Mapinduzi ya Kijeshi Mali: Rais Ibrahim Boubacar Keita na Waziri Mkuu Boubou Cisse watiwa nguvuni na Vikosi vya Jeshi

Mapinduzi ya Kijeshi Mali: Rais Ibrahim Boubacar Keita na Waziri Mkuu Boubou Cisse watiwa nguvuni na Vikosi vya Jeshi

Milio ya risasi imesikika katika kambi ya jeshi iliyo karibu na mji mkuu wa Mali Bamako, na kuzusha hofu ya kwamba Jeshi linataka kufanya uasi kwa Serikali iliyo madarakani katika Nchi hiyo ya ukanda wa Sahel inayoghubikwa na mzozo na maandamano ya Raia wakishinikiza Rais kuachia madaraka.

Bado hakuna taarifa za kutosha kubainisha kilichotokea, Mashahidi wa kiraia na wa kijeshi wamesema kuwa milio hiyo ya risasi ilitoka katika kambi ya jeshi ijulikanyo kama Kati, iliyo umbali wa takribani kilomita 15 kutoka Bamako.

Taarifa zinasema Wanajeshi wengi hawafurahishwi na hali ya kisiasa inayojiri nchini humo, na wanataka mabadiliko.
( via @dw_kiswahili )
Ndanda kuchele
 
Jeshi la makada wa ccm haliwezi kamweeeeee kuasi chama la wana
Wananchi tuu wanatosha kuwatoa ccm madarakani..
1597707271160.jpeg
 
Hii ndiyo Africa bana kila mmoja anafanya kulingana na uwezo wake ,rais
hatian na wazir wake ngoja tuone muda utasema tu
 
Africa hali zinajulikana kina keita na wenzake wamechokwa na wananchi sasa mapinduz ya kijeshi usishangae atakae kuja madarakani pia akapinduliwa japokuwa aliaminika pia ni mkombozi wao this is Africa no one care
 
Rais wa Mali, Ibrahim Boubakar Keïta na Waziri Mkuu, Boubou Cissé wamewekwa chini ya ulinzi na wanajeshi walioasi nchini humo alasiri ya leo.

Jaribio la mapinduzi ya kijeshi ambalo bado linaendelea limeanza ndani ya kambi ya Jeshi nje kidogo ya mji mkuu Bamako.
 
Safi sana kwa madikteta ndivyo inavyotakiwa. Bila hivyo Afrika haitoboi maana yamegeuza nchi kama mali zao binafsi na magenge yao. In short hawakutakiwa hata "kumchelewesha" kupunguza milolongo isiyo na sababu wala tija.
Ukumbuke pia huko kutokumchelewesha Gadaffi kumesababisha nchi imerudi utumwani
 
Back
Top Bottom