpiga na kombeo kichwani

Inaaminika kwamba Wafilisti walikuwa ni mijitu yenye miili mikubwa hivyo Daud Muisrael alikuwa na kamwili kadogo lakini alimshinda Goliati kwa kuwa Mungu alikuwa pamoja naye na ndugu zake Waisrael

Pia kwa kuwa kwa mujibu wa maandiko ya dini Mungu aliwaahidi Waisrael kuwapa mji huo wa Kanani wa Wafilisti (Wapalestna) ndio maana kila wakati kwenye vita kati ya pande hizo mbili Wasrael ndio wanaoshinda na kuungwa mkono na mataifa makubwa ya dunia hii

Awali maandiko kwenye misahafu na maandishi ya wanazuoni wa dini vinasema kuwa wana Wa Israel walikwenda utumwani nchini Misri kwa kipindi kirefu takribani miaka elfu nne

Mungu alisikia kilio cha Israel kutokana na mateso waliokuwa wakiyapata nchini Misri baada ya ndugu yao Yusufu aliyekuwa akiaminiwa na mfalme Farao (Firauni) kufariki dunia

Hivyo Mungu akawahidi wana wa Israel kuwapa nchi ya maziwa na asali ambayo ni Kanani

Ndipo Mungu alipomuinua Musa aende kwa Farao kuwapa ruhusa watu wake Israel watoka utumwani hapo Misri ili waende kumuabudu Mungu na kumtolea sadaka kwenye nchi hiyo ya ahadi Kaanani

Firauni alikuwa mbishi kuwaachia wana wa Israel lakini mapigo aliyopigwa na Mungu hatimaye mwenyewe alisalimu amri akawapa ruhusa Waisrael watoke Misri

Aidha kutokana na Waisrael kutokuwa wavivu na kuwa watu wanafanyakazi nyingi vizuri na ngumu pale Misri na kuifanya nchi hiyo kujitegemea kwa chakula ukilinganisha na Waarabu wenyeji wa Misri

Lakini nabii Musa alimkera Mungu ndipo Mungu alipomwambia hataingia Kaanani hakika atakufa kwa hiyo Waisrael waliingizwa nchi ya ahadi ya Kanani na nabii Joshua

Waisrael walipoingia Kaanani wakauteka mji huo kwa kushinda vita dhidi ya wenyeji wa mji huo ambao ni Wafilisti (Wapalestina) na kuwafurusha na kukaa eneo hilo

Wakati wa vita kuu ya pili ya dunia Adolf Hittler alilisambaratisha Taifa la Israel na kuwaua Wayahudi wengi wale wachache waliosalia wakakimbilia uhamishoni kwenye nchi mbalimbali duniani

Ndipo kipindi hicho Wapalestina wakarejea kwenye mji wao huo wa zamani wa asili wa mababu zao wa Kanani

Baadaye kwenye miaka ya 60 Waisrael wakajiunda tena wakazaliana wakaongezeka na kudai kurejea eneo la Mahariki ya kati kwenye miji yao ya asili waliyopewa na Mungu ya Jerusalemu, Kanani na maeneo mengine ya wakiamini ndio asili yao wakitumia ramani ya kwenye kitabu chao cha dini ya Kiyahudi

Ndipo Umoja wa Mataifa wakagawa baadhi ya miji wakapewa Wapalestina na baadhi wakapewa Waisrael mfano kwenye mji mkongwe wa Jeusalemu upande wa mashariki wa mji huo wamepewa Wapalestina na magharibi wanapewa Israel lakini bado kila mmoja haridhiki na eneo alilogawiwa

Hivyo sababu hiyo ya kugombea ardhi ndio uhasama ulipo kati ya Israel na Wapalestina tangu enzi za nabii Daudi hata kabla ya Kristo mpaka zama hizi za kizazi cha kisasa cha dot com na kistaarabu bado tu hakuna uelewano kati yao

Aidha inasemekana ugomvi huu wa pande hizi mbili kati ya Israel na Palestina hauwezi kwisha mpaka MASIHI WA BWANA YESU KRISTO ATAKAPO RUDI TENA MARA YA PILI DUNIANI UKIONA UGOMVI HUO UMEISHA UJUE KIAMA KIMEKARIBIA TUTUBU DHAMBI ZETU
Ugomvi ulianzia tumboni mwa mama yao
 
Waisraeli sio Wakanaani.

Ugiriki (Greece Empire) na Roma (Roman Empire) zilikuja baadaye sana Mashariki ya kati. Hawana vinasaba (DNA) yoyote na Waisraeli

Unajua Waisraeli waliambiwa wasioe au wasiolewe na wa Kanaani walipoingia nchi ya ahadi

Lakini baadhi ya Waisraeli walianza kuoa na kuolewa na Wakanaani

Inamaanisha kuna damu ilichanganyika ya Waisraeli na Wakanaani (Wapalestina)
Sasa unaposema Waisrael sio Wakaanani unamaani nini hapo?
 
Sasa unaposema Waisrael sio Wakaanani unamaani nini hapo?
Kuna kabila la Ngoni kutoka S.A walikuja Tanzania wakachanganyika na jamii ya Watanzania je, tutasema Watanzania ni Wasouth?

Au wale watumwa kutoka Afrika magharibi wakauzwa South America (Latin America) kama Brazil n.k wakachanganyika na jamii za kule je, tutahalalisha kuwa wale Afro-Latinos wa Latin America ni Waafrika?
 
Miaka ya nyuma kabla ya kuzaliwa Kristo (BC) kulitokea mapigano kati ya Waisrael na Wakaanani ambao ndio wenyeji wa eneo hilo wa kabila la Wafilisti ambao ndio Wapalestina wa sasa

Waisrael walikuwa wakiaminika kuwa ni wacha Mungu na Wafilisti walidaiwa kuwa wapagani kwa wakati huo

Katika vita hiyo nabii Daudi alipambana Goliati ambaye alikuwa Mfilisti na Daudi kufanikiwa kumuua Goliati kwa kumpiga na kombeo kichwani

Inaaminika kwamba Wafilisti walikuwa ni mijitu yenye miili mikubwa hivyo Daud Muisrael alikuwa na kamwili kadogo lakini alimshinda Goliati kwa kuwa Mungu alikuwa pamoja naye na ndugu zake Waisrael

Pia kwa kuwa kwa mujibu wa maandiko ya dini Mungu aliwaahidi Waisrael kuwapa mji huo wa Kanani wa Wafilisti (Wapalestna) ndio maana kila wakati kwenye vita kati ya pande hizo mbili Wasrael ndio wanaoshinda na kuungwa mkono na mataifa makubwa ya dunia hii

Awali maandiko kwenye misahafu na maandishi ya wanazuoni wa dini vinasema kuwa wana Wa Israel walikwenda utumwani nchini Misri kwa kipindi kirefu takribani miaka elfu nne

Mungu alisikia kilio cha Israel kutokana na mateso waliokuwa wakiyapata nchini Misri baada ya ndugu yao Yusufu aliyekuwa akiaminiwa na mfalme Farao (Firauni) kufariki dunia

Hivyo Mungu akawahidi wana wa Israel kuwapa nchi ya maziwa na asali ambayo ni Kanani

Ndipo Mungu alipomuinua Musa aende kwa Farao kuwapa ruhusa watu wake Israel watoka utumwani hapo Misri ili waende kumuabudu Mungu na kumtolea sadaka kwenye nchi hiyo ya ahadi Kaanani

Firauni alikuwa mbishi kuwaachia wana wa Israel lakini mapigo aliyopigwa na Mungu hatimaye mwenyewe alisalimu amri akawapa ruhusa Waisrael watoke Misri

Aidha kutokana na Waisrael kutokuwa wavivu na kuwa watu wanafanyakazi nyingi vizuri na ngumu pale Misri na kuifanya nchi hiyo kujitegemea kwa chakula ukilinganisha na Waarabu wenyeji wa Misri

Lakini nabii Musa alimkera Mungu ndipo Mungu alipomwambia hataingia Kaanani hakika atakufa kwa hiyo Waisrael waliingizwa nchi ya ahadi ya Kanani na nabii Joshua

Waisrael walipoingia Kaanani wakauteka mji huo kwa kushinda vita dhidi ya wenyeji wa mji huo ambao ni Wafilisti (Wapalestina) na kuwafurusha na kukaa eneo hilo

Wakati wa vita kuu ya pili ya dunia Adolf Hittler alilisambaratisha Taifa la Israel na kuwaua Wayahudi wengi wale wachache waliosalia wakakimbilia uhamishoni kwenye nchi mbalimbali duniani

Ndipo kipindi hicho Wapalestina wakarejea kwenye mji wao huo wa zamani wa asili wa mababu zao wa Kanani

Baadaye kwenye miaka ya 60 Waisrael wakajiunda tena wakazaliana wakaongezeka na kudai kurejea eneo la Mahariki ya kati kwenye miji yao ya asili waliyopewa na Mungu ya Jerusalemu, Kanani na maeneo mengine ya wakiamini ndio asili yao wakitumia ramani ya kwenye kitabu chao cha dini ya Kiyahudi

Ndipo Umoja wa Mataifa wakagawa baadhi ya miji wakapewa Wapalestina na baadhi wakapewa Waisrael mfano kwenye mji mkongwe wa Jeusalemu upande wa mashariki wa mji huo wamepewa Wapalestina na magharibi wanapewa Israel lakini bado kila mmoja haridhiki na eneo alilogawiwa

Hivyo sababu hiyo ya kugombea ardhi ndio uhasama ulipo kati ya Israel na Wapalestina tangu enzi za nabii Daudi hata kabla ya Kristo mpaka zama hizi za kizazi cha kisasa cha dot com na kistaarabu bado tu hakuna uelewano kati yao

Aidha inasemekana ugomvi huu wa pande hizi mbili kati ya Israel na Palestina hauwezi kwisha mpaka MASIHI WA BWANA YESU KRISTO ATAKAPO RUDI TENA MARA YA PILI DUNIANI UKIONA UGOMVI HUO UMEISHA UJUE KIAMA KIMEKARIBIA TUTUBU DHAMBI ZETU
Ukitaka kuelezea hii historia anzia kwa baba wa Imani, Ibrahim. Kwamba baada ya Sara kupata mtoto wake wa kiume Isaka ilimlazimu Hajir aliyekuwa kijakazi wa Kimisri (Mwarabu) aliyezaa na Ibrahim afurushwe na Mwanae Ishumael. Wakati huo Ibrahim alikaa maeneo ambayo kwa leo ni Iraqi, na huyu Ishumael ndiye chimbuko la Wapalestina wa leo wakati Isaka ndiye chimbuko la Waisrael wa leo kupitia kwa Mwanae Yakobo (Israeli mwenyewe) aliyewazaa akina Yusufu na nduguze 11.

Hivyo kusimulia hii historia kwa mlengo wa kiimani utaona hivi vita ni vya wanandugu wa baba mmoja yaani Ibrahim, lakini mama tofauti. Vita wakati wa Daud na Goriat ulikuwa ni mwendelezo wa uhasama uliokuwa umehasisiwa toka kuzaliwa kwa hawa wanandugu. Waisrael kukaa Kaanan na baadae kutawanyika na kurudi tena hakukuanzia na kukomea kwa Musa tu, hata hii ya kurudi kwao miaka ya 1948 baada ya kufurushwa na Hitler ilikuwa ni muendelezo wa kile kilichoanza enzi za Musa kuwatoa utumwani Misri.
 
Ukitaka kuelezea hii historia anzia kwa baba wa Imani, Ibrahim. Kwamba baada ya Sara kupata mtoto wake wa kiume Isaka ilimlazimu Hajir aliyekuwa kijakazi wa Kimisri (Mwarabu) aliyezaa na Ibrahim afurushwe na Mwanae Ishumael. Wakati huo Ibrahim alikaa maeneo ambayo kwa leo ni Iraqi, na huyu Ishumael ndiye chimbuko la Wapalestina wa leo wakati Isaka ndiye chimbuko la Waisrael wa leo kupitia kwa Mwanae Yakobo (Israeli mwenyewe) aliyewazaa akina Yusufu na nduguze 11.

Hivyo kusimulia hii historia kwa mlengo wa kiimani utaona hivi vita ni vya wanandugu wa baba mmoja yaani Ibrahim, lakini mama tofauti. Vita wakati wa Daud na Goriat ulikuwa ni mwendelezo wa uhasama uliokuwa umehasisiwa toka kuzaliwa kwa hawa wanandugu. Waisrael kukaa Kaanan na baadae kutawanyika na kurudi tena hakukuanzia na kukomea kwa Musa tu, hata hii ya kurudi kwao miaka ya 1948 baada ya kufurushwa na Hitler ilikuwa ni muendelezo wa kile kilichoanza enzi za Musa kuwatoa utumwani Misri.
Ni kweli Ishamaeli mtoto wa mjakazi wa kimisri ambaye alikuwa mchepuko wa Ibrahim ndiye aliyezaa na Ibrahimu ndio uzao wa Waarabu na Waisrael ni uzao wa Mtoto wa ndoa wa Ibrahim toka kwa Sarah mkewe wa ndoa

Sasa Wapalestina wamatokana na ukoo wa nabii Nuhu ambaye alikuwa na watoto wawilili mmoja shem ambaye ndio climb uko la Wayahudi na mwingine akiitwa Hamu ndio chimbuko la Wapalestina na Waswahilii

Kula chuma hicho
 
Ni kweli Ishamaeli mtoto wa mjakazi wa kimisri ambaye alikuwa mchepuko wa Ibrahim ndiye aliyezaa na Ibrahimu ndio uzao wa Waarabu na Waisrael ni uzao wa Mtoto wa ndoa wa Ibrahim toka kwa Sarah mkewe wa ndoa

Sasa Wapalestina wamatokana na ukoo wa nabii Nuhu ambaye alikuwa na watoto wawilili mmoja shem ambaye ndio climb uko la Wayahudi na mwingine akiitwa Hamu ndio chimbuko la Wapalestina na Waswahilii

Kula chuma hicho
Sawa kabisa Boi Manda, lakini huyo kijakazi hakuwa mchepuko bali Ibrahim alishauriwa na mkewe wa ndoa yaani Sarah, ajishindie huyo kijakazi ili apate walau mtoto atakae kuja kuwa mrithi wa mali za Ibrahim. Basi bwana, baada ya huyo kijakazi kumzalia Ibrahim huyo mtoto wa kiume, kijakazi akakunjua makucha na kuanza kumdharau Sarah ambae kwa muda mrefu wa ndoa alikuwa ajabahatika kupata mtoto.

Mara tu baada ya Sarah kumpata mtoto Isaka ktk umri wa uzee nae kalianzisha huku akimsii mzee Ibrahim amshughulikie huyo kijakazi na kitoto chake. Ndiyo ukawa mwanzo wa kuwafukuza kijakazi na mtoto wake waende wasikokujuwa.

Ni uzao huu huu wa Ishimael mtoto wa kijakazi, mtume Mohamed alikuja kuzaliwa baada ya vizazi vingi, na vilevile ni uzao ule ule wa Isaka mtoto wa Sarah ambao baadae Yesu alikuja kuzaliwa baada ya vizazi vingi.

Hivyo utaona kwa msingi wa historia ya kiimani, uhasama wa hawa watu ni wa vizazi na vizazi kuanzia kwa mama zao.

Lakini je, kwa ulimwengu tulio nao sasa hivi, mauwaji yanayoendelea huko Gaza ni ya kuacha yaendelee bila kukemewa na jumuyia ya kimataifa? Hapana, stop war in Gaza, stop killing the innocent.
 
Waisrael na Wapalestine wenyewe wanasemaje kuhusu huo mgogoro wao na sababu zake.

Maana wayahudi wenyewe hawaukubaki ukristo wala uislam lakini humu jukwaani sababu ya uhasama inanasibishwa na ukristo na uislam.

Wao humezesha vitu gani vizazi vyao? Huwapa sababu gani watoto wao za kupigana na kuwachukia wenzao
 
Waisrael na Wapalestine wenyewe wanasemaje kuhusu huo mgogoro wao na sababu zake.

Maana wayahudi wenyewe hawaukubaki ukristo wala uislam lakini humu jukwaani sababu ya uhasama inanasibishwa na ukristo na uislam.

Wao humezesha vitu gani vizazi vyao? Huwapa sababu gani watoto wao za kupigana na kuwachukia wenzao
Mgogoro huu inategea unauangalia kwa jicho gani. Ukiuweka kwa kuangalia haki za kibinadamu kinachofanywa na Israeli ni kitu kibaya sana thidi ya ubinadamu, lakini je kilichofanywa na Hamas kwa Waisrael
 
Mungu alimuahidi Ibrahim miaka mingi sana kuwa wazao wake au kizazi chake kingerithi nchi hiyo. Mpaka anakufa hakuona ahadi hiyo ikitimia.

Baadaye WAKANAANI wakaenda kuishi hapo kabla ya ahadi ya Mungu kutimia.

Inaweza kusemwa kwamba Wakanaani walikuwa wakaaji wa nchi ambayo haikuwa yao, tayari Mungu alipanga Waisraeli waishi hapo

Kizazi cha kipindi cha YOSHUA ndicho ambacho kiliona utimizo wa maneno ya ahadi hiyo aliyopewa babu yao Ibrahim miaka mingi iliyopita

Mungu aliruhusu Wasraeli wakiongozwa na jemedari Yoshua kuwaangamiza WAKANAANI na kutwaa eneo hilo.

Moja ya WAKANAANI waliopona kwenye shambulizi hilo ni yule kahaba RAHABU na familia yake

NB: WAKANAANI walikuwa wavamizi kwenye eneo ambalo tayari Mungu alipanga kimbele Waisraeli waende kuishi. Kwa hiyo natives ni watu wa kizazi cha Ibrahim (Waisrael)
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mungu alimuahidi Ibrahim miaka mingi sana kuwa wazao wake au kizazi chake kingerithi nchi hiyo. Mpaka anakufa hakuona ahadi hiyo ikitimia.

Baadaye WAKANAANI wakaenda kuishi hapo kabla ya ahadi ya Mungu kutimia.

Inaweza kusemwa kwamba Wakanaani walikuwa wakaaji wa nchi ambayo haikuwa yao, tayari Mungu alipanga Waisraeli waishi hapo

Kizazi cha kipindi cha YOSHUA ndicho ambacho kiliona utimizo wa maneno ya ahadi hiyo aliyopewa babu yao Ibrahim miaka mingi iliyopita

Mungu aliruhusu Wasraeli wakiongozwa na jemedari Yoshua kuwaangamiza WAKANAANI na kutwaa eneo hilo.

Moja ya WAKANAANI waliopona kwenye shambulizi hilo ni yule kahaba RAHABU na familia yake

NB: WAKANAANI walikuwa wavamizi kwenye eneo ambalo tayari Mungu alipanga kimbele Waisraeli waende kuishi. Kwa hiyo natives ni watu wa kizazi cha Ibrahim (Waisrael)
Code:
Baadaye WAKANAANI wakaenda kuishi hapo kabla ya ahadi ya Mungu kutimia.
Siyo kweli kwa sababu,

Mwanzo 15,
17 Ikawa, jua lilipokuchwa likawa giza, tazama, tanuru ya moshi na mwenge unaowaka ulipita kati ya vile vipande vya nyama.
18 Siku ile Bwana akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,
19 Mkeni, na Mkenizi, na Mkadmoni,
20 na Mhiti, na Mperizi, na Mrefai,
21 na Mwamori, na Mkanaani, na Mgirgashi, na Myebusi.

Makabila hayo 10 yote yalikuwepo eneo hilo kabla ya Ibrahim kupewa.
 
Acha kupotosha umma wa watanzania. Wafilisti (Philistines) ni jamii nyingine kabisa ambayo iliishi katikati ya Gaza na Ashkelon. Jamii hii kwa kuwa ilikuwa Hila za kuwaangamiza Wana wa Israel, Mungu alimtumia mfalme Nebkadnezer kuwa chukua utumwani na Wengine kuwaua katika vipindi hivyo hivyo wana wa israel alipochukuliwa utumwani. Tofauti na wana wa israel ambao Mungu aliwarudisha katika nchi yao, Mungu alihakikisha Wafilisti hawarudi kwao na hivyo walipotelea huko huko utumwani Tafadhali soma Amos 1:8, Ezekiel 25:16,17 Jeremiah 47:4 and Isiah 14:29 kuhusu uangamizo wa Philistines.
Wapalestina wa sasa hivi kiukweli ni Waarabu. kuna clip nitakurushia hapa hata wenyewe baada ya kuona wenzao wanawaacha solemba kwenye hili sakata, Mpalestina huyo analamika kuwa Jamani sisi ni ndugu zenu na KAMA UTATUFUATILIA SISI WOTE TUNA ASILI YETU EGYPT, SAUDIA NA NCHI NYINGINE ZA KIARABU.
Land of Palestine neno hilo lilitumika kwa mara ya kwanza na mwandishi mgiriki akimaanisha ile nchi yote takatifu ambayo kwa wakati anatamka neno hilo nchi hiyo ilikuja mpaka huku Jordan. Warumi ( waroma) walipojenga himaya yao kwenye eneo la kusini mwa syria na eneo la Judea katika karne ya 6 CE wakaamua kuliita eneo hilo palestine. Kuhusu taifa la Palestine, hiyo ni hila ya Waislamu waarabu wakisaidiwa na KGB ya Urusi katika miaka ya 60 kuanzisha Taifa hilo na kuwabatiza Waarabu wa eneo hilo kuwa ni wapalestina ili wajenge uhalali wa kudai nchi yote ikiwa na maeneo wanayoishi wayahudi. Kiujumla nchi hiyo wala haijawahi kuwa ya Waarabu bali ilikuwa ya Wayahudi na Wafilisti
Hivi huwa mnazingatia kitu gani kusema waisrael siyo waarabu?.

Ebu nisaidie kunielewesha kwa kuzingalia ramani hizi,
4-Abraham-journey-2.jpg
israel-and-arab-world.gif
israel_davids_kingdom_shg.jpg
 
Waliokuwa wanaugomvi tangu kwenye tumbo la mama yao ni Esau na Yakobo baadaye huko mbele ya safari ndio kinakuja kuzaliwa kizazi cha nabii Rutu ndio kinatokea kizazi cha Waisrael na Palestina
Luti na Ibrahim waliishi pamoja mpaka pale walipoanza kugombania maeneo ya malisho na ndipo Ibrahim alimuacha Luti katika bonde lote la Jordan na yeye Ibrahim akaelekea upande ambao ni kati ya mto Nile na mto Efrat.
Mwanzo 13,


5 Na Lutu aliyesafiri pamoja na Abramu, yeye naye alikuwa na makundi ya ng'ombe na kondoo, na hema.
6 Na ile nchi haikuwatosha, ili wakae pamoja; maana mali zao zilikuwa nyingi, hata wasiweze kukaa pamoja.
7 Kukawako ugomvi kati ya wachunga wanyama wa Abramu, na wachunga wanyama wa Lutu; na siku zile Wakanaani na Waperizi walikuwa wakikaa katika nchi.
8 Abramu akamwambia Lutu, Basi, usiwepo ugomvi, nakusihi, kati ya mimi na wewe, wala kati ya wachungaji wangu na wachungaji wako; maana sisi tu ndugu.
9 Je! Nchi hii yote haiko mbele yako? Basi ujitenge nami, nakusihi; ukienda upande wa kushoto, nitakwenda upande wa kuume; ukienda upande wa kuume, nitakwenda upande wa kushoto.
10 Lutu akainua macho yake, akaliona Bonde lote la Yordani, ya kwamba lote pia lina maji, kabla Bwana hajaharibu Sodoma na Gomora, lilikuwa kama bustani ya Bwana, kama nchi ya Misri hapo unapokwenda Soari.
11 Basi Lutu akajichagulia Bonde lote la Yordani; Lutu akasafiri kwenda upande wa mashariki; wakatengana wao kwa wao.
12 Abramu akakaa katika nchi ya Kanaani, na Lutu akakaa katika miji ya lile Bonde; akajongeza hema yake mpaka Sodoma.
 
Waisrael na Wapalestine wenyewe wanasemaje kuhusu huo mgogoro wao na sababu zake.

Maana wayahudi wenyewe hawaukubaki ukristo wala uislam lakini humu jukwaani sababu ya uhasama inanasibishwa na ukristo na uislam.

Wao humezesha vitu gani vizazi vyao? Huwapa sababu gani watoto wao za kupigana na kuwachukia wenzao
Kuna uhusiano kati ya Uyaudi, Ukristo na Uislamu, chimbuko la hizi dini ni moja japo kila upande unaamini uko sahihi kuliko upande mwingine. Kabla ya kuzaliwa Yesu kulikuwa hakuna ukristo na kabla ya kuzaliwa Mohamed kulikuwa hakuna Uislamu lakini Uyaudi ulikuwepo.

Uyaudi ulichagizwa na ahadi za Mungu kwa Ibrahim na uliendelea hata pale Waisrael walipokuwa Misri hadi kurudi kwao Kaanan. Yesu alipozaliwa aliukuta Uyaudi, na Wayaudi wenyewe hawakumuamini hivyo walibaki na dini yao, japo hata Yesu mwenyewe alikuwa Myaudi kwa asili. Misingi inayojenga ukristo ni ileile iliyojenga uyaudi tofauti ni kwamba Uyaudi unaamini ktk Torati tu.

Uislamu ulikuja miaka zaidi 500 baada ya ukristo. Sitaki kuongelea sana maana wao ktk mafundisho yao wanadai hata Ibrahim mwenyewe alikuwa Muislam!!! Ninachojuwa ni kwamba Ibrahim baada ya kupata ahadi toka kwa Mungu alikuja kuzaa watoto wawili kwa mama tofauti. Mama wa kwanza Muyaudi Mwenzie alimzaa Isaka na mama wa pili kijakazi wa Kiarabu alimzaa Ishimael. Ni katika uzao huo zilikuja kutokea hizi dini. Yaani ktk uzao wa Isaka kulikuja kutokea Uyaudi na baadae Ukristo, na ktk uzao wa Ishimael kulikuja kutokea Uislamu.

Kisa cha ugomvi kati ya Waisrael na Wapalestina ni hadithi ndefu, ambayo kama ni kwa kufuatilia maandiko ya vitabu vya dini, ina chimbuko kuanzia kwa mama yake Ishimael na mama yake Isaka pamoja na watoto wao. Sababu utofautiana tu kulingana na kizazi lakini uhasama ni wa tangu jadi.
 
Kuna uhusiano kati ya Uyaudi, Ukristo na Uislamu, chimbuko la hizi dini ni moja japo kila upande unaamini uko sahihi kuliko upande mwingine. Kabla ya kuzaliwa Yesu kulikuwa hakuna ukristo na kabla ya kuzaliwa Mohamed kulikuwa hakuna Uislamu lakini Uyaudi ulikuwepo.

Uyaudi ulichagizwa na ahadi za Mungu kwa Ibrahim na uliendelea hata pale Waisrael walipokuwa Misri hadi kurudi kwao Kaanan. Yesu alipozaliwa aliukuta Uyaudi, na Wayaudi wenyewe hawakumuamini hivyo walibaki na dini yao, japo hata Yesu mwenyewe alikuwa Myaudi kwa asili. Misingi inayojenga ukristo ni ileile iliyojenga uyaudi tofauti ni kwamba Uyaudi unaamini ktk Torati tu.

Uislamu ulikuja miaka zaidi 500 baada ya ukristo. Sitaki kuongelea sana maana wao ktk mafundisho yao wanadai hata Ibrahim mwenyewe alikuwa Muislam!!! Ninachojuwa ni kwamba Ibrahim baada ya kupata ahadi toka kwa Mungu alikuja kuzaa watoto wawili kwa mama tofauti. Mama wa kwanza Muyaudi Mwenzie alimzaa Isaka na mama wa pili kijakazi wa Kiarabu alimzaa Ishimael. Ni katika uzao huo zilikuja kutokea hizi dini. Yaani ktk uzao wa Isaka kulikuja kutokea Uyaudi na baadae Ukristo, na ktk uzao wa Ishimael kulikuja kutokea Uislamu.

Kisa cha ugomvi kati ya Waisrael na Wapalestina ni hadithi ndefu, ambayo kama ni kwa kufuatilia maandiko ya vitabu vya dini, ina chimbuko kuanzia kwa mama yake Ishimael na mama yake Isaka pamoja na watoto wao. Sababu utofautiana tu kulingana na kizazi lakini uhasama ni wa tangu jadi.
Aisee umenitoa tongotongo.

Kwa maana hiyo kila kizazi kina sababu zake as kwanini wanapigana sivyo??

Kwa hivyo sababu za vita ya 1960's, 70's na miaka hiyo kabla ya 2000 inaweza kua sio sababu inayofanya wachapane zaidi??
 
Back
Top Bottom